SIMULIZI: Salhat SEHEMU YA 01

SIMULIZI: Salhat SEHEMU YA 01

ChikoTz

Member
Joined
Feb 26, 2019
Posts
37
Reaction score
33
Simulizi: SALHAT

Sehemu: 01

Mtunzi: Salma Ramadhani

Ulikuwa usiku wa manane ulioambatana na radi za kutosha huku mvua nyingi na Kubwa ikiendelea kunyesha katika maeneo ya Arusha mtaana wa Moshono karibu kabisa na uelekeo wa chekereni alionekana msichana mmoja akiwa na Mtoto mdogo mbele ya kifua chake huku akikimbia kwa hofu Kubwa sana na kutizama nyuma ambako ndiko kulikomfanya hofu yake itande zaidi.
Alijikwaa na kusimama tena kisha akambeba Mtoto yule na kuendelea kukimbia naye alikimbia naye hadi mahali alipohisi sasa ni salama kama atajificha hapo. Alijibanza katika kibanda kimoja na kuhisi kuwa hapo anaweza akawa salama wakati huo wote Mtoto yule mwenye miezi kama Minne alianza kulia na hivyo mama yule alichukua jukumu la kumnyamazisha kwa kumnyonyesha Mtoto yule ambaye alilipokea ziwa lake na kuanza kulinyonya akiwa hapo hapo liliingia kundi la watu wanne huku wakiwa wamevalia mavazi meusi na kushikilia bastola mikononi mwao huku wakiendelea kumtafuta hapo hapo liliingia gari jeuc na mlango ulifunguliwa na mmoja kati ya watu wale wanne waliowahi kutangulia. Vilishuka viatu vya kike vyenye rangi ya kijani na suruali nyeuc iliyoweza kumbana barabarah huku ikipokelewa na kibody cheupe kilicho chomekezwa ndani ya suruali ile na kikoti cha jeans cha kitop kilichoweza kuishia kwenye kifua chake.
Alitoa miwani yake na kivua kofia iliyokuwa imefunika uso wake alikuwa ni binti ambaye makamo yake hayakuweza kupishana na mama yule mwenye mtoto........Jina lake aliitwa Badra.

"Mmeshampata huyo Malaya???!! Aliuliza. "Hapana bossi bado hatujampata ila nahisi hawezi kukimbia umbali mrefu Kwani tayari tulishamjeruhi kwa risasi katika mbavu zake changa. Alijibu msichana mmoja ambaye aliongozana naye huyu waliimwita Mainda.

"Sawa nazihitaji mahiti zao hapa ziletwe sasa hivi hasa hasa huyo Mtoto" alizungumza Badra ambaye hakuonekana kuwa na hata roho ya huruma kwa Mtoto yule ambaye hata kujitambua bado.

Watu wale wanne walianza kumtafuta mama yule mwenye Mtoto wakiongozwa na Mainda.

Badra akiwa pale alifanikiwa kuyaona matone ya damu yakiwa yanaelekea katika njia ambayo ndimo alikojificha mama yule.

Alitabasamu na kucheka kinafki kisha akaanza kuzifuata alama zile za damu huku akiita.

