Simulizi: Mwanafunzi Mchawi (A Wizard Student)

Mhuuuu ingelikuwa powà hii ikawa na uzi wake special make apa ni story za eddy .dorice,Doreen na nk..maonii yangu lakiniiiiii ...tunasubiria season 2
 
Mkuu Gregoire's hii ni true story? kavipi anzisha uzi wako tofauti tutaifuatilia hukohuko
 
Nitashukuru kama ungeanzisha thread tofauti mkuu
 
Riwaya: MWANAFUNZI MCHAWI

(MSIMU WA 2)

MTUNZI:ENEA FAIDY


SEHEMU YA KWANZA.


Watu wengi nchini Tanzania walikuwa wametulia tuli kutazama runinga zao majira ya Saa moja kamili jioni. Kwani kipindi kizuri chenye simulizi ya kweli na ya kusisimua kutoka


. kwa Doreen Mbwana kilikuwa kikiendelea katika kituo kimoja cha televisheni maarufu sana nchini kilikuwa kinarusha matangazo yake mubashara kutoka hospitali aliyokuwa amelazwa Doreen.

Wanafunzi wa shule ya Mabango ambao walikuwa wamefunga shule siku ile ya Ijumaa walikuwa bwaloni wakitazama televisheni kwani hawakuruhusiwa kuondoka kwa siku ile na utaratibu wao ilibidi waondoke Siku ya kesho yake . kwa hivyo walokuwa na Uhuru wa kutazama televisheni kadri wawezavyo.

Maandishi makubwa yaliyokolezwa kwa wino wa bluu yalipita chini ya kioo cha televisheni na yakazidi kuwatia hamasa wanafunzi wale ili waweze kutazama kwa umakini kipindi kile."KAA TAYARI KWA KIPINDI MAALUMU KUTOKA KWA DOREEN MBWANA AKIELEZEA CHANZO CHA YEYE KUWA MCHAWI"

Tangazo hilo lilikuwa na nguvu ya kuwavuta watazamaji wengi na kutulia kama maji ya mtungini ili waweze kusikia vizuri na kwa umakini mkubwa.


Umakini huo haukuwa kwa wanafunzi na walimu wa Mabango pekee bali ni nchi nzima. Familia ya akina Pamela ilikuwa imetulia tuli na kwa mshangao wa hali ya juu wakisubiri kusikia kitu kutoka kwa Doreen.

Pia Mwalimu John na familia yake hawakuacha kukodoa macho yao kwa umakini sana ili wasipitwe na neno lolote kutoka kwa Doreen Mbwana.


Haukupita muda mrefu sana picha ya Doreen ilitanda kioo kizima cha televisheni na alikuwa tayari kuanza kipindi huku machozi yakimbubujika kwa kasi mashavuni mwake lakini akaamua kujikaza kisabuni kwa kujifuta machozi Ili aweze kuzungumza vizuri na kusikika kwa watazamaji wake.

Kamera ilienda moja kwa moja kwenye majeraha makubwa ya Doreen yaliyositiriwa kwa bandeji kisha ikauweka sawa USO mzuri wa Doreen ambao ulichakazwa kwa kilio cha muda mrefu pamoja na vipigo. Muda wa Doreen kujieleza yw moyoni ukawadia akakohoa kidogo kisha akaanza kuuambia umma kile alichokusudia kukisema.


"Ni aibu kubwa sana kwa binti mdogo kama Mimi Doreen, kupata tuhuma za uchawi tena si kidogo Bali kwa kuangamiza watu wengi sana wasiokuwa na hatia na kuwaharibu binadamu ambao hawakunikosea kitu. Nakiri kuwa na makosa makubwa sana tena nakiri kuwa Mimi ni zaidi ya mnyama wala sistahili adhabu yoyote zaidi ya kifo... Roho yangu inanisuta sana ndio maana nimeamua kutangaza hili ili walau nijipunguzie mzigo mzito nilioubeba.. Najuta sana! Naomba radhi kwa Mola wangu pia kwa wote niliowakosea" alisikika Doreen kwa sauti iliyojaa uchungu na simanzi akijutia kile alichokifanya kwa muda mrefu.

"Nitasimulia maisha yangu kwa ujumla... Nanyi mtakuwa hakimu na kunihukumu kadri ya vile ninavyostahili... Mengi sikuyajua ila nilisimuliwa na mama yangu Bi Hamisa Hamis... Kwa namna moja au nyingine naweza sema namchukia sana mama! Najuta ni kwanini alinizaa!" Alisema Doreen kauli hiyo tata iliyowaacha watu wengi midomo wazi na kumwona Doreen kama binti asiye na adabu hata kidogo! Kwanini atamke wazi kuwa hampendi mama yake wakati alimbeba tumboni kwa takribani miezi Tisa? Tena akamlea kwa mapenzi mazito hatimaye akawa binti mkubwa tena mzuri kupita kiasi?

Doreen alishusha chozi lake kisha akaanza simulizi yake ya kusisimua sana.


******

Kumbukumbu zikarudi nyuma sana mpaka miaka 20 iliyopita kama ambavyo Doreen alisimuliwa na mama yake.


Katika wilaya ya Pangani mkoani Tanga ndiko alikokuwa akiishi Bi Hamisa Hamisi ambapo alitokea katika familia duni sana ya Bwana Hamisi Mandevu. Binti Huyo aliyekuwa na uzuri wa aina yake alipata bahati ya kuolewa na mfanyabuashara maarufu sana mkoani humo aliyefahamika kwa jina la Adrian Mbwana. Kiukweli ilikuwa bahati kubwa sana kwa Hamisa kwani mumewe angekuwa chanzo cha kuiinua familia yake kiuchumi.


Licha ya kwamba Bwana Adrian Mbwana alikuwa na dini tofauti na Hamisa Hilo halikuwa tatizo kabisa kwani mapenzi mazito yaliyochipua haina yao yalikuwa na nguvu tosha ya kuzivunja tofauti zao za kidini.

Licha ya kwamba Bwana Hamis Mandevu alijaribu sana kuzuia ndoa ile lakini ilishindikana. Hamisa na Alitokea kumpenda sana Adrian Mbwana hivyo akajiomba radhi mwenyewe na akamwomba radhi mola wake kwa kuvunja taratibu za kidini.

"Kwa ninavyompenda Adrian. Sina jinsi kama ni kutengwa na familia basi sio shida ili mradi tu nafsi yangu iridhike.. Kwanza Adrian ni mzuri sana pili ana pesa nyingi sana zitakazotosha kubadilisha maisha yangu...!" Aliwaza Hamisa kisha akatabasamu.


Kwa kuwa Hamisa aliridhia kuwa Bwana Adrian hivyo akaolewa naye na akakubali kuifuata dini ya mumewe bila kinyongo kwani siku zote Mapenzi yakisema ndio hakuna anayeweza kupinga. Mapenzi yana nguvu kuliko sumu Kali inayoweza kuua, mapenzi yana nguvu kuliko kimbunga kinachoweza kuharibu makazi ya watu. Ni mapenzi hayohayo yaliyomfanya Hamisa kujitenga na ndugu zake na kuishi na Adrian.


Maisha ya ndoa kati ya Hamisa na Adrian yaliendelea kuwa ya amani na furaha. Na baada ta kuishi miezi mitatu Hamisa aliamua kurudi kwa wazazi wake ili kuwaomba msamaha kwani aligundua alikosea sana.

"Nikupe nini mke wangu mpenzi uende kwa wazazi?" Aliuliza Bwana Adrian.

"Nipe pesa ninunue zawadi ambazo zitawafaa..." Alisema Hamisa.

"Hakuna tatizo mke wangu.. Nakupenda sana" alisema Adrian na kumpa pesa kiasi mkewe ili afanye manunuzi ya zawadi na kuwaomba radhi wazazi wake.


Kesho yake Hamisa alivaa gauni refu pamoja na ushungi uliomsitiri vyema kisha akafunga safari kwenda nyumbani kwao. Aliongozana na dereva wake ambapo walifika mapema sana nyumbani kwao.

Hamisa alijawa na woga sana, alitembea taratibu sana mpaka alipochukua uamuzi wa kugonga mlango wa ndani. Hakuna aliyeitikia hodi yake ndipo Bwana Mandevu alipotokea nyuma akiwa ameshika mifuko michafu ya mkaa, Hamisa alitambua moja kwa moja kuwa baba yake alikuwa kwenye biashara zake za kuuza mkaa.

"Shkamoo baba" alisalimia Hamisa kwa woga kidogo. Bwana Mandevu alimtazama Hamisa bila kujibu salamu yake.

"Umefata nini hapa?" "Nimekuja kuomba radhi baba... Naomba tuingie ndani ili tuzungumze" alisema Hamisa.