"Samia!!! Samia!!!! Samia!!!!! Njoo rafiki yangu kipenzi kwanini unanipa wakati mgumu mimi wa kukutafuta wewe jaman ilihali unajua mimi sina shida sana na wewe zaidi ya huyo Mtoto wa Naseeb. Kwani huyo Mtoto anakipi kikubwa mpaka mnamficha hivyo jaman , Naseeb kafa leo kwaajili yake eti utaamini hilo. Samia!! Nilee tu huyo Mtoto hapa. Aliendelea kuongea huku akisogea karibu zaidi, wakati huo Samia alikuwa akitetemeka na asijue kipi cha kufanya ghafla mwanaye alianza kulia na kuwashtua hata wale waliokuwa hawajui ni upi upande alioko alimziba mwanaye mdomo na ghafla nayeye alizibwa mdomo na Mtu aliyetokea nyuma yake alijitahidi kumng.ata lakini Mtu yule alimgeuza na kumpa ishara ya kuwa anataka kumsaidia aliwasha simu yake iliyokuwa na mwanga hafifu kisha akaiplay sauti ya Mtoto iliyokuwa ikilia ndani ya simu na kumpa ishara ya Samia aondoke eneo lile pindi watu wale watakapoanza kumfuata yeye. Kijana yule alianza kupiga hatua na kuelekea chini kabisa ambako kulikuwa na kama bonde dogo tu lililobinuka kwa chini kidogo. Watu wale walianza kumfuata wakiamini ya kuwa ni Samia akiwa na mwanaye.
Wote walianza kumfuata na kumuachia nafasi Samia ambaye aliinuka eneo lile na kuanza kutembea taratibu huku akihisi maumivu makali sana upande wa kushoto katika mbavu zake na hii ni kutokana na risasi aliyokwisha tayri kupigwa na Badra.

Badra alipofika mbele kidogo baada ya kumfukuza Samia na kutokomea kusiko julikana alianza kuchezwa na machale na kuhisi tu huko siko baada ya kuanza kuisikia tena sauti ile ya Mtoto iliyokuwa ikilia kwa style ile ile tena kwa kujirudia wakati huo zilibaki mingurumo kadhaaa iliyokuwa ikisikika juu ya mbingu na radi chache zilizoweza kufanya waweze kuona hata kama siyo kwa mbali sana.

Badra alishtukia mchezo ule na kugeuka nyuma ambako alifanikiwa kumuona Samia akianza kutokomea maeneo yenye vibanda.

Samia alijitahidi kutembea lakini alishindwa kutokana na kidonda alichonacho wakati anaendelea kujisogeza zaidi aliviona viatu vya kike vikianza kumsogolea.

"Tafadhali Badra, Tafadhali usiniulie mwanangu!!! Alizungumza Samia akijitahidi kumtizama ni nani aliyekuwa akisimama mbele yake alipofika usoni hakuweza kumtambua vzuri na Kwani tayari alishaanza kuona kizungu zungu hakuchukua muda mrefu alipokonywa na Mtoto na hapo hapo alidondoka chini na kuzimia.

***** ****** ******

Ilikuwa acubuh yapata saa mbili kamili alionekana Badra akiwa amevalia gauni la kulalia na kutoka chumba kimoja ndani ya jumba Kubwa la kifahari alilokuwa akiishi tajiri mmoja aliyeweza kufahamika kutokana ma wingi wa Mali anazomiliki Jina lake walimwita Mr Matata huyo alikuwa tajiri aliyebahatika kuwa na Mtoto mmoja tu wa kiume ambaye alimpenda sana baada ya mkewe kufariki lakini mambo yalibadilika baada tu alipomuowa Badra Kwani hakumpenda tena mwanaye na mwisho wa siku kutokana na visa vya Badra baba huyo alimfukuza mwanaye ndani ya nyumba yake na kuishi na Badra.

Badra alijinyoosha na kuelekea moja kwa moja kwa friji ambapo aliiifunua na kuanza kukagua kipi cha kutumia kwa asubuhi yake hiyo. Aliichukua juice mango na kuelekea kwenye glass kisha akaimimina na kuanza kuitumia taratibu kabisa huku akitizama TV.

"Unaelekea wapi??! Aliuliza Badra baada ya kumuoma Mr Matata amevaa asubuhi asubuhi.

"Nataka kwenda kumchukua mjukuu wangu sitaki akae na baba mpuuzi na mama kama yule Kwani mazingira wanayoishi hayatamfaa yeye" aliongea Mr matata na kuondoka zake.

Badra alishikwa na hasira na kuitupa glass anayoitumia ukutani.

"Mpumbavu wewe Salhat...... Unawezaje kuwa kikwazo kwangu ukiwa na miezi michache tu!! Aliongea kwa hasira na kuuma meno yake kisha kuyatoa macho yake yaliyokuwa makubwa naya mviringo.

******* *******

Samia kutokana na jua alilokuwa akipigwa nao usoni na mawimbi ya habari kuwa makali kwa siku hiyo hakuweza kulala kwa muda mrefu. Alishtuka na kuita
"Salhat"!!! Pembeni yake alimuona mwanamke mmoja aliyekuwa amembeba Salhat na kumpatia uji.
Alimchukua mwanaye Salhat na kumuuliza.

"Wewe ni nani???!! Na hapa ni wapi??! Tafadhali okoa maisha ya mwanangu yeye ni mdogo sana hajui wala hatambui chochote Tafadhali!! Aliongea Samia akihisi ya kuwa Mtu yule ni mbaya wake, hapo hapo aliingia kijana aliyeweza kumsaidia Jana ucku ili asikamatwe.

"Huyu ni mke wangu anaitwa Lidia, mimi na yeye Jana tulisaidiana kwa pamoja kwaajili ya kuokoa maisha ya mwanao, na sasa usijali Kwani haupo tena Arusha alizungumza na kufungua upande aliotokea huku akimfanya Samia kuona bahari njee.

"Huku wapi??!!! Aliuliza kwa mshangao.

"Dar es salaam ila usijali pia kwasabab kesho kutwa tutaenda mwanza na huko itakuwa vigumu kwa Mtu yule kukufuatilia tena....... Lakini Dada!!!
Aliongea na kunyamaza huku akihisi azungumze au.

"Endelea" kauli ya ruksa ilitolewa na Samia.

"Kwanini wnamuandama Mtoto mdogo namna hiyo??!!

Samia alitizama chini na kumtizama mwanaye mdogo Salhat. Kisha akawaambia.

"Kweli kwenye maisha kuna kupanda na kushuka, na siku zote unaambiwa fadhila mfadhili mbuzi binadamu anamauzi, na nimeamini mbuzi akikuuzi utamnywa mchzi ila mkataapo pema pabaya panamuita" alizungumza maneno hayo ya mafumbo na kuwa kama ameendelea kuwachanganya zaidi Joseph na mkewe Lidia ambao wlitizamana tu na kurudisha macho kwa Samia aliyekuwa akiendelea kulia tu baada ya kuyazungumz maneno Yale Kwani aliyaelewa mwenyewe.

Kip kitafuata katika sehemu ya pili ya cmuliz hii ya Salhat ikiw huu ndyo mwanzo tu wa simuliz hii usikose kuifuatilia

CHANZO
bongosimulizi.com
SIMULIZI%20%E2%9D%A4%20ELIMU%2020181208_162333%20(1).jpeg
 
SIMULIZI: Salhat SEHEMU YA 2




Simulizi: SALHAT
Sehemu: 02
Mtunzi: Salma Rashid


Tulipoishia

Ni baada ya Samia kuzungumza maneno ambayo aliyaelewa yeye mwenyewe lakini ilikuwa ngumu kwa Lidia na mmewe Joseph kuyaelewa.

*** *** *** ***

Huku nako Mr matata akiwa nyumbani kwake huku kundi Kubwa la watu wakiwa wamekaa mafungu mafungu na wengi wakiwa wamevalia nguo nyeusi.

Alionekana kama Mtu anayejaribu kuvuta kumbukumbu kama vile anataka kukumbuka kitu lakini hakiingii akilini mwake. Alimwita mkewe Badra.

"Badra......watu wanasema nilimfukuza Naseeb nyumbani, lakini mbona mimi sikumbuki hivyo nitawezaje kumfukuza Mtoto wangu wa pekee ndani ya nyumba niliyojenga na mama yake ambayo ni halali yake hapo ndiko ambako nashangaa" aliongea kwa kujishangaa ni kweli wala haikuwa akili yake Bali akili hiyo ni kutokana na madawa anayopewa na Badra.