"Wewe si una jeuri? Ondoka hapa kwangu... Sitaki uniabishe kama ulivyonitia aibu" alisema Mandevu kwa hasira. Hamisa aliamua kupiga magoti na kuzidi kumwomba radhi baba yake lakini Mzee Mandevu hakumwelewa kiurahisi.

"Baba unakumbuka kama ulinikubalia siku nilipokuambia nimepata mchumba?"

"Nilikubali kabla sijajua dini yake... Nilidhani ni mwenzetu katika imani kumbe sivyo... "

"Naomba basi nikuambie kitu"

"Kitu gani?"

"Mume wangu amebadili dini na amekuwa kwenye dini yetu... " alidanganya Hamisa ili kumshusha hasira baba yake.

"Unachosema ni kweli?" Aliuliza Mandevu akiwa amepunguza jazba kidogo.

"Ndio baba... Na tumefunga ndoa upya kabisa!"

"Hayo ndio maneno... Haya karibu ndani..." Alisema Bwana Mandevu baada ya kumuamini haraka binti yake. Waliingia ndani na kuketi vitini.


"Mama yupo wapi?"

"Alienda sokoni atarudi sasa hivi.." Alisema Bwana Mandevu kisha wakaendelea na mazungumzo mengine. Punde Mama Hamisa aliwasili nyumbani pale. Kwanza alishtuka kukuta gari imepaki nje ya nyumba yake akajiuliza sana.

"Gari hii imetoka wapi?" Kwani kwa kipindi kile magari yalimilikiwa na watu wachache sana wenye pesa nyingi.

Mama Hamisa akaishia kuguna tu Kisha akaingia ndani kwake na kustaajabu alichokikuta kwani hakutaraji kama Hamisa angekuwa ndani ya nyumba ile.

"Hamisa!" Aliita kwa mshangao mama Hamisa.

"Abee mama... Asalam aleykum!" Aliitika Hamisa huku akitabasamu.

"Walleykum Salam! Umefika muda gani mwanangu mie!" Alisema Mama Hamisa huku akienda mbio kumkumbatia mwanae.

"Nilikukumbuka mno... Kila siku nilimwomba baba yako akusamehe tu" alisema mama Hamisa huku akiwa amemkumbatia mwanaye kwa furaha sana. Walikumbatiana kwa dakika kadhaa kisha

Wakaachiana na wote wakaketi.

"Ile pale ni gari yako?"

"Ndio mama alinipa mume wangu.."

"Kuna MTU nimemwona kwa mbali kwenye ile gari ni nani"

"Ni dereva wangu nilimwacha ili asijue naongea nini na wazee wangu.." Alisema Hamisa huku tabasamu mwanana likiupamba uso wake.

"Mh mume wako ni tajiri sana eeh?"

"Kidogo tu.."

"Si kidogo... Mpaka amekupa gari?"

"Mke wangu... Mwanetu ameleta taarifa nzuri" alisema Mandevu huku akitabasamu.

"Zipi hizo?"

"Mumewe amekubali kubadili dini na wamefunga ndoa ya kidini"

"Ya kweli hayo?"

"Ndio mama" alijibu Hamisa.

Kiukweli jambo lile liliwafurahisha sana na kuwafanya wawe na matumaini mapya ya kukomboa familia yao. Licha ya kwamba jambo lile halikuwa na ukweli wowote lakini lilibaki kuwa siri ya Hamisa pekee.

Mama Hamisa aliandaa chakula wote wakala wakafurahi. Na kwa muda huo dereva aliitwa ndani na wakashiriki chakula kwa pamoja.

Hamisa aliwakabidhi wazazi wake zawadi alizowaletea na wakafurahi sana.


Baada ya chakula Mama Hamisa alimwita binti yake kwenye chumba kimojawapo ndani ya nyumba yao ile iliyochoka sana na kuonekana duni mno.


Baada ya Hamisa kuingia kwenye chumba kile chenye Giza kiasi, mama Hamisa akafunga mlango na kabla ya kuufunga alitazama huku na kule akahakikisha hakuna mtu aliye jirani.

"Hamisa mwanangu nilikasirika sana ulivokuwa mbali na Mimi... Nilitumia kila mbinu ili baba yako akusamehe ili wewe usiwe na kikwazo cha kuja hapa!" Alisema Mama Hamisa kwa sauti ya chini sana.

"Leo nimefurahi sana umekuja na sitokubali uondoke kabla hujakubali kufanikisha suala langu." Alisema Mama Hamisa kwa sauti ndogo.