"Tumia kwanza haya maji kisha nitakuelezea kwann ulimfukuza nyumbani Naseeb"

Mr matata aliichukua glass ile aliyopewa na Badra lakini aliitizama tu na kumtizama sana Badra usoni kisha akaipasua ile glass chini.

"Nakuuliza kipi kimetokea mpaka Naseeb akaondoka nyumbni ww unanipa maji mimi, ilihali mwanangu tayri ameshakufa nitamwambia nini mm mke wangu aliyeweza kuyatoa maisha yake kwaajli ya Naseeb eti Leo na yeye kafa nitaiweka wapi sura yangu baada ya mwanangu kwenda kukutana na mama yake akimwambia kuwa mimi ndye niliyemfukuza nyumbani" aliongea akiwa mwingi wa hasira.

Hapo hapo walikuja vijana kama ishirini waliokuwa wakiongozwa na kiongozi wao aliyeitwa Rajab.

"Nauliza Yuko wapi mtoto wa mwanangu??!!

"Tumefuatilia kwa makini ila hatujagundua lolote lile Kwani hata nyumba waliyokuwa wakiishi hakukuwa na Mtu yoyote tena zaidi ya damu ya Naseeb" alijib Raja.

"Nimesema sitamzika Naseeb kama Mtoto wake hatakuwepo hapo kushuhudia maiti ya baba yake, mtafuteni huyo mwanamke popote alipo na mniletee mjukuu wangu hapa kwa garama yoyote namtaka mjukuu wangu"!! Aliongea na kuwaambia waendele kumtafuta.

Hapo hapo waliingia kikosi cha jeshi la polisi kilichokuwa kinaongozwa na IGP Saidi.

"Tumegundua ya kuwa Naseeb aliuwawa kwa kupigwa bastola tatu katika upande wa kushoto wa kifua chake ila bado hatujajua ni nani muuwaji kama tunavyohisi ni mkewe Samia na pia kuhusu habari za Mtoto bado hatujazipata"

"Yeyote aliyehusika na mauji ya mwanangu sitamuacha mzima hata kama ni nzii akamatwe na aletwe hapa" aliamuru na kupiga simu mahali huku polisi wale wakiondoka.

"Haloo hao wapelelezi wa kujitegemea umewapata wangapi, 30 sawa, kazi ianze Mara moja mission yao ni kumpata mjukuu wangu ndani ya masaa 24. Alikata simu na kupiga tena.

" halooo Raisi, Tafadhali naomba msaada wako!!!!!

Nchi nzima ilichafuka kutokana na msako uliokuwa ukipita nyumba kila nyumba kwaajili ya kumtafuta Samia pamoja na Salhat huku ndege zote zilizokuwa zikitakiwa kusafiri kwaajili ya kwenda nchi za njee zikizuiliwa haikuwa kwa ndege tu Bali hata magari ya kusafiri ya kwenda mikoani meli na hadi pikipiki zote hazikufanya safar yoyote watu wote walitakiwa kuwa nyumbani kwao hivyo hata waliokuwa wakiuza masokoni siku hiyo walifunga.

"Jamani leo kuna nini mbona hivyo?!??! Waliulizana wanawake wawili waliokuwa wamefunga vibanda vyao na kuanza kurejea nyumbni kwao ambako barabara nzima ilikuwa imepoa hakukuwa na hata kelele ya cm kuita kwa siku hiyo.

"Siku zote uaambiwa pesa inaongea ni tajiri Matata anamtafuta mjukuu wake baada ya Mtoto wake kuuwawa na mke wake'

"Heeee wewe usiniambie kwahiyo mwanamke akamuuwa Mme wake kisha akaondoka na Mtoto sindiyo…......…… sasa Kwani alikosa nini kwenye familia ya Mr Matata mbona ipo na kila kitu jaman???!! Aliuliza kwa kutia huruma.

"Navyosikia ni kuwa mwanaye hakuwa anaishi kwenye nyumba yake alikuwa akiishi kwingne kabisa na mke wake... Na Mr Matata ndye aliyemfukuza mwanaye!!!!"" Aliongea mmama yule.