"Kufanikisha suala lipi?" Aliongea Hamisa kwa sauti kidogo kuzidi ile aliyotumia mama yake.

"Ssh! Ongea taratibu kwani hii ni siri yangu Mimi na wewe! Baba yako hajui lolote"

"Sikuelewi..."

"Huelewi nini malaika wangu? Mbona tulishawahi zungumza kwani umesahau..?"

"Sikumbuki..."

"Usijali nitakukumbusha tu...." Alisema Mama Hamisa na kuinuka pale alipokuwa amekaa. Hamisa alikuwa na maswali mengi mno juu ya maneno ya mama yake ila hakuwa na haraka akasubiri kukumbushwa.


Mama Hamisa alisogea karibu na kona moja kisha akachimbua chini kwani nyumba ile ilikuwa haijasakafiwa hivyo kulikuwa na vumbi tu. Alipomaliza kuchimba pale chini akatoa kitu Fulani na kumsogelea Hamisa.

"Hamisa!"

"Nini hicho mama?" Hamisa alishtuka sana.


..................................

Itaendelea
 
Reactions: Lee


Riwaya:MWANAFUNZI MCHAWI (-2) MTUNZI:ENEA FAIDY SEHEMU YA 2 ....Hamisa alimshangaa mama yake huku akimtazama kwa woga. Mama Hamisa aliachia
tabasamu mwanana na kumtazama binti yake kisha kwa sauti ya upole sana akamnong'oneza. "Chukua ule mwanangu..ni zawadi yako." "Mmh! Mama!" Alisema Hamisa huku akisitasita kupokea zawadi ile anayopewa na mama yake. Kila alipojaribu kuinua mkono wake ukawa mzito kupokea akabaki ameduwaa tu huku akimtazama mama yake aliyejawa na tabasamu. Kutokana na giza lililokuwamo ndani mle Hamisa alishindwa kuona vizuri kitu alichopewa. "Hamisa! Kwasababu umeolewa na mume tajiri ndio chanzo cha kunidharau Mimi? Kumbuka Mimi ni mama yako... " alisema kwa sauti iliyoonesha kutopendezwa na tabia ya Hamisa. Na kutokana na upendo pamoja na adabu aliyokuwa nayo Hamisa katu hakutamani kumkwaza mama yake wala kumfanya ajisikie vibaya kwaajili yake. Ili kumridhisha mama yake Hamisa aliamua kupokea zawadi kutoka kwa mama yake kipenzi. "Aah kumbe ni apple!" Alisema Hamisa kwa mshangao huku akitabasamu na kupokea tufaha lile kubwa lililokomaa vizuri na kufanya rangi nyekundu ionekane vizuri kuliko kijani. "Sasa ulifikiri ni nini? Ni apple kwaajili yako mwanangu kipenzi" alisema mama Hamisa kwa furaha huku akihakikisha sauti yake haivuki nje ya chumba kile walichokuamo. "Sasa mbona ulilihifadhi chini ? Kwanini usiweke kwenye chombo kisafi?" Aliuliza Hamisa. "Utanikera na maswali yako.. Hebu kula haraka tutoke huku!" Alisema mama Hamisa kwa sauti ya ukali kidogo kwani aliufahamu vizuri utii wa binti yake hivyo akajua hatoendelea kudadisi zaidi. "Halijaoshwa mama.. Nitakula vipi?" Aliuliza Hamisa huku akikunja USO kwa kinyaa cha kula tunda chafu. "Kula hivyo hivyo binti yangu...jitahidi wala hakuna madhara yoyote!" Alisema mama Hamisa. Hamisa aliamua kumsikiliza mama yake na kula tufaha lile bila kuoshwa. Cha ajabu na cha kushangaza tunda lile lilikuwa tamu kupita kawaida hivyo likamhamasisha binti yule mrembo kula haraka haraka mpaka alipomaliza. Mara tu alipomaliza alihisi uchungu sana mdomoni mwake, uchungu ule ulikuwa zaidi ya Pilipili kichaa. Hamisa akabadilika uso akatamani kulia kwani alishindwa kuvumilia uchungu ule akataka kutema mate chini. Ghafla mama yake akamshika kinywa chake. "Usiteme mate hayo! Meza!" Alisema mama Hamisa. Ghafla sauti ya Mr Mandevu ikasikika ikiita kwa nguvu. "Mama Hamisa!" Lakini mama Hamisa hakutaka kuitikia akabaki kimya tu. "Mbona huitiki?" "Sitaki baba yako ajue nipo huku... Na usithubutu kumwambia chochote kuhusu tulichofanya sawa?" "Kwanini?" "Ni siri yetu.. Mimi na wewe na ukimwambia mtu mwingine yeyote utakuwa umeharibu kila kitu.." "Mbona sikuelewi mama... Apple lina tatizo gani" "Hahaha.. Ipo siku utafahamu. .. Vipi uchungu umeisha?" "Ndio ila kuna ukakasi kidogo.." "Usijali utaisha tu.. Ila nashukuru sana mwanangu umenitoa aibu..." Alisema mama Hamisa na kumfanya Mwanae abaki njia panda kwani kauli zile zilikuwa na utata sana kwake. Akajiuliza sana iweje tufaha lile Liwe na masharti mengi kiasi kile? Pia kwanini mama yake aseme limemtoa aibu wakati ni tunda la kawaida tu? Hamisa hakuwa jibu wala hakutaka kuuliza zaidi kwani mama yake alimwambia watoke chumbani mle haraka sana. Baada ya kutoka kwenye chumba kile walifika sebuleni na kuketi kama kawaida. Mandevu akamtazama binti yake ns kutaka kumuuliza jambo lakini ghafla akasita na kumuuliza jambo lingine mbali na alilokusudiwa. "We Hamisa kulikoni? Mbona upo hivyo?" Aliuliza. Hamisa akashtuka kidogo. "Nipo vipi?" "Mbona macho mekundu.. Halafu mdomoni kwako kuna damu?" Aliuliza Mandevu kwa mshangao. Hamisa alishtuka sana, lakini ghafla mama yake akamjibia maswali Yale. "Alijigongesha hapo nje... Kama umjuavyo mwanao kwa woga .. Si akaanza kulia" alisema Mama Hamisa kisha akamsogelea na kumfutafuta binti yake. "Mh! Inaonekana umeumia sana..!" Alisema Mandevu. "Ndio... Ila sasa hivi sina maumivu sana" "Oh! Pole..nataka mumeo aje huku ili tufahamiane zaidi maana ilikuwa kama ugomvi wala hatujawahi kukaa naye karibu hatujaongea chochote..!" "Sawa baba atakuja" alisema Hamisa. *** Hamisa alirudi kwa mumewe akiwa na furaha tele moyoni mwake kwani kupokelewa na wazazi lilikuwa Jambo jema sana kwake. Alimsimulia kila kitu mumewe na jinsi alivyowadanganya wazazi wake kuhusu dini ya mumewe. Lakini kwa suala hill Adrian alionekana kutokubaliana kabisa na mkewe. "Siwezi kukataa dini yangu.." Alisema Adrian. "Tafadhali mume wangu... Nakupenda sana, sitaki ndoa yetu iharibike kwaajili ya jambo hilo... Simaanishi kuwa utabadili dini ila cha msingi tu tuwaridhishe wazazi wangu... Nakuomba sana!" Alisisitiza kwa sauti ya kubembembeleza sana. Na kutokana ufundi wa kubembeleza aliojaaliwa Hamisa aliweza kumshawishi mumewe mpaka akakubali na wakapanga siku ya kwenda kuwatembelea wazazi wa Hamisa. Hamisa alizidi kuwa na furaha ingawa kuna jambo moja tu lilizidi kumtatiza na mara zote akifikiria basi amani yake ilipotea ghafla. Siku moja akiwa amekaa sebuleni akiwa peke yake ghafla akasikia kelele nyingi za vyombo jikoni kwake. Hamisa akainuka haraka na kwenda jikoni kutazams kilichokuwa kinaendelea. Na kadri alivyokuwa akisogelea ndivyo kadri alivyosikia vyombo vikianguka sakafuni na kuvunjika. Hamisa aliogopa sana. Akaingia jikoni na kutazama kabati la vyombo lakini cha kushangaza hakukuwa na chombo chochote kilichoanguka wala kuvunjika. Hamisa alipigwa na butwaa akaishia kushangaa tu kisha akarudi tena sebuleni. Aliporudi sebuleni Hamisa alishtuka tena baada ya kukuta vitambaa vyote alivyotandika kwenye sofa vipo chini, akakumbuka pindi anatoka aliacha vitambaa vyote vikiwa sehemu yake. Hamisa akapigwa bumbuwazi, akashangaa kwa muda kisha akajipa moyo kuwa labda upepo ulipiga kwa nguvu na kuangusha vitambaa. Hamisa akainama chini na kuokota vitambaa vyote na