"Sasa.......... Kama alimfukuza anamtafuta ya nn tena labda........ Wakiwa wanaendelea kuzungumza hapo hapo mbele yao walikutana uso kwa uso na Mr Matata ambaye sasa aliona kama gari linamchelewesha kumpata mjukuu wake.

"Mnapenda sana kuzungumza siyo??? Aliwauliza na kuwapita bila kuwasemesha neno. Alikuwa maeneo ya Chekereni na huko ndiko Samia alikopita wakati anakimbizwa na na Badra damu haikuweza kuonekana kutokana na mvua iliyoweza kuendelea kunyesha hata Alama za viatu pia ziliweza kupotea kutokana na kuwa kulikuwa na watu waliokuwa wakiingia sokoni na kutoka, haisi zilizokuwa zikileta abiria na kuwachukua hivyo ilikuwa vigumu kupata ushahidi au kutambua ya kuwa Samia na mwanaye walipita eneo lile.

Akiwa anatembea mbele zaidi Mr matata alikanyaga kitu kilichomfanya mguu wake ushtuke na kuutoa mguu wake kisha kutizama ni nini amekikanyaga hiyo ilikuwa ni cheni ambayo alimnunulia mkewe Saumu kama zawad baada ya kugundua kuwa ana mimba na alipofariki baada ya kumzaa Naseeb cheni hiyo alimpa mkewe na kumwambia amvalishe mwanaye.

" hii cheni mwanagu Naseeb ndyo alikuwa nayo!! Imefikaje hapa???! Aliuliza kwa mshangao na kuiokota cheni ile.

"Tafadhali iweke hapa alizungumza IGP Saidi aliyetoa kitambaa chake na kumuomba Mr matata aweke hapo.

Mr Matata aliitazama na kuiweka kama alivyoambiwa.
IGP alipiga simu na kuomba askri baadhi waongezwe kwaajili ya kuja kufanya upelelezi zaidi.


Hapo hapo aliingia kijana mmoja na kuzuiliwa na mabodyghard wa mr matata.

"Nina kitu chamaana nataka kuzungumza naye,, mr matata alitoa ruhusa ya kijana yule aachiliwe na aje mahali alipo.

"Unashida gani???!

Kijana aliingiza mkono wake mfukoni na kutoka na simu.

"Yanini??! Aliulizs Mr matata.

Aligusa simu ile na kumuonyesha picha ya Naseeb akiwa na mwanaye Salhat.

"Nipe hiyo simu!! Aliongea mr matata baada ya kumuona mjukuu wake.

"Hapana nataka million 20 ili nikupe kama hutaki naifuta hii picha" alizungumza kijana yule akiwa tayr ameshaanza kugusa kitufe cha kudelete.

"Hapana nakupa"

Aliingia mfukoni na kutoa check aliyotaka kuaza kuandika.

"Hapana mimi siyo mjinga waweza kuninyang.anya pindi nitakapokupa simu hii"

"Hapana niamini mimi!sitafanya chochote kile na utakuwa salama nipatie picha ya mwanangu na mjukuu wangu.

Kijana yule alitoa simu ile na alipewa pesa yake kama alivyoahidiwa hpo hapo alikamatwa.

"Itabidi ukalisaidie jeshi la polisi umeipata wapi hii simu. Alimkamata IGP na kuondoka naye eneo lile.

*** **** ***

Baada ya muda kupita Badra akiwa ndani ya nyumba yake alishngaa baada ya kuona picha zake zote alizozigaramikia na kuziwekea nakshi za kutosha zikitolewa na kubandikwa picha nyingne.

" nyie mnafanya nini aliuliza baada ya kuona watu waliokuwa wageni katika upeo wa macho yake.

Alishuka ngazi haraka haraka na kwenda kutizama hizo zilikuwa picha za Salhat zilizokuwa tayri zimesharembwa na kuwekwa kwenye fremu Kubwa kabisa na nyingne akiwa na baba yake.

"Nilisema tu nilijua tu haka katoto cha huyu jini haka!!! Aliongea kwa hasira na kuyatoa macho yake kwa hasira na ghadhabu.

***** ****** ****

Huku nako Samia akiwa na Lidia wakiwa wamerejea baada ya kukuta hakuna magari yoyote yanayosafiri kuelekea mikoani kwa siku ya Leo.

"Samia nakuamini naamini hujafanya vile wanavyosema ila kasheshe ni kwamba utatokaje hapa, ungemrudisha huyu Mtoto kwa babu na wewe uangalie jinsi ya kujisaidia kwa maisha yako Kwani sasa yako hatarini.

"Lidia, siyo kwamba napenda haya maisha ya mihangaiko hapana lakini sina cha kufanya wala siwezi kumpeleka mwanangu kule,Kwani nitakuwa nimemuuwa mwanangu mwenyewe" alizungumza na kumtizama Lidia ambaye alibaki akitizama.

"Inabidi nirejee tu nyumbani na nikapokee adhabu yoyote nitakayopewa na hiyo ni kwaajili ya usalama wa Salhat wangu" alizungumza na kumtizama Salhat aliyekuwa amelala.

Je kipi kitafuata usikose

CHANZO
bongosimulizi.com
 
Simulizi: SALHAT
Sehemu: 03
Mtunzi: Salma Rashid


Ni baada ya Samia kuhitaji kurudi nyumbani kwao na mwanaye Salhat.

***** ******* ***

" itabidi tumzike Kwani hatutaweza kusubiri siku nyingne zaidi!! Aliongea shehe ambaye aliamuru maiti ya Naseeb ichukuliwe na kuanza kufanyiwa utaratibu wa mazishi.

Mr Matata ndye ambaye alishindwa kuelewa mtoto wa mwanaye Yuko wapi sasa!! Kwani tayri alishamtafuta bila mafanikio yoyote, alishindwa kuizuia maiti ya mwanaye isizikwe Kwani hakuwa na lakufanya tena.

"Abdul nakuahidi mwanangu nitamtafuta Mtoto wako na nitamlelea mimi" aliongea huku akitizama nguo za Salhat na baadhi ya vitu vilivyoletwa baada ya kupatikana katika nyumba waliyokuwa wakiishi.

Badra alitizama kwa hasira sana Kwani kila kitu sasa katika jumba lile kubwa la kifahara lilitawaliwa na Salhat pasina uwepo wake.
Aliingia ndani ya chumba chake na kutizama chumba kuzima hakukuwa na Mtu alitoa kijiti ndani ya kabati lake na kukupiga mlangoni kisha akapotea katika hali ya kutatanisha sana.

Alitokea katikati ya msitu ambao miti yake majani yake yalikuwa vichwa vya watu huku ardhi yake ikitawaliwa na mifupa ya binadamu, mito yake ikiwa inatiririsha damu kwa wingi pasina kukoma alipofika mtoni hapo pembeni yake kulikuwa na kiganja cha mkono wa Mtu ambapo alikichukua na kukitekea damu ile kisha kuinywa na baada ya hapo alipotea tena na kutokea sehemu nyingne.
Huko alikotokea sasa kulitawaliwa na nyoka kila mahali waliokuwa wazima wakipisha katikati ya miguu yake na wengine wakimpanda.
Kitendo hicho hakikuweza kumtishia Kwani tayri alishawazoea na huwa anakuja kila Mara anapohitaji msaada zaidi. Alitembea hadi kufikia Mti mmoja ulioko pekee yake na uliochongoka kisha kutoa shepu ya mlango alipofika hapo aliinama na kuingia ndani hatimaye Mti ule ulijifunga na hakukuwa tena na alama yoyote ya mlango wala Mti wowote pale.

Alitokea sehemu nyingne akiwa tayri ameshavalia mavazi meusi yani akiwa amejifunga kaniki ambayo ilianzia kifuani na kuishia juu ya magoti yake cheni zilizoweza kubebana ndani ya shingo yake pamoja na bangili zenye rangi nyeusi huku akisindikizwa na ngozi yenye rangi nyeusi miguuni mwake na kuonekana kama vikuku ndan ya miguu yake yote miwili.