kuvirudisha sehemu yake. Hamisa akakaa tena kwenye kochi huku akiwa na mawazo tele kichwani mwake juu ya kile kilichotokea ndani ya nyumba yake. Akiwa katika mawazo hayo mazito ghafla usingizi ukamvamia na kumteka kwa mbwembwe nyingi. Hamisa hakuwa na ujanja ilibidi atii amri na kukubali usingizi umwendeshe kadri awezavyo. Mumewe akiwa ameambatana na mwanamke mmoja aliyevalia nguo nyeusi waliingia ndani na kufika sebuleni pale wakiwa wameshika visu huku wakimnyooshea Hamisa kifuani kwake. "Kumbe hunijui ee! Mimi ndo Adrian Mbwana... Naitaka roho yako haraka sana!" Ilisikika sauti ya Adrian akiongea kwa ukali sana. Hakuwa Adrian yule mpole, mnyenyekevu na mwenye mapenzi mazito ila alikuwa kama mnyama wa pori asiyejali uhai wa mtu. "Kaka usichelewe bwana.. Mchome kisu namimi namalizia" ilikuwa sauti Kali ya Dada yake Adrian akiwa hana hata chembe ya huruma. Adrian akakitazama kisu kile kirefu, chenye mng'ao wa shaba na kilichongoka vyema kwenye ncha ya mwisho ambayo ilimwelekea Hamisa. Adrian alikunja sura kikatili kisha akakibusu kisu kile na kukiinua kwa ghadhabu ili atue kifuani kwa Hamisa huku akiachia sonyo Kali ya dharau. Kabla kisu kile hakijamfikia Hamisa, Hamisa alishtuka sana usingizini huku akihema kwa nguvu sana. "Adriiiiiaaaaan!" Aliita kwa nguvu bila kutarajia lakini hakukuwa na mtu yeyote ndani ya nyumba ile zaidi yake yeye mwenyewe. Hamisa aliona kitini ni parefu sana akaamua kushuka na kukaa sakafuni huku akihema kwa nguvu. Woga ulimshika sana, akaangaza macho huku na kule Ili kutazama kama ndoto ile ina ukweli lakini bado hakuona chochote ndani ya nyumba ile wala hakukuwa na mtu mwingine yeyote. "Hii ndoto ina maana gani?" Alijiuliza Hamisa kisha akaanza kuunganisha matukio yote ya siku ile. Akakumbuka tukio la vyombo na vitambaa kisha akaunganisha na ndoto ile. "Niliambiwa Adrian ni mchawi... Anatumia uchawi katika biashara zake ili ziende vizuri..... Yawezekana kuna ukweli... Isije ikawa anapanga kuniua!" Aliwaza Hamisa huku kijasho chembamba kikimtoka kwa kasi sana usoni kwake. Aliwaza sana bila kupata majibu akiwa bado amekaa pale chini. Zilipita takribani dakika arobaini na Tano Hamisa akiwa katika dimbwi zito la mawazo. Ghafla akazinduliwa mawazoni na sauti ya mlango ukiwa unagongwa. Hamisa alishtuka, bado akasikia mlango ukigongwa. Taratibu alinyanyuka pale chini na kwenda kutazama nani alikuwa mgeni wake kwani hakuwa na wazo kama mumewe angerudi wakati ule kwani kikawaida mumewe alitoka kazini SAA moja jioni na akichelewa basi saa mbili. Na kwa muda ule ilikuwa ni saa Tisa alasiri. Hamisa alifungua mlango, alishtuka sana kuona mumewe akiwa ameambatana na mwanamke yuleyule aliyemuota. Tena wakiwa na mavazi yale Yale ya ndotoni. Mumewe alivalia Suti nyeusi, shati jeupe na tai nyekundu, mwanamke yule alivalia gauni refu jeusi na viatu vyeusi na alikuwa amejitanda mtandio mweusi. Moyo wa Hamisa ukampasuka paah! Akashinda hata kumkubatia mumewe kama ilivyokuwa kawaida yake! Kwani Siku zote Hamisa alimpokea mumewe kwa kumbatio zito la mahaba huku mabusu kama mvua yakimpoza uchovu bwana Adrian bila kujali aliambatana na nani lakini Siku hiyo hali ilikuwa tofauti sana.................................... JE NINI KITAENDELEA? USIKOSE KUFUATILIA.
 

Hatar sana
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…