Alitembea kwa hatua kadhaa baada ya hapo alifika mahali na kupiga magoti.

"Nimewasili eeee malikia wa kuzimu wa ukoo wetu wa Abandandi Alizungumza kwa heshima Kubwa sana huku akiwa amekiinamisha kichwa chake.

"Nimepokea heshima yako Mtoto wa malikia wa kuzimu wa ukoo wa Abandandi" alijibu mwanamk Yule ambaye aligeuka na kuweza kuonekana sura yake ikiwa ya kutisha na kustaajabisha Kwani ilikuwa imejaa mabaka ya nyoka na macho makali sana yenye kuwaka mithili ya pakaa.

"Razzio kwanini mpka sasa umeshindw kumuuwa yule adui yetu kwann mpaka sasa Yuko hai!!!?? Aliuliza malikia wa kuzimu.

"Nisamehe malikia wangu, ila nilijitahidi kwa kila mbinu ikashindikana Kwani kwa mbinu za kishetani hatumuwezi hata za kibinadamu pia ziligonga mwamba" aliongea Badra ambaye jina lake la kuzimu ni Razzio.

"Tulikupeleka duniani mapema kwaajili ya kuidhibiti nyota ya Naseeb ambayo ingeweza kumleta mshindani mkubwa katika ukoo huu wa Abandandi, tulitumia nguvu zetu nyingi kukupeleka duniani na kukupa sura ya kibinadamu kwaajili ya kumuulia mbali Naseeb lakini ulishindwa kutokana na upumbavu wako wa kumpenda binadamu, tukakupa sharti la kulala naye ili umchafulie nyota yake hilo nalo ulishindwa na ukaishia kulala na baba yake ambaye hana faida kwetu. Pia ukashindwa zuia asikutane na msichana ambaye anatoka koo pinzani na sisi na hatimaye wakampata Mtoto atakayekuwa tishio kwa ukoo wetu sasa hata huyo mtt kummaliza umeshindwaaa!!!!, alizungumza kwa kueleza na kwa hasira zaidi malikia huyo wa kuzimu.

"Kama kazi imekushindana sasa nitaenda mimi mwenyewe duniani kwaajili ya kupambana naye" alizungumza na kusimama juu yake chake na hapo ndipo tulipogundua ya kuwa hakuwa na miguu ya kawaida Bali miguu ya mikono ya wanadamu.

***** ****** *****

Tukirudi duniani Mwili wa Badra ulikuwa uko kitandani tu pasina kujigusa wala kufanya chochote kwasababu nafsi yake tayri iisharudi kuzimu na alipatiwa adhabu baada ya kushindw kufanya kazi aliyopewa na mama yake.

***** ***** *****

Samia aliwaaga na kuamua kuondoka.

"Sasa lakini utawezaje kutoka hapa watu wamejaa kila mahali wakikutafuta wewe na nihatari sana" aliongea Joseph.

"Sasa tutamsaidiaje mume wangu?? Aliuliza mkewe Lidia.

Samia alitabasamu na kuwatizama kisha akayazungumza haya yafuatayo.

"Hakuna Mtu atakayekuwa na uwezo wa kuniona kama mimi sijataka yeye anione labda mpaka awe na imani Kali sana"

"Unamanisha nini?? Aliuliza Lidia.

"Mimi siyo binadamu!! Alizungumza na hapo hapo alijibadilisha katika umbile lake la kijini.

Alivaliaa gauni jeupe ndefu mpaka chini taji lililoweza kurembwa na mauwa ya kila rangi likiwa limezunguka nywele zake ndefu zilizokuwa kichwani mwake na kujiachia mpka kufika makalioni mwake uso wake ulioweza kurembeka kwa nakshi nakshi za Mtoto wa kike na harufu Kali ya marashi iliyoweza kupenya katikati ya tundu zao mbili za pua baina ya Lidia na Joseph.

Walibaki wakimtizama na kushindwa kuelewa ni kipi kinatokea mbele ya macho yako.
Ni kweli Samia hakuwa binadamu Bali ni Jini aliyeweza kutoka katika ukoo wa Sultan Shariphu baada ya kumpenda Naseeb na kuamua kuishi naye maisha ya kawaida kama waishivyo binadamu wengine.

**** ***** ***** ****

Katika kitu ambacho kilimshangaza Mr matata ni picha za Samia Kwani ziliweza kuonekana kwenye simu tu lakini alipotaka zitolewe katika majarida kwaajili ya kuandika matangazo ya kuwa anatafutwa hazikuweza kutoka kabisa.

"Kwanini iwe hivi alijiuliza wakati huo akiwa hospitalini na akiwa amekaa pembeni kabisa ya Badra ambaye hakuwa yeye Bali mwili tu alioutumia pindi anapokuwa duniani.

Hapo hapo dactar aliingia jina lake aliitwa Hassan huyu alikuwa dactari bingwa sana na alijulikana Africa nzima kutokana na kazi zake za kuweza kufanya operation pasina Mtu yoyote aliyemfanyia operation kupoteza maisha.

"Ammmnhhh Mr matata najaribu kulitizama ni lipi tatizo la mkeo lakini nimeshindwa kugundua Kwani tumepima vipimo vyote na hatujaona sehemu yoyote yenye tatizo Kwani blood pressure yake iko normal, mapigo yake ya moyo yako kawaida tu presha pia iko kiasi, labda nahisi kafaint kutokana na mawazo yake kuwa mengi ila atarejea katika hali yake ya kawaida baada ya kurelax hivyo ungeweza kumpeleka tu nyumbni kwaajili ya kuendelea kupumzika zaidi aliyatoa maelezo hayo na kumpatia Mr matata.

"Sawa docta Hassan nakushukuru lakini kuna jmbo lingne linaniumiza kichwa sana ni kuhusu hii picha aliitoa simu na kumuonyeshea picha ya Samia.

"Nashangaa kwanini haitaki kutoka ndani ya hii simu ikiwa na hali hii hii Mara ukiweka katika laptop utaona picha zote hizi zake hutoziona nikitaka itoke katika majarida picha zake hazionekani vizuri hili nalo litakuwa tatizo gani ???!! Aliuliza baada ya kuhisi hilo nalo laweza kujibiwa na docta Hasan.

Dr alizitazama zile picha kisha akamtizama Mr matata ambaye alionyesha anahamu kubwa kulisikia jibu lake.

"Kwa kweli sijui" alijibu tu kwa ufupi kisha akamwambia.
"Mr matata nafikiri hata wewe hali yako siyo nzuri basi naomba nikufanyie vipimo kidogo" alizungumza Dr Hasan baada ya kuona ya kuwa Mr matata anachokizungumza hakiwezi kuwa ni cha kweli. Ila alizungumza ukweli mtupu na picha hizo za Samia alibahatika kuziona yeye mwenyewe tu ila watu wengne waliona ni peusi tu hivyo walifikiri ya kuwa mzee huyo anaanza kuwa kichaa.

**** ***** ***

Samia akiwa na mwanaye na kuelekea ngomeni kama alivyosema alianza kuona miti mingi ikicheza huku upepo mkali ukivuma.

"Jitokezee, sipendi kupigana Vita vya mafichonimekwambia jitokeze"

Ghafla ulisikika mlio wa Mtu kutua nyuma ya mgongo wake na hapo Samia taratibu kabisa alianza kugeuza shingo yake na kutaka kujua ni nani huyo"

Je kipi kitafuta!!, na unafikiri ni nani aliyoko nyuma ya Samia don't miss it

CHANZO
bongosimulizi.com
 
Endeleza hii story we boya.

Kabla sijakuchongea kwa moderator wakufukuze hapa jf.

Alaaaaa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom