Simulizi: Equatorial forest (msitu wa Equatorial)

Simulizi: Equatorial forest (msitu wa Equatorial)

bioto

JF-Expert Member
Joined
Oct 1, 2017
Posts
1,261
Reaction score
2,099
SIMULIZI: EQUATORIAL FOREST (msitu wa
Equatorial)
MTUNZI: AISHA KHAN
SEHEMU YA 01
UTANGULIZI: kwa Jina naitwa Najma Abdallah, Nina
umri wa miaka 22 na soma university mwaka wa
pili sasa, wazazi wangu wote wapo hai ila baba
yangu mzazi alifungwa jela sasa ni mwaka mmoja
kwa kesi ya uchochezi wa wana nchi ili waweze
kuleta mgomo selekalini kuwa mshahara waliopewa
ulikuwa mdogo.
Nakumbuka siku hio baba na wafanyakazi wenzie
(walikuwa ni wajenzi) hivo walipata tenda kutoka
kwa mkuu wa mkoa ili waweze kujenga shule za
wanafunzi wa primary, baba na wenzie tenda hio
waliichukuwa kwa mikono miwili Baada ya
kukubaliana kipato kizuri, walipomaliza mkuu wa
mkoa na ma supervisor waliokuwa wakiwasimamia
takribani wa nne waliwapa pesa ndogo sana kama
asilimia arobaini kwa ile waliokuwa wamekubaliana
hali ya kuwa selekali ilitoa pesa ya kutosha, kitendo
cha kupewa pesa ndogo kiliwafanya wachukie na
kudai pesa yao, siku moja baba na wenzie ishirini
Walikubaliana waende kwa viongozi wa Juu
wakaombe msaada ikiwezekana wawawekee hata
asilimia kumi Juu zingine wakaushie ila kila
waliekuwa wakimlilia aliwapotezea kama vile
wanamsumbua, waliamua wachukuwe uamzi wa
kwenda kituoni kulipotia swala lile ajabu mkuu wa
mkoa aliwazunguka wote wakawekwa Chini ya ulinzi
kwa kesi ya kuleta vurugu nchini, hivo Walikaa siku
nne sero.
Siku hio ya nne supervisor mmoja aliwafuata sero
akawaambia wapotezee ile kesi Ila baba akazidi
kuwapa moyo wenzie waendelee kutetea haki yao
Ipo siku mheshimiwa Raisi litamfikia Jambo hilo na
atawachukulia hatua, mwishowe baba alichezewa
mchezo wenzie wakamzunguka Baada ya kupewa
pesa ndogo wakampachika kesi kuwa Yeye ndie
alikuwa anawachochea waje kuleta vurugu selekalini
ili kuwachafulia Jina hali ya kuwa pesa walipewa
zakutosha hivo kesi Ilikuwa kubwa tena kubwa Mara
dufu, kila Tukienda Mimi na mama yangu kuuliza
tulikuwa tukiambiwa kesi imeshikiliwa mahakamani.
*******************************************
Mama yangu Umu-kulsum toka baba aingie jela
alipatwa na ugonjwa wa presha kutokana kutulea
Mimi na mdogo wangu Latina ilikuwa kazi kubwa
kwake ukija kuangalia sote tulikuwa Wa kubwa na
tulikuwa sote tunasoma university Mimi mwaka wa
pili mdogo wangu Latina mwaka wa kwanza na
pesa yote ya Ada ya chuo ulikuwa ni mkopo baba
aliouchukuwa selekalini akiamini angelipa taratibu
taratibu ila majanga ndo hayo mwaka sasa yupo
jela, hilo ndilo lilizidi kumchanganya mama licha
kila siku tulikuwa tukimpa moyo asijali tupo kwa
ajili yake tukimaliza chuo tukapata kazi nzuri
tutamsaidia baba na tutalipa madeni yote
tunayodaiwa.
SONGA NAYO!
Asubuhi mapema ya tarehe 2 may mwaka 2019
Mimi Latina Pamoja na mama yetu tulijiandaa
tukaelekea mahakamani iliopo dar es salam Maana
Sisi makazi yetu yalikuwa dar es salam maeneo ya
kijitonyama, tulipofika mahakamani kesi za watu
wengine zilisomewa mwishowe baba akaletwa
kizimbani ili kusomewa hukumu yake, aisee
nilipomuona baba yangu anahofu nyingi na sio
Kawaida yake machozi yaliyatawala macho yangu
Nikajilazimisha kumpa moyo huku nikitabasamu,
baba alipoiona familia yake imekuja kumpa moyo
alifurahi moyoni huku akiendelea kututazama, kesi
yake haikuwa na wakili hivo alikatiwa kifungo cha
miaka mi tano au faini ya milioni tano, mama
aliposkia hivo nguvu zilimuishia akalegea huku
akipumua vibaya, Tulianza kumpepea huku tukilia
Pamoja na wasamalia wema waliokuwa hapo,
kitendo kile kilimfanya baba aanze kumuita mama
kwa uchungu: Umu Umu Umu mke wangu !!!
Mapolisi walimchukuwa baba na kumrudisha jela,
Baada ya lisaa limoja kupita tulikuwa tupo njiani
tunarudi nyumbani huku mama akionekana vizuri
tofauti na Muda uliopita.
Tulipofika nyumbani Nilimpa moyo mama asiwaze
Sana milioni tano sio pesa nyingi atatoka jela muda
sio mrefu.
Siku hio ilipita kila mtu Hana raha, siku moja
Baadae niliporudi nyumbani Baada ya kutoka shule
Latina kwa presha aliniambia: mama hali yake sio
nzuri.
Nikashangaa na kumuuliza: Kulikoni?
Latina: ndio toka asubuhi anaongea maneno ya
ajabu ajabu hata simwelewi.
Nikamuuliza: anaongeaje?
Latina: Njoo umuone mwenyewe.
Tuliingia ndani nikamkuta mama akiwa amekaa
sebuleni huku akivuta vuta uzi taratibu uliopo
kwenye nguo aliokuwa amevaa, nilikaa pembeni
yake na kumuuliza: mama nini shida?
Mama hata hakuniangalia aliendelea kufanya
alichokuwa Anafanya ndipo Nikamuuliza tena:
unafanya nini mama???
Mama alikurupuka na kunisukuma kisha akasema
kwa sauti ya Juu: Mume wangu yupo wapi???
Mimi na Latina Tulimshangaa ndipo mama akatoka
nje anakimbia huku akipiga kelele, Tulitoka hapo
tukamfuata haraka ila kwa mbio alizokuwa nazo
Alituacha mbali, siku nzima iliisha tukiwa
tunamtafuta ila hatukuweza kumuona.
Majira ya jioni tukiwa tupo njiani Mimi na Latina
mwenye umri wa miaka 20 njia nzima tulikuwa
tunalia bila kujuwa wapi tutamuona mama, tukiwa
tunazidi kulanda Landa mtaani mdada jilani yetu
alitusimamisha na kusema: mnisubiri Kidogo.
Tulisimama ndipo akatufikia na kusema: mama
yenu nimemuona kule Chini ya barabara kuelekea
Ilala.
Tuliposkia hivo tulimuomba atusaidie atupeleke
huko nae hakuwa mgumu kwetu alitupeleka huku
tukikimbia Sana, tulipofika maeneo aliotuambia
alisema: ndo Yuleeee..
Tulimuona mama kwa mbali alikuwa ametugeuzia
mgongo huku akiwa amekaa Chini kama vile kuna
kitu anachambua, muonekano wa mama ulinifanya
niangue kilio kikali ndipo mdada Yule akanipa moyo
nisijali Allah yupo Pamoja na Sisi, mdada Yule
Alituacha hapo akaenda nyumbani maana muda
ulikuwa umeenda, tulimaliza kama dakika kumi
tukiwa tunamtazama kwa mbali ndipo Latina
akaniambia: tukimfuata akatuona wallah
hatutampata tena Sasa sijui tunafanya nini.
Nikamjibu: Kikubwa tunamuona, Ngoja mi niende
kumuona Yule Doctor Rafiki yake baba nikamuambia
ikiwezekana aje kutusaidia.
Tulikubaliana hivo Mimi nikaenda kumtafuta mzee
huyo, Baada ya muda tulikuja nae akiwa
ameongozana na Manesi wengine wanaohusika
kuwalinda Wagonjwa wa hakili, tulipofika
walimsogelea taratibu ile kuwaona tu alishtuka Ila
walikuwa tayari wamemchoma sindano ya
kumpunguza nguvu mwilini.
Tukiwa tupo hospital doctor aliniambia: mama yako
amepata mshtuko mkubwa Ila hili ni tatizo dogo
mambo yatakuwa vizuri.
Siku hio ilipita mama alihifadhiwa hospitalini nasi
tukarudi nyumbani.
Baada ya siku nne kupita bila kwenda chuo
kutokana na Matatizo ya familia, siku hio tulikuwa
tumekaa sebuleni Mimi na mdogo wangu ndipo
Latina akaniambia: dada pesa ni ndefu Sana sasa
Kama sindano moja ni Elfu stini hio gharama
tutaiweza kweli?
Nikamjibu: kesho twende chuo mambo mengine
tutayajuwa Baadae.
Latina: tunaendaje chuo na Hali ya familia Ipo hivi?
Nikamjibu: shule tuliifanya mkombozi Wa familia
yetu Acha tusome baba Ndo anavyotaka
ikiwezekana nikahitimu mambo yote yatakuwa sawa
Najuwa baba nikimtoa jela Halafu mama akamuona
basi atapona na familia yetu itarudi kwenye furaha
kama mwanzo.
Latina: sawa.
Siku iliofuata tulielekea chuo, kizuri sote tulikuwa
tunasomea science hivo chuo kilikuwa kimoja
tulipofika tulishangaa kukuta maandalizi sio ya
Kawaida mpaka tukashindwa kuelewa ndipo mdada
Rafiki yangu Jina lake Joyce alikuja tulipokuwa
tumesimama na kusema: come on Najma mbona
hivo?
Nilitabasamu na kumjibu: Kwani nipoje?
Joyce: Jana nakupigia haupokei simu why?
Nikamjibu: mama yangu amechanganyikiwa Baada
ya hukumu ya baba Ndo maana siku hizi sifiki chuo.
Joyce: Oohh my God pole Sana my dear.
Nikamuuliza: kuna nini mbona Mishe Mishe Sana?
Joyce: my dear hapa tuna ugeni mkubwa Si
unamjuwa Yule specialist mkubwa hapa Tanzania
kwa maswala ya upasuwaji wa moyo! atakuja
kutembelea chuo chetu Leo na atatoa somo kwa
masaa ma wili Baada ya hapo anaenda England
aisee Najma yaani sio Mimi ntaona Nimeiona sura
yake naskia watu wanamsifia ni kijana mdogo
mdogo tena handsome.
Nikamjibu: tatizo you talk to much.
Joyce alicheka kisha akaondoka zake kwa maringo,
Latina aligeuka kuniuliza: mbona hukutaka
kumsikiliza?
Nikamjibu: Nina raha gani?
Latina: Ila huyo specialist wa masuala ya upasuwaji
wa moyo unamjuwa? maana nahisi atakuwa peke
yake hapa Tanzania nzima kama atakuwa mbongo.
Nikamjibu: Anaitwa Derick ni mwana science
mkubwa alisomea wingereza anauwezo mkubwa
Sana na nitegemezi nchi nyingi za Africa mpaka ma
ulaya.
Latina alishtuka na kuniuliza: ulijuwaje?
Nilimpita huku nikimjibu: niliambiwa na teacher.
Latina alitabasamu kisha akanifuata kwa nyuma.
Baada ya muda tulijipanga freshi baadhi ya
wanafunzi walisimama mkono wa kushoto Wengine
mkono wa kulia katikati kuelekea ofisini kwa
mwalimu mkuu walitandika red-carpet Chini ili ugeni
Huo mkubwa tuuoneshe kuwa tunaujali sana, nikiwa
nimesimama mawazo yalienda mbali
nikamkumbuka mama hali alionayo nikajikuta
nakosa furaha kwa dakika mbili, Latina akiwa
amesimama upande wa pili aliponiona Nimeingia
kwenye emotion mbaya alinipa moyo kwa
kunionesha dole gumba ndipo nikatabasamu na
kumrudishia dole gumba, muda Huo kwa mbali
tuliona gari za kifahari kama tatu, watu macho
yaliwatoka wakitamani kujuwa Nani anaekuja Ila
Mimi sikuwa na habari nao.
Gari Zile zilipakiwa sehemu maalumu kisha
wakatoka vijana wawili na Wazee wa nne, walipofika
pale red-carpet inapoanzia walitabasamu kwa furaha
kisha wakaanza kupiga hatua huku wakisalimia
mwanafunzi kwa mwingine kupitia mikono,
wanafunzi walipomuona Derick walitamani Sana
kumuuliza maswali mengi kuhusu science ila muda
ulikuwa bado, mdogo wangu Latina alipomuona
Derick alijawa na tabasamu isio ya Kawaida ila
Mimi hata kupoteza muda eti nipo nawatazama
wala.
Derick kila mwanamke Aliekuwa akimpa mkono
alionekana kushoboka Haina mfano, Derick alipofika
mbele yangu na kuiona sura yangu alishtuka Ila
Mimi nilijifanya kumpotezea ndipo akanipa mkono,
Nilimpa bila kujali ndipo akaushika mkono wangu
kwa dakika mbili huku akinitazama usoni Mpaka
kila mtu hapo akashangaa kwa kile kinachoendelea,
aibu ilinitawala nikaamua kujikohowesha ili aniachie,
ndipo akaniachia na kuendelea bila hata
kuwasalimia wanafunzi waliokuwa wamebaki maana
alionekana kuchanganyikiwa baada ya kuniona,
Baada ya muda Wageni wakiwa wapo ofisini kwa
mwalimu mkuu Latina alinifuata na kuniuliza: hivi ni
wewe Wa Muda ule?
Muda Huo alifika Joyce na kuniuliza: Najma it's
you?
Niliwapotezea nikaamua kuondoka zangu.
Baada ya muda somo ilianza na Aliekuwa
akiendesha somo alikuwa ni Derick, wana science
wote kuanzia mwaka wa kwanza kuendelea tulikuwa
kwenye class moja, nikiwa nimekaa na mdogo
wangu Latina nilimuambia kwa sauti ya Chini:
tukitoka hapa twende magereza kumuona baba ili
tumpe taarifa kuhusu mama.
Latina: Nikweli ila hujaniambia Derick Muda ule
alikuwa anakuambia nini?
Nikamjibu: Potezea.
Latina: Mbona sasa anabaki anakutazama Muda
wote?
Nikamjibu: kama huwezi kusoma toka nje.
Latina: sawa basi yaishe.
Derick alianza kuzunguka darasa taratibu, alipofika
nilipo alisimama kama vile kuna jambo anataka
kuniambia, muda Huo watu wote waligeuka
kumuangalia Derick huku kila mtu akijiuliza maswali
bila kupata majibu, Na mimi Muda Huo nilijikausha
kama vile simuoni, Derick uzalendo ulimshinda
akasogea kwenye dawati yangu akaweka mikono
huku akinitazama usoni, Latina alishtuka mpaka
akabaki anashangaa ninavyompotezea, wanafunzi
hawakuamini haswaa Mabinti wenzangu, Derick
alishusha pumzi kwa kasi kama mtu mwenye hasira
vile, Na mimi wala sikumpa muda macho yangu
pembeni tu, ndipo Derick akaniuliza huku akiwa
yupo serious: Kwa nini unanifanyia hivi?
Latina uzalendo ulimshinda Akajishika kwenye
mdomo ishara ya mshangao, bila wasi wasi wala
kuteteleka nikamjibu: Kwani wewe Nani?
Wanafunzi waliokuwa nyuma yetu hawakuamini,
Latina alishindwa aseme nini akajibu pahali yangu:
muelewe ana matatizo Muda huu.
Latina alinigeukia na kuniambia huku akiwa
amebananisha meno: Ndio nini sasa mtu mkubwa
Kama Huyu kumjibu utakavyo?
Sikumjibu Niliendelea kufanya inshu zangu ndipo
Derick akasema: unanipa wakati mgumu Sana, kila
siku nafikiria Upo wapi Kumbe upo hapa hapa
Tanzania why hukunitafuta?
Nikamjibu: Kwani Mimi nakuhusu tena?
Derick: somo ikiisha usiende bila kuonana na Mimi
please!
Derick Alichukuwa kauntbook yangu ajabu akaandika
namba, alipomaliza Akaniambia: this's my fone
namba please ni call kabla ya kwenda nyumbani.
Derick aliondoka wala hakutoa somo tena alitoka
moja kwa moja nje ndipo akaingia mzee waliekuja
nae ili kuendeleza somo, wanafunzi walitamani Sana
kuniuliza maswali kadhaa Ila kwa kuwa soma
nyingine ilianza waliamua wakaushie, muda wote
Latina macho kwangu Mpaka akashindwa aniweke
kwenye Aina gani ya binadamu.
Simo ilipoisha tu! wanafunzi waliniwahi kama wote
maswali yalianza kutoka kila kona * Najma
ulimjuwaje Derick *
*Najma ulikuwa unajuwana nae kabla na Derick *
*Najma mbona kakushobokea sana Kulikoni? *
Nilinyanyuka na kusema kwa sauti ya Juu: Simjui,
hanijui mniacheeee.
Niliwapita nikatoka zangu nje huku Joyce na Latina
wakiwa wananikimbilia, waliponifikia Joyce alisema:
Shostiii Mbona upo hivo?
Nikamjibu: nipoje?
Joyce: why hili swala unalikwepa sana Huyu mtu
mnajuwana Eee???
Latina akadakia: dada sema ukweli bwana Mbona
kama vile anakujuwa sana na wewe unamjuwa Sana
Ila ukaamua kumpotezea na Kwa nini Sisi watu
wako wa karibu hutaki kutwambia?
Joyce: wallah atuweke wazi Nipo nakuambia Derick
mpaka walimu wametamani namba zake
hawakuzipata ila wewe kirahisi rahisi hata
Haujamuomba amekuandikia unajuwa hata Watoto
wa maraisi wanatamani Sana kufanyiwa
alivyokufanyia, wallah siwezi kukuelewa.
Nilipaza sauti kwa hasira huku nikiwajibu:
niacheniiii! Eti Watoto waraisi wanaitamani nafasi
ile, hivi wewe unawajuwa Watoto waraisi vizuri?
sasa kwa taarifa yenu naondoka na sitampigia
kwanza na namba nachana.
Nilichana ile karatasi iliokuwa imeandikiwa namba
ya Derick kisha nikarudia nikachana Chana vipande
vidogo vidogo kwa hasira na kutupa Chini, Latina na
Joyce walibaki wameachama kwa mshangao ndipo
nikawapita na kuondoka zangu.
Nikiwa nipo njiani naelekea magereza machozi
yalianza kunitiririka nikasema:........!!!!!
Unahisi nini kitatokea!
Usikose mkasa huu!
Ukiihitaji yote kwa haraka unanunua kwa Elfu 2
namba 0l+255757449871.
TANGAZO!
Simulizi hii itakuwa inarushwa Mara mbili tu kwa
wiki ijumaa nne na ijumaa.
 
SEHEMU YA 02
TULIPOISHIA: Nilichana ile karatasi iliokuwa
imeandikiwa namba kisha nikaichana Chana vipande
vidogo vidogo kwa hasira na kutupa Chini, Latina na
Joyce walibaki wameachama kwa mshangao ndipo
nikawapita na kuondoka zangu.
Nikiwa nipo njiani naelekea magereza machozi
yalianza kunitiririka ndipo nikasema:........!!!!!
SONGA NAYO!
Ndipo nikasema: Kwa nini Mimi!!
Latina alinifikia na kusema: sorry dada kama
ntakuwa nimekukosea.
Nikamjibu: ni sawa tu.
Latina: Ila dada mi sintachoka kukuuliza embu
niambie jamani Mimi mdogo wako ujuwe.
Nikamjibu: kuhusu?
Latina: kuhusu Derick.
Nikamjibu: Yule ni mpuuzi sana staki hata
kukumbuka habari zake.
Latina: ila ulimjua Kabla?
Nikamjibu: ndio.
Latina: alikuwa Nani kwako?
Nikamjibu: mpenzi wangu.
Latina alishtuka na kuniuliza: kiaje sasa?
Nikamjibu huku nikiendelea kusonga mbele taratibu:
unajua Latina wanaume ni wa baya Sana.....
Ndipo nilianza kumuadithia ilivyokuwa Mpaka
nikajuwana na Derick * miaka kumi iliopita nikiwa
na miaka kumi na mbili nilikuwa napita pita zangu
mtaani huku nikielekea Sokoni kwa bahati mbaya
tukagongana na kijana mmoja na kijana huyo
alikuwa ni Derick nae alikuwa bado mdogo na
alionekana kumkimbia mtu flani au kitu flani maana
alikuwa anapumua kwa kasi ndipo Nilinyanyuka na
kusema: samahani kwa hili.
Alinyanyuka nae pia na kuniambia: Mimi ndo
wakukuomba msamaha Jina langu naitwa Derick.
Alinipa mkono bila wasi wasi nikampa wangu na
kusema: Mimi Najma.
Derick: sorry unaweza kunizungusha mtaani
ntakulipa.
Niliposkia Malipo Nilikubali nikaamua kuairisha
safari yangu ya kuelekea Sokoni na hapo yalikuwa
ni Majira ya saa nne asubuhi nikachukuwa jukumu
la kumtembeza maeneo mbali mbali, kwa kuwa
tulitembea kwa mguu aisee nilichoka Sana siku hio
mpaka kujutia kukubali jukumu hilo Ila Derick
hakuonekana kuchoka maana alionekana kuvutiwa
Sana na Mazingira yale, nilipoona kama vile
ananipotezea Muda nilimuambia aende kwao Nami
niende zangu Sokoni ila aliniambia atanilipa milioni
tano, aisee Niliposkia hivo nguvu ziliniingia nikaanza
kumpeleka sehemu mbali mbali ila kila
nimtazamapo kuongea kwake aisee hakufanana
kabisa na Watoto choka mbaya ndipo Nikamuuliza:
kwenu wapi?
Derick: sipajui Kwani kwetu wapi?
Nilitabasamu na kumjibu: Acha Utani.
Derick: twende sehemu Inaitwa Kariako.
Nikamjibu: sawa ila nawahi.
Tulienda kariako yalikuwa tayari ni Majira ya Mchana
saa nane, tulipofika Derick alianza kushangaa watu
walivyo wengi na mambo yanayouzwa kwenye soko
ile, tulizunguka nikijaribu tena kumuambia kuhusu
kurudi nyumbani akaniambia anaongeza pesa
mpaka ikafikia milioni kumi Na mimi pesa
ilivyokuwa inapanda ndivyo nilizidi kupata moyo wa
kumzungusha.
Kwa kuwa tulitembea Sana Tuliamua tupumzike
ndipo Nikamuuliza: kwenu wapi?
Derick: maeneo ya Kuleeeeeee.
Nikamuuliza: sasa wewe Mbona unataka
nikuzungushe mtaani Kwani toka uzaliwe hujawahi
kuzunguka?
Derick: naskia njaa unaweza kunikopa hela Tukienda
kwetu ntakurudishia na Zile milioni kumi!
Nikamjibu: pesa ni ya baba amenituma nikahemee.
Derick: si ndo hivo unikope kwanza.
Nilichomoa Elfu tano tukanunua chakula tukaanza
kula Ila Mimi niliamini Sana pesa ile Kama ntapewa,
Baada ya kumaliza Tulianza upya kuzunguka kwenye
soko ile Mpaka saa kumi jioni, Na mimi kutokana
nilipenda pesa kuliko haikuwa mbaya kwangu
maana nilihesabu akinipa milioni kumi ntamkabidhi
baba na atafurahi, tukiwa tupo njiani Derick
aliniambia: twende kuona movie.
Nilishangaa na kumuuliza: movie?
Derick: eeehh.
Nikamjibu: kwanza wewe ni tapeli Mimi na wewe
viishie hapa maana naona nimegeuzwa mdoli na
pesa yako baki nayo usinijuwe nisikujuwe.
Derick: Ila wewe ndo mwenyeji wangu nisaidie
tukitoka kuangalia movie nakuahidi tunaenda
nyumbani na pesa yako Ntakupa.
Nikamuuliza: wewe si umesema kwenu haupajui?
Derick: niamini.
Nilimtazama machoni Nikaona Labda yupo sahihi
kwa kile anachokiongea ndipo Tulienda
wanakoonesha movie tulipofika tulimkuta
muhudumu mwanamke akatuambia tuchaguwe
movie, nilipoona cover ya Movie inayohusu
wapendanao niliichagua na kusema: Tutaangalia hii.
Mdada Yule Akaniambia: Nyinyi ni wapenzi?
Tulishtuka na kuangaliana ndipo nikamjibu: Hapana
Sisi ndugu.
Mdada Yule akasema: hii inahusu mtu na mpenzi
wake na watu wakubwa sio Watoto, kama unahitaji
movie ya Watoto chaguweni hii.
Tulipoangalia cover Ilikuwa ni Movie ya vita vita
kiukweli Mimi sikupenda Ila Derick alionekana
kuipenda sana ndipo mdada Yule akasema: watu
wawili Elfu ishirini.
Nilishtuka na kusema: heee!! Turudi bwana.
Derick akasema: Hapana tuone ntakurudishia na ile
hela yako Baada ya movie please.
Nilikuwa mjinga sana pesa ya mahemezi Elfu ishirini
na tano yote niliitoa kwa mambo ya ujinga, tuliingia
tukaanza kuona movie Ila Mimi movie za kivita vita
sikuzipenda hivo kutokana na uchovu Wa kutembea
siku nzima nilijikuta namuegamia begani Derick na
Usingizi ukanivuta, Derick aliendelea kuangalia
Mpaka usiku saa mbili Na mimi Usingizi nilizidi
kuvuta taratibu, Baada ya movie kuisha aliniamshaa
nikaamka na kusema: bado tupo hapa?
Derick: eeeehhh!
Nilinyanyuka kwa hasira kisha nikatoka nje, Derick
Baada ya kuona nimetoka nje nae alinifuata
aliponifikia aliniuliza: kwahio unaondoka?
Nilimkata kibao kwa hasira na kusema: umenigeuza
mjinga sana.
Derick Baada ya kupigwa kibao alijishika shavuni Na
mimi Muda Huo nilikuwa nimeondoka.
Nikiwa nipo njiani naelekea nyumbani njia nzima
nilikuwa nalaani maana baba yangu licha alikuwa
sio mkali sana Ila kwa hili sizani kama
angenisamehe, ghafla niliskia sauti ya Derick
akiniita Ila sikutaka kusimama bali Niliongeza
mwenda, Derick alipoona Kama vile nampotezea
alinifuata akikimbia aliponifikia alinishika mkono na
kusema: sorry please niskilize kwanza.
Nilimkazia jicho na kusema: unahitaji nikupige?
Derick: Hapana.
Nikamjibu: pesa baki nayo niachie uzima.
Derick: Ila Mimi ukweli ukiniacha hapa I'll die
maana I don't know home ukweli Mimi ni mgeni
nasomea wingereza hapa Nimekuja holiday Nikaona
nitoroke ili niuangalie mji vizuri please nisaidie
kwetu sipajuwi vizuri.
Nilimtazama kwa umakini kisha nikampushi na
kuondoka zangu na kumuacha akinisindikiza kwa
macho, ukweli aliponiambia Ooh anasomea
wingereza kwanza nilimuona tapeli flani.
Nikiwa nazidi kusonga nilisimama nikamkumbuka
alivyokuwa anayashangaa Mazingira na alivyokuwa
anaongea kingereza Kidogo nikamuamini ndipo
niliona nirudi nyuma kumtazama nilipofika eneo lile
nilipomuacha nilianza kumuangaza angaza Ila
sikumuona, nikiwa naendelea kumuangaza nilimuona
akiwa amekaa pembeni ya nyumba flani, ukweli
nilimuonea huruma kwa sauti ya Chini Nikamuuliza:
utalala hapo?
Aliponiona alinifuata, aliponifikia aliniuliza: umerudi?
Nikamjibu: usijali tupo Pamoja ntakusaidia.
Derick: nipeleke kituoni watanitangaza.
Nikamjibu: usilete mambo ya kimama mama! hapa
sio ulaya twende nyumbani kwetu ni wakalimu sana
ikifika asubuhi baba atakupeleka kwenu maana
anajuwana na matajiri wengi.
Tulianza safari ya kuelekea nyumbani tulipofika
niliogopa kubisha hodi Ila Nikaona potelea Kote
Kama nikupigwa acha iwe hivo maana nilikosea
sana, niliingia ndani moja kwa moja na Derick
akanifuata nyuma, sebuleni niliwakuta wazazi wangu
wawili wakiwa kama vile wanajadiri kitu flani
nikajuwa hapo nazungumziwa Mimi, waliponiona
walinikimbilia na kuanza kuniuliza hali yangu ndipo
nikawajibu: mi mzima Ila baba I'm sorry.
Baba: Kikubwa ni wewe Upo Salama Huyu nae
Nani?
Sikutaka kuwaficha niliwaeleza kila kitu ndipo baba
akamuambie Derick: pole Sana kijana hapa umefika
jiskie huru ntatoa taarifa kituoni kuhusu wewe
nikizani wazazi wako watakupata kirahisi sasa
Najma mpelekee maji mwenzio bafuni aoge.*
Kabla sijamaliza kumuadithia Latina aliniuliza: siku
hio nilikuwa wapi Mbona sikumuona?
Nikamjibu: wewe si ulikuwa Unasoma bodingi!
Latina: sawa Nimekumbuka Enhe ikawaje?
Nikaendelea kumpa story * Baada ya pale tulilala
asubuhi ilipowadia tuliamshwa na minghurumo ya
gari tulipotoka nje tulishangaa kuona gari tatu nzuri
za kifahari kweli zimepaki karibu na mlango wetu
Na watu Kama Sita akiwemo mama flani
alieonekana kupaniki kuliko wote, baba kwa sauti ya
Kawaida aliwasalimia na kuwauliza: sijui tuwasaidie
nini?
Yule mama akasema: tumepigiwa simu kituoni
maana tulikuwa tumelipotia kuhusu mwanetu
aliepotea toka Jana asubuhi sasa police
walitutaarifu kuwa mlitoa taarifa kuwa kijana wetu
yupo hapa.
Baba: ndio yupo hapa.
Yule mama alishusha pumzi kwa furaha ndipo baba
Akaniambia: kamuamshe mwenzio.
Nilirudi ndani nikamkuta bado amelala ndipo
nikamuamsha akaamka tukatoka nae nje, mama
Yule alieonekana kama mama yake alipomuona
alimkimbilia na kumkumbatia kisha akaanza
kumuuliza kuhusu Hali yake, Derick akamuambie
yupo sawa, ndipo mama yake alimshika mkono
akaondoka nae Baada ya kuwashukuru sana wazazi
wangu ila Derick kuondoka kwake jicho lilikuwa
kwangu hata walipopanda gari aliendelea
kunitazama Mpaka mama akanitania kuwa mtoto wa
watu watanifunga* hivo ndo ilivyokuwa.
Nilimaliza kumsimulia tukawa tayari tumefika
magereza, kabla hatujaingia ndani Latina alinishika
mkono na kuniuliza: Baada ya hapo ilikuwaje?
Nikamjibu: sikumuonaga tena Mpaka miaka Sita
ikapita bila salamu wala kumuona.
Latina: sasa mbona wewe uliniambia mlikuwa
wapenzi embu niambie vizuri.
Nikamjibu: Ntakuambia tukitoka kumuona baba.
Tuliingia ndani, Baada ya muda baba aliletwa
tukakumbatiana kwa furaha maana siku zilikuwa
nyingi bila kumuona tukiwa tumekaa baba aliniuliza:
maisha huko yanasemaje mbona siku nyingi mama
yenu haji kuniona hata Nyinyi pia nilikuwa na wasi
wasi.
Tulitazamana machoni Mimi na Latina ndipo
nikamjibu: baba sorry kwa hilo.
Baba: Ila Nyinyi wawili Mnasoma vizuri kweli?
Maana msiwe mmevunjika moyo kisa mimi mpaka
mkaacha shule.
Nikamjibu: tunasoma baba ila I'm sorry
tumeshindwa kumfanya mama aweze kulichukulia
swala lako kikawaida.
Baba: una maana gani?
Nikamjibu: ukweli mama kwasasa amepatwa na
ukichaa toka uhukumiwe.
Baba alishusha pumzi na kuniuliza: kivipi sasa?
Nilianza kulia ndipo nikamjibu: kwasasa yupo
kwenye hospito ya vijaa Ila sorry.
Baba: usiseme hivo Namjua mke wangu ananipenda
sana ndo maana yote yametokea.
Nikamjibu: Ila usijali tutakutoa jela.
Baba: miaka mitano ni mingi sana mnisamehe
Watoto wangu siwezi kuwapa vile mnavyovihitaji
kama baba.
Nikamjibu: usiseme hivo baba Sisi tunajitosheleza
Kikubwa wewe mzima kuhusu Sisi isikupe tabu
kwasasa tupo watu wazima na kuhusu mama
atapona Allah yupo.
Baba alitushika Mimi na mdogo wangu akatulaza
mabegani kwake ili kutufariji kisha akasema:
nikiwaona nafarijika Sana.
Baada ya muda tulitoka magereza, tukiwa tupo
kwenye mlango wangu geti kuu ya magereza kwa
mbali nilishtuka kuona gari ya Derick aliokuja nayo
Muda Si mrefu shuleni inakuja magerezani, nikajuwa
atakuwa Yeye, kichwani nikaanza kuwaza Huyu mtu
kafuata nini huku?
Kabla...........
Unahisi nini kitatokea!
Usikose mkasa huu!
 
SEHEMU YA 03
TULIPOISHIA: Baba alitushika Mimi na mdogo
wangu akatulaza mabegani kwake ili kutufariji kisha
akasema: nikiwaona nafarijika Sana.
Baada ya muda tulitoka magereza, tukiwa tupo
mlangoni kwa mbali nilishtuka kuona gari ya Derick
aliokuja nayo Muda Si mrefu shuleni nikajuwa
atakuwa Yeye kichwani nikaanza kuwaza Huyu mtu
kufuata nini huku?
Kabla...........
SONGA NAYO!
Kabla gari lile halijatufikia nilimshika mkono Latina
na kukimbia nae Mpaka kwenye mfereji mmoja
uliokuwa pembeni ya barabara ya kutoka magereza
kuelekea mjini, Latina akiwa haelewi elewi
alipandisha kichwa juu akaona gari inapaki mbele
ya mlango wa geti kuu ya magereza ndipo
nikamshusha kwa haraka na kusema: unataka
nionekane?
Latina: Mbona kama vile gari la Derick.
Nilimnyamanzisha: shiiiii!!!
Latina alitabasamu kisha akapandisha kichwa
taratibu akamuona Derick anatoka kwenye gari na
Rafiki yake wakaingia magereza ndipo akasema:
wameingia hivi wamekuja kufuata nini?
Nikamuuliza: wameingia ndani?
Latina: ndio.
Nikamjibu: twende nyumbani.
Tulitoka hapo tukikimbia Ila Latina alikuwa bado
hajajuwa chanzo cha Mimi kukimbia, tulipofika mjini
tulijipumzisha ndipo Latina akaniambia huku akiwa
ameyashika magoti yake: hakikisha utoe sababu za
msingi za kumkimbia Derick.
Nikamjibu: ni sawa ila kabla ya kwenda nyumbani
twende kumuona kwanza mama.
Latina: sio mbaya Ila dada haya yote ya nini?
Muda mdogo simu yangu iliita nikapokea na kuuliza
Nani mwenzangu maana namba Ilikuwa ngeni, ajabu
sauti ya Derick iliskika akiniambia: Najma Kwa nini
unanifanyia hivo?
Nilichomoa macho na kumuuliza: kukufanyia nini?
Derick: sielewi Kwa nini unanifanyia haya yote basi
please Nipe muda tuongee.
Nikamuuliza: namba zangu kakupa Nani?
Derick: kwasasa natoka magereza nilienda kumuona
baba yako Kanipa namba yako embu niambie upo
wapi nije tulizungumzie swala la baba yako?
Nikamjibu: swala la baba yangu liache hivo na
usinipigie tena.
Nilikata simu kisha nikazima kabisa ili asinipate
tena ndipo Latina akaniambia: wewe ni mjinga wa
kiasi gani ila sorry kwa kukuita hivo ila unayataka
wewe.
Nikamjibu: acha iwe hivi.
Latina: ila ungekubali Labda angetusaidia!
Nikamjibu: Sina imani hivi Latina Mbona unaongea
Sana unajuwa kilichotokea Baadae?
Latina: Kwani kilitokea kitu gani?
Nikamjibu: baada ya pale.......
Nilianza kumsimulia* Derick hakuweza kuonana Na
mimi tena mpaka nikamsahau kabisa, nilipokuwa
nasoma secondary hapo nilikuwa na miaka 18
Derick alikuja shule Kama hivi alivyotangazwa chuo
aliponiona tu akaanza kuniomba msamaha Oohh
amenimiss Ooohhhh siku nyingi kweli. ukweli Na
Mimi nilikuwa nimemmiss alinichukuwa kama siku
ile utotoni nilivyo zeze nikaanza kumtembeza eneo
mbali mbali nikajikuta nimevutika nae Mpaka
nikasahau nyumbani, Derick alinipeleka supermarket
akaniomba nichague vitu vinavyoendana na milioni
kumi ile hela alioniahidi ila kwa kuwa Mimi
nilimsaidiaga kipindi kile kiroho Safi sikutaka anilipe
nilikataa ila akazidi kunilazimishia Ila sikuwa tayari,
alinipeleka kwenye hoteli kubwa akaagiza chakula
cha thamani tukala wote kwa furaha hakika nikazidi
kuzama kwake, Baada Ya hapo alinipeleka kwenye
movie kama vile vile siku Zile tupo wadogo ila
tuliangalia movie inayohusu watu wawili
wanaopendana kwa dhati movie ya Romeo na Juliet
Baada ya kuona movie ile Ilikuwa tayari ni saa moja
usiku Tulitoka nikidai kurudi nyumbani mapema
Kama siku Zile, tulirudi nyumbani mdogo mdogo
kwa mguu huku akinisindikiza Hakuna Aliekuwa
akiongea na mwenzie sikujuwa ni Nini ndipo
aliniomba nisimame nikasimama akazunguka nyuma
yangu Akachomoa kitu flani mfukoni Kumbe
kilikuwa ni kidani chenye thamani ya milioni tano
akanivalisha, nilifurahi Nikamuuliza: chanini hichi?
Alisogeza mdomo wake karibu na skio langu la
kulia Akanijibu kwa sauti ya Chini saana huku akiwa
bado yupo nyuma yangu: Naomba kama hautojali
niweze kuwa kama Romeo mbele yako.
Sikuamini kwanza nilisisimka mno kwa pupa
nikageuka kumtazama tukagonganisha Vichwa
Tulianza kucheka hovyo ndipo akaniambia: I'm
serious about this! Nipe nafasi ukweli nilikupenda
toka siku ile bado tupo wadogo unajuwa nilitamani
Sana hii zawadi nikuvishe maana niliachiwa na
marehemu bibi yangu aliniambia cheni hii
alivalishwa na Babu siku ya kwanza anamuomba
uchumba akaihifadhi miaka hamsini ndo akanipa
Mimi ili ikifikia hatua nikampata nimpendae basi
nimpe zawadi hii please Najma Nipe nafasi hio.
Ukweli sikutaka kumficha maana hata mimi nilitokea
Kumpenda nikamkubalia Akachomoa milioni kumi
akanipa akimaanisha siku ile tuliahidiana atanipa Ila
hakunipa sasa ameniletea ahadi yangu, ukweli
sikuzichukuwa pesa zile maana Mimi sizowei kula
vya watu vingi.
Alinipeleka Mpaka nyumbani hakutaka kufika
Tuliagana akarudi, ukweli siku hio sikuweza kupata
Usingizi ukija kumuangalia Derick nikijana smart na
ana kila Sifa ya kuitwa mwanaume hata ya bila
pesa, kila Mara nilimtumia ujumbe hata Yeye pia
Alinitumia ujumbe, Uliza sasa Baada ya Yeye kurudi
kwao kama Ndo wingereza.*
Latina akaniuliza: Kwani ilikuwaje?
Nikamjibu: hata salamu, hata simu, basi hata barua
ya bure mwenzio niligeuka kichaa chakula kilikuwa
hakipiti kinywani ukweli mdogo wangu wanasema
Hisia mtu pekee ndie anaziendesha Ukitaka
Kumpenda mtu Sana ni wewe Ukitaka kumchukulia
Poa ni wewe ila kwangu hio haikuwepo Nilishindwa
kabisa kuzizuia Hisia zangu kwake kila siku nilikuwa
mwenye majonzi nikiamini Ipo siku ntapata ujumbe
kutoka kwake ila Mpaka sasa Leo hii ndo anarudi
anakuja na ukichaa wake ohh tuonane au anataka
anifanye kama siku zote akija huku niwe wa
kumliwaza tu, Mimi sio mwanamke wa Aina hio
mdogo wangu.
Latina alishusha pumzi na kuniuliza: kwahio ile
cheni unayokuwaga nayo siku zote ndo hio
aliokupa?
Nikamjibu: ndio.
Latina: inathamani ya milioni tano?
Nikamjibu: ndio.
Latina: heee! Mbona tunapata pesa ya kumtunzisha
mama.
Nikamjibu: kwahio tuuze?
Latina: Eee.
Tulikubaliana hivo tukaalisha safari ya kuelekea
hospital ya Vichaa tukaelekea nyumbani ili tukauze
ile cheni, tulitafuta mteja siku hio kila tuliekuwa
tukimpa anadai atupe Elfu hamsini wengine Mpaka
Elfu ishirini tukajikuta tunakata tamaa.
Baada ya siku mbili kupita nikiwa nipo darasani
huku somo ikiendelea, professor aliendelea kutoa
somo mwishowe akaanza kugusia ugonjwa wa
Ebola: ugonjwa wa Ebola umekuwa sugu kwasasa
Mpaka nchi jilani Kenya watu asilimia 2
wamegundulika wana ugonjwa Huo Na kwasasa
ambao wameshapoteza maisha ni watu stini hii Hali
imeitia Hofu nchi yetu sana Kikubwa mjilinde
msipokee Wageni kwasasa Mpaka ugonjwa huu
utulie.
Tulipotoka nje wanafunzi walianza kulijadiri swala
lile ndipo Rafiki yangu Joyce akanifuata na
kuniambia: unajuwa Najma Mpaka sasa mambo
yako siyaelewi.
Nikamjibu: Rafiki yangu Matatizo ya familia.
Joyce: pole Ila huu ugonjwa wa Ebola umekuja kwa
kasi kubwa Sana tofauti na siku zingine.
Nikamjibu: kwanza nimeshangaa kuskia.
Joyce: aisee siku hizi zote ndo habari ya mjini ila ni
kwasababu wewe Upo kwenye wakati mgumu ndo
maana hujali chochote.
Nilitabasamu kisha tukaendelea kuelekea nyumbani.
Baada ya siku tatu ugonjwa Huo wa Ebola Ulianza
kusadikika kuwa tayari vijiji jilani na Kenya baadhi
ya watu wamepimwa ikagundulika virus hio
imewapata, Raisi wetu Pamoja na viongozi wengine
wakiwemo wanasayansi wakubwa wa nchi
walichanganyikiwa mno kila siku kwenye vyombo
vya habari waliwatuliza wana nchi wasijali ni
ugonjwa mdogo utaisha Ila wajilinde Sana Kama
atatokea mtu yeyote mwenye dalili zifuatazo kama
kuchemka sana (homa Kali) hivo usimguse
yakupasa ukatoe taarifa kwenye vituo maalumu
walivyoviteua.
Chuoni kwetu maprofesa walianza kuchakachua
vitabu mbali mbali vinavyohusu ugonjwa wa Ebola
hivo kila somo tuliokuwa tukipewa ni kuhusu Ebola
ni namna gani tunaweza kujiepuka na ugonjwa Huo
ikiwezekana kuuteketeza kabisa.
Siku hio mimi na Latina tulikuwa chumbani huku
tukijadiri kuhusu ugonjwa Huo.
Latina: mbona kila mwaka ugonjwa Ukitaka kuamka
huwa Unaanza Kongo?
Nikamjibu: ndio inasadikika watu wanaoishi
mapolini wanakula nyamafu sana bila kujuwa
wanyama Hao wameuwawa na Nini hivo wanajikuta
wanaambukia na wanaanza kuambukiza wengine.
Latina: hapo sasa ndo nataka kujuwa, hao wanyama
wanapatapataje Huo ugonjwa?
Nikamjibu: mara nyingi Nyani ndo wanaleta ugonjwa
Huo.
Latina: kwahio Nyani akishakufa wao wanamla bila
kujuwa nikipi kimemuua si eti?
Muda Huo simu yangu iliita nikapokea na kuuliza:
huwezi kupiga Muda mwingine tofauti na huu?
Alikuwa ni Joyce Akanijibu: nakupigia muda wowote
ninaojiskia Upo!
Nilitabasamu na kumuambia: Umekosa Usingizi mi
nakujuwa.
Joyce kwa sauti ya Chini akaninong'oneza: oyo
niskilize kwa umakini wanasayansi wakubwa nahisi
kuna Jambo ambalo wameligundua kuhusu Ebola ila
bado Ni Siri sijaelezewa vizuri.
Tuliangalia na Latina maana nilikuwa nimeweka
kwenye sauti ya Juu sana ndipo Nikamuuliza: Nani
kakuambia?
Joyce: si Unajuwa kuwa professor Rodrigo ni
mpenzi Wangu.
Nikamjibu: fuatilia vizuri Utanipa habari nzima sawa.
Joyce: Poa.
Asubuhi ilipowadia chuoni walitutangazia turudi
nyumbani tutaanza kusoma hili swala likishatulia
hivo walituomba tukakae majumbani kwetu kwa
usalama zaidi maana tayari ndani ya jiji la dar es
salam imebainika kuna mtoto amengundulika
anaugonjwa Huo hivo Nihatari sana kwetu kukaa
sehemu moja, tulipotoka tu majadiriano Kati yetu
wana chuo yalianza, hakika swala lilo liliyayusha
Ubongo wa watu wengi.
Nikiwa narudi nyumbani Pamoja na Latina, Joyce
alikuja na kuniomba tuongee nilimuambia Latina
aende kumuangalia baba magereza ikiwezekana
akamuambie kuhusu Hali halisi ya nchi aweze
kujilinda huko, Mimi na Joyce tukarudi nyuma,
tulielekea moja kwa moja ndani Ofisi ya professor
mkuu wa chuo hicho tukamkuta professor Rodrigo
mpenzi wake Joyce amekaa ndipo tukamsalimia na
kukaa, Rodrigo kwa sauti ya Chini kama vile
anajiogopa akasema: Najma nikizani unanijuwa
Mimi Nani?
Nikamjibu: ndio wewe ni professor Rodrigo mtoto
wa professor mkuu wa hapa.
Rodrigo: sawa kwahio baba yako unajuwa anadaiwa
shiingapi hapa?
Nikamjibu: ndio Najuwa ila pesa hio kwasasa
Hawezi kuilipa maana yupo jela.
Rodrigo: sawa kwasasa hapa wewe na mdogo
wako mnadaiwa milioni kumi, bado baba yako yupo
jela inatakiwa mmtowe kwa milioni tano ili asipige
miaka mi 5 huko, na bado mama yako ni mgonjwa
anatakiwa afanyiwe matibabu, nahisi ili apone
inaweza kughalimu milioni moja na nusu au milioni
mbili, Najma unawapenda wazazi wako pia hata
wewe unajipenda, vipi hio hela utaitoa wapi?
Nilijiinamia nikashindwa nimjibu nini ndipo
akaendelea kusema: ndo maana Nimekuita hapa uje
tulijadili swala lako ikiwezekana lipatikane
ufumbuzi.
Machozi yalikuwa tayari yameanza kuelelea machoni
kwangu ndipo Rodrigo akasema: usijali hapa kuna
inshu ya Chini Chini inaendelea Ila bado ni Siri na
inahitajika iwe Siri ndo maana nimewaiteni hapa
kwenye Ofisi ya baba yangu nilijuwa kuna usalama
Tosha kwanza kwa hili ninalotaka kukuambia
ulimeze usithubutu kumueleza mtu yeyote.
Nikamjibu: siwezi kufanya ujinga Huo.
Rodrigo: huu ugonjwa wa Ebola umekuwa tishio
kubwa hapa nchini na sio hii nchi tu Mpaka Kenya,
burundi, Rwanda sasa hivi Hali ni mbaya sana
haswaa kongo ndo usiseme kabisa, hapa tumefanya
uchunguzi tumegundua chanzo cha ugonjwa huu wa
Ebola.
Mimi na Joyce tulishtuka na kumuuliza: unasemaje?
Rodrigo: semeni taratibu.
Joyce: kwahio mmejuwa chanzo?
Rodrigo: ndio! huu ugonjwa wanyama wanautoa
kwenye mti flani uliopo ndani ya msitu wa
Equatorial mti Huo ukitoa matunda wanyama Kama
Nyani wanayapenda sana matunda Yale wanayala
mwishowe yanawaletea maradhi wanakufa na watu
wakiona Mnyama amekufa wanamchukuwa
wanamchoma hawahakikishi wanamchoma vizuri ili
mavairasi yaweze kufa wanamla hata hajawiva vizuri
madhara yake ugonjwa unatokea hapo.
Jasho Ilikuwa imeanza kutufumuka Mimi na Joyce
ndipo Nikamuuliza: kwahio Sisi tunafanyeje?
Rodrigo: hapa kuna kikosi kinaandaliwa watu Kama
kumi na tano hivi ila ni kimya kimya licha selekali
inajuwa ila laia hawatakiwi kujuwa chochote
wameona wachague wanasayansi ambao maswala
haya wanayaelewa vizuri waende kutalii huko
ikiwezekana wajuwe chanzo cha ugonjwa huu ili
swala Hili liweze kuchukuliwa hatua bado mapema
hata Mimi hapa Nipo miongoni mwahao waliotuliwa,
sasa basi, nimewaita ili kuwashilikisha ikiwezekana
na nyinyi muungane nasi.
Moyo wangu ulisita Ila Joyce alikubali ndipo
Rodrigo akaniuliza: Najma haupo tayari?
Nikamjibu: nahisi sipo tayari.
Rodrigo: vipi kuhusu wazazi wako? Na vipi kuhusu
madeni ya baba yako?
Joyce akadakia: Najma kubali Baada ya zowezi hili
tutapata mabilioni ya pesa acha kuwa mzembe.
Nikamuuliza: sasa Rodrigo itakuwaje mbona Mimi
sielewi.
Rodrigo: tunaelekea huko Kongo ndipo kuna msitu
Huo wa Equatorial sema Ndio au Hapana maana
hapa hatuna muda, je! Upo tayari?
Unahisi nini kitatokea!
Usikose mkasa huu!
 
SEHEMU YA 04
ENJOY YOUR WEEKEND!
TULIPOISHIA: Rodrigo: vipi kuhusu wazazi wako?
Na vipi kuhusu madeni ya baba yako?
Joyce akadakia: Najma kubali Baada ya zowezi hili
tutapata mabilioni ya pesa acha kuwa mzembe.
Nikamuuliza: sasa Rodrigo itakuwaje mbona Mimi
sielewi.
Rodrigo: tunaelekea huko Kongo ndipo kuna msitu
Huo wa Equatorial sema Ndio au Hapana maana
hapa hatuna muda je Upo tayari?
SONGA NAYO!
Kichwa kiliwaka nikapiga mahesabu ukweli
walichokuwa wanakiongelea kilikuwa sahihi Licha
moyo wangu ulikuwa unasita, sikuwa na chaguo
nilijikuta nakubali, ndipo Rodrigo akasema: kwahio
tutajuzana itakavyokuwa.
Nikamuuliza: Malipo ni vipi?
Rodrigo: milioni hamsini kwa kichwa cha mtu Kama
tutafanikiwa.
Nikamuuliza: ila jamani tutafanikiwa kweli? Mbona
wazungu hili swala hawajalifuatilia Sisi ndo
tutaweza?
Rodrigo: Uliza Kwanini malaria Ipo huku Africa tu
huko nchi zilizoendelea Mpaka South Africa Huo
ugonjwa haupo na Mbu wapo, Kwa nini hio anti
Malaria wasituletee na sisi? Acha Sisi tufuatilie
tusitegemee kila siku kutaftiwa sawa!
Tulikubaliana hivo tukaagana, Mimi na Joyce
tukaenda manyumbani.
Nilipofika nyumbani nilimueleza kila kitu Latina
ndipo akasema: hii bahati hatuwezi kuipotezea
lazma twende huko au unasemaje!
Nikamjibu: wewe haumo utabaki unawaangalia
wazazi.
Latina: dada Acha nije embu fikiria mtu mmoja
milioni hamsini tunalipa Deni mwingine milioni
hamsini tunapata mtaji tunafungua duka la madawa
Unaonaje.
Nikamjibu: Hapana Latina.
Latina: please mwenzio nataka kwenda sasa hapa
ntabaki nafanya nini Mimi ni mwana science ujuwe!
Lazma niende kutalii ili kujiongezea ujuzi zaidi,
niruhusu please.
Nikamjibu: Nikweli Acha twende wawili tuache
tumemuambia doctor amtazame mama baba nae
kule yupo Salama.
Latina: eeeehhh.
Baada ya siku chache kupita Tulianza kujiandaa ili
kuondoka, upande wa Derick alikuwa bado hajarudi
wingereza kutokana na tatizo hilo la Ebola
lilimfanya asubiri kwanza ajuwe mwisho wake
utakuwaje.
Siku yenyewe ya safari yalikuwa ni Majira ya saa
tano usiku tulielekea airport ili kuchukuwa usafiri wa
ndege tuelekee huko Kongo, Tulifika kwenye
chumba maalumu wakatufanyia vipimo ili tusiende
na ugonjwa Huo wa Ebola, wakatukuta tupo Salama,
wenzetu Kama Saba waschana wawili wanaume
watano tulisalimiana wote hao walikuwa levo ya Juu
Sisi tu levo yetu ki science ndo Ilikuwa Chini kidogo,
mwishowe tulipanda ndege tukapewa siti zetu,
maprofesa wa tatu akiwemo Rodrigo Waliingia nao
wakakaa, kuna kijana mrefu mwenye weusi wake
Wa mng'aro, mwenye bodi kubwa yaani mwili wake
alifanana kupenda mazowezi sana, alipotupita alikaa
Siti ya mbele yetu ndipo Rodrigo kwa nyuma
akanitikasa na kuniambia: huyo ni mwanajeshi,
selekali imemteuwa Yeye aje kuimalisha ulinzi wetu.
Mimi na Latina tukamjibu: ndo maana.
Watu wote Waliingia na safari ikaanza kimoyo
kimoyo nilianza kuwaaga wazazi wangu: I'm sorry
mamy and dady hatuna chaguo ila hapa karibu
tutakuwa Pamoja na mtafurahi.
Baadhi ya watu walianza kulala, tukiwa tunazidi
kusonga Latina aligeuka kunyuma kumuangalia
Joyce ndipo Joyce kwa ishara akamuambie
aangalie pembeni Latina alipoangalia pembeni
hakuamini kumuona Derick akiwa amekaa huku
akisoma gazeti taratibu, Latina macho
yalimchomoka akageuka kunitazama ndipo
Nikamuuliza: nini?
Latina: flani.
Nikamuuliza: nani?
Latina: Derick.
Nilishtuka na kumuuliza: Kafanyaje?
Latina: tupo nae.
Nikamuuliza: wapi?
Latina: yupo nyuma yetu.
Pumzi nusu kukata Baada ya mimi kugeuka nyuma
nikamuona amekaa ndipo nikageuka haraka na
kuangalia mbele, Latina akaniuliza: tunafanyaje?
Nikamjibu: usigeuke tena Mpaka tufike.
Latina: subiri jamani Mara moja tu.
Nikamjibu: Ndo Matatizo yako.
Latina aligeuka nyuma akamtazama kama sekunde
kadhaa akageuka na kuniambia: dada pembeni yake
kuna hicho kigoli huwezi kuamini.
Nikamuuliza: binti mzuri?
Latina: huwezi kuamini ni kama malaika.
Upande wa Derick mdada Yule Aliekuwa amekaa
nae muda wote alikuwa anamtazama Derick jicho la
wizi wizi, Derick alipogundua alitabasamu na
kumuuliza: samahani tunaweza kujuwana?
Mdada Yule akatabasamu na kusema: naitwa
Amanda.
Derick alitabasamu na kusema: Mimi Derick.
Walianza kupiga story taratibu Amanda akaonekana
mcheshi sana na mpenda Utani, Amanda alipocheka
Derick alimtazama anavocheka aisee binti Yule
alikuwa mrembo Sana, taratibu Derick akaanza
kuvutika nae.
Upande wetu Usingizi ulituvuta tukalala.
Hatukuchukuwa siku Tulifika katika mkoa uliopo
Kongo uitwao Bandundu wana science wa huko
walikuja kutupokea tukafikia kwenye hotel kubwa ya
kifahari kila mmoja akaoneshwa chumba chake,
Mimi na Latina tulihakikisha hatujajionesha mbele
ya Derick maana sikutaka ajuwe kuwa tupo kwenye
msafara mmoja.
Kwenye hoteli hio hatukuchukuwa siku mbili
tulipewa mwana science mwenzetu wa hapo Kongo
ili kutusindikiza na safari ikaanza ili kuelekea
kwenye msitu Huo wa pili kiukubwa dunia nzima,
tulipofika kwenye usafiri wa basi tulioandaliwa
walianza kusalimiana ili waweze kujuwana kiundani
Sisi tukiwa tupo nyuma ya mgongo wa Joyce na
Rodrigo Latina alitoka na kusema: aisee hatuwezi
kuendelea kujificha mtu ambae tupo nae kwenye
msafara mmoja.
Alisogea karibu kama wengine Na mimi Nikaona
isiwe kesi nikaamua kujitokeza, mkaka flani
tulietoka nae Tanzania alisema: tuhakikishe
tunabeba mafuta ya kutosha.
Mwingine akamjibu: uliambiwa msitu upo hapa!
Bado safari Ipo tena ndefu kuliko ile iliotutoa
nyumbani.
Walitabasamu nilipomtazama Derick Muda Huo
Yeye alikuwa bize na Yule binti Amanda mwenye
alikuwa na muonekano tofauti na waschana wote
hapo, kijana mmoja alimpa mkono professor
Rodrigo na kusema: Abdul.
Rodrigo: naitwa Rodrigo.
Joyce akasema: Mimi Joyce.
Latina: Latina hapa.
Nami nikasema: Najma.
Binti Aliekuwa pembeni yetu akasema: Sofia.
Mkaka mwingine akasema: zakayo.
mwingine: Chande.
Mwingine: Patrick.
Mdada mwingine: Hamisa.
Mwanaume mwingine alieonekana kuwa mpole
Sana akasema: Jina langu naitwa Joseph.
Yule mkongo aliekuja ili kutuongoza akasema:
naitwa chilunga.
Abdul: chi! Chi! chi....
Zakayo: utakatika ulimi.
Tulicheka sote kwa Pamoja.
Professor mwingine akasema kiutani: naitwa
husband (mume).
Tuliangua kicheko Mara dufu ndipo Abdul
akamtazama Derick na kumuuliza: samahani
mheshimiwa Jina lako Nani?
Derick alitabasamu kama Kawaida yake kisha
akasema: naitwa Derick.
Patrick kwa Utani akasema: na huyo wa pembeni
yako jamani.
Amanda kwa aibu aliangalia Chini ndipo Derick
wakaongea kwa kingereza mwishowe Derick
akasema: ameskia aibu ntamsemea Mimi Anaitwa
Amanda.
Wanaume wote wakasema: wow!
Walicheka wote hata Derick pia Ila ile Hali ya
kucheka huku akiangalia angalia watu maana
zilikuwa nyuso ngeni kwake alishangaa kuniona
nikiwa bize naangalia Mazingira ya hapo, macho
yalimtoka akataka kunifuata ila Amanda alimshika
mkono na kumuuliza: kuna nini?
Derick akaamua apotezee.
Upande wetu Zakayo alimtazama Yule mwanajeshi
na kusema kwa sauti ya Chini: yule Jamaa nani
atamuuliza Jina lake?
Wote Tulimtazama kiukweli Alikuwa anastahili Sifa
za kuitwa mwanajeshi maana muda wote alikuwa
amekunja uso Kiufupi no shobo.
Tukiwa tunaendelea kumtazama aligeuka
kututazama akashaa watu wote macho kwake ndipo
akavua headfone moja na kutuuliza: kuna nini?
Wote Tulianza kujing'ata ng'ata kwa aibu ndipo
Zakayo akaamua aseme: Mimi naitwa Zakayo sijui
mwenzangu?
Mjeda Yule alitabasamu na kusema: Dominic.
Wote wakarudilia Jina lake: aaahhh Dominic!
Ndo mimi na Latina tukajuwa Kumbe ni Dominic,
tuliangaliana kisha tukatabasamu.
Professor mwingine Kidogo Yeye umri wake ulikuwa
umeenda alikuja na dereva kisha akasema kwa
sauti ya juu: let's go! time's money (twendeni muda
ni pesa)
Watu walianza kuingia ndani ya basi Ila Derick
macho kwangu.
Safari ikaanza njiani story za hapa na pale Ila
Zakayo na Patrick walikuwa wacheshi sana tulijikuta
kwenye safari yetu Hakuna upweke.
Baada ya siku kadhaa Tulifika kwenye msitu ule
kupitia usafiri wa boti, ukweli msitu wa equatorial ni
msitu unasifika kwa baridi mno, unaambiwa Mvua
inanyesha Miezi yote 12, ukweli tulijipanga na
Makoti ya kutosha.
kila mmoja alianza kupiga picha kupitia simu
Wengine camera zao, masaa ma nne kupita
tulishuka kwenye boti tukaanza kutembea kwa
mguu, sikutaka kabisa Mazowea na Derick maana
Yeye alitamani tuongee hata kwa dakika mbili Ila
Mimi habari hio sikuitaka, Tuliendelea kusonga
Mpaka watu Wakaanza kuchoka, Kidogo Mtandao
ukakata ndipo professor Rodrigo akasema: Jambo
la Kawaida Sana hilo wala msiwe na wasi wasi.
Zakayo: bado njia ya kunirudisha nilikotoka
naikumbuka vizuri.
Tulicheka sote ndipo Sofia akasema: Ki Zakayo
kinaogopa.
Hamisa: walitudanganya eti Mvua haikati huku.
Patrick: subiri bado hatujazama ndani ya msitu
vizuri vizuri tunakoelekea ni ndani ya friji.
Upande wangu Latina alinipa begi yake nimsaidie
maana alikuwa amechoka ndipo tukazidi kusonga,
nikiwa nipo nyuma ya wote kutokana na mzigo
kuwa mkubwa kiasi nilijishika kwenye magoti huku
nikipumua kwa kasi, ghafla nilishangaa kuona chupa
ya mji mbele yangu ndipo nikageuka kuangalia
atakuwa Nani kanipatia aisee alikuwa ni Derick,
nilishusha macho taratibu kisha nikainua mgongo ili
Kutaka kuondoka, Derick akaniambia: maji haya
yatakusaidia maana yanaongeza nguvu.
Nikamuuliza: Kwa nini sasa umenipa Mimi?
Derick: come on Najma!
Amanda akiwa mbele alishangaa kutuona tukiwa
tunazungumza ndipo akarudi nyuma, alipotufikia
alimshika mkono Derick na kusema: wanatuacha
Wengine.
Derick alitabasamu na kuniambia: wahi twende.
Wao wakatangulia Mimi nikabaki nawatazama tu
huku nikijipumzisha, ukweli nilikuwa nimechoka
sana, juu ya mti niliona kandege kazuri kenye
malangi ya njano na mekundu aisee ndege hizo ni
adimu sana kuziona kule kwetu Mara nyingi
zinapatikana Sana kwenye msitu Huo wa Equatorial,
nilichomoa simu nikaanza kukapiga picha huku
nikiendelea kukafurahia kanavyotikisa mabawa yake.
nikiwa nipo hapo sikuweza kuwaona wenzangu tena
kama walikatia njia nyingine au Waliendelea mbele
sikuwaona tena, Kidogo Hofu ikanitawala Nikaona
Acha niwafuate Kama nikupumzika nimepumzika
vya kutosha, kabla sijapiga hatua aisee huwezi
kuamini niliskia mgh'urumo mkubwa ulionifanya
nipigwe gazi mwilini nikajikuta Natamani kujuwa
nikipi kipo nyuma yangu kinangh'uruma namna hio ,
taratibu niligeuka huwezi kuamini nili........
Unahisi nini kitatokea!
Usikose mkasa huu!
 
SEHEMU YA 05
TULIPOISHIA: nikiwa nipo hapo sikuweza kuwaona
wenzangu tena kama walikata njia nyingine au
Waliendelea mbele sikuwaona tena, Kidogo Hofu
ikanitawala Nikaona Acha niwafuate Kama
nikupumzika nimepumzika vya kutosha, kabla
sijapiga hatua aisee huwezi kuamini niliskia
mgh'urumo mkubwa ulionifanya nipigwe gazi mwilini
nikajikuta Natamani kujuwa nikipi kipo nyuma
yangu, taratibu niligeuka huwezi kuamini nili........
SONGA NAYO!
taratibu niligeuka huwezi kuamini nilichokiona mbele
yangu kilipita kama radi Mfano wake ulikuwa Kama
fuvu ya mtu aliekufa muda mrefu, Hofu iliongezeka
kupumua nikashindwa nilivyopiga kelele hata
sikujuwa nilishtukia nimeguswa begani, nilipogeuka
kutazama Sikuamini kumuona Dominic (mjeda) ndie
Kaja Baada ya kuskia kelele zangu, kwa dakika
mbili niligeuka kichaa bila kujielewa Nilimkumbatia
Dominic kwa nguvu huku nikihema vibaya mno
mpaka Dominic mwenyewe akashangaa, muda Huo
Derick nae alifika maana waliposikia sauti yangu
walikuja wanakimbia wakiwa wawili, ile Hali ya
mimi kukumbatiwa na Dominic aisee Derick aliumia
mno ila hakuwa na chaguo akasogea mpaka pale
tulipo, Dominic akaniuliza: kuna nini Najma?
Sikumjibu bali nilimshikilia kwa nguvu, Dominic
alimtazama Derick kisha akasema: anaonekana ana
hofu nyingi.
Derick alisogea karibu na kichwa changu kisha
akaniuliza: Najma it's me Derick, what's problem do
you've?
Niliinua kichwa taratibu nikamtazama huku Jasho
usoni Ikiwa inazidi kutiririka.
Derick: kuna nini?
Nilimuachia Dominic wala sikutaka kumuambia mtu
yeyote kwa kile nilichokiona nilianza kusonga mbele
bila kuangalia nyuma, Dominic alisema kwa sauti ya
Chini: Labda ana Matatizo.
Derick: nahisi.
Tulipowafikia wenzetu walikuwa wametusubiri kwa
hamu, wa kwanza kuja kuniuliza hali yangu alikuwa
ni mdogo wangu Latina ila sikuweza kumjibu
chochote, wote walitaka kujuwa nikipi kimenisibu Ila
niliona iwe Siri yangu tu.
Professor mkuu akasema: jamani tuendelee na
safari kuhusu Najma msaidieni hio mizigo Labda
atakuwa amechoka.
Walichukuwa Yale mabegi kisha mdogo mdogo
tukaanza kusonga mbele, moyo ulinisunta Nikaona
kama ntakaa kimya tukazidi kusonga mbele na
tatizo nimeliona Hali ya kwamba tukirudi nyuma
Hakuna umbali mkubwa maana tulikuwa bado
hatujazama katikati ya msitu vizuri, inaweza kuleta
balaa kwangu, ndipo nikajikakamua na kusema:
msubiri kwanza.
Walisimama ili kunisikiliza, nilipiga hatua kadhaa
nikawafikia kisha nikasema: jamani hapa tupo
hatarini.
Waliendelea kunitazama ndipo Dominic akaniuliza:
una maana gani?
Nikamjibu: nilipokuwa pale Napiga picha ndege
flani niliskia sauti yenye kishindo kikali ambacho
toka nizaliwe sikuwahi kuskia...
Wote walitamani kujuwa nikipi nilichokiona ndipo
nikaendelea kusema: huwezi kuamini nilipogeuka
kwa macho yangu mawili wala sio story Hapana hii
ni true mwenyewe nimeona fuvu imesimama ghafla
ikatoweka.
Wote kwa Pamoja waliachia kicheko cha Utani
ndipo professor mkuu akasema: sio vizuri Najma
kuunda mastory story ya ajabu tukiwa tupo eneo
hili.
Nikasema: wallah naapa turudi nyuma kabla ya
Matatizo hayajatukuta.
Yule mkongo alietuleta akasema kwa kiswahili
chao: usiseme hivo Jolie niko mukukwambia huku
kwa hii poli hio mambo ya namna hio haikuwake
kabisa mie Nilizani uko mkuzungumzia ma Leopard,
ma Antilope, ma Lion Kumbe bitu namna hio
vraiment hii poli yetu Iko bien Sana.
Wote walimuamini mawazo yangu wakayapinga
ndipo Zakayo akamuuliza kwa kuigizia kiswahili cha
kongo: papa eti Jolie Ndo nini?
Akamjibu: Jolie ni mutoto muzuri sana.
Zakayo alinisogelea na kusema: si umeskia mpaka
amekusifia embu Achana na hayo mawazo
yakutishana atakupa zahabu Huyu Jamaa.
Wote walicheka kisha tukaendelea na safari.
Baada ya siku nne bado tu tunafuata ile ramani
tuliopewa iliopo kwenye kikaratasi Kikubwa, Majira
ya saa moja tulikaa sehemu tukatafuta kuni
tukawasha kisha story zikaanza wakulala wakalala
maana mchoko ulikuwa sio wa Kawaida ni ile
kupenda pesa tu, nikiwa nipo na mdogo wangu
Latina nilimuambia: kwa Yale niliyokuambia bado
huwezi kuniamini?
Latina: I'm sorry kweli Sikuamini ila dada unampa
wakati mgumu Sana mwenzio embu angalia
anavyohangaika kila mara anakuangalia mpaka watu
wengine wameanza kugundua.
Nikamuuliza: nani?
Latina: Derick jamani.
Nikamjibu: Yeye si ana mtu wake.
Latina nilipomuambia hivo alinyanyuka akamfuata
Derick alipokaa alipomfikia akamnong'oneza:
samahani Dada anakuita.
Derick hakuamini alinyanyuka kisha akanifuata,
nilishangaa kuona anakuja Ila sikujuwa nikipi
ameongea na Latina, Derick aliponifikia alikaa
pembeni yangu kisha akaniuliza: umeniita?
Watu wote macho kwetu mpaka mwenyewe aibu
ndipo Nikamuuliza: nani kakuambia?
Derick: moyo wangu Ndo umeniambia Ila Najma
Kwa nini unanifanyia hivi?
Nikamjibu: Mimi na wewe Hatuna mahusiano
yoyote.
Baada ya Derick kunitazama shingoni na kuona ile
cheni alionipa nimeivaa aliniuliza: Kumbe bado
unanikumbuka?
Nilipoona ameiona niliishusha Mtandio wangu kisha
nikasema: sio yenyewe.
Derick: kosa langu silijui nilitaka siku ile tukae
tujadiri namna ya kumtoa baba ila sasa wewe
ukakataa angalia tumekuja huku na Yeye bado yupo
jela.
Nikamjibu: ulitaka iwe kama siku zote?
Derick: una maana gani?
Nikamuuliza: hata wewe huniamini kwa kile
nilichowaambia Muda ule?
Derick: Achana na hizo story.
Usiku Sana Kama saa Sita hivi Usingizi uliniishia
nikaamka Baada ya kukumbuka ile fuvu nilioiona
jana, nilipoangalia pembeni nilishangaa kumuona
Derick kalala karibu yangu bila kujifunika chochote
na baridi muda Huo ilikuwa inampiga, nilipojiangalia
Mimi nilishangaa kuona nimefunikwa shuka ya
kimasai ndo nikajuwa Derick alinifunika Mimi ndo
maana anapigwa na baridi, niligeuka kumtazama
usoni nikatabasamu na kujisemea moyoni: Nina
Hofu sana Derick.
Nilichukuwa kile kimasai nikamfunika vizuri kisha
nikakaa huku nikiangalia Mazingira, muda Huo
Joseph kijana Aliekuwa mpole kuliko wote alikuwa
amekaa huku akiwa anaangalia movie kwenye simu
yake pia amevaa headfone maskioni, nilipoona
nimepata kampani Nilisogea pale alipo kisha
Nikamuuliza: tunaweza kuangalia wote?
Joseph alishtuka kisha akatoa headfone na
kuniuliza: bado haujalala?
Nilikaa karibu yake kisha nikasema: Usingizi
Hamna.
Joseph: nikweli unajuwa Mimi Sina imani kama
tutapata kile tunachokihitaji?
Nikamjibu: yawezekana tukapata.
Tuliendelea kupiga story mpaka tukazoweana Haina
Mfano, ukweli upole wa Joseph niliufurahia sana,
tukiwa tunaendelea kupiga story Derick aliamka ile
kuangalia mbele akatuona mimi na Joseph tukiwa
tume share headfone moja huku tukiangalia movie
na furaha tuliokuwa nayo Ilikuwa sio ya Kawaida
mpaka Derick moyo wake ukaanza kumuuma.
Asubuhi ilipowadia watu Waliendelea kujipumzisha
Ila professor Rodrigo alichukuwa begi lake na
kusema: mchaka mchaka Unaanza.
Tulianza kuamka taratibu.
Baada ya muda tukiwa tupo njiani tulishtuka kuona
kitoto cha simba Kidogo kikipita mbele yetu, Nyoyo
zilitutoka zakayo kwa uoga akasema: kama
mmemuona mtoto wa simba basi kaeni mkijuwa
simba yupo karibu, let's go.
Tulianza mbio kama tumewekewa betri kwenye
miguu, tulipofika mbele Kidogo tulijipumzisha
wakulaani Wakaanza kulaani ndipo professor
akasema: Kwani mlijuwa huu msitu hauna wanyama
wakali wakali?
Abdul: aisee nilivyokuja huku sikuagana vizuri Na
mpenzi Wangu mjuwe.
Patrick: na Mimi na mama yangu.
Dominic alitabasamu na kusema: tupumzike kwanza
mengine tutayajuwa kesho.
Tulikaa, Amanda akiwa yupo karibu na Derick
akamuuliza: wewe specialist mkubwa wa nchi
uliruhusiwa vipi kuja huku?
Derick alishangaa na kumuuliza: Kumbe
unanifahamu?
Amanda: Hakuna mwana science asiekufahamu
wewe.
Derick alicheka kwa furaha kisha akasema: kumbe!
Nashukuru.
Mimi nikiwa na Latina tulikuwa tunawatazama
wanavyocheka ndipo Latina akasema: Derick nae
anaboa!
Nikamjibu: ndo alivyo hivyo.
Upande wa professor Rodrigo pamoja na mpenzi
wake Joyce walikuwa zao pembeni huku wakijipiga
selfie taratibu.
Mjeda Dominic alikuwa zake pembeni ametulia,
akiwa yupo hapo akakumbuka nilivyomkumbatia
siku ile alipogeuka kunitazama kwa bahati mbaya
muda Huo na Sisi tulikuwa tunamuangalia Nikajikuta
nimegonganisha nae macho bila kutarajia, aisee
Nilipigwa shoti ya umeme machoni nikaamua
kushusha macho taratibu.
Tukiwa tupo hapo tulishtuka kuona Zakayo na Abdul
Pamoja na Patrick wanakuja wanakimbia kwa kasi,
ile Hali ya wao kuja wanapiga kelele nikaunganisha
ile fuvu nilioiona siku ile aisee nilivomshika mkono
Latina na kuanza kukimbia nae sikujuwa, watu hapo
kutokana na ile yao ya kutokuamini kila kitu
Waliendelea kuwatazama kwa mshangao, Patrick
aliwapita moja kwa moja bila kusimama Ila Zakayo
na Abdul walisimama wakiwaomba wale waliokaa
wanyanyuke wakimbie, wakiwa bado wanajilemba
lemba mara Wengine viatu vyangu, wengine simu
yangu, Wengine begi yangu Ipo wapi huwezi
kuamini jeshi la sokwe wenye miili mikubwa
mikubwa Kama ishirini hivi ilitia timu, aisee wenzetu
ile kushangaa shangaa waliwekwa Kati wote
nikimaanisha walizungukwa na sokwe wale.
Unahisi nini kitatokea!
Usikose mkasa huu!
 
SEHEMU YA 06
TULIPOISHIA: Patrick aliwapita moja kwa moja bila
kusimama Ila Zakayo na Abdul walisimama
wakiwaomba wale waliokaa wanyanyuke wakimbie,
wakiwa bado wanajilemba lemba mara Wengine
viatu vyangu, wengine simu yangu, Wengine begi
yangu Ipo wapi huwezi kuamini jeshi la sokwe
wenye miili mikubwa mikubwa Kama ishirini hivi
ilitia timu, aisee wenzetu ile kushangaa shangaa
waliwekwa Kati wote nikimaanisha walizungukwa na
sokwe wale.
SONGA NAYO!
Upande wetu tukiwa tunakimbia bila kujuwa nikipi
kimetokea sauti ya Patrick tuliisikia akitusimamisha,
nasi tukaona kusimama, alipotufikia Nikamuuliza:
kuna nini huko?
Patrick: sokwe Kama Elfu moja walikuwa
wanatukimbiza hivi niongeapo wale wazembe sijui
kimewakuta nini huko.
Mimi na Latina Tulishtuka mno kisha nikasema:
kama sokwe ni wengi Sana na bado Sisi hatujaskia
kelele za wenzetu basi huko wanachezea kichapo
twende kutoa msaada.
Tulijadiri namna ya kutoa msaada tukapata suruhu,
Baada ya muda tulikuja Mimi nilikuwa nimeshikilia
tawi la mti uliokauka Ila Kidogo majani yake
yalikuwepo huku tawi lile likiwa linawaka moto
kweli, Latina nae vile vile hata Patrick, ndipo
tukatokea pale sokwe na wenzetu walipo tukaja
Kama vile tumevuta bangi zisizo za kawaida kwa
kasi ya kufa mtu huku tukipiga ukunga:
aaaaaaaahhhhhhhhh.
Mbio zetu, kujiamini kwetu pia na fujo zetu
ziliwafanya sokwe wale waingiwe na uoga ukija
kuangalia tulivyokuwa tunakuja na ule moto ndo
kabisa sokwe wale wakajikuta wanakosa uvumilivu
wakatoka hapo nduki, na Sisi nyuma tukadata
tukawapita wenzetu tuwafukuzia sokwe wale mpaka
wakatokomea mbali ndo tukaona kurudi, tulipofika
pale tulipowaacha wenzetu huwezi kuamini
hatukukuta hata mtu hata mmoja aisee Tulicheka,
haraka tukachukuwa simu walizoziacha pia na begi
zao kisha tukaanza kuwatafuta.
Tukiwa tunawalalamikia ndugu yangu huwezi
kuamini kama vile sasa tunapuliza filimbi ya kuwaita
simba walitokea mbele yetu simba jike wawili na
dume mmoja alioshiba nyama za swala maana
kwenye msitu Huo watu adimu sana kuwapata,
tumbo ya Latina ilishuka ikawa ndogo Kama mpiga
mazowezi vile, misuli nayo ikasema tumechelewa
nayo ikajituna freshi, Juu yangu kulikuwepo mti flani
mrefu kiasi, ndugu yangu Latina alinirukia sekunde
chache nikashangaa kumuona Juu ya mti ule, ile na
geuka kumuangalia Patrick sikujua saangapi kafika
Juu ya mti uliokuwa nyuma yangu na muda Huo
simba jike mmoja alikuwa Chini ya mti alipokuwa
Latina na mwingine kwa Patrick Mimi nikabaki hapo
sasa na mzee baba simba dume.
Macho yangu kwake nayo macho kwangu, Kawaida
ya simba ukiwa imara nae anatulia akikusomea
Ramani huku akinghuruma taratibu ili kukutisha,
machozi sikujuwa muda gani yalanza kunitiririka
mashavuni, kichwani nikaingiwa na kichaa cha
kusema nirudi nyuma tu nikimbie zangu kama kufa
tayari Mimi maiti, wee saangapi sijatupa mizigo
yote nikaanza kukimbia, nae simba akasema yes
wewe wangu, nilipiga kama hatua ngapi simba
alikuwa tayari amenifikia na kuushika mtandio
wangu kwa nyuma, niseme bahati nzuri au mbaya
ile Yeye kanishika mtandio Na mimi nilikuwa
nimefika eneo mbaya yenye kishimo chenye Kina
kirefu nikajikuta nadondokea humo na simba
nikamuachia mtandio tu.
Simba alihangaika kuona kitoeo chake
kimemponyoka kizembe akaanza kuzunguka
zunguka Juu huku akiniangalia vizuri, muda Huo
nikiwa ndani ya Shimo lile macho yangu kwake
kama vile tunaviziana, Dua Za kila Aina wallah
niliomba Mpaka nikaanza kuomba msamaha kwa
Muumba wangu anisamehe zambi zangu zote,
nikiwa nipo hapo ndugu yangu nilishtuka kuskia
mlusi flani karibu na skio yangu, kwanza nikaganda
huku nikiskilizia kwa umakini, taratibu nikageuza
shingo ili kuangalia je ni nini kinachoendelea! aisee
uso kwa uso, macho kwa macho na nyoka Aina ya
Kobla, nyoka huyo ni mkali kuliko nyoka wote
unaowajuwa, nilijifikiria Imekuwa kuwaje Mpaka
Kichwa chake kikawa sambamba na kichwa changu
namna hio hali ya kuwa nimesimama, taratibu
nikashusha mboni tu Hapana kichwa chote wee
nilikuwa nimepooza, ile kuangalia Chini ukubwa wa
nyoka yule ulinipagawisha Nikajikuta Napiga
ukunga, ile Hali ya kupiga kelele bila kujitambua
nilijikuta naipiga mkono nyoka ile sehemu mbaya
maeneo ya shingoni nikaibamiza kwenye ukuta wa
udongo bila kujuwa, nikaja kushtukia damu
inanirukia usoni, sikujuwa nikipi kinaendelea
niligeuka kuangalia alipo nyoka Yule, Sikuamini
kumuona nikiwa nimemuua ajabu amedondokea
Chini, aisee hapo sikuweza kuvumilia tena nilizimia
taratibu.
Upande wa Latina hata kumkumbuka dada yake
alikuwa hakumbuki kwa Muda Huo alijiona Yatima
nikimaanisha alizaliwa mwenyewe hivo ndivo hakili
zake zilimuambia, isikukute Upo Juu ya mti Chini
simba nae katulia Mpaka kulala akikusubiri utoke
Juu, hata upande wa Patrick Ilikuwa hivo hivo,
upande wangu simba dume hakukata tamaa kabisa
aliendelea kukaa pale akinisubiri kwa hamu.
Muda Huo mwanajeshi Dominic alifika akatoa
bastola mfukoni kisha akapiga lisasi Juu baada ya
kuona simba wale, ule mlio uliwashtua Sana wale
simba wakajikuta wanakosa uvumilivu wakatoka
hapo nduki.
Dominic aliwashusha Kina Latina ndipo akaanza
kuwauliza kuhusu Mimi Ila Hakuna aliemjibu maana
hakili nikama zilikuwa zimeruka, Kama dakika nne
kupita walianza kujitambua ndipo Dominic akauliza:
mwenzenu yupo wapi?
Wakamuuliza: mwenzetu nani?
Dominic alimgeukia Latina na kusema: dada yako?
Latina bila kujielewa akasema: Kwani mi nina dada?
Dominic aliishiwa na kusema: dada yako Najma
yupo wapi?
Ndipo Latina hakili zikarudi akasema: jamani dada
yangu yupo wapi?
Dominic: ndo nakuuliza wewe.
Latina aligeuka akawa anatafuta huku akisema: mara
ya mwisho nimemuona maeneo hayo Sikumbuki nini
kiliendelea Kwani kuna nini mbona sielewi?
Dominic akajuwa Huyu alipagawa Baada ya tukio,
muda Huo Patrick alikuwa kimya hata alikuwa
haelewi nini kinaendelea.
Dominic alipokumbuka Yule simba dume alipo kuwa
muda ule akaamua kusogea ili kuangalia pale Yule
simba alikuwa amefuata nini, alipofika ndo akaona
Shimo kuangalia ndani akashangaa kuniona ndani
nikiwa Nimelala na nyoka pembeni yangu Ndo
akajuwa basi Mimi tayari nimeshakufa, aliniita kwa
sauti ya majonzi ila sikuweza kuzinduka.
Latina aliponiona nimetulia alianza kulia akihisi
Labda sipo tena duniani.
Dominic kwa kuwa Yeye alikuwa mwanajeshi alizijua
mbinu za kunitoa mle, iwe ni mekufa au bado,
alitafuta mti mlefu akaungiza ndani ya Shimo lile
kisha akaanza kunitikisa ili kuhakiki je Nikweli sipo
tena duniani, ile Hali ya mimi kuguswa na mti ule
nilizinduka na kupiga kelele, Patrick na Latina
walifurahi sana kuona Mimi bado mzima.
Dominic alinituliza baada ya kuona nimedata, haraka
akaenda kutafuta kamba mwishowe wakanitoa ndani
ya Shimo lile, tulikumbatiana na Latina kwa furaha
ndipo Dominic akatuambia: fanyeni mpango tutoke
eneo hili.
Patrick: wenzetu wapo wapo?
Dominic: twende huku wametongoja.
Tulianza safari nilipopiga hatua kama kumi
nilidondoka Chini maana muda ule nilipodondokea
ndani ya Shimo lile niliteuka mguu, na kutokana
moyo ulikuwa bado upo Juu Juu nilivyotolewa
sikuskia maumivu yoyote ila kwa kuwa damu
imetulia ndo maumivu yakaamka.
Wote walinikimbilia wakaniuliza hali yangu
nikawajibu kwa sauti ya maumivu: mguu wangu
jamani.
Latina: jikaze basi.
Patrick: utaweza kutembea?
Walinishika mkono nikasimama taratibu, nilipojaribu
kupiga hatua tena sikuweza maana maumivu
yalikuwa makali ndipo Dominic akachuchumaa
mbele yangu na kusema: panda mgongoni.
Nilishtuka na kumtazama Latina.
Latina alitabasamu na kusema: panda.
Nikamjibu: aaahhh! wee! Mwaya mjeda I'm alright.
Dominic alisimama na kuniuliza: utaweza?
Nikamjibu: eeeehhh ntaweza mbona.
Dominic: OK twende.
Ile Kuinua mguu tu nikapiga kelele ndipo Patrick
kwa sauti ya hasira akaniambia: si unaona sasa?
Nikamjibu: ntajaribu.
Dominic: panda mgongoni usitupotezee muda.
Wote walinikazia nipande mgongoni, sikuwa na
namna nilipanda kwa aibu.
Tulipowafikia wenzetu walipokuwa wametusubiri
aisee walikuwa wamepondeka na kichapo cha
sokwe wale, Derick aliponiona Nipo kwenye
mgongo wa Dominic moyo ulimuuma sana,
nilipomtazama niligundua ameumia ila nikapotezea,
aliponiweka Chini tu, aisee huwezi kuamini kilitokea
kitu juu kikadondoka Chini, watu wote wakapiga
kelele huku wakitazama kitu kile.........
Unahisi nini kitatokea!
Usikose mkasa huu!
 
SEHEMU YA 07
TULIPOISHIA: Tulipowafikia wenzetu walipokuwa
wametusubiri aisee walikuwa wamepondeka na
kichapo cha sokwe wale, Derick aliponiona Nipo
kwenye mgongo wa Dominic moyo ulimuuma sana,
nilipomtazama niligundua ameumia ila nikapotezea,
aliponiweka Chini tu, aisee huwezi kuamini kilitokea
kitu juu kikadondoka Chini, watu wote wakapiga
kelele huku wakitazama kitu kile.........
SONGA NAYO!
Tulipoangalia vizuri kilikuwa ni kitoto cha Nyani
kilitoka juu kikadondokea Chini, waschana wote
waliogopa Ila wanaume Walitupa moyo, professor
mkuu alikasogelea katoto kale ka Nyani akaanza
kukashika shika huku akikapa pole ndipo
akatuambia: mmemuona mama yake kule...
Tuliangalia juu ya Mti uliokuwa pembeni yetu
tukaona Nyani dike akiwa anamtazama mwanae
kwa Hofu ndipo professor mkuu akaendelea
kusema: alikuwa anamfundisha mwanae jinsi ya
kuruka miti sasa mwanae bado hajazowea matokeo
yake Ndo haya.
Professor aliomba tumpishe Nyani Yule aje
kumchua mwanae, Nyani Yule alipoona tumempisha
alitoka juu ya Mti ule taratibu akaanza kusogea pale
tulipo, alipoona hatuoneshi hali yoyote ya Kutaka
kumzuru alimchukua mwanae akaondoka zake.
Joyce alishusha pumzi kwa kishindo Mpaka kila
mmoja akacheka.
Tulikaa hapo wakucheza Wakaanza, wakupiga story
wakaendelea.
Nikiwa nipo mwenyewe huku nikimfikiria mama
yangu mgonjwa ambae nimemuacha kwenye
mikono ya watu ambao sio ndugu zangu nilikuwa
nahofu Sana nikihisi Labda hawatomjali ipasavyo.
Derick alisogea pale nilipo akanisalimia na kusema:
mguu vipi?
Nilimtazama na kumjibu: nipo sawa Kidogo.
Derick alikaa kisha akatoa dawa flani ya maji maji
akaomba anifanyie huduma ya kwanza, nilimruhusu
akaanza kunipaka dawa ile.
Muda Huo professor Rodrigo alianza kutupiga story
ilivyokuwa muda ule sokwe walipowavamia, ndipo
Zakayo akasema: naskia huu msitu unasifika kwa
sokwe wakubwa kama wale.
Professor mkuu: huu msitu una wanyama wengi
wakali ila tumuombe Mungu.
Hamisa alimfuata Abdul akamuomba wakapiga nae
picha pembeni ya maeneo Yale ndipo Patrick
akacheka na kusema: Subutu ndugu yangu kwasasa
utakuja unakimbizwa na tembo.
Abdul: siwezi kufanya huo ujinga aende mwenyewe.
Chande alinyanyuka na kusema: achana nao waoga
tu, twende zetu.
Waliongozana kwa Pamoja.
Chilunga muda Huo alikuwa amekaa na Sofia huku
wakipiga stori.
Chilunga: hii kazi ambayo mumekuya kufanya iko
ngumu Kidogo alakini muko na asilimia mia ya
kufanikisha.
Sofia: kwanza niambie kuhusu zahabu naskia huku
kwenu zinapatikana Sana!
Chilunga: kwa mutoto muzuri Kama weye ni rahisi
kupata.
Sofia alitabasamu kwa maringo Baada ya kusifiwa
ndipo akamuuliza: una maana gani na wewe!
Chilunga: shie vijana wakongo tuko na makuta ya
mingi sana.
Sofia: makuta ndo nini?
Chilunga: madolale.
Sofia: wow! Vipi kuhusu zahabu?
Chilunga: tuko nayo ya mingi, ni weye tu.
Sofia alicheka na kusema: mimi tena kiaje!
Chilunga: Ukisema niko tayari Mbona mimi
mwenyewe ntakupashiaga.
Sofia: I'm sorry kupashiaga ndo nini?
Chilunga: it's mean I'll give you.
Sofia aliachia kicheko kikali Mpaka wote
wakamuangalia, ndipo akatuambia: Jali yenu.
Tulimpotezea tukaendelea na mambo yetu.
Chilunga: banamuke bote banakusikilia wivu.
Sofia: hata sijui Kwanini.
Chilunga: si juu uko mkuongea na mtu mkubwa.
Sofia alitabasamu na kusema: kweli?
Chilunga: Eee bale ba filles bote ni bambaya ndo
maana siongei nabo.
Sofia: filles ndo nini?
Chilunga: banamke.
Sofia: Mbona wewe Upo unaongea na mimi
haliyakuwa Nipo wa Kawaida?
Chilunga: shiweji ongea na fille mbaya weye
kuongea na mie juwa uko wa bien zaidi yao utapata
madolale mama!
Sofia raha ilimuua akamuuliza: Kwani Yule namzidi?
Alimnooshea kidole Amanda maana Yeye alikuwa
mrembo tena mwenye pesa ndipo chilongo
akamuambie: eeee! mbona Iko wa Kawaida Sana
mbele yako mamaa! Yule si chochote kwanza Iko
mukokuogopa sana njo maana Hawezi kujongea
ulipo weye, Nimeshakuambia weye ni Jolie kuliko
bote hapa.
Sofia aliendelea kutabasamu kwa furaha, upande wa
Abdul na zakayo story ziliendelea.
Abdul: Duh! Sofia anaonekana amemuelewa sana
Jamaa.
Zakayo: sound za wa Kongo unaziweza.
Abdul: Demu bado tupo DSM nimemuomba namba
kanitolea nje ila Huyu Jamaa wanacheka nae Mpaka
siamini kama Ni yeye.
Zakayo: kama ulikuwa unamfukuzia huyo manzi
mteme tu maana huwezi kupata ubavu wa ku share
mschana na mkongo.
Abdul: una maana gani?
Zakayo: wanajuwa kupetepeti sana Hawa majaa sijui
waliumbwa je!
Upande wa Chilunga story ziliendelea mwishowe
akamtongoza.
Sofia kwa furaha akasema: Aku mi siwezi! kwanza
Nyinyi wa Kongo mnaoa sana.
Chilunga: banafanyaga hivo juu habayapataga
bamomo saa weye, ngoyela Nikwambie Hakuna
kijana wa hapa Kongo au wa dunia nzima anaweza
pata mrembo ambae ameumbika kama weye Halafu
akamuowea mwanamke wa pili juu Haiwezekani
mama!
Bako mukuoae ba bimdogo juu babimkubwa ni
babaya saa hibi bibinti hapa, umenielewa cherie!
Usiwe na probleme Ntakupa ma diamond, ma or ma
dollar ya kimarekani utaishi saa malikia Elizabeth.
Sofia kwa maneno Yale alijikuta anamkubali
Chilunga mia mia.
Muda Huo Dominic alikuwa bize anaimalisha ulinzi
kama Kawaida ya majukumu yake.
Upande wetu Derick alimaliza na kuniambia: utulie
Kama saa nzima.
Nikamjibu: Asante.
Derick alinitazama usoni na kuniuliza: Yule Jamaa
Kwa nini anakujali sana?
Nikamuuliza: Nani?
Derick: Dominic.
Nikamuuliza: Kwa nini unaniuliza?
Derick: by the way! why ulikuja huku?
Nikamuuliza: na wewe Ulianza anzaje kuja huku na
uprofeshino ulionao?
Derick: Nimekuja huku kwa ajili ya kuokoa
mamilioni ya watu.
Nikasema: hata mimi nipo hapa Kwa ajili ya mama
na baba.
Derick: mengi nahitaji kuongea na wewe ila nafasi
sipati.
Nikamuuliza: kama?
Derick: I love you.
Nilitabasamu nilipomtazama Amanda niligundua
hajafurahia kuniona nikiwa nipo na Derick ndipo
nikamuambia: mfuate Rafiki yako ana upweke.
Derick alipomtazama Amanda akagundua kweli
anajiona mpweke sana, aliniacha hapo na kumfuata
Amanda.
Baada ya masaa kadhaa hatukuweza kusonga tena
maana wengi walikuwa na maumivu kutokana na
kichapo kile cha sokwe, hivo wakaomba tuweke
makazi hapo ikiwezekana kesho tutaanza safari.
Latina alinifuata na kuniambia: dada Nipe ruhusa
nikapige picha ndege.
Nikamjibu: Hapana kaa hapa.
Latina: please dada sichukui muda nawafuata Kina
Hamisa.
Nikamjibu: Hapana Latina.
Latina: unanibania sasa!
Nikamjibu: basi nenda ila usikawe.
Latina alifurahi kisha akanikiss na kuondoka na
simu yake tu.
Tukiwa tupo hapo nilijaribu kunyanyuka kwa bahati
nzuri nikaweza aisee dawa ya Derick ilinisaidia
sana.
Professor mkuu akasema: nendeni mlete kuni za
usiku si mnaona giza inaanza kuingia.
Watu wote walipotezea ndipo nikasema: Ntaenda
Mimi.
Professor mkuu: utaweza mwenyewe?
Nikamjibu: ndio.
Professor mkuu: Chagua mtu Mwende nae.
Nilimchangua Joseph maana Kidogo yeye nilikuwa
nimeanza kumzowea.
Tukiwa tupo mbali Kidogo na hapo, Tulianza
kucheza mimi na Joseph taratibu.
Upande wa Latina alipoona muda unazidi kwenda
alianza kurudi alikotuacha, kabla hajapiga hatua tano
alishangaa kuona pembeni yake kuna kimvuli cha
mtu taratibu akageuka kuangalia akihisi Labda kina
Hamisa wamekuja Ila cha ajabu kimvuli Kile
kilitoweka na mtu yule hakufanikiwa kumuona, Hofu
ilimtawala mdogo wangu Latina akaanza kuita kwa
sauti ya uoga: dada Hamisa ni wewe? We Chande
ni Nyinyi Mpo hapo?
Ukimya ulitawala kwa sekunde kadhaa, ghafla
akashangaa kuona fuvu la mtu likiwa lipo mbele
yake, kuongea alishindwa vile vile na kupiga kelele
alishindwa, akiwa anajiuliza afanye nini kwa muda
ule fuvu lile lili..........
Unahisi nini kitatokea!
Usikose mkasa huu!
 
SEHEMU YA 08
TULIPOISHIA: Ukimya ulitawala kwa sekunde
kadhaa, ghafla akashangaa kuona fuvu la mtu likiwa
lipo mbele yake, kuongea alishindwa vile vile na
kupiga kelele alishindwa, akiwa anajiuliza afanye
nini fuvu lile lili..........
SONGA NAYO!
Latina akiwa anajiuliza afanye nini kwa muda ule
fuvu lile lili muingia ndani ya mwili wake
ikampelekea kupiga kelele mara moja (aaaaaa).
Upande wangu sauti ya Latina niliiskia freshi moyo
wangu ukalaluka nikadondosha kuni Chini na
kusema: umeskia?
Joseph: eeee Kwani Kulikoni?
Nikamjibu: nimeskia sauti inatoka huku twende
kwanza.
Tuliacha kila kitu Chini tukaanza kufuata sauti
tulipoisikia muda ule, tulipofika eneo lile ambapo
Latina alikuwepo hatukuweza kumuona Ila Joseph
aliogota simu na kuniuliza: sio simu ya mdogo
wako?
Nilishtuka mno Baada ya kuona simu ile, kwa sauti
ya Chini nikasema: Kumbe Hisia zangu zilikuwa
zipo sahihi!
Joseph: turudi kule walipo wenzetu kwanza.
Kabla hatujachukuwa uamzi wowote Latina alitokea
nyuma yetu, nilipogeuka kumuangalia baada ya
kusikia mchakacho Sikuamini kumuona maana
macho yake yalikuwa yamebadirika rangi, ukweli
hali ya mdogo wangu kwa muda ule ilikuwa tofauti
mno.
Moyo wa huruma uliniingia nikaanza kumsogelea
huku nikisema: imekuwaje my dear!
Joseph baada ya kugundua kuwa Latina ninaemjua
Kama mdogo wangu sie kwa muda ule alinifuata
haraka na kunisukuma ili nisimshike, ile Hali ya
mimi kudondokea Chini niligeuka kumtazama
Joseph na kumuuliza: Ndio nini sasa!
Joseph akiwa anamtazama Latina Akanijibu: huyu
sie tukimbie!
Kabla Joseph hajapiga hatua yoyote huwezi kuamini
Latina alimuwahi na kumshika kwenye koo Jambo
ambalo upande wangu lilinifanya nizidi kushangaa,
vidole vya mdogo wangu vilikuwa na kucha ndefu
mno.
Latina akiwa anamnyoga Joseph damu zilianza
kuchirizika shingongo mwa Joseph maana aliingiza
kucha Zile kwenye kolomeo.
Baada ya mimi kuona atakuja kumuua na mimi nipo
naangalia nilinyanyuka ili kwenda kumzuwia, kabla
sijamfikia Latina alinigeuzia macho akanitazama
jicho mbaya Mpaka mwenyewe nikaogopa.
Muda Huo Huo Hamisa na Chande walifika,
walipoona tukio lile walishtuka kwa mshangao
mkubwa huku wakiwa wamekodoa macho,
haikuchukuwa muda wenzetu nao wakafika eneo lile,
kila mmoja alishtuka mno Baada ya kuona macho
ya Latina, tukiwa tunatafuta njia ya kumzuia ili
asimuue, Latina alimrusha pembeni kwa nguvu
zisizo za Kawaida ishara tayari Joseph hatupo nae
tena kisha akasema kwa sauti nzito ambao kila
mmoja hakuamini kuskia sauti ile: ntaua mmoja
baada ya mwingine.
Hapo hapo Latina akapotea, aisee ile Hali ya kuona
mwenzetu anauwawa mbele yetu na Latina akapotea
baada ya kutupa vitisho vikali sote tulikimbia huku
tukipiga kelele.
Baada ya dakika kadhaa Tulifika eneo lile
tulipokuwa tunataka kuweka makazi yetu kwa Muda
kila mmoja akiwa anahema vibaya.
Moyo wangu haukuweza Kutulia, nilijiuliza mengi
kuhusu mdogo wangu ila sikupata picha, wenzangu
walianza kulijadiri swala lile Mpaka wakanisogelea
ili kuniuliza.
Patrick: Najma imekuwaje mbona hatuelewi?
Nilianza kulia huku nikisema: sijui nini kimemkuta
mdogo wangu, Mimi mwenyewe sauti yake Ndo
ilinishtua tukaongozana na Joseph maskini bila
kujua kuwa mwenzangu nampeleka eneo hatari
Sana.
Amanda kwa presha Akaniambia: funga bakuli wewe
na mdogo wako mnayajua haya, Haiwezekani
umchague Joseph peke yake na watu hapa tulikuwa
wengi, yeye tu ndo ukamchagua inaonekana ni plani
zenu, Kwani Yule si ni mdogo wako?
Maneno ya Amanda yaliniumiza mno ukija kuangalia
hata mimi pia sielewi ni kipi kimemkuta Latina,
nilikosa namna ya kujitetea nikaendelea kuwaangalia
huku nikilia mno.
Sofia akiwa Analia akasema: jamani mwenzenu
naogopa, wallah Najma wewe na mdogo wako
mnalijua hili.
Kabla sijajieleza chochote baadhi walianza
kunilaumu wakimaanisha Mimi na mdogo wangu
tumeamua kuwazunguka.
Hasira ilinipanda kwa sauti ya Juu nikawanyamanzis
ha: basi!!!!
Wote waliniangalia kwa umakini, ndipo nikasema
huku nikiwa nalia: ndo nini kunilaumu? hivi niulize
Kati Kati yenu Nani anamaumivu kunizidi mimi?
Yule ni mdogo wangu na mtu aliefariki ni Rafiki
yangu mnapo niambia niseme ukweli kuhusu hili je
niseme nini? Moyo unaniuma mno sijui Kwa nini
kipenzi changu amebadirika kuwa namna ile.
Amanda Akanijibu: usijitetee kila kitu wewe unajua.
Professor mkuu alipoona nalaumiwa sana alimpiga
kofi Amanda Mpaka kila mmoja akashangaa.
Mimi sikujali wanachokifanya nilitupa simu Chini,
nikavua koti niliokuwa nimevaa, taratibu nikaanza
kuvua viatu huku kila mmoja akiwa ananishangaa,
Nilipomaliza nikasema: Ntaenda kumtafuta
mwenyewe acha niwape amani.
Nilitoka hapo nikiwa nakimbia huku nikilia mno,
Derick alipoona vile hakutaka kuniacha niende
alinifuata mpaka akanifikia, alinishika mkono kisha
akanivuta Na kunikumbatia kwa nguvu.
Moyo ulizidi kuniuma mno, nikazidisha kilio Mara
dufu, Derick kwa sauti ya Chini akaniambia: usijali
mambo yatakuwa vizuri.
Nikiwa nalia Nikamuuliza: mdogo wangu nini
kimemkuta?
Upande wa huku professor mkuu akiwa anatuangalia
akawaambia wenzie: mkimgombeza namna ile
mnataka afe au? Kwa hali alionayo mnaona kweli
Yeye ndie kapenda iwe vile? msimulaumu tena hapa
Kikubwa Nikujua namna ya kulihendo tatizo hili.
Asubuhi na mapema wote walikuwa bado wamelala
Ila Mimi Usingizi sikuweza kuupata, kila nikimfikiria
mdogo wangu nilikuwa sipati picha, kilichonitesa
zaidi nilipokumbuka alivyonikiss, nilihisi Labda ile
tabasamu ndo Ilikuwa ya mwisho upande wake,
kimoyo moyo nikawa najisemea huku machozi
yakiwa yananibubujika mashavuni: mama na baba
watanichukuliaje kama sintorudi na wewe? Labda
huko uliko mdogo wangu baridi inakusumbua sana,
I'm sorry my love nimeshindwa kukuwekea ulinzi wa
kutosha.
Nilijikumbata huku nikiendelea kulia, muda mfupi
professor ambae anajiita husband aliamka
aliponiona Nipo kwenye dimbwi nzito la mawazo
alisogea pale nilipo akanipa moyo akisema: hatuna
muda tutakuwa tumefika, usijali mambo yatakuwa
sawa.
Nikamuuliza: mdogo wangu vipi?
Professor: hata Yeye pia atapatikana.
Watu wote waliamka wakaanza kujadili baadhi
tusonge Wengine turudi nyuma ndipo Dominic
mwanajeshi akasema: hapa tupo kama uwanja wa
vita, Hakuna kurudi nyuma tuendelee kusonga mbele
lazma swala hili tulimalize kwasababu hata
tukisema turudi nyuma Hakuna kitu cha kukomboa
Ndo hivo tumewapoteza wenzetu na hapa tulipo
tupo KatiKati ya msitu kwahio nawaombeni
tuendelee na safari.
Professor mkuu akasema: Nikweli kila Jambo lenye
kheri lazma changa moto zipatikane yawezekana
kwenye hizi balaa ndo mafanikio yanatokea kwahio
niwaombeni tutulize Nyoyo zetu na Tuzidi kuomba
Dua.
Upande wangu nilikuwa nimelishikilia begi la Latina
huku nikilitazama kwa umakini kama vile
sintomuona tena.
Hamisa akiwa Analia akasema: ukweli Mimi
naogopa sana nisiwe muongo Huo Ndo ukweli
wangu naombeni nirudi zangu nyuma.
Professor Rodrigo akamjibu: hapa Hakuna maswala
ya kurudi nyuma umeshaambiwa na Labda hauoni
kama Hakuna mawasiliano yoyote!
Joyce Rafiki yangu alipoona bado mimi hakili
hazijakaa sawa Zidi ya mdogo wangu alinisogelea
na kunipa maji ya kunywa, Nilichukua nikanywa na
kumuuliza: atapatikana Latina?
Joyce: usijali lazma apatikane.
Patrick alimsogelea Chilunga alipokuwa amesimama
na kumuambia: nisaidie simu yako dakika mbili
maana naona hapa kilevi kilichopo ni muziki tu.
Chilunga alimpa simu yake kisha Patrick akasogea
sehemu yake huku akiwa anatafuta Miziki ya kikongi
asikilize, alivaa headfone akaanza kusikiliza muziki
taratibu huku macho akiwa ameyaelekeza kwenye
simu.
Muda Huo Huo Latina akiwa ametapakaa damu
mwili mzima, uso wake ukiwa haugunduliki tena
alitokea nyuma ya Patrick Ili kumuua na yeye pia,
watu wote walipomuona aisee Hakuna aliekimbia na
begi, baadhi walikimbia bila viatu, mimi ile
kumuona mdogo wangu nilianza kumfuata taratibu
huku nikisema: usifanye hivo ni mimi Najma dada
yako.
Joyce hakutaka nimfikia Latina alianza kunivuta huku
akiniomba nisifanye chochote ila Mimi
nikang'ang'ana, Joyce alipoona namzingua alinipiga
bonge la kofi na kuniambia kwa hasira: sio Latina
we mshenzi jitambue eee.
Nilijitambua tukatoka hapo mbio, Patrick bila
kujuwa hili wala lile kwasababu ya muziki kuwa
mnene kwenye headfone alizokuwa amevaa
aliendelea kuinjoi bila kujuwa kuwa wenzie
wamekimbia Amebaki mwenyewe na kizaa zaa kipo
nyuma yake.
Unahisi nini kitatokea!
Usikose mkasa huu!
 
SEHEMU YA 09
TULIPOISHIA: Nilijitambua tukatoka hapo mbio,
Patrick bila kujuwa hili wala lile kwasababu ya
muziki kuwa mnene kwenye headfone aliendelea
kuinjoi bila kujuwa kuwa wenzie wamekimbia
Amebaki mwenyewe na kizaa zaa kipo nyuma yake.
SONGA NAYO!
Latina kwa nyuma alikuwa anamsomea ramani
Patrick.
Patrick alipoangalia mbele hakuweza kuona mtu
yeyote ndipo akajisemea moyoni: wameenda wapi?
Latina nyuma alinyoosha mkono ili kushusha kucha
zake shingoni mwa Patrick.
Patrick bila kujielewa Alichomoa headfone mziki
ukaendelea kulia kupitia simu, ajabu nyuma yake
akaskia mchakacho unazidi akaanza kujiuliza nini
kipo kinachezesha majani Chini, taratibu akageuka
kuangalia aisee nusu kuzimia uso kwa uso na
Latina akiwa hatambuliki tena kama ni mrembo,
kilichomshangaza zaidi Patrick nikuwa Latina
alikuwa anacheza lumba ile iliokuwa inapigwa
kwenye simu ya Yule mkongo Chilunga ambayo kwa
muda Huo Patrick ndo Alikuwa nayo.
Patrick baada ya kuona vile hakutaka kupoteza
muda aliachia simu ikadondoka Chini kisha
akakimbia nduki.
Upande wetu wasichana wote walikuwa wanalia,
wanaume nao walikuwa wanalaani sana, kiukweli
lawama zile walizielekeza kwangu, moyo uliniuma
nikatamani kuwaeleza kuwa sio mimi ila
ikashindikana.
Tukiwa tupo hapo kwa mbali tulimsikia Patrick
akiwa anapiga kelele, fasta Dominic akamfuata,
dakika kadhaa akaja nae, hakili za Patrick ziliruka
dakika mbili kila akiulizwa hili anajibu tofauti ndipo
Rodrigo akasema: mpeni muda kwanza.
Tulikaa chini kila mmoja hakutaka kumuongelesha
mwenzie kwa muda huo.
Baada ya masaa kadhaa tulinyanyuka na safari
ikaanza.
Joyce akiwa yupo na mpenzi wake Rodrigo
alimuuliza: Najma si atageuka chizi pindi jambo hili
likizidi?
Rodrigo: mimi na wewe ndo tulimshawishi umeona
madhara yake!
Joyce: najilaumu sana.
Patrick kwa nyuma akawaambia wenzie ambao ni
Zakayo na Abdul: Latina alicheza muziki muda ule.
Sote tuligeuka kumuangalia maana muda wote
alikuwa hajazungumza chochote kuhusu alichokiona,
haraka tukarudi nyuma na kumsogelea ili atuambie
vizuri.
Patrick alituadithia kile alichokiona ndipo Chilunga
akasema: labda hio mizimu inapenda sana muziki
wa kwao.
Joyce akamuuliza Patrick: alicheza kabisa?
Patrick: nimemuacha anacheza mpaka sasa hivi.
Tulijiuliza nini tufanye ila hatukupata majibu.
Baada ya siku mbili kupita tuliendelea na safari ila
kwa bahati nzuri hatukuweza kumuona Latina tena
kilichotusumbua ni baridi na Mvua isiokata.
Tukiwa tupo sehemu tumejipumzisha, waangalia
ramani walikuwa bize kuangalia tumebaki na safari
ya kiasi gani.
Nikiwa nipo bize naangalia ndege wanavyoruka ruka
Derick alisogea nilipo na kusema: usihofu lazma
Latina atapatikana.
Nikamjibu: amekuwa kitu cha ajabu mno halafu
nakumbuka alisema ataua mmoja baada ya
mwingine.
Derick: tusiliamini sana jambo hilo, sipendi kukuona
ukiwa kwenye hali hio ukweli mimi nakupenda.
Nikamjibu: tatizo wewe haupo siriazi.
Derick: kwanini?
Muda huo tuliambiwa safari iendelee, ndipo tulikata
maongezi yetu tukaanza safari.
Tukiwa tupo njiani, Hamisa na chande walikuwa
mbele ndipo zakayo akawauliza: mbona mpo mbele
yetu?
Chande: eeee wanyuma ndo wanapataga tabu siku
zote.
Abdul: kwahio mnatugeuza chambo si eti.
Wote walicheka huku wakiendelea kutaniana, tukiwa
tunazidi kusonga mbele huwezi kuamini mbele yetu
Latina alikuwa amesimama kama vile kuna mtu
kamsubiri.
Hamisa na Chande ndio walikuwa wa kwanza
kumuona aisee hakuna cha kupoteza muda tulianza
mbio huku tukirudi nyuma, hata kina Hamisa
hawakutaka kupoteza muda.
Hamisa akiwa yupo nyuma yetu sisi wote kwa
bahati mbaya Latina alitokea mbele yake na
kumshika kwenye koo huku akiziingiza kucha zake.
Kelele za Hamisa akiomba msaada tulizisikia
ikatubidi kusimama ili kuangalia nyuma, masikini
mwenzetu alikuwa anarusha rusha miguu na mikono
huku akituomba Msaada.
Chande uzalendo ulimshinda ukija kuangalia ni
kama walikuwa wameanza mahusiano yao, ndipo
akaamua kumfuata huku sisi wote tukimsisitiza
aache twende ila hakuweza kutusikiliza, alipomfikia
Latina alivuta gogo ndogo kiasi akaanza kumpiga
nalo kichwani ila cha ajabu Latina hata kutikisika
hakuweza kutikisika bali aliendelea kumumalizia
Hamisa, haikuchukuwa muda Hamisa alikata roho
kisha Latina akamrusha pembeni.
Tulipoona anamgeukia Chande aisee kila mmoja
alimuombea kwa Allah amlaze mahali pema sote
tukakimbia, tukiwa tupo njiani huku tukikimbia kwa
kasi kubwa, sauti ya mwisho ya Chande Tuliisikia
akipiga kelele ishara anauwawa, wengi walianza
kukimbia huku wakilia mno.
Baada ya muda baadhi yetu walikaa wengine
wakawa wamesimama huku tukiwa tunaulizana nini
kimetokea.
Zakayo alianza kunilaumu mpaka wengine
wakamuunga mkono ndipo profesa mkuu akasema:
yeye sio chanzo.
Patrick: ukisema yeye sio chanzo mbona mdogo
wake ndo anafanya mauwaji? Mimi naona huu ni
Mchezo tupo tunachezewa maana haiwezekani mtu
kubadilika tu inaonekana kwao wachawi.
Baadhi ya wengine wakakubali maneno ya Patrick.
Hapo sikuwa na cha kujieleza mbele yao tena
Niliendelea kulia, wakiwa wanazidi kuongea huwezi
kuamini Latina alitokea katikati yetu kabla hatujakaa
sawa profesa ambae alijitambulisha kuwa jina lake
ni husband yeye ndie alikuwa kati kati yetu kwa
muda huo, Latina hakutaka kupoteza Muda alimkata
na kucha tumboni profesa wetu damu ikaturukia
sote, mwanajeshi Dominic alichomoa bastola yake
ili kumshtuti Latina ila nilimuwahi akajikuta anapiga
lisasi juu, utumbo tumbo wa profesa ukamwagika,
hakuna Aliebaki hapo Tulitoka hapo tunakimbia bila
hata uchovu.
Kila mmoja alienda na njia yake kwa wale
waliobahatika kwenda wawili wawili ilikuwa bahati
kwao, ila mimi nilienda njia yangu.
Patrick akiwa yupo na profesa mkuu kwa mbali
waliona Simba dume inawafuata kwa kasi sio ya
kawaida, bila kupoteza muda wakakimbia, kwa
kuwa patrick alikuwa ni kijana hakujuwa ni saa
ngapi kapanda mti alijikuta yupo juu ya mti ndipo
akamuambia profesa mkuu awahi aje kupanda ila
profesa alishindwa maana umri kidogo ulikuwa
umeenda, simba yule aliruka juu akaja kutua kwenye
kichwa cha profesa, yote Patrick alikuwa
anashuhudia kwa macho yake mawili.
Profesa mkuu alianza kupalangana na simba yule
huku akizidi kupaza sauti aje kusaidiwa, maskini
profesa nguo Pamoja na Ngozi yake vilichanwa
chanwa na simba yule mwishowe akazidiwa nguvu
akafariki hapo hapo, Patrick nusu ageuke kichaa
akitetemeka hali ya kwamba akashindwa kujizuia
akaanza kulia kama mtoto mdogo.
Akiwa yupo hapo alishangaa kuona vitoto vya simba
yule kama visita hivi vikaja vinamkimbilia baba yao
ila simba yule baada ya kuviona vina hamu sana ya
nyama alianza kuvitishia kisha akaanza kuburuza
mwili wa profesa wetu ndipo simba na wanae
wakatokomea na mwili wa profesa wetu msituni.
Upande wangu machozi zidi ya mdogo wangu
yalikuwa yamekata ilikuwa imebaki mimi kujitetea
mwenyewe, nikiwa nazunguka zunguka niliona kitu
kama mti mkubwa mno ambao ulikatwa yaani
umebaki Kama kisiki ndipo nikaona acha nikapande
ili kuomba msaada kwa wenzangu nilipofika
nilipanda juu nikaanza kuwaita wenzangu kwa sauti
kubwa, ajabu nikiwa naita kama vile pale nilipo
simama panabonyea kimtindo flani, nilipojaribu
kuangalia nikashangaa sehemu ile inabadili marangi
tofauti, nikipeleka mguu pembeni nashangaa rangi
inakuwa ya bluu, nikitoa mguu inakuwa rangi ya
kawaida nyeusi, nikawa najiuliza Kulikoni hichi kitu.
Ile naangalia pembeni aisee sikuweza kuamini
kuona kichwa cha mtu ila kama cha mwana mama
hivi, ajabu alikuwa ametulia kama vile kasinzia,
nilijiuliza mengi kuhusu kichwa kile huku nikijiuliza
moyonii: je nikichwa cha mtu kilichokatwa
kikawekwa karibu nahichii kisiki? Lakini mbona
kama vile kichwa kimeambatana na hichi kisiki?
Yote nilijiuliza huku nikiwa nimechomoa macho kwa
uoga.
Nilipoangalia vizuri kichwa kile cha mwana mama
Yule nikajaribu kuunganisha kile kichwa na kile
kisiki aisee niligundua ni nyoka yenye kichwa cha
binadamu na pale niliposimama imejikunja ikawa
kama mduwala flani Ndo maana nikahisi ni kisiki
cha mti mkubwa uliokatwa na ndo maana
nilivyokuwa naruka ruka kulikuwa kuna bonyea.
moyo wangu ulikata ghafla Mpaka kupumua
nikashindwa kwasababu ya uoga.
Unahisi nini kitatokea!
Usikose mkasa huu!
I'm sorry my fans nimechelewa kupostieee! Ila
usiumie we dondosha like yako ili nikuletee
mapema!
 
SEHEMU YA 10
TULIPOISHIA: Ile naangalia pembeni sikuweza
kuamini kuona kichwa kama cha mama flani ajabu
alikuwa ametulia kama vile kasinzia,
nilipomuangalia vizuri nikagundua ni nyoka yenye
kichwa cha binadamu na pale niliposimama
imejikunja ikawa kama mduwala flani Ndo maana
nikahisi ni kisiki cha mtu mkubwa uliokatwa.
SONGA NAYO!
Moyo ulinishuka nikaanza kujiuliza Ntatoka tokaje
pale, muda huo Derick na profesa Rodrigo pamoja
na Chilunga na Dominic walifika, taratibu nikawapa
tahadhari wasimame wasisogee ikiwezekana warudi
nyuma taratibu kupitia ishara ya mikono maana
Mimi nilijuwa kutoka eneo lile aisee ni Allah tu.
Aisee kumbe nyoka yule alikuwa anatuchola vizuri
kwa kile tunachokifanya.
Wenzangu hawakuweza kuelewa nikipi kinaendelea
wakawa wanajiuliza sasa yule vipi.
Kabla sijafanya chochote nyoka yule alinirusha
nikawaangukia wenzangu, aisee huwezi kuamini
nyoka yule alijikunjua, ukubwa wake hata
wakuambie upime urefu wake au upana wake
hungeweza, sote tuliishia kushangaa nyoka yule
alivyo wa ajabu, kilichotuua zaidi ni kile kichwa cha
binadamu, muda huo zakayo na Amanda walifika
vile vile na Abdul na Joyce, ile wao kushuhudia
walirudi nyuma kimya kimya, tukiwa bado
tunashangaa shangaa nyoka yule alipitisha mkia
wake juu ya Vichwa vyetu matawi ya miti ikakatika.
Hatukuchelewa tulianza mbio ili kujitetea na nyoka
yule hakutaka kutuacha akaendelea kutufukuzia,
nyoka yule mkukimbia nia yake anipate mimi,
Dominic alianza kumpiga lisasi ila haikusaidia
chochote, nyoka yule baada ya kuona Dominic
anataka kupinzana nae alimpiga mtama akaenda
chini kisha nyoka yule akakata mti ukamdondokea
kwenye miguu Dominic ikamfanya asiweze kutoka
eneo lile, wenzangu kila wakikata sehemu nyingine
nyoka yule hakuwajali bali alizidi kunifukuzia mimi
tu.
Nilikimbia bila kujielewa kwa bahati mbaya
nikadondokea kwenye bonge la kolongo, kina chake
kilikuwa kirefu mno na chini sana kulikuwa na
majabali makubwa mno, nikiwa nipo njiani huku
nikizidi kuteremka kwa mbali sauti yangu ilisikika
ninavyopiga kelele, nyoka yule alijinyoosha
nikashangaa kuona mkia wake, na fasta ikajikunja
kwenye mwili wangu kama kamba kisha ikanirusha
juu kwa juu nikaangukia karibu ya Dominic
Alipokuwa amegandishwa na muda huo wenzetu
walikuwa wanajaribu kumtolea ule mti, nikiwa bado
sijanyanyuka aisee huwezi kuamini mbele yangu
alikuja yule nyoka huku akiwa anajiburuta chini, sote
presha ilipanda kukimbia tukashindwa nikaanza
kurudi nyuma baada ya kuona kama vile ananilenga
mimi, nilipoufikia mti flani niliusegamia huku
nikijaribu kusimama, moyo ulinienda mbio
tulipogonganisha macho na nyoka yule ndo kabisa
nikaanza kulia.
Nyoka yule mwenye kichwa cha binadamu kama
mwanamama wa kikongo flani, alianza kutoa ndimi
zake mbili huku akitaka kunizuru, dakika mbili
alipanua mdomo wake ukawa mkubwa sana ili
kunimeza, na mimi nikajiandalia kufa, taratibu
nikafumba macho huku nikijiuliza je! Ntaenda
peponi au motoni.
Nikiwa nimefumba macho nilishtuka kusikia kama
kishindo cha mtu mbele yangu ndo nikaanza
kujiuliza kuna mtu kati ya wenzetu amekuja
kunikinga nisidhurike, taratibu nilifumbua macho
yangu nikashangaa kumuona mtu akiwa yupo kifua
wazi, kichwani alikuwa na nywele nyingi mno,
nilipopitisha macho pembeni nikamuona yule nyoka
bado yupo pale pale ila kama vile kuna kitu wapo
wanaongea na mkaka yule ambae sikuweza
kumtambua alakini bila kutoa sauti.
Upande wa kina Derick jasho ilikuwa inawatoka
kama mvua, muda huo Patrick, Safia, Amanda,
Zakayo, Joyce na Abdul walifika eneo la tukio,
aisee hawakuamini walichokiona.
Nyoka yule kwa macho yetu Tulimuona akawa
mpole kisha akaondoka kama vile kaambiwa kitu
na kijana yule.
Nilipomuangalia vizuri kijana yule aliekuja kutupa
msaada alikuwa na asili ya kizungu licha alikuwa
amechakaa sana.
Baada ya muda tulikaa kikao huku yule kijana
mzungu akiwa anatuambia mengi kuhusu msitu huo.
Dominic: huyu nyoka kwanini anakichwa cha
binadamu?
Mkaka yule ambae hakuweza kutueleza jina lake
akatuambia kwa kingereza: mwaka Elfu moja Mia
Sita themanini na tano mama huyu alikuwa ni
mwadamu wa kawaida, aliweza kutenda usaliti zidi
ya kabila lake.
Rodrigo: kabila gani? na ilikuwaje?
Akasema: zamani hapa Kongo makabila yalikuwa
na mfalme wao kipindi hicho kabila la kibembe
lilikuwa ni kabila lipo chini sana lenye kumiliki vitu
vya thamani mno, hivo makabila mengine yalihitaji
kuteka kabila lile ili kuwafanya kuwa watu wao
ikiwezekana walifutie mbali kabila lile, ila wabembe
walikuwa na malikia wao ambae walipenda kumuita
malikia wa kibembe, malikia huyo alikuwa na nguvu
za ziada wao waliamini aliteremshwa kutoka
mbiguni, hivo makabila yenye nguvu yalipopata
taarifa kuwa yupo kiziwizi anaewafanya watu wale
wawe na jeuli walianza kumtafuta kwa njia zote,
baada ya kabila lile la wabembe kupata taarifa kuwa
malikia wao wanamtafuta ili waweze kumuua
alienda kufichwa kwenye pango flani ya miungu yao,
sasa huyu mwanamama ambae ni nyoka kwasasa
hivi akaenda kutoa siri ya kabila lao kwasababu ya
tamaa zake wakamfuata malikia yule wakamchukua
ila kabla hajafa alimuachia laana hii, ndo maana
yupo namna hio.
Tulishusha pumzi kwa pamoja ndipo Amanda
akamuuliza: ilikuwaje sasa kwa hilo kabila la
kibembe?
Profesa Rodrigo akamjibu: hilo silo linalotufanya
tuwe hapa sijui umenielewa?
Amanda: nimekuelewa.
Rodrigo: mbona profesa mkuu hajatokea?
Patrick akamjibu: muda mrefu hatupo nae.
Tulishtuka na kumuuliza: amekufa?
Alitupa mkasa ilivyokuwa aisee kila mmoja aliumia
maana mzee yule alikuwa anatufanya tuwe na
nguvu.
Rodrigo akamuambia yule kijana kwa kingereza
maana alionekana hata hasikii kiswahili: sisi
utuonapo hapa tumetoka nchi jilani Tanzania
tumekuja huku kufuatilia maswala ya huu ugonjwa
wa ebola sasa Tumekutana na kizaa zaa cha ajabu
mpaka sasa niongeapo watu kama watano hatupo
nao tena, kuna ndugu yetu tumekuja nae huku cha
kushangaza amebadirika anatuua hovyo, sasa sijui
unaweza kutusaidia nini hapo, tunahitaji kutoka
ndani ya msitu huu.
Mkaka yule akasema: ndio wengi wanaokuja kwa
lengo hilo la ebola huwa wanapotezaga maisha
wote ila niwaambie tu kuwa tiba ya ebola ipo na ipo
ndani ya msitu huu.
Tulishangaa kwa pamoja huku tukiendelea
kumsikiliza kwa pamoja, ndipo akaendelea kusoma:
mwaka 1859 Kuna mzee flani alishtumiwa kuwa
yeye nimchawi na Nikweli alikuwa mchawi mkubwa
zama hizo, enzi hizo wafalme walikuwa wakali mno
mzee huyo baada ya kuzingiziwa kuwa yeye ndie
kahusika na kifo cha mwana wa mfalme ambae
alitarajiwa kuwa mfalme wa baadae, mfalme
aliamua kuua wa toto wote wa huyo baba mchawi
pamoja na mkewe kipenzi vile vile hata yeye pia ila
kabla hajafa mzee Yule aliwatangazia wana nchi
wanaoishi katika nchi nzima ya kongo milele
watadhulika kwa malidhi hayo licha hawakujuwa ni
ugonjwa gani alikuwa anazungumzia Ila kwasasa
Sisi tunayaita Ebola, nahisi hicho ndo chanzo.
Aisee kijana yule Tulimuona mtu mwenye hakili
mno maana historia ile hakuna ambae aliweza
kuisikia kabla, ndipo nikamuuliza: ilikuwaje
akapandikiza dawa ile?
Akanijibu: baada ya kufa walipokuwa Wamemzika,
fuvu lake lilitoka ndani ya kabuli lake likaja huku
Kaskazini mwa kongo lilipofika ndani ya msitu huu
wa equatorial lilitengeneza maji ya ajabu ambayo
yana rangi ya bluu, zama hizo wengi walikufa mno
bila kujuwa nini kinawauwa kwa wingi, Labda
niwaambie kuwa maji hayo ndio ugonjwa tosha wa
ebola na ndio tiba tosha ya ebola.
Rodrigo akamuuliza: una maana gani ukisema ndio
tiba na ndio maradhi?
Akasema: yapo kwenye kibuyu flani ambacho kipo
juu ya mti flani mwenye matunda mazuri ambayo
matunda hayo Nyani wanayapenda mno, sasa mti
huo upo karibu na mto flani unaoteremsha maji
uitwao Ebola, mwaka 1976 ndo ugonjwa Huo ukaja
kuvumbuliwa na mtafiti mzungu akaamua kuupa
Jina ya Ebola kutokana alifanya uchunguzi
akagundua virusi ile inatoka ndani ya mto ule, sasa
inakuwa hivi kibuyu kile huwa kinamwaga maji yale
ndani ya mto ule baada ya mwaka, kikisha mwaga
maji fuvu lile linakuja linaongeza mengine na ndo
maana utasikia wanasema Ebola inakuja mwaka
kwa mwaka.
Aisee vichwa vilichanganyikiwa kwa dakika mbili
ukija kuangalia tulikuwa wana science wazuri Ila
taarifa ile Ilikuwa ngeni kwetu, ndipo profesa wetu
Rodrigo akasema: watafiti wanatuambia Ebola ni
virusi vinavyopatikana ndani ya mwili wa nyani
ambae amefariki kisha sisi binadamu tukamchukua
na kumla vipi hapo unalizungumziaje?
Akasema: Nikweli baada ya nyani wale kula yale
matunda wakashiba huwa wanadestuli ya kunywa
maji yaliopo kwenye mto ule na maanisha
wanakunywa maji kutoka ndani ya mto wa Ebola
sijui mnanielewa!
Tulitikisa kichwa ishara tupo nae Mia mia.
Akaendelea kusema: sasa siku wakija kunywa yale
maji ikakutana siku hio yale maji ya ajabu
yamejimwaga ndani ya mto ule madhara yake huwa
nao virusi hio inawapata wanaporudi kwenye makazi
yao wanaanza kuzoofika mwishowe wanapoteza
maisha, ikiwa hivo watu sasa wanaona nyamafu
wanaichukuwa wanaikula, wakishakula ndo maradhi
ya Ebola yanatokea hapo.
Aisee kijana yule alijizolea sifa nyingi kutoka
kwenye nyoyo zetu ndipo nikamuuzi: vipi kuhusu
mdogo wangu anasumbuliwa na nini mbona
amebadirika kuwa kiumbe cha ajabu?
Akanijibu: fuvu lile la yule baba wa kale alieuwawa
na mfalme kwa kesi ya uchawi yeye yupo ndani ya
msitu huu ili kulinda laana ile alioiacha, sasa kila
anaeingia ndani ya msitu huu kwa lengo la kuja
kujuwa mengi kuhusu ebola huwa inamuua, mkiwa
mpo wengi kama nyinyi hapo linamchagua mmoja
wenu linamuingia mwilini kisha linaanza kutumikia
ndani ya mwili wake ili kuua wenzie.
Tuliangaliana usoni wenzangu ambao walikuwa
wananilaumu muda wote wakatamani kuniomba
msamaha.
Patrick nae akamuuliza: kwanini akiskia mziki
anacheza?
Unahisi nini kitatokea!
Usikose mkasa huu!
 
TULIPOISHIA: Tuliangaliana usoni wenzangu ambao
walikuwa wananilaumu muda wote wakatamani
kuniomba msamaa.
Patrick nae akamuuliza: kwanini akiskia mziki
anacheza?
SONGA NAYO!
Mkaka Yule mzungu akamjibu: Asili ya mtu wa
Kongo ni muziki wa kwao, hio ndio dawa Tosha ya
kumfanya asiwadhuru kama mnamiziki ya Kongo
muwekeeni pale mtafanya kila mtakacho na mtarudi
salama, huo ndo ubovu wake.
tulishangaa mno ndipo Dominic akamuuliza: vipi
kuhusu wewe umekuja kufanya nini?
Akamjibu: Nilikuja ndani ya msitu huu mimi na baba
yangu nikiwa na miaka 7 Ila kwasasa Nina miaka
30.
Tulishangaa ndipo Joyce akamuuliza: una maana
gani?
Akasema: tulipotelea huku, na Sisi pia tulikuwa
tumekuja kwa ajili ya masuala hayo ya Ebola.
Rodrigo: ilikuwaje?
Akasema: baba kuna makosa aliafanya kipindi
hicho, muombeni Mungu msikutane na kabila la
wambote (pygmy) ni binadamu wa Kali mno.
Rodrigo akamgeukia Zakayo na kumuuliza: wewe si
ulisomea Kidogo masuala ya Utafiti Enhe! tuambie
Wambote ni wakina nani?
Zakayo: Nyinyi hamjui?
Rodrigo: Sisi wana science bwana Ukitaka kuuliza
mavairasi Njoo utaambiwa Mpaka wapi
wanapatikana Mara nyingi.
Tulicheka kisha Derick akasema: usijitetee!
Rodrigo: Mwaya Zakayo tuambie.
Zakayo: Nikabila la watu wa fupi mno hapa Kongo,
Halafu wananguvu Sana na inasadikika wao ndio
watu wa kwanza kuishi ndani ya nchi hii ya Kongo,
wao wamejitenga Sana na binadamu wengine mara
nyingi wanaishi mamistuni.
Aliishia hapo sote tukamuelewa ndipo Rodrigo
akamuambia yule mzungu: tumeelewa kuhusu hio
kabila.
Akasema: pygmy wanakula nyama za watu...
Tulishtuka mno huku tukiendelea kumuangalia kwa
umakini ndipo akaendelea kusema: walitaka kunila
mimi ila baba akamtwanga risasi mke wa mkuu wa
kabila lile, iliwauma sana ndipo wakatuambia
kikwao hatutotokaga ndani ya msitu huu milele na
milele, kwahio naweza kuondoka zangu?
Nilimzuwia na kumuuliza: vipi baba yako yuko wapi?
na je Kwanini Huyu fuvu Hawezi kuwazuru Nyinyi?
Alitabasamu kisha akanisogelea akaninong'oneza
maskioni: siraha ya pekee kumuangamiza huyu
kiumbe ni Yale maji.
Alipoongea hivo aliniachia kisha akanipiga piga
begani na kuondoka zake, nilibaki hapo nimeduwaa
huku nikijiuliza alimaanisha nini Ila sikupata jibu.
Wenzangu baada ya kuona nimenong'onezwa kitu
ambacho wao walihisi Labda ni muhimu kwetu
walinisogelea Wakaanza kuniuliza nini kaniambia
ndipo nikawajibu: ameniambia hivi siraha ya pekee
ya kumuangamiza huyu kiumbe ni Yale maji, sasa
sijui kama ni ule mto au ni Yale maji ya ajabu.
Walishangaa ndipo Zakayo akasema: Labda ni Yale
maji ya ajabu.
Profesa Rodrigo: nahisi! Ila Huyu mtu anaonekana
baba yake ni Mtafiti Sana mambo ambayo wengi
hawayajui Ila yeye anayajuwa kiundani.
Abdul akamuuliza: Kwanini wao Huyu fuvu
hawazuru?
Rodrigo: wazungu wakienda sehemu hawaendi
kihorera horera kama Sisi wanajipanga kwanza ndo
maana alievumbua maradhi haya ni mzungu.
Nikauliza: hapa kila mmoja maji Yapo shingoni
mnampango gani? je! turudi nyuma au tusonge
mbele?
Rodrigo: Goma tumelianzisha wenyewe sasa kila
mmoja nikujuwa jinsi gani atalicheza, kurudi nyuma
Haiwezekani hapa tupo Katikati ya msitu mimi
naona hivi tujitahidi twende kwenye huo mto
ikiwezekana kama alivyosema tuweze kumteketeza
kwanza huyo kiumbe mambo mengine yatafuata
Baadae.
Patrick: muongee hivo mkumbuke Ramani hatuna
hapa.
Nikamuuliza: tumeiacha wapi?
Patrick: Muda ule tunakimbia profesa husband ndo
alikuwa nayo.
Ndo tukakumbuka muda ule alikuwa anaangalia
Ramani ndipo Latina alitokea na kumuua.
Derick alishtuka na kusema: lazma nirudi kule.
Nilishtuka na kumuuliza: wapi?
Derick: kule tulikokuwa mwanzo.
Nikamuuliza: kufanya nini?
Derick: begi yangu nimeiacha na Kuna vitu vyangu
vya thamani vipo mle.
Niliposkia hivo uzalendo ulinishinda nikamuwahi na
kumshika mkono kisha nikamuambia: Nihatari sana
wewe kwenda kule please Achana Navyo kwasasa
kitu muhimu ni nafsi yako.
Derick: lazma nirudi tu kwasababu bila Ramani
tunaelekea wapi?
Wote walimuunga mkono akaamua kuondoka,
Nilikata tamaa ya kumuona tena maana nilihisi
atafanyiwa Kibaya na Latina.
Kwa sauti ya Juu nikamuambia: nisubiri.
Derick alinisubili nilipomfikia nilichomoa kakisu
kangu kadogo ka kutumia kulia matunda
nikamkabidhi na kumuambia: hakikisha umerudi
ukiwa upo Salama.
Derick alinitabasamia kisha akaondoka.
Baada ya muda Tuliweka makazi hapo huku
tukimsubiri Derick arudi, baridi Muda wote ilikuwa
inatupiga maana msitu wa equatorial Mvua haikati.
Upande wa Derick alienda moja kwa moja mpaka
ile eneo tulikokuwa tumekaa muda si mrefu,
alipofika aliukuta mwili wa profesa husband bado
upo pale, alisikitika mno na kusema: lala mahali
pema tuvumilie hatuwezi kukuzika.
Alianza kutafuta Ramani kwa bahati nzuri akaiona
ndipo Akaichukuwa pia akachukuwa na begi yake
akavaa kisha akatoka eneo lile.
Upande wetu Zakayo alianza kurusha mawe juu ya
mti ambao Sisi tulikuwa tupo Chini yake huku
tukizidi kumsisitiza aachane navyo atakuja
kuumizana ndipo akasema: Muda wote nilikuwa
siskii njaa sasa nimetulia njaa ya toka Juzi
imeniingia.
Amanda: sasa hapo unaona kuna matunda?
Zakayo: Kama hauyaoni Sisi tunayaona.
Patrick akasema: mimi hapa ngoma ya kikongo
yenye ninayo ni ile ya Inno's Bella na diamond
platnumpz sasa sijui Nyinyi huko.
Nikamjibu: na Mimi ni hio hio.
Nikasema: aisee usilolijua sawa sawa na usiku wa
giza! Leo ndo nimeamini huo msemo.
Amanda: una maana gani?
Nikamjibu: na maanisha tungejuwa kuhusu huyu
kiumbe tungekuja na sabufa tukawasha musiki
mnene na tungepata kilichotuleta.
Wengi simu zao zilipotea tulikuwa wachache sana
ambao tumebaki na simu ndipo Dominic
Akachomoa kasimu kadogo kenye memory card
akaomba arushiwe huyo mziki.
Tukiwa tupo hapo huku Zakayo akiendelea kufanya
yake ghafla alirusha kipande cha mti kikapiga nyoka
Aliekuwa juu ya mti ule moja kwa moja nyoka yule
akamdondokea Sofia, aisee Sofia alipige kelele huku
akimkunguta nyoka yule ndipo nyoka yule akaenda
Chini, haraka Dominic Akachomoa bastola yake
akamtwanga nyoka yule risasi ya kichwa kisha
akafa hapo hapo.
Tulishusha pumzi huku Wengine wakimlaumu
Zakayo ndipo Dominic akasema: risasi muda
wowote zinakata.
Upande wa Derick akiwa anazidi kusonga mbele
huku akiwa anaangalia Ramani ile alishtuka kuskia
mchakacho nyuma yake, akasimama huku akiwa
anaangalia kona zote ila hakuweza kuona kitu,
alipopiga hatua mchakacho ukazidi akaangalia tena
nyuma ila hakuweza kuona chochote, ile anaangalia
mbele alishangaa kuona Mbwa mwitu Kama
thelathini wakiwa wapo mbele yake huku wakiwa
wanamvisia kimtindo flani, uzalendo ulimshinda
akatoka hapo mbio huku akielekea sehemu tofauti
na kule tulipo, kizuri alikimbia huku akipiga kelele
mno, Mbwa mwitu wale kwa kukimbia farasi
wakasome.
Upande wetu kelele za Derick tulizisikia maana
haikuwa mbali sana na eneo tulipo, bila kupoteza
muda tukamfuata huku tukikimbia mno.
Derick alizidi kukimbia, ile Mbwa mwitu wale
wanamfikia alifika eneo mbaya akajirusha ndani ya
korongo flani kina chake kilikuwa cha Kawaida na
Chini kulikuwa mto mkubwa ulikuwa unateremsha
maji, Derick alipaza sauti huku akizidi kuteremka.
Mbwa mwitu wale Waliendelea kumtazama kwa
uchungu maana wao kuingia ndani ya maji
Haiwezekani, Tulipofika eneo lile tuliwaona Mbwa
mwitu wengi wakizunguka zunguka, ndipo Dominic
alichomoa bastola yake akapiga lisasi Juu, ule mlio
uliwafanya Mbwa mwitu wale wakimbie.
Fasta tukasogea pale ambapo Mbwa mwitu wale
walikuwa wamesimama, aisee Sikuamini kumuona
Derick akiwa ni mzima wa hafya, wenzangu wote
walianza kucheka kwa furaha huku wakimtazama,
ndipo Abdul akamtania akisema: kurudi bila wewe
Tanzania tunawekwa jela, Fanya utoke ukiwa Salama
mwana.
Derick akiwa yupo kati Kati ya mto ule, huku akiwa
bado ameshikilia kile kisu mkononi alitabasamu
kwa furaha na kusema: lazma niwe hai kwa muda
huu.
Derick Akiwa yupo hapo anatafuta njia ya kuweza
kumtoa hapo, huwezi kuamini nyuma yake ilitokea
nyoka kubwa mno Mfano wa chato, nyoka Yule Sisi
tukiwa tumeduwaa bila kumshtua Derick
alijinyoosha kisha ikashuka fasta kichwa chake pale
Derick alipokuwa amesimama na...... ..... Huku Sisi
tukiwa tunaendelea kushangaa shangaa.
Unahisi nini kitatokea!
Usikose mkasa huu!
 
SEHEMU YA 12
TULIPOISHIA: Derick Akiwa yupo hapo anatafuta njia
ya kuweza kumtoa hapo, huwezi kuamini nyuma
yake iliibuka nyoka kubwa mno kutoka ndani ya
maji ikajinyoosha kichwa kisha ikashuka fasta pale
Derick alipokuwa amesimama na...... ..... Huku Sisi
tukiwa tunashangaa shangaa.
SONGA NAYO!
Nyoka yule alishuka fasta pale Derick alipokuwa
amesimama na kummeza haraka huku Sisi tukiwa
tunashangaa shangaa.
Nyoka yule bila kupoteza muda akazama ndani ya
maji.
Nililia mno Baada ya kuona tukio lile, pia hata
wenzangu walinisaidia kuomboleza.
Tukiwa tupo hapo bila kujuwa hili wala lile ghafla
nyoka yule kwa Mara nyingine aliibuka katoka ndani
ya maji akajinyoosha, ajabu akamtapika Derick
pembeni kisha akarusha damu nyingi ambayo hata
Sisi pia ilitufikia, baada ya hapo nyoka yule
aliishiwa nguvu taratibu akaangukia ndani ya maji
Kama vile kupoteza uhai, wote Tuliendelea
kushangaa ndipo akapelekwa na maji.
Mimi bila uoga wowote niliwaacha wenzangu pale
nikajirusha ndani ya maji Yale huku wakizidi
kunisisitiza niache tayari Derick hayupo tena duniani
Ila sikutaka kuwapatia maskio bali nilitaka kuhakiki
mwenyewe.
Nilianza kupiga mbizi nikimfuata Derick, nilipomfikia
nilianza kumvuta nikimtoa ndani ya mto ule, baada
ya dakika kadhaa nilifanikiwa kumuweka pembeni
Kidogo ambapo maji yalikuwa hayafiki.
Mwili wa Derick ulikuwa umejaa vitu kama
makamasi vilikuwa vinalenda kama mlenda lenda,
Ila Mimi sikujali hayo nilianza kumtikisa.
Nilipomuangalia kwenye mkono wa kulia niliona
kashikilia kile kisu nilichomkabidhi muda ule ndipo
nikamuambia huku nikilia Kama mtu aliejikatia
tamaa: Kwanini umeshindwa kujitetea hali ya kuwa
kisu unacho mkononi! Usinifanyie hivo mwenzio
nakupenda.
Derick Muda Huo alikohoa akaanza kutema maji
Jambo ambalo wote hatukuweza kuamini, , nilifurahi
mno nikawaita wenzangu waje Derick ni mzima.
Baada ya muda tulikuwa tumemsafisha Derick huku
tukiwa tumemlaza Chini ya mti.
Rodrigo: akipona lazma awe chizi.
Patrick: Natamani sana kujua nikipi kimemfanya
akawa hai!
Amanda Muda Huo alikuwa pembeni huku
akimuangalia Derick.
Tulikaa hapo mpaka Majira ya usiku Derick alikuwa
bado hajazinduka, tukiwa tumetulia tulishtuka
kumsikia akipiga chafia, kwa kuwa Mimi ndie
nilikuwa karibu yake Nilimuwahi na kumshika Ila
Amanda alikuja akanisukuma na kumshika yeye,
wengi walimshangaa ila wakapotezea ndipo Zakayo
akasema: ndugu zanguni kwa wale ambao
wamebahatika kuwa na kasimu kumbukeni kale
kamuziki ka diamond na inno's Bella mukaweke
kwenye emergency.
Sote Tulicheka maana alibadiri sauti.
Derick alijitahidi akakaa kisha akatuuliza: hapa nipo
wapi?
Tulishtuka maana tulihisi Labda atakuwa amepoteza
Kumbukumbu ndipo Nikamuuliza: mimi ni Nani?
Derick: wewe ni mpenzi Wangu.
Wote waligeuka kunitazama kwa mshangao Mpaka
Amanda mwenye ndipo nikasema ili kujitetea:
atakuwa hayupo vizuri huyu Ndo maana neno
linalokuja Ndo anaongea.
Tulifurahi kumuona Derick ni mzima tena ndipo
Rodrigo akamuuliza: muda ule ilikuwaje Baada ya
wewe kumezwa na nyoka?
Derick: aisee ni Mungu pekee ndie kanipigania
maana alivyonimeza ni kama vile niliingiwa na
nguvu za ajabu kile kisu Najma alikuwa amenipa
nilimchana kwenye mfumo mzima wa kupumulia
sasa ukiniuliza baada ya hapo kilitokea nini sijui
kweli.
Profesa Rodrigo akasema: Duh! una bahati Sana,
inaonekana ulivyomchana alikosa pumzi maana
alikutema kisha akaturushia Sisi damu.
Derick: najuta kuja huku.
Alinitazama na kuniuliza: Upo Salama wewe?
Kabla sijamjibu Zakayo akasema: mbona unamjali
Jali sana?
Joyce akadakia: Eee ni wapenzi Upo? kama Ndo
ulitaka umtongoze Najma Utalamba lolo.
Zakayo: Mmmhhhh naanzaje kwamfano hata hayo
mashaili ya kumtongoza nayatoa wapi kwenye balaa
hili! Msione tunatembea Wengine Tukifika dar es
salam tunapelekwa kwenye hospital ya vichaa.
Wengi walicheka Muda Huo mimi nilikuwa
namtazama Derick simshibi maana tumaini ya
kumuona tena Ilikuwa imepotea, ndipo Rodrigo
akamuuliza: Ramani umefanikiwa kuja nayo?
Derick: muda ule Mbwa mwitu walipokuwa
wananikimbiza sijui ilikuweje kuhusu Ramani maana
nilikuwa nayo mkononi.
Wote tuliishiwa nguvu ndipo Amanda akasema:
sasa tunafanyaje?
Dominic: tusonge mbele tuufuate huu mto nahisi
ndo mwenyewe.
Tulishangaa na kumuuliza: huu mto Derick
aliokuwemo?
Dominic: Ndio, tupumzike mchaka mchaka kesho.
Joyce alinyanyuka na kusema: Rodrigo twende
kuzunguka kwanza.
Nikamuuliza: bado mna moyo wa kuzunguka
zunguka?
Joyce: hatukawi.
Joyce na profesa Rodrigo walitoka maeneo hayo
wakatuacha hapo, ukweli baridi iliopo ndani ya
msitu Huo aisee sikuwahi kusikia kabla, usiombe
ikafika usiku, watu wote walikuwa wanatetemeka
mno kutokana na baridi kuwa nyingi.
Nikiwa nimejikumbata imani yangu lazma mdogo
wangu ntamuona tena akiwa yupo kwenye Hali yake
nzuri.
Upande wa Joyce na mpenzi wake walikuwa
wanapiga story za Kawaida kuhusu wakitoka hapo
wataenda kuoana.
Wakiwa wapo hapo alitokea Latina nyuma ya Joyce
Ila hawakuweza kumuona ndipo Joyce akasema:
mpenzi Wangu naomba Usije kunisariti.
Ukimya ulitawala maana Rodrigo alikuwa amejificha
kwenye mti flani ili wacheze kombolela ndipo Joyce
akamuita kwa hofu: Rodrigo!!
Joyce alipogeuka nyuma aliona mtu akiwa
amesimama akahisi Labda ni mpenzi wake Rodrigo
bila kujuwa kuwa ni Latina maana giza lilikuwepo
ndipo Joyce akashusha pumzi na kusema: usiwe
unanitisha hivo twende mi nimeanza kuogopa.
Rodrigo aliposikia mpenzi wake anaongea Kama
vile kuna mtu anamuambia, alijitokeza na kusema:
Kumbe muoga Sana eee?
Joyce alishtuka huku akiwa anajiuliza huyu ambae
nimemshika begani ni Nani? Bila kupoteza muda
aligeuka kumtazama Rodrigo, baada ya kugundua
kuwa ambae kamshika sie alimuambia Rodrigo kwa
sauti ya juu akasema: tukimbie!!!
Maskini Joyce kabla hajapiga hatua yoyote Latina
aliingiza mkono wake wenye kucha ndefu ndani ya
mgongo wa Joyce akavunja uti Wa mgongo,
ikampelekea Joyce kuganda huku akiangaliana na
mpenzi wake kwa jicho la mwisho bila kujuwa.
Rodrigo aliendelea kushangaa ndipo Joyce kwa
sauti ya Chini mno akamuambia: Kimbia.
Damu zilianza kumtoka Joyce mdomoni, Rodrigo
alipoona hivo aliamua kukimbia ili kuokoa maisha
yake.
Upande wetu tukiwa tumetulia profesa Rodrigo
alifika huku akihema vibaya mno, bila kupoteza
muda tuliamka fasta na kuanza kuulizana kuna nini
kinaendelea, kabla hajaongea chochote Latina
alitokea mbele yangu na............................
..........Huku nikiwa namuangalia machoni, vile vile
na Yeye akiwa amenikazia macho.
Unahisi nini kitatokea!
Usikose mkasa huu!
 
SEHEMU YA 13
TULIPOISHIA: Upande wetu tukiwa tumetulia profesa
Rodrigo alifika huku akihema vibaya mno, bila
kupoteza muda tuliamka fasta na kuanza kuulizana
kuna nini kinaendelea, kabla hajaongea chochote
Latina alitokea mbele yangu na............................
..........Huku nikiwa namuangalia machoni, vile vile
na Yeye akiwa amenikazia macho.
SONGA NAYO!
Kabla profesa Rodrigo hajaongea chochote Latina
alitokea mbele yangu na kunishika shingoni Huku
nikiwa namuangalia machoni, vile vile na Yeye
akiwa amenikazia macho.
Watu wote walikimbia Ila Derick alijaribu
akashindwa kukimbia maana nguvu alikuwa Hana
tena, nilipoona Latina muda wowote anaweza kuniua
nilianza kujaribu kujitetea ila nguvu alizokuwa nazo
zilikuwa sio za Kawaida, taratibu nikaanza kuona
mawenge, wenzangu waliopoteza maisha ndani ya
msitu Huo nikawa kama vile nawaona ndo nikajua
punde si punde nakata roho, bila kupoteza muda
huku mkono wangu wa kushoto ukiwa umemshika
mkononi Latina ili Aache kuninyonga nilishusha
taratibu mkono wangu wa kulia nikauingiza kwenye
mfuko wa suluwali niliokuwa nimevaa taratibu
nikatoa simu yangu na ku play muziki wa Inno's B ft
Diamond platnumpz.
Kama bahati Latina aliniachia nikadondoka Chini na
simu yangu ikaangukia pembeni, bila kupoteza
muda akaanza kucheza nyimbo ile, sikutaka
kupoteza muda nilimfuata Derick alipo kuwa
anahanya hanya nikamshika tukaanza kutoka eneo
lile, tukiwa tupo njiani nikamuambia: jitahidi tuwahi.
Derick: kwahio ule muziki haujausave ujirudie rudie?
Nikamjibu: nilisevu Ila tatizo chaji inaisha bado
asilimia tano simu izime.
Tuliongeza spidi.
Usiku wote ulituishia tukiwa tunatembea tembea
tukiwatafuta wenzetu.
Alfajiri upande wa wenzetu walikuwa wamekata
tamaa kuhusu Sisi ndipo Amanda akamuuliza
Dominic: Mbona hukumpiga risasi Latina?
Zakayo akadakia: angekuwa wewe ungeweza?
Patrick akasema: pale wengi tunakimbia kwa
mkumbo unasikia "huyo hapo" hujamuona
unakimbia, sasa wewe Amanda upewe hio bastola
ungefanyaje kwa Mfano?
Amanda akaanza kulia akisema: Naumia kuhusu
Derick.
Sofia akiwa Analia akasema: Najma, Derick, Joyce
tumewapoteza kwa siku moja jamani hata Sisi
muda wowote tutakufa naogopa sana.
Upande wetu tuliamua kujipumzisha Chini ya mti
ndipo Derick akaniambia: wewe ni wa thamani
kwangu.
Nikamuuliza: kwa nini?
Derick: wote wamekimbia Hakuna alienikumbuka Ila
wewe ukanikumbuka nakupenda sana Najma.
Nilitabasamu na kusema: Kikubwa sote turudi
tukiwa hai Halafu mtu anaehitajika kurudi akiwa
Salama ni wewe.
Derick: kwa nini?
Nikamjibu: wewe umeyasaidia maisha ya wa bongo
wengi, Istoshe nchi yetu inajivunia uwepo wako.
Derick: huu msitu una mengi.
Nikamuuliza: ulivyoingia ndani ya tumbo ya nyoka
yule ilikuwaje?
Derick: ni marefu.
Nikasema: nimeyaona macho ya Latina, mdogo
wangu kwa sasa atakuwa anahangaika sana.
Derick: una nini shingoni?
Nikamuuliza: kuna nini?
Nilipogusa nikaangalia mkono nilishangaa kuona
damu ndipo Nikamuuliza: kuna nini?
Derick: Latina amekuumiza na inaweza kuleta
Matatizo mbeleni.
Nikweli damu Muda wote zilikuwa zinatiririka ila
nilikuwa sijaona wala kusikia kuwa Nimeumia ndipo
Derick alivua begi lake akatoa dawa flani
akaniwekea shingoni kisha akaniwekea bandeji na
kusema: hii cheni uliitunza sana.
Nilitabasamu na kusema: kwahio ulikuja na vifaa
vyako?
Derick: baadhi ya dawa.
Nilimshukuru.
Baada ya masaa kadhaa tulianza kuwatafuta
wenzetu huku tukiwaita.
Mvua muda wote ilikuwa inanyesha mpaka
tukazowea hali ile, tukiwa tunazidi kusonga huku
Derick akiwa ameanza kupata nafuu Tulisikia sauti
ya wenzetu Kama vile kuna kitu kimewatokea, fasta
tukawafuata.
Tulipowafikia tulimkuta mwenzetu Zakayo akiwa
amezama ndani ya tope huku Dominic akiwa
amemshika mkono ili asizame mzima mzima
maana alikuwa anaonekana kuanzia kifuani kupanda.
Profesa Rodrigo akasema: mtu asiingie kule
atazama.
Zakayo akiwa Analia akasema: mnisaidiene jamani.
Dominic akasema: jitahidi sasa na wewe.
Nilipoona Dominic Hawezi kumtoa akiwa mwenyewe
na kama vile ameanza kuchoka nilitoa Wazo, bila
kupoteza muda tukalitendea kazi, Chilunga
alimshika kiunoni Dominic akafuatia Patrick,
akafuatia Abdul kisha mimi tukaanza kumvuta huku
Wengine wakiwa wanatuangalia Kama TV.
Kwa kuwa tulikuwa wengi tulishilikiana kwa Pamoja
tukafanikiwa kumtoa Zakayo eneo lile.
Tulijipumzisha huku tukiwa tumelala ndipo Zakayo
akiwa amelala akasema: huu msitu Miezi kumi na
mbili kuna nyesha Mvua ndo maana kuna sehemu
ardhi imeshakuwa laini kama uji sasa vihere here
kama Sisi tunaenda bila kuangalia madhara yake
Ndo haya.
Tulicheka Licha tulikuwa kwenye balaa ndipo Abdul
akanipa mkono na kusema: umetoa Wazo nzuri
maana muda wowote mwenzetu tungemkosa
kiuzembe, Ndo maana nililia sana nilipokuacha kule.
Nilinyanyuka na kusema: jamani mliobaki na
Masimu wallah ndio yatatusaidia.
Sofia: unataka useme na wewe ndo imekusaidia?
Nikamjibu: eeee!!!
Sofia simu yake Ilikuwa imezima kutokana na
kunyeshewa sana na Mvua ndipo nikauliza:
tumebaki na simu ngapi?
Watu waliokuwa wamebaki na simu ni Patrick na
Dominic tu.
Dominic alikuwa na kasimu Kake kadogo ndipo
Nikamuuliza Derick: simu yako vipi?
Derick: chaji imeisha.
Abdul akamuuliza: au Imeharibika kwasababu ya
Mvua?
Derick: simu yangu hata niiweke ndani ya maji
haiwezi kuharibika.
Nilipomtazama profesa wetu Rodrigo kwa Muda
Huo alikuwa amejitenga na Sisi ndipo Nikamuuliza
Sofia: Joyce yupo wapi?
Sofia: hatupo nae tena.
Alinipa mkasa wote, aisee moyo uliniuma sana
maana Joyce alikuwa ni Rafiki yangu mkubwa,
taratibu nilimfuata profesa Rodrigo nikamkuta akiwa
anatiririkwa na machizi ndipo nikakaa karibu yake
na kusema: yote ni matokeo, vipenzi vyetu, nafsi
zetu vyote tutaviacha hapa, Hakuna atakaetoka
akiwa ni mzima tafadhali jipe moyo kwa hizi dakika
zilizobaki hata wewe pia utaenda kuonana nae
punde si punde.
Profesa Rodrigo aligeuka kuniangalia kisha
akaniuliza: una maana gani?
Nikamjibu: mimi Kifo kipo karibu yangu kila
nikifumba macho wenzangu waliopoteza maisha
nawaona na hio ni ishara mbaya Sana.
Rodrigo: Nisamehe Sana, pia msamehe Joyce
tuliweza kukushawishi ukaja huku Labda angekuwa
unamuuguza mama yako na mdogo wako angekuwa
yupo vizuri.
Nilitabasamu na kusema: yote tunayoyafanya kwa
hii dunia ni Allah pekee anaeyaelewa usijali wala
usijilaumu.
Baada ya muda tulikuwa tupo njiani tunaufuata ule
mto, ile kusonga mbele tukaona kijiji flani ambacho
nyumba zilikuwa zinashangaza ndipo nikasema:
kwenye baridi hii kuna binadamu wanaishi huku?
Wenzangu waliomba tusonge tukaangalie
ikiwezekana tukaombe msaada, Tulifika ajabu
hatukuweza kuona hata mtu hata mmoja, kwa
umakini wa hali ya juu tukaanza kuangaza angaza
kona zote, ghafla niliskia sauti za watu Kama vile
zinakuja tulipo ile kuangalia nyuma aisee kilikuja
kikosi cha watu wa fupi mno hatujapata kuona,
wakiwa wameshikilia siraha zao za kiasiri (mikuki)
ile kuangalia mbele Wengine wakatokea tukajikuta
tunawekwa mtu Kati, walikuwa ni wababa wenye
Ndevu zao na vijana walioshiba ila wafupi mno.
Zakayo kwa sauti ya Chini akasema: Hawa ndo
wale pygmy wanakula nyama za watu na Kumbukeni
tatizo wanaongea lugha yao hawajui kiswahili hata
Kidogo sasa hapa muda wowote tunatengenezwa
msosi.
Tuliposikia eti hio ni ile kabila ya ajabu tulishtuka
mno huku kila mmoja akiwa anajiuliza tunawatoka
vipi Hawa watu?
Unahisi nini kitatokea!
Usikose mkasa huu!
Kwa mia 5 unaipata yote wsp 0757449871
 
SEHEMU YA 14
TULIPOISHIA: Zakayo kwa sauti ya Chini akasema:
Hawa ndo wale pygmy wanakula nyama za watu na
Kumbukumbu tatizo wanaongea lugha yao hawajui
kiswahili hata Kidogo sasa hapa muda wowote
tunatengenezwa msosi.
Tuliposkia eti hio ni ile kabila ya ajabu tulishtuka
mno huku kila mmoja akiwa anajiuliza tunawatoka
vipi Hawa watu?
SONGA NAYO!
Haikuchukuwa dakika mbili walitupulizia dawa flani
tukazimia.
Baada ya dakika kadhaa kupita tulikurupuka
tukajikuta ndani ya chumba flani huku tukiwa
tumefungwa kamba mikononi na miguuni ndipo
Abdul akaulizia: tupo wapi?
Nikamjibu kwa sauti ya Chini: wametuteka.
Dominic kwa kuwa Yeye mbinu za kijeshi alikuwa
anazijua alijifungua ile kamba kisha akatufungua na
Sisi kisha akasema: hapa nikutafute njia ya
kuchomoka kabla noma haijatokea, mnisubiri
kwanza.
Dominic alitoka nje akawaona wote wakiwa
wamesimama sehemu moja kama vile kuna Jambo
wanalijadili ndipo Chilunga alitokea nyuma yake na
kusema: usifanye chochote ngoyela nikaongea nabo
batanielewa.
Dominic alimuamini Chilunga akarudi tulipo.
Alipotukifikia akasema: Chilunga anaenda kuongea
nao.
Nikamuuliza: wataelewana?
Patrick: si ni mkongo mwenzao.
Baada ya muda Chilunga alikuja na kusema:
nimeongea nabo bamenielewa kwahio msijali,
nimebaeleza kilichotuleta bamesema ile rivier ni ile
ile kwahio tungoyele batatupeleka.
Tulitoka nje ili kupunga hewa, kabila ile ya watu
ambao bado wanamila za kizamani walikuwa
wanatuangalia kwa mshangao ndipo nikasema:
mbona hapa hapanyeshi kama kule, ukweli hii Hali
niliitamani sana.
Zakayo: Hawa watu wachawi sana wanasimamisha
Mvua Mbona.
Baada ya muda nilianza kucheza na Watoto wa pale,
Abdul na Sofia wakanifuata na kuniomba tucheze
wote, nilifunga mpira kisha tukaanza kucheza mpira
wa miguu Pamoja na Watoto wale, tulicheza kwa
furaha maana sote tulikuwa matobwe, watu wote
walisogea pale wakawa wanafurahi tunavyocheza.
Chilunga alimchukuwa Derick akaingia nae kwenye
nyuma flani wakamkuta baba flani akiwa amelala
huku tumbo likiwa limevimba, na mkewe alikuwa
pembeni yake ndipo Chilunga akasema: Huyu papa
ana miaka Sita amelala hapa kitandani sijui Iko na
ugonjwa gani, je huwezi kumusaidia juu haba
viumbe Bako na nguvu Kidogo banaweza kutusaidia
tukatoka huku bien.
Derick: Nikweli Kwani Anasumbuliwa na nini?
Chilunga: weye ungemuangalia juu uko professional
na magonjwa kama haya.
Derick Alitabasamu kisha akaanza kumsikiliza ana
matatizo gani, Derick kwa kuwa alikuwa anauwezo
wa Hali ya juu aligundua mzee Yule anamatatizo ya
moyo ndipo akamuomba Chilunga amletee begi
yake, fasta Chilunga akaleta begi ndipo Derick
akamuuliza: tumfanyie upasuwaji?
Chilunga alitoka nje akaonana na baadhi ya Wazee
kwa kuwa wao mambo ya matibabu wanajua ya
kiasiri hawakuelewa chochote walimruhusu afanye
ndipo Chilunga akarudi ndani ya nyumba ile.
Alipofika alimuomba mwanamke yule atoke, nae
hakuwa Mbishi akatoka na kuwaacha ndani wakiwa
watatu, ndipo Derick akamuuliza Chilunga:
imekuwaje?
Derick: wapo tayari we mfanyie upasuwaji maana
huyu Ndo mkuu wao akipona na Sisi tumepona.
Baada ya dakika kadhaa kupita Derick alikuwa
ameanza kumfanyia upasuwaji mzee Yule huku
akiwa anasaidizana na Chilunga licha ilikuwa hatari
Sana.
Saa moja ilipita huku Sisi tukiendelea kucheza,
upande wa Derick alifanikiwa kumtibu mzee Yule
akamshona freshi akamuwekea dripu ya maji ndipo
Chilunga akasema: weye ni mutu muhimu Sana
Njoo maana Tanzania banakukamata saa liyai.
Derick alitabasamu na kusema: ukiwa umesomea
kitu ni bora zaidi.
Chilunga: by the way! weye ni kipaji ulipewa toka
kwa Mungu, Mbona sote tumesomea ila
uprofeshino huo hatuna lakini ulitembea na vitu
vyote hivyo juu ya nini?
Derick: Sisi ni kama wanajeshi hakuna mwanajeshi
anaetembea bila siraha, ni kama Mimi lazma
nitembee na baadhi ya vifaa.
Chilunga alitabasamu na kusema: Tanzania najuwa
sasa Bako mkulia.
Derick alitabasamu na kusema: naona Huyu mzee
atakuwa sawa.
Muda Huo niliingia nilipoikuta ile Hali nilishtuka na
kusema: mmemfanyia operation?
Derick: moyo ulikuwa tayari imeanza kuoza
kutokana na uvimbe mdogo ulikuwa umejitokeza
pembeni kwahio tumeona tumsaidie.
Nikauliza: sio hatari upande wetu?
Chilunga akadakia: nimeongea nabo bamekubali.
Nikamuuliza: lugha yako na ya kwao si ni tofauti
Sana?
Chulunga: Eee ila Mimi najua kama lugha kumi za
hii pays yetu.
Niliamua kupotezea nikamuomba Derick tutoke nje
tukaongee, kabla hatujatoka nje Waliingia Wazee
kama Sita Wakaanza kumkagua mgonjwa wao,
hawakuongea chochote wakatoka haraka tukabaki
tunaangaliana, nje tukaanza kusikia watu wanapiga
kelele kama vile kuna kitu kimetokea bila kupoteza
muda tukatoka nje ili kuangalia, aisee tulikuta
wenzetu wamewaweka Chini ya ulinzi, hatujakaa
sawa nasi tulikamatwa na kuchwangwa na wenzetu.
Macho yalitutoka huku tukiwatazama wanavyoongea
kwa hasira ndipo Nikamuuliza Chilunga: wanaongea
nini?
Chilunga: wanadai mumemuua mutu yao juu hakuwa
vile.
Nikamuuliza: wanataka watufanyeje?
Chilunga: banata batukule.
Nilichanganyikiwa kwa dakika mbili baada ya
kusikia kuwa wanataka kutufanya msosi ndipo
Nikamuuliza: huwezi kuongea nao?
Chilunga: habaniaminii tena bananiona muongo.
Wenzetu waliposikia hivo Sofia akasema: sasa Sisi
tunageuzwaje chakula Ila muda ule tungeondoka tu.
Nikamuuliza: kwanza Dominic yupo wapi?
Sofia: Mimi sijui.
Dominic muda ule hakuwa Pamoja na Sisi na
hakuna aliejuwa wapi alipo.
Wana kabila lile walikuja na siraha zao ili kuweza
kutukata baadhi ya viungo, wa kwanza kukamatwa
alikuwa Mimi.
Wenzangu walipoona vile walianza kupiga kelele
huku wakijaribu kujitoa kwenye kamba zile ila
matokeo yake walipigwa Fimbo wanaume wote ili
kuwapunguza nguvu, aisee walipigika mpaka damu
zikaanza kuwatoka mwilini.
Muda wote kwangu nilihisi Labda hizo ni story tu za
kusema eti wambote wanakula nyama za watu.
Nikiwa nimetulizwa mbele ya wenzangu ililetwa
jabali kubwa ikawekwa mbele yangu kisha vijana
nane walioshiba wakaja wakanikamata ki sawa
sawa kisha wakaunyoosha mkono wangu wa
kushoto wakauweka kwenye jabali lile.
Presha ilinipanda nikaanza kutoa macho huku
nikijiuliza ni kweli ni Mimi?
Mkaka mwingine Kati ya wale pygmy alikuja na
panga kubwa ambayo imenolewa vizuri mno
ukiiangalia mara nyingi inapatikana machinjoni.
Aisee ile kuiona tu Ndo nikajuwa Kumbe mambo
yanayofanyika yana u serious ndani yake, mkaka
Yule aliponifikia alipandisha panga ile juu huku
akiwa ameweka sura ya kazi.
Aisee uzalendo ulinishinda nikapiga kelele huku
nikijaribu kufurukuta Ila haikuwezekana maana
nilivyokuwa nimeshikwa na wale wa mbote aisee
Ilikuwa ngumu kujitoa kwa wale vijana walioshiba
nyama za watu, taratibu upanga ukaanza kushushwa,
fasta aka.............. Nikabaki nimeshangaa bila
kuamini kilichotokea.
Unahisi nini kitatokea!
Usikose mkasa huu!
 
SEHEMU YA 15
TULIPOISHIA: Aisee uzalendo ulinishinda nikapiga
kelele huku nikijaribu kufurukuta Ila haikuwezekana
maana nilivyokuwa nimeshikwa na wale wa mbote
aisee Ilikuwa ngumu kujitoa kwa wale vijana
walioshiba nyama za watu, taratibu upanga ukaanza
kushushwa, fasta aka.............. Nilibaki
nimeshangaa bila kuamini kilichotokea.
SONGA NAYO!
Taratibu upanga ukaanza kushushwa, fasta
akashusha, kabla hajafikisha kwenye mkono wangu
lisasi ilisikika ikipigwa juu, ikamfanya mkaka Yule
kusitisha tukio lile ikawa kama Pona Pona yangu.
Nilipogeuka nyuma Nilibaki nimeshangaa bila
kuamini kilichotokea maana Dominic alikuwa
ameshikilia bastola yake juu huku akitutazama.
Mkaka Yule aliepewa panga na wana kabila wenzie
ili kukata mikono yetu mmoja baada ya mwingine
alipuuza akapandisha tena panga ile ili kunikata
mikono, haraka akashusha panga Ila kwa bahati
nzuri akapigwa lisasi ya karibu na bega ila
haikuweza kumuingia ilipita na Ngozi tu kisha
akadondokea pembeni.
Walipoona mwenzao amedondokea Chini waliniacha
wakamfuata kumuangalia hali yake, vile vile na
wana kabila wote.
Dominic bila kupoteza muda akatufuata
akamfungulia kamba mmoja Baada ya mwingine
mpaka akafanikisha.
Tukiwa tunajiandaa ili kuondoka mzee flani alinua
uso wake akakunja uso na kuongea maneno flani ya
ajabu huku akiwa anaendelea kututazama.
Kabla hatujapiga hatua yoyote aisee huwezi kuamini
kilitokea kimbunga ambacho wenyewe tulishindwa
kuelewa, kikatukusanya sote tukaanza kuzunguka
kwenye kimbunga kila bila kuona mbele wala hakili
kukaa sehemu moja.
Kimbunga kile cha upepo mwingi Sana
kilitupandisha juu kwa juu huku tukiendelea kupiga
kelele tukiomba msaada, taratibu Kikaanza
kutupeleka sehemu nyingine tofauti na ile.
Wana kabila lile la pygmy walitusindikiza kwa
macho.
Tukiwa tupo angani kabisa, juu ya miti yote iliopo
ndani ya msitu ule wa equatorial Tuliendelea
kubebwa na kimbunga kile kisha kikatusambaza kila
mmoja akaenda sehemu yake.
Aisee balaa tulioikuta katika msitu ule ilikuwa sio ya
kitoto.
Mimi niliweza kuangukia sehemu ambayo Ilikuwa na
Miba mingi, ikanichoma baadhi ya sehemu ya mwili
wangu, Hofu ilinitawala nikatoka eneo lile huku
nikiwa nachomoa chomoa miiba ile.
Upande wa zakayo yeye alidondokea juu ya mti
akanasa, kutoka akashindwa akabaki amening'inia
huku kichwa kikiwa kinaangalia Chini, miguu nayo
Ikiwa imenasa juu.
Profesa Rodrigo Yeye alidondokea sehemu yenye
nyasi nyingi Pamoja na majani.
Upande wa Dominic Yeye haikuwa tabu Sana maana
alidondokea sehemu Salama Kidogo.
Upande wa Patrick alidondokea ndani ya mto ule wa
mwanzo Derick alipodondokea ila tofauti na eneo
lile.
Chilunga upande wake alidondokea juu ya mti
akaanza kutafuta namna ya kutoka Juu.
Amanda yeye alijigonga kwenye kwenye mti flani
akapoteza fahamu hapo hapo.
Derick na Sofia kwao ilikuwa sawa maana
walikutana njiani Wakaanza kututafuta.
Nikiwa nazidi kusonga huku nikiwa nawaita
wenzangu, nilianza kulia kwasababu ya uoga, kwa
mbali nikasikia sauti ya mtu akiomba Msaada ndo
nikajua atakuwa ni moja Kati yetu, fasta nikaanza
kufuata sauti inapotoka.
Nilipofika nilishangaa kuona zakayo akiwa
ananing'inia huku Vitoto vya simba Kama kumi
vikiwa vipo Chini yake huku vikijaribu kuruka ruka ili
kuweza kumfikia, maskini Zakayo aligeuka kama
chizi kwa dakika mbili.
Uoga uliutawala moyo wangu kwa sauti ya Chini
nikajisemea: ukiogopa mwenzio atakufa kiuzembe.
Bila kupoteza muda nikaanza kurudi nyuma,
nikaokota mawe mengi nikayaweka kwenye nguo
yangu, taratibu nikaanza kupanda mti uliokuwa Upo
pembeni yangu.
Nikiwa nipo kwenye mti ule nilianza kupiga mawe
simba wale wadogo bila kuangalia wapi narusha,
kama Kawaida yangu huwa nadata nikiona mambo
ya minyama mikali mikali, nilirusha mawe Kama
Mvua Mpaka mengine nikamrushia zakayo
ikamfanya kurudisha Kumbukumbu zake maana
muda Huo alikuwa sio Yeye kihakili.
Simba wale wadogo walitoka huku wakikimbia mno.
Nilipoona nimewatimuwa Nilicheka kwa Ushindi.
Zakayo akajitahidi akajipandisha juu kisha
akajinasua eneo lile na kushuka Chini huku akiwa
anajisifia kuwa Yeye ndie kajisaidia mwenyewe.
Nikiwa nipo juu huku nikimtazama Zakayo Chini
anavyojigamba nilisikia munghurumo wenye
kishindo kikali nyuma yangu, kwanza nikaganda ili
kusikilizia kwa Mara nyingine, Niliposikia Hakuna
kitu taratibu nikageuka nyuma ili kuangalia je ni nini
kipo nyuma yangu! Au nimetembelewa na Latina?
Aisee huwezi kuamini uso kwa uso na mzee baba
chui mkubwa alieshiba Kumbe mwanzo alikuja
kwenye mti ule ili kumsomea ramani Zakayo muda
ule alipokuwa ananing'inia, na nilipokuja nikapanda
mti chuwi Yule alikuwa pale pale ila sikuweza
kumuona na muda wote alikuwa ananisomea ramani
vizuri.
Aisee kwa hilo sikuweza kuvumilia tena nilijirusha
Chini nikamdondokea Zakayo bila kupoteza muda
Nikanyanyuka na kukimbia mbio, Zakayo
alipoangalia vizuri akaona chuwi anaruka aisee hata
Yeye pia alitoka hapo nduki huwezi kuamini
akanipita hata mimi nilikuwa nimetangulia.
Mbio za chuwi ndugu yangu huziwezi, dakika mbili
tulikuwa tupo sambamba.
Zakayo huwezi kuamini alivaa vazi la ushujaa
akasimama akachukuwa jiwe kubwa kiasi.
Muda Huo mimi na chuwi, chuwi na Mimi.
Chuwi Yule alipoona Kama vile anapoteza Muda
aliruka ili kunirukia kichwani kwa bahati nzuri
Zakayo akampiga jiwe lile kichwani na chuwi yule
akaenda Chini na kuzimia.
Nikiwa nahanya hanya huku nikiwa nipo Kama vile
nimedata, Zakayo alinifuata na kuniambia: tuondoke
Huyu kazimia kwa Muda tu.
Sikuweza kumsikia nikaendelea kusimama huku
nikiwa naangalia chuwi yule alivyomkubwa ndipo
Zakayo akanipiga bonge la kofi na kusema: vipi
Hapo?
Hakili zilirudi na kusema: Eee!!!
Zakayo: mimi ni nani?
Nikamjibu: wewe Zakayo.
Zakayo: sawa hakili zimerudi.
Nilipoangalia Yule chuwi kwa Mara nyingine nilipiga
kelele maana nilikuwa sijitambui tena.
Moja kwa moja tukatoka hapo nduki.
Upande wa Derick na Sofia story zilikuwa
zinaendelea.
Sofia: Chilunga aliniahidi tukitoka hapa Salama
atanioa ila nahofia tunaweza kupoteza maisha Sisi
wote.
Derick: hapana tutaishi.
Sofia: kwa baridi hii wallah Hakuna mtu anaweza
kuishi.
Derick: sisikii baridi yoyote Mbona.
Sofia: ni kwasababu tuna Hofu muda wote, subiri
wewe ukienda mjini ugonjwa utaamka kutokana na
nyoka yule aliekumeza, pili huu mchoko nahisi
wengi tutafika na kufa hapo hapo.
Waliendelea kusonga huku wakizidi kupiga story.
Upande wa Chilunga alianza kututafuta huku na kule
kwa bahati nzuri akamuona Amanda alipojigonga
kwenye mti akazimia, fasta akamfuata, alipomfikia
alimuamsha kwa dakika kadhaa Amanda akazinduka
na kusema: twende party.
Chilunga alitabasamu na kusema: inaonekana weye
ulikuwa unapenda mambo ya kujirusha saa mie.
Amanda: tupo wapi?
Chilunga: tumerushwa na ba pygmy.
Amanda: wenzetu wapo wapi?
Chilunga: ondoa Hofu tutabapata saa hii.
Amanda: Asante kwa Msaada wako.
Chilunga: niwaajibu wangu kumusaidia mwanamke
wa Kiana saa weye.
Amanda: mwanamke wa Kiana?
Chilunga: Eee weye ni mrembo.
Amanda alitabasamu na kumjibu: Asante.
Chilunga: Natamani tutoke eneo hili nikupeleke
Kinshasa nikakutambulishe na ba papa ba kule
Bako na franka mingi Sana, unajuwa Cherie weye
Upo tofauti Sana uko Jolie.
Amanda: mbona Jolie ulisema ni Najma.
Chilunga: yule nilimsifia ili asijione wajabu
mugroupe yetu, mama weye unabakula namba
kwanza usitetemeke juu ya baridi niko hapa.
Alivua nguo yake ya Juu akabaki kwenye singledi
kisha akampa Amanda avae, hakika kwa muda Huo
Amanda alijiona mwenye bahati sana, ndipo kwa
sauti ya madeko akasema: Mbona upo karibu sana
na Sofia?
Chilunga: kale ni kakatuni mama!
Amanda alicheka na kusema: yaani Chilunga wewe!
Chilunga: ntakupatia madolla, ntakupatia ma
diamond mengi shie kwetu tuko na ma diamond
mengi Cherie, je nikupe ya kuyala ndoo au pipa?
Hapo alimumaliza Amanda, alinyanyuka na
kumkumbatia, Chilunga kama Kawaida ya wanaume
wa kikongo kupetepeti, alianza kumchezea huku
akiwa anamuimbia lumba taratibu.
Wakiwa wanaendelea kucheza kwa furaha na Utani
mbali mbali, Amanda alichukuwa jiwe dogo mno
akamtupia Chilunga kiutani ila kwa bahati mbaya
jiwe lile likaenda kupiga kitu flani kilikuwa pembeni,
aisee huwezi kuamini Kumbe ilikuwa ni ile nyoka
yenye kichwa cha binadamu, hasira iliipanda baada
ya kuona kama vile inachokozwa hali ya kuwa
ilikuwa imetulia zake.
Hapo hapo nyoka ile yenye kichwa cha binadamu
ilijinyoosha haraka na ku.........
Unahisi nini kitatokea!
Usikose mkasa huu!SEHEMU YA 16
TULIPOISHIA: Hapo hapo nyoka ile yenye kichwa
cha binadamu ilijinyoosha haraka na ku.........
SONGA NAYO!
Nyoka ile yenye kichwa cha binadamu Ilijinyoosha
haraka na kuwachota mtama wote wawili Amanda
na Chilunga wakaenda Chini, ile Hali ya kuona
kiumbe kile kikiwaangalia kwa hasira walipiga
kelele ikapelekea Sisi wote kuwasikia, kila mmoja
akafuata sauti ile.
Amanda na Chilunga wakanyanyula na kuanza
kukimbia Ila nyoka yule kama Kawaida humfuata
mtu aliemuuzi, fasta ikaanza Kumkimbiza Amanda.
Haikuchukuwa Muda sote tulifika eneo la tukio.
Maskini Amanda hakupiga hata hatua tano nyoka
yule alimzingira akamkunjia katikati huku Sisi kila
mtu aliokota chochote ili kumuokoa kisha tukaanza
kumrushia nyoka yule, wengi tulikuwa na mawe Ila
haikusaidia chochote.
Dominic alichomoa bastola yake akampiga lisasi
nyoka yule Ila huwezi kuamini zilidunda na
mwishowe lisasi ziliisha tukaendelea kuangalia
Kama show bila kukimbia.
Amanda akiwa anaomba msaada huwezi kuamini
nyoka yule akiwa amemkaba kisawa sawa kama
Kawaida ya nyoka wakubwa kama chato mara
nyingi kwa kuua huwa anajikunjia kwa mtu kisha
anajinyoosha huku akiwa anavinja vunja mifupa ya
mwilini ya mwadamu yule.
Nyoka yule alijinyoosha huku Amanda akizidi kupiga
kelele, alipohakikisha amemaliza kumvunja vunja
mifupa alimuacha hapo na kuondoka zake bila
kuzuru watu wengine.
Amanda moja kwa moja alienda Chini, damu
zilianza kumtoka puani, maskioni pia na mdomoni,
Tulimuwahi sote kwa Pamoja tukamshika huku
tukimtaka asiweze kufariki.
Amanda akiwa anatetemeka alisema kwa sauti ya
Chini mno: specialist Derick unahitajika kuendelea
kuishi, wewe ni muhimu Sana kwa watu wote.
Derick alilia mno na kusema: hata wewe pia
unahitajika kuendelea kuishi.
Amanda alitabasamu na kupoteza maisha akiwa
yupo kwenye mikono ya Derick.
Nguvu zilituishia, kulia tulishindwa maana kama
kulia tulilia sana mpaka machozi yakakauka, kila
mmoja hapo alishuka Chini na kukaa huku akihisi
Labda Yeye ndie anaefuatia.
Chilunga kwa uchungu aliangua kilio na kusema: I'm
sorry Amanda Labda mie ndie chanzo cha Kifo
chako.
Sote hatukuweza kumuelewa wala hatukutaka
kujuwa.
Tukiwa tupo hapo huwezi kuamini Latina nae
alitokea nyuma ya Chilunga, sote baada ya kumuona
tulinyanyuka haraka na kukimbia, ile Chilunga
anaangalia nyuma Aisee alitabasamu kimoyo moyo
akijisemea: ndio mwisho wangu.
Nikweli Latina hakuchukuwa Muda alimshika
shingoni akaingiza kucha zake ndefu kisha
Akachomoa koo ya Chilunga, sauti ya mwisho
tuliisikia akikoloma Chilunga.
Kukimbia kwetu tulikimbia huku kila mmoja akiwa
Analiamno, mwishowe Tulifika sehemu flani
tukasimama huku kila mmoja bila kumuongelesha
mwenzie.
Tulikaa kimya kama dakika kadhaa ndipo profesa
Rodrigo kwa sauti ya huzuni akasema: tunafanyaje,
je turudi au tusonge?
Patrick kwa hasira akasema: huu ni upumbavu tupo
tunafanya, watu tumeisha, mtu mmoja mmoja
anaondoka, Ipo siku hata Sisi hapa tutakufa, huu ni
ujinga tupo tunafanya.
Zakayo akasema: siku ile Labda tungemuamini
Najma tukarudi nyuma Labda sote tungekuwa
wazima kwa sasa.
Alitukumbusha siku ile nawaambia tupo hatarini
maana niliona fuvu nyuma yangu ila hawakuweza
kuniamini.
Abdul kwa hasira akasema: mi narudi nyuma kama
nikufa bora nife nikiwa narudi nyumbani.
Patrick na Zakayo walimuunga mkono ndipo
Dominic akasema: Kwani mnahisi mkirudi nyuma
ndo mtakuwa mmepata ufumbuzi wa tatizo hili?
Kumbukeni hapa tulipo hatujui tupo wapi, hatujui
tunaelekea wapi, je! mkisema mnaondoka mtaenda
na njia ipi?
Hawakuweza kumsikiliza wakaondoka kwa hasira.
Tulibaki hapo kila mmoja akiwa anawaza yake,
muda Huo Sofia alikuwa anamlilia mpenzi wake
Chilunga, nilipoona ni kama mpweke sana
Nilimsogelea pale alipo na kumuambia: pole Sofia
jikaze my dear.
Sofia alinikumbatia na kusema: nahofia maisha
yangu, tafadhali niweze kuishi, mama, ndugu zangu
wote wananitegemea mimi Halafu mimi ndie
niliteuliwa kwenye familia yetu nikasomeshwa ili
niweze kuiokoa familia yetu, ntafanyaje sasa Mbona
hata mpenzi wangu ameondoka.
Nilimtuliza na kusema huku nikiwa nimeanza kulia:
hata mimi my dear ni hivo hivo, kwanza wewe ni
bora zaidi yangu, mimi baba yangu yupo jela, mama
yangu nimgonjwa wa hakili na mdogo wangu wa
pekee sijui kama ntamuonaga tena, jipe moyo
tutafanikiwa.
Baada ya muda tulikaa mimi na Derick huku
tukipiga story.
Derick: ndoto za watu wengi zimeishia hapa.
Nikamjibu: hata Sisi pia tupo njiani.
Derick: hivi wewe usingekuwepo je! hii misuko suko
ningeiweza?
Nilitabasamu na kumuuliza: Kwa nini Unasema
hivo?
Derick: kwasababu nikikuona ukiwa bado upo na
mimi napata nguvu.
Nikamjibu: furaha yangu ni Latina aweze kuwa hai.
Derick: kwahio mimi Sina nafasi kabisa?
Muda Huo Dominic alikuwa anatuangalia, baada ya
Derick kugundua kuwa Dominic anatuangalia
aliniambia: Dominic ni kama anahisia na wewe za
kimapenzi.
Niligeuka nikamtazama Dominic tukakutanisha
macho kwa aibu kila mmoja akaangalia Chini ndipo
nikasema kwa sauti ya Chini: wengi toka tuanze
mpela mpela masuala ya mapenzi walisahau.
Derick: kama Mimi sometimes huwa nakusahau.
Nilitabasamu na kusema: si unaskia sasa kumbe
yote ulikuwa unanidanganya.
Derick: simu yangu yenye vitu vya thamani
imepotea.
Nilishtuka na kumuuliza: ilipotelea wapi?
Derick: nahisi Muda ule tunapeperushwa na
kimbunga.
Nikamjibu: si unaona sasa! Siku ile unakoswa
koswa na Mbwa mwitu ungekufa kisa hio simu na
ajabu imepotea tena.
Derick: sitaki kuifikiria Sana kwasababu naweza
kuchanganyikiwa.
Upande wakina Zakayo walikuwa wanazidi kusonga
mbele bila kujuwa wanaelekea mashaliki au
manghalibi ndipo Zakayo akasema: toka nizaliwe
nilikuwa naona kwenye movie haya mambo.
Patrick: simu imebaki na asilimia moja izime
kwanza Nikifika nyumbani naweka bonge la part.
Abdul: Mimi ntaitisha wanawake wa kila Aina kama
ishirini waje kunikanda kanda kwanza.
Walicheka kwa Pamoja ndipo Patrick akasema: ila
inashangaza Kidogo ile nyoka ilimuua Amanda Ila
Sisi ikatuacha na muda ule tulikuwa kama vile
hatujielewi.
Zakayo: nahisi kuna kitu kilitokea Ndo maana.
Patrick: mrembo Kama Amanda unajua kwao
wanapesa ndefu kiasi gani, sijui hii taarifa ikiwafikia
wazazi wake itakuwaje.
Abdul: mzungumzieni Huyu Derick kwanza sijui Kwa
nini alikuja huku.
Zakayo: kale kajamaa usikaone kapo pale kana hela
Mpaka zingine ni chakula cha panya.
Wakiwa wanazidi kusonga mbele huwezi kuamini
Latina alitokea mbele yao, Watoto wakiume nguvu
ziliwaishia wakaendelea kumshangaa huku kila
mmoja akiwa anajiuliza ni mimi au.
Ile wanataka kurudi nyuma ili wakimbie, Abdul
ali.............. Wote wakashangaa huku Patrick akiwa
anatafuta simu yake mfukoni.
Unahisi nini kitatokea!SEHEMU YA 17
TULIPOISHIA: Ile wanataka kurudi nyuma ili
wakimbie, Abdul ali.............. Wote wakashangaa
huku Patrick akiwa anatafuta simu yake mfukoni.
SONGA NAYO!
Abdul alikamatwa na Latina akageuzwa wakawa
wanaangaliana uso kwa uso, Zakayo na Patrick
wote wakashangaa huku Patrick akiwa anatafuta
simu yake mfukoni.
Alifanikiwa kuitoa Ila alichelewa ku play muziki
maana Latina aliingiza kucha zake kwenye tumbo ya
Abdul na muda Huo muziki Ukaanza kulia.
Latina kusikia muziki tu alichomoa mkono kutoka
ndani ya tumbo ya Abdul kisha akaanza kucheza.
Abdul kwa kuwa damu zilianza kumbubujika alikosa
nguvu akadondokea Chini.
Zakayo na Patrick walimuwahi mwenzao Wakaanza
kumburuta Chini ili waweze kuondoka nae ila Abdul
alimshika mkono Patrick na kumuambia kwa sauti
ya maumivu mno: kimbieni, niacheni jamani.
Patrick akiwa ameanza kulia akasema: lazma
twende wote Jikaze.
Abdul: ulisema chaji inaisha muda wowote ondokeni
sasa.
Maskini Abdul alizidi kuwasisitiza wenzie waondoke
haikuchukuwa sekunde nyingi akapoteza maisha
papo hapo, ukweli Zakayo, Abdul Pamoja na Patrick
walikuwa ni marafiki wakubwa toka wapo chuo,
walianza kumlilia mwenzao bila kupoteza muda
wakanyanyuka na kuanza kukimbia na muda Huo
muziki ulikata Latina akawaangalia wanavyokimbia.
Mbio za Kina zakayo na fujo zao Tulianza kuzisikia
ikatufanya kusimama ili kuangalia nikipi
kinaendelea.
Baada ya muda walitufikia huku wakipumua kwa
kasi kubwa, ndipo nikawauliza: mwenzenu yupo
wapi?
Walianza kulia kuashilia hatupo nae tena.
Baada ya muda Walitupa mkasa mzima kuhusu
kilichotokea ndipo Derick akasema: simu ni
muhimu kwetu.
Nikasema: hapa aliebaki na simu ni Dominic tu.
Dominic alichomoa simu ile ndogo akanikabidhi na
kusema: itakusaidia.
Nilichukuwa na kumuuliza: Mbona inawaka Waka
hivi?
Dominic: maji yameingia ndani.
Profesa Rodrigo akasema: viherehere vyenu
vimemponza mwenzenu.
Patrick na Zakayo Waliendelea kujilaumu.
Sofia akamuambia Dominic: wewe ni mwanajeshi
Huna mbinu yoyote kuhusu Huyu kiumbe?
Dominic akamjibu: Huyu kiumbe ana nguvu za
miujiza unahisi ni simba au chuwi?
Sofia: sasa tunafanyaje?
Dominic: kilichopo ni Sisi kuanza mchaka mchaka
bila kupumzika tuelekee huko kunakosadikia mti
ndo Upo.
Sofia alianza kulia upya.
Muda Huo profesa Rodrigo alikuwa kwenye msongo
wa mawazo akiwa anaangalia pembeni.
Tulikaa hapo bila kujali Latina atakuja au laa,
maana watu wote tulikuwa tumechoka mno Istoshe
hata njaa Ilikuwa inatusumbua.
Siku hio tulitulia pale mpaka Majira ya usiku
tukalala pale pale.
Asubuhi ilipowadia Dominic alituamsha haraka
haraka akisema: muda ndo huu tuanze mchaka
mchaka.
Tuliamka kwa unyonge mwigi kisha safari ikaanza,
cha kwanza Tulianza kutafuta wapi mto ulipo Patrick
akatupa maelekezo maana mwanzo Yeye ndie
alidondokea kwenye mto ule Baada ya
kupeperushwa na pygmy wale.
Tulipofika kwenye ule mto tulivaa Nyoyo za
kikomando tukakubaliana kufa ama kupona ilimradi
tuwe tupo Tunapambana, bila kupoteza muda
tulianza mbio kupanda Juu ili tuweze kupata
mwanzo wa mto ule maana inasadikika ndiko mti
ule upo.
Tukiwa tupo njiani sauti nzito tuliiskia ikisema:
ntaua mmoja baada ya mwingine.
Sote tukajawa na uoga maana aliesema hivo
mwanzo ni yule kiumbe aliemuingia mwilini Latina,
Dominic alipoona tunaanza kupunguza kasi kwa
kukimbia alisema: kuweni mashujaa msiogope
tukaze mwendo.
Tukiwa tunazidi kukimbia Sofia alisimama na
kusema: siwezi kuendelea.
Dominic alirudi nyuma na kumuuliza: huwezi
kukimbia tena?
Sofia akiwa anahema vibaya akasema: siwezi
nendeni tu naona ntakuwa mzigo bure kwenu.
Dominic akambeba mgongoni na safari ikaendelea.
Tulizidi kusonga mbele muda Huo Patrick na
Zakayo walikuwa nyuma yetu huku wakiwa
wanakimbia wanapiga story.
Zakayo: tukipona tutapelekwa tukaokoe watu
Somalia maana Sisi ndo tutakuwa wanajeshi mahili
kuliko wote.
Patrick: unahisi haya ni mazowezi ya vitani?
Zakayo: Eee kwasababu vitani inatakiwa uwe na
moyo mgumu Kama huu tulionao, Unamuona
mwenzio anafariki ila unasonga mbele.
Patrick: bunduki unaweza kuikama vizuri?
Zakayo: aaahhh Patrick kama umeweza kuishi
mpaka sasa si unaona kuwa wewe ni shujaa.
Patrick: kuishi kwetu mpaka sasa hivi sio ushujaa
wala nini ni Mungu tu.
Zakayo: umenifunga ila acha kuendea nyuma kama
eagle.
Patrick: nimechoka sana ni ile kujikaza tu.
Upande wa Dominic, Sofia alimuonea huruma
Dominic akamuomba amshushe ndipo Dominic
akamuuliza: utaweza kukimbia?
Sofia: ntaweza Nashukuru.
Dominic Alimshusha Chini Wakaanza kukimbia kwa
Pamoja.
Upande wa kina Patrick nyuma yao Zakayo alimuona
Latina akiwa anatufuata mdogo mdogo, kwa sauti
ya Juu sana akasema: kimbieni sana anakuja.
Patrick alipoangalia nyuma yake akajuwa hapa yeye
ndie atakuwa wa kwanza.
Tuliongeza spidi Ila Patrick alikuwa nyuma yetu Sisi
wote.
Zakayo ile Hali ya kukimbia Kimbia bila kuangalia
huku wala kule aliweza kufinyaga karibu na mti flani
ulikuwa umesimama freshi, Kidogo mguu wake
ukaponyea Ila akafanikiwa kupita Salama, Patrick
alipofika pale zakayo alipotaka kukwama huwezi
kuamini Kumbe mti ule kwa Chini ulikuwa tayari
umeoza muda mrefu kutokana na ardhi kuwa
nyepesi sana maana Mvua kila muda inanyesha
ndani ya msitu ule, aisee mguu wa Patrick ulizama
Kidogo papo hapo mti ukakatika na kumuangukia
kiunoni kisha Patrick akaanguka Chini, kujinasua
sehemu ile akashindwa akaanza kuomba msaada
kwetu Maana Latina alikuwa anasogea mdogo
mdogo.
Tuliposkia kelele za Patrick tulisimama na kugeuka
nyuma, aisee mwenzetu tulimuonea huruma sana
kwa wakati ule maana hakuna ambae angeweza
kumsaidia ndipo Dominic kwa sauti ya Juu
akamuambia: jaribu kujitoa hapo.
Patrick akamjibu: nendeni tu hapa siwezi kutoka
eneo hili.
Latina akamfikia Patrick, bila kupoteza muda
ali.............sauti ya Zakayo ilisikika akisema: no!!!!!
Unahisi nini kitatokea!
Usikose mkasa huu!
 
SEHEMU YA 18
TULIPOISHIA: Tuliposkia kelele za Patrick
tulisimama na kugeuka nyuma, aisee mwenzetu
tulimuonea huruma sana kwa wakati ule ndipo
Dominic akamuambia: jaribu kujitoa hapo.
Patrick akamjibu: nendeni tu hapa siwezi kutoka
eneo hili.
Latina akamfikia Patrick, bila kupoteza muda
ali.............sauti ya Zakayo ilisikika akisema: no!!!!!
SONGA NAYO!
Bila kupoteza muda Latina alimkata kichwa Patrick
kupitia kucha zake ndefu zenye ukali kuliko hata
wembe mpya, maskini kichwa cha mwenzetu Patrick
kikandondokea pembeni tukiwa tunashuhudia.
Sauti ya Zakayo ilisikika akisema: no!!!
Dominic alimuwahi Zakayo akamshika mkono
tukaanza kukimbia.
Majira ya Mchana baada ya kukimbia makilometa
mengi bila kupumzika tulisimama ili kujipumzisha.
Zakayo alikuwa amejiinamia muda wote ndipo
Nikamuuliza: umekata tamaa?
Zakayo aliniangalia na kuniambia: muda mwingi
kwa kuwa uso ni wa mdogo wako nahisi Labda ni
mchezo mnatuchezea ila sio kweli ni fikra zangu
mbovu.
Nilitabasamu kwa uchungu nikasema: yeah ni kweli
lazma makosa yote niyabebe mimi maana Yule ni
mdogo wangu na kila mtu anajifikiria kwa nini
Najma Hafi Wengine Ndo wanabaki wanakufa tu?
Zakayo Akanijibu: neno la muhimu ambalo Patrick
aliongea mara ya mwisho aliniambia Sisi tuliohai
tusijione mashujaa kwasababu hatujafa, Hapana!
Kila mtu anakufa kwa wakati wake na yote ni
mipango ya Mwenyezi Mungu.
Nikamjibu: Asante kuona hilo unalijua.
Profesa Rodrigo akauliza: tumebaki na kilometa
ngapi?
Dominic akamjibu: sio nyingi tunataka kufika.
Tulifurahi na kumuuliza: kufika?
Dominic: msipatini.
Sofia akiwa ametulia zake akasema: naskia njaa
jamani.
Nikamuambia: my dear Vumilia, hapa matunda
tunayatoa wapi?
Sofia: ukweli siwezi kupumua tena.
Dominic akasema: mnisubiri naenda kuwataftieni
chochote.
Nilishtuka na kumuuliza: utakuwa Salama kweli?
Dominic: Mungu ndie anaelinda si ndio
mlivyosema?
Niliendelea kumtazama kisha akaondoka.
Derick akiwa ametulia Nilimsogelea na kumuambia:
ukiwa kwenye Hali hio vipi kuhusu Sisi.
Derick: nahisi kitu tofauti Sana ndani ya mwili
wangu.
Nikamjibu: utakuwa ni uchovu tu we usijali.
Derick: ni kweli vipi kuhusu wewe Upo Salama
mwilini?
Nikamjibu: nipo freshi licha harufu ya mtoa roho
nabaki naisikia kila muda.
Derick alitabasamu na kusema: una maana Kifo
kipo karibu na wewe.
Nikamjibu: kipo karibu yangu kuliko moyo wangu.
Derick: usikate tamaa.
Nikamuambia: kila mtu anakuambia wewe uweze
kuwa hai.
Derick: kwasababu wanahisi mimi ni muhimu ila
wanasahau mbele ya Kifo hata uwe umehifadhi
vitabu vya kila Aina kichwani ili kusaidia watu, Kifo
kikiwa kimekulenga haijalishi, nakumbuka enzi za
zamani kuna mama flani Alikuwa ndani ya pango na
mwanae mchanga sana na pango hilo lilikuwa mbali
mno ambapo watu kufika eneo lile inachukuwa
miezi kadhaa ila huwezi kuamini Kifo kilimfikia
mama Yule akiwa yupo pangoni na mwanae
mchanga akapoteza maisha akamuacha mwanae,
jiulize Yule mama ni bora kiasi gani kwa mtoto
wake muda ule ila akachukuliwa sembuse mtu
Kama Mimi.
Nilishusha pumzi na kusema: kwa story yako
umenifanya nisiogope Kifo.
Derick: lazma uogope maana kinaogopeka sana.
Nikasema: Kitambo Sana Sijaiskia story zako hivi
Derick uliwazaje kukaa kimya bila kuongea na mimi
kipindi kile chote?
Derick alijishika masikio na kusema: Nisamee sijui
mwenyewe.
Nilitabasamu na kusema: sijui tukifa tutaonana tena.
Derick: maneno gani unaongea!
Muda Huo Dominic alifika akiwa na matunda sote
tulipomuona tulifurahi maana tulitegemea
hangeweza kurudi ndipo nikamtania: tulikuwa
tumesubiri kusikia msaaaadaaaa!!!
Wote walicheka kisha Dominic akaweka Chini
matunda Yale na kusema: Tuleni ili kesho
ikiwezekana tuanze mchaka mchaka.
Nikasema: ninavyokimbia muda mwingine nahisi
nimewekewa miguu ya bandia maana maisha yangu
ya Kawaida tu huwezi niambie kuhusu kukimbia
mimi.
Dominic akaniuliza: huwa haufanyi mazowezi?
Nikamjibu: ya nini sasa!
Sofia akadakia: sio wewe mwenyewe mimi hapa
nakuwaga kama kiwete Ila ninavyokimbia
mwenyewe sijiamini.
Zakayo akasema: jamani hapa Sina imani ya kuishi
tena Naomba ujumbe huu atakaefanikiwa kupona
awafikishie wazazi wangu waambieni hivi nilikuwa
kwenye harakati ya kutafuta maisha Ila Nawapenda
Sana.
Profesa Rodrigo alichukia na kusema: unaongea nini
sasa!
Nikadakia: Mwaya hata mimi atakaefanikiwa kupona
aende kuangalia hali ya mama yangu kwenye
hospitali ya vichaa Ila usimuambie chochote pili
nenda umuangalie baba yangu jela umuambie Mimi
na Latina tunamsalimia sana Ila usimuambie kuwa
nimeshakufa.
Sofia akasema: Mimi utaambia familia yangu Yule
mtoto wetu wa mwisho wamsomeshe kama Mimi ili
kesho aje kuwasaidia maana Mimi sintoweza
kufanya hivo.
Nilianza kulia nikisema: naongea hivi mpaka
uchungu nauamsha tena.
Derick: sote hapa tutapona masuala sijui ya
kumtuma mtu flani acheni.
Siku iliofuata Tulianza mchaka mchaka upya,
tulikimbia mpaka Majira ya saa tisa Mchana,
tulipunguza spidi maana tulikuwa tumechoka, tukiwa
tunazidi kusonga mbele Sofia aliona kitu mbele
Kama kisiki cha mti mkubwa akakifuata na kukaa
juu huku akisema: ngoja tupumzike kwanza.
Nilipoangalia vizuri nikakumbuka siku ile mimi
niliona kitu kama hicho nikapanda juu matokeo yake
nilichofanyiwa sintoweza kusahau, kwa sauti ya
Chini nikamuambia: toka hapo!
Sofia akaniuliza kwa sauti ya Juu: nini na wewe!
Aisee nyoka yule mwenye kichwa cha binadamu
Alimrusha juu ya miti kisha akamfuata na............
Huku Sisi tukiwa hatuelewi ni nini kinaendelea.

SEHEMU YA 19
TULIPOISHIA: Nilipoangalia vizuri nikakumbuka siku
ile mimi niliona kitu kama hicho nikapanda juu
matokeo yake nilichofanywa sintoweza kusahau,
kwa sauti ya Chini nikamuambia: toka hapo!
Sofia akaniuliza kwa sauti ya Juu: nini na wewe!
Aisee nyoka yule mwenye kichwa cha binadamu
Alimrushia juu ya miti kisha akamfuata na............
Huku Sisi tukiwa hatuelewi ni nini kinaendelea.
SONGA NAYO!
Nyoka yule mwenye kichwa cha binadamu baada ya
kumrusha juu ya miti Sofia alimfuata na kupotea nae
Huku Sisi tukiwa hatuelewi nini kinaendelea.
Macho yalitutoka tukaanza kumuita Ila haikusaidia
chochote ndipo Dominic akasema: Kumbe huyu
kiumbe ana nguvu za miujiza!
Nikasema: nahisi ukimchokoza akiwa ametulia zake
anakuua.
Derick: muonekano wake alikuwa ni mtu hatari
Sana.
Rodrigo: kwasababu anatembelea laana.
Zakayo: vipi kuhusu mwenzetu?
Rodrigo: Sofia?
Zakayo: Ndio.
Rodrigo: habari yake imeishia hapa si unakumbuka
Amanda kilichomtokea.
Zakayo: aisee Na maneno alioyaongea Jana Kumbe
alikuwa yupo serious.
Rodrigo: tunafanyaje? Kama muonapo tumebaki
wachache mno.
Dominic: hapa Hamna kurudi nyuma lazma
tupambane hata akibaki mmoja usife kizembe
Pambana ufe ukiwa upo kwenye harakati kwasababu
tukisema turudi nyuma tunasafari ndefu kuliko hii
tumebaki nayo ili kumaliza tatizo hii, pili tutakufa
wote.
Zakayo: Ni kweli maana siku ile mimi na wenzangu
tulihisi tukisema tunaachana nayo tutapona kumbe
tatizo lipo pale pale.
Nikasema: yule mzungu maskini ningemuona tena
Labda angetupa miindumbinu mingine.
Dominic: acha kumfikiria yule, kama ni Msaada
tayari ametusaidia vya kutosha hapa kilichobaki ni
Sisi wenyewe kujibeba.
Nikamuuliza: tunajisaidiaje kwa Mfano?
Dominic: tusonge mbele.
Tulianza safari tukiwa tumebaki jeshi ya watu wa
tano hali ya kuwa tulikuja tupo watu zaidi ya kumi
na 15.
Njia nzima kila mmoja alikuwa anamuomba
Muumba wake huku pia akiomba wazazi wake kwa
Hisia wamuombee msaada kwa Allah, Hofu na
uoga tuliokuwa nayo Ilikuwa sio ya Kawaida,
nilipojaribu kumkumbuka Sofia Aliposema kuwa Ana
njaa Nikakumbuka tena maneno alioyaongea kama
ujumbe kwa familia yake aisee machozi yalianza
kunitiririka mashavuni.
Majira ya usiku tuliweza kupumzika Kwa Muda,
Usingizi Hakuna alieweza kuupata ndipo nikasema:
muda kama huu huu ndugu yetu Sofia tulikuwa nae.
Zakayo Akanijibu: unajua Najma Tukifanikiwa kutoka
hapa wengi tutapata maradhi mengi sana.
Nikamjibu: sometimes nafikiria kwa nini Nilikuja
huku nakosa majibu yake.
Zakayo: Ni kweli Ukiona nchi za ulaya na ndo watu
wanajifanya viherehere kwa maswala kama haya
wapo zao kimya wala hawataki kufuatilia, Ila Sisi
toka nchi yetu iumbwe Hakuna mtanzania aliewahi
kuvumbua kitu chochote kupitia Utafiti wa
kuzunguka eneo hatari kama hii ili basi Na Sisi
tuseme tumekuja huku kwasababu mtafiti flani
aliwahi kwenda sehemu flani akafanya hivi akarudi
Salama Hakuna ndo tunategemea tutapona kweli!
hili tayari limeshakuwa tatizo ndoto za watu 16 wote
zimepotea kirahisi rahisi kweli?
Nikamuuliza: wewe kama vile hauamini
kinachoendelea?
Zakayo: naamini sana sema tu najilazimisha
kutokuamini.
Nikamuuliza: kwanza nimekumbuka kuna Jambo
flani silielewi, hivi muda ule ili mti umdondokee
marehemu Patrick ilikuwaje?
Zakayo: mwenyewe sielewi, ila nahisi nilivyokuwa
nakimbia kuna sehemu nilifinyaga nahisi ule Mti
ulikuwa mbovu kutokana Chini ulikuwa kama vile
umeoza.
Ndo nikapata picha na kusema: Ndo maana
ulikatika hii ardhi nahisi sio nzuri.
Zakayo: Ipo baadhi ya miti hukuwa vizuri kutokana
na hii Mvua ya kila siku ndo maana unaona ni
mirefu sana na mingine ili iweze kuwa na hafya
nzuri yahitaji Mvua na jua, mambo hayo mawili moja
ikikosekana matokea yake ni Yale.
Nikamjibu: wewe mambo mengi unayaelewa sana.
Zakayo: Nina Jamaa yangu Anaitwa Philip maswala
ya Utafiti ni namba one, lugha anazozijua kingereza,
kiswahili, kifaransa, kichina na huku Kongo anajua
lugha Kama Sita za kabila tofauti.
Nilishangaa na kumuuliza: Yeye ni kabila gani?
Zakayo: nimkongo ila kabila yake Mbembe.
Nikasema: Oohh kabila moja na Yule mama nyoka.
Zakayo: eeehh ila anaishi dar es salam.
Nikamuuliza: anasoma chuo gani?
Zakayo: amehitimu, nimtafiti mzuri sana Mara nyingi
anatembea nchi mbali mbali.
Nikamuuliza: Kumbe tajiri!
Zakayo: Hana hela nyingi Ila ni mtu mwenye hakili
nyingi, si Unajuwa ukiwa mwenye hakili huwezi kufa
na njaa.
Nikakubali na kumuuliza: Kwa nini hakuungana na
sisi kwa hii inshu?
Zakayo: Alikataa.
Nikamuuliza: au anajua kilichomo humu?
Zakayo: may be! ila sina uhakika.
Nikamuuliza: ulimjuaje?
Zakayo: mwanafunzi mwenzangu tulikutania mwaka
wa pili university ya Uganda.
Nikamuuliza: ulisoma international university
Makerere?
Zakayo: yeah! Mwaka wa kwanza na wa pili.
Nikasema: Oohh! naona wote wamesinzia.
Zakayo: wataamshwa na kelele zetu wasubiri tu.
Nikamjibu: Natamani tuliobaki hapa tufanikiwe
kutoka Salama.
Zakayo: sio wewe tu hata mimi pia.
Nikasema: muda ule tupo kwenye kile kimbunga
cha wale pygmy si Unajuwa tulikuwa tupo juu ya
msitu wote!
Zakayo: Eeeee.
Nikamjibu: nilitamani kupiga kelele ikiwezekana
Tanzania wasikie.
Zakayo: ungesemaje?
Niliweka mikono yangu kwenye mdomo kisha
nikasema: jamani msaada tumekwama hukuuuuuu!!
Zakayo alicheka huku akiendelea kuniangalia.
Baada ya muda tuliamshwa asubuhi na sauti za
ndege tukaamka kila mmoja akiwa anajishangaa
kulala muda mrefu namna ile, maana ilikuwa tayari
saa 2 asubuhi.
Dominic alinipa mkono nikamshika kisha akaniinua
na safari ikaanza.
Mchaka mchaka kama Kawaida yetu tulikuwa
tunakimbia, njiani nguvu ziliniishia nikasema huku
nikikimbia: pumzi inakata.
Derick ambae alikuwa karibu yangu akaniambia:
jikaze muda si mrefu tunafika.
Tukiwa tunazidi kusonga mbele aisee huwezi
kuamini Latina alipita karibu na zakayo kama radi
aka............... Zakayo akapiga kelele kwa maumivu
makali.

SEHEMU YA MWISHO YA 20
TULIPOISHIA: Mchaka mchaka kama Kawaida yetu
tulikuwa tunakimbia, njiani nguvu ziliniishia
nikasema huku nikikimbia: pumzi inakata.
Derick ambae alikuwa karibu yangu akaniambia:
jikaze muda si mrefu tunafika.
Tukiwa tunazidi kusonga mbele aisee huwezi
kuamini Latina alipita karibu na Zakayo kama radi
aka............... Zakayo akapiga kelele kwa maumivu
makali.
SONGA NAYO!
Latina alipita karibu na Zakayo kama radi akamkata
mkono akaenda nao, Zakayo akapiga kelele kwa
maumivu makali.
Tulimuwahi mwenzetu tukamshika huku tukimuuliza
hali yake, maskini Zakayo alilia mno kwa maumivu
huku akisema: Kwa nini asingeniua tu.
Nilimziba mdomo na kumuambia: usiseme hivo
jitahidi twende.
Zakayo: Naumia Sana dada yangu mwenzio siwezi
kuyavumilia haya maumivu.
Nilianza kulia huku nikizidi kumpa moyo.
Baada ya muda Nilimpa profesa Rodrigo kasimu
kale kabatani nilikopewa na Dominic ndipo profesa
akaniuliza: Unaogopa?
Nikamjibu: wewe utapona.
Rodrigo: kwasababu unaona sifi?
Nikamjibu: nahisi tu wewe utaishi.
hatukuchoka kukimbia tulizidi kusonga mbele licha
Zakayo alikuwa na maumivu makali nae pia
alijikaza.
Baada ya muda Latina alianza kutusumbua Mara
apite mara apotee, haikuchukuwa dakika mbili
kilikuja kimbunga kikali kikaturusha kila mmoja
akaenda sehemu yake.
Muda Huo mimi na Dominic tulienda sehemu yetu.
tukiwa tumeanguka kifudi fudi kuna nyoka mdogo
alimdondokea mgongoni Dominic, akaanza
kujikunguta na Mimi huku nikiwa namuangalia.
Ile Hali Dominic anarusha rusha mikono huku akirudi
nyuma huwezi kuamini alifika mwisho sehemu flani
kulikuwa na korongo ndefu mno na Chini
yalikuwepo maji ambayo hayateremki wala kupanda,
aisee mguu wa kushoto wa Dominic uliteleza
kwenye jiwe flani akateremka Ila kwa bahati nzuri
akashikilia kwenye mawe flani huku akiwa
ananing'inia.
Maskini Dominic alipoangalia Chini aisee Kina
kilikuwa kirefu mno hali ya kwamba akidondokea
mule Hawezi kupona.
Nikiwa najiuliza Dominic kapatwa na nini aliniita
niende kumsaidia, bila kupoteza muda nikawahi
aisee kuangalia Chini tu nilisikia kizungu zungu,
nikamuangalia Dominic na kumuambia: sasa hivi
nakutoa.
Dominic alitabasamu ishara ananiamini.
Pembeni kulikuwepo mti flani ulio imara nikaushika
kisha nikampa mkono wangu wa kulia, alinishika
freshi nikaanza kumvuta kwa nguvu.
Ukweli tumaini ya kumtoa eneo lile ilikuwepo Ila
huwezi kuamini tatizo lingine lilijitokeza pale pale.
Dominic akiwa bado hajapanda juu alishtuka na
kuniambia: angalia nyuma yako.
Niligeuka fasta aisee Sikuamini kukutanisha macho
na Latina akiwa yupo karibu yangu, maskini ya
Mungu kutokana na mshtuko uliochanganya na
uoga ndani yake nilijikuta naishiwa nguvu bila
kujielewa nikamuachia Dominic, kwa mbali sauti
yake Nikaisikia akipiga kelele, nguvu ziliniishia
machozi yakaanza kuniteremka maana moja
nimemuua mwenzangu pili muda si mrefu na Mimi
naenda kufa.
Taratibu Nilinyanyuka huku nikiwa nimejiandalia
Kifo, ile Latina analeta kucha zake karibu na kifua
changu ili kuchomoa moyo wangu huwezi kuamini
Zakayo alijitokeza na kunizuwia mimi kisha yeye
akaingizwa kucha zile ndani ya kifuata chake, nikiwa
nashangaa shangaa Zakayo Aliniambia kwa sauti ya
maumivu makali: wahi profesa Rodrigo ameona
Yale maji.
Nilishtuka kuondoka nikashindwa Zakayo akazidi
kunisisitiza, nikiwa nalia nilimuambia: Asante
zakayo please usinisamehe kwa hili.
Nilianza kukimbia, zakayo akauwawa papo hapo.
Spidi niliokuwa nayo Ilikuwa sio ya Kawaida, njia
nzima nilikuwa siamini kama nimemuua mwenyewe
mwanajeshi Dominic, machozi yalizi kunibubujika
huku nikizidi kukumbuka tulioyafanya Mimi na
Dominic, Kumbukumbu zilinirudisha nyuma
nikakumbuka Zakayo alivyokuja kujitolea akafa Yeye
ili mimi niweze kupona, aisee nilikimbia nikiwa nalia
kwa kupaza sauti.
Ile mkukimbia Kimbia tuligongana na profesa
Rodrigo kila mmoja akaangukia pembeni.
Derick alifika akiwa anachechemea kwa maumivu
ndipo Nikamuuliza: kuna nini kwenye mguu wako?
Derick hakutaka kunijibu kuhusu mguu wake
akatuambia: nyanyukeni tuwahi ni pale vile
tumefika.
Alinyoosha mkono akatuonesha aisee ishara tu
ilikuwa inaonesha ndio sehemu husika, nikawaambia
kwa sauti ya maumivu: Dominic na Zakayo hatupo
nao tena.
Walisikitika kwa Muda Huo, bila kupoteza muda
nikanyanyuka na kumpa mkono profesa Rodrigo ili
kumuinua, kabla hajainuka huwezi kuamini Latina
alifika akiwa amechukia mno, tukajuwa basi Ndo
tumekwisha sote, Derick akiwa anachechemea
akaanza kurudi nyuma akielekea kule kule sehemu
husika, hakutaka kuniacha akanishika mkono huku
akimuangalia Latina.
Kwa sauti ya Juu Nikamuuliza profesa Rodrigo:
huwezi kunyanyuka?
Profesa: acheni niwe chambo tu! ili Ninyi muweze
kupata nafasi, Nyie nendeni, kwanza siwezi
kutembea maana miguu yangu imevimba haiwezi
kufanya kazi tena.
Tukiwa tunamsikiliza Latina alimuwahi profesa
Rodrigo akaingiza kucha kwenye koo ya profesa
wetu huku Sisi tukiwa hatuamini.
Derick alianza kunivuta kwa uchungu nikaendelea
kumtazama profesa wetu.
Profesa Rodrigo kwa ushujaa aliokuwa nao aliingiza
mkono wake ndani ya mfuko wa suruwali yake kisha
Akachomoa kale kasimu kadogo na kunirushia.
Papo hapo Latina akavuta koo ya profesa Rodrigo
akapoteza maisha hapo hapo.
Sasa kimbembe kikabaki kwetu, mguu wa Derick
ulikuwa mbovu, Mimi tena ndo Yale Yale, na kizuri
mto ulikuwa nyuma yetu Kidogo, taratibu Latina
akaanza kutufuata huku Sisi tukiwa tunarudi nyuma
taratibu, kasimu kale kadogo nilikawasha huku
nikiwa namuangalia usoni Latina anavyonisogelea,
nikafanikiwa ku play muziki wa diamond na Inno's
B, huwezi kuamini Latina alianza kucheza Jambo
ambalo lilitupa tumaini ya kuweza kufanikiwa
zowezi lile.
Derick kwa nyuma akaanza kutabasamu ishara ya
Ushindi, sekunde Kama mbili aisee betri ya simu
ikadondoka Chini maana mfunikio wa simu ile
ulikuwa umepotea toka Dominic anaimiliki, hapo
hapo muziki ukakata.
Nyuso zetu zilijikunja kwa kusubiria Kifo.
Latina alisimamisha kucheza kisha akaanza
kutufuata taratibu, siku zote wanasema Allah akitaka
kukusaidia hata uwe kwenye mdomo wa mamba
utatoka tu, tena ukiwa ni mzima.
Kama bahati nikaanza kuimba nyimbo ile tena vile
vile Kama nimemezeshwa sidi aisee huwezi kuamini
Latina akaanza kucheza, Derick alipoona hivo nae
akaanza kunisaidia tukapaza sauti ili kumlewesha
kabisa, nyimbo ile nilikuwa Naijuwa kuiimba kwa
kubabaisha ila siku hio nilijishangaa niliimba vizuri
kuliko hata mwenye nayo.
Kuimba kwetu huku tukirudi nyuma na Latina alizidi
kutufuata maana alifuata muziki unapoelekea.
Moja kwa moja ndani ya mto ule, tukazidi kusonga
Latina nae akaingia ndani ya maji Yale, nilipoona
anacheza taratibu aisee huwezi kuamini lingala
ilipanda kichwani kama mtoto aliekulia Kinshasa
nikaanza Kuimba nyimbo flani ya Fally pupa Inaitwa
Original, aisee Latina alikata mauoni kwa furaha
Baada ya kuskia nyimbo ile.
Derick alipoona nazidi kumlewesha yeye aliniacha
pale akasogea mpaka pale kunako kile kibuyu
akakichukuwa kwa umakini mkubwa, Derick
alipoyaangalia Yale maji alikubali kuwa ndio
yenyewe maana yalikuwa ya kijani mno.
Muda Huo Nyani juu ya mti ule walikuwa wanakula
Yale matunda taratibu huku wakitushangaa
tunachokifanya.
Derick aliponifikia uzalendo ulinishinda Baada ya
kuona kitu ambacho siku nyingi tumekitafuta na
kimeweza kuwauwisha watu wengi aisee
nilistopisha kuimba nikamshika mkono Derick ili
kushilikiana nae kuweza kuangamiza kiumbe kile, ile
Kuacha kuimba tu, kiumbe kile ambacho kipo ndani
ya mwili wa Latina kilichukia baada ya kuona
tumeshika kitu chake cha thamani, kikapandisha
Mzuka ili kutuua sote ila kilikuwa kimechelewa
maana tulikimwagia maji Yale ya ajabu yote huku
tukipumua kwa kasi.
Kilianza kuwaka moto huku Sisi tukiwa tunashuhudia
wenyewe, vitu kama mfuke vikaanza kumtoka Latina
na kupanda Juu huku kikipiga kelele kwa sauti ya
Juu mno iliowafanya Nyani wale watoke eneo lile.
Maajabu fuvu lile kwa Muda wote lilikuwa likiishi
ndani ya mwili wa mdogo wangu Latina lilitoka
ndani ya mwili wake likasimama pembeni, macho
kwa macho na kipenzi changu Latina Ila huwezi
kuamini Latina alipeperushwa na upepo akatoweka
eneo lile.
Macho yalinitoka mbele yangu fuvu lile lilikuwa
linawaka moto kwa macho yetu tukalishuhudia, fuvu
lile liliweza kutema sumu ile ambayo ni maji ya
ajabu yakaenda kuangukia kwenye mti ule ule
unaotoaga matunda ambayo Nyani wanapenda sana,
maji Yale yakapotelea ndani ya majani Yale ya ule
mti.
baada ya hapo fuvu lile liliteketea tukiwa
tunashuhudia kwa macho yetu
Nilimuangalia Derick, furaha, huzuni vilitawala ndani
ya nyoyo zetu tukakumbatiana kwa nguvu kuashilia
Ushindi.
Maana kubwa ya Yule kiumbe wa ajabu (fuvu)
kupuliza dawa ile inamaanisha hivi: ugonjwa wa
Ebola upo pale pale hata Mti ule ukikatwa Baada ya
mwaka mmoja au zaidi lazma utaota na majani
yake ndio yanasumu ile, hivo Jani moja ikidondokea
ndani ya maji Yale virus ya Ebola itasambaa na
maradhi yataendelea kuzunguka miaka yote hapa
Duniani kupitia Nyani kunywa maji ya ule mto
uitwao kwasasa Ebola.
+****************************************+
Huu ndio mwisho wa simulizi yetu nzuri sana
iitwayo Equatorial forest
 
SEHEMU YA 18
TULIPOISHIA: Tuliposkia kelele za Patrick
tulisimama na kugeuka nyuma, aisee mwenzetu
tulimuonea huruma sana kwa wakati ule ndipo
Dominic akamuambia: jaribu kujitoa hapo.
Patrick akamjibu: nendeni tu hapa siwezi kutoka
eneo hili.
Latina akamfikia Patrick, bila kupoteza muda
ali.............sauti ya Zakayo ilisikika akisema: no!!!!!
SONGA NAYO!
Bila kupoteza muda Latina alimkata kichwa Patrick
kupitia kucha zake ndefu zenye ukali kuliko hata
wembe mpya, maskini kichwa cha mwenzetu Patrick
kikandondokea pembeni tukiwa tunashuhudia.
Sauti ya Zakayo ilisikika akisema: no!!!
Dominic alimuwahi Zakayo akamshika mkono
tukaanza kukimbia.
Majira ya Mchana baada ya kukimbia makilometa
mengi bila kupumzika tulisimama ili kujipumzisha.
Zakayo alikuwa amejiinamia muda wote ndipo
Nikamuuliza: umekata tamaa?
Zakayo aliniangalia na kuniambia: muda mwingi
kwa kuwa uso ni wa mdogo wako nahisi Labda ni
mchezo mnatuchezea ila sio kweli ni fikra zangu
mbovu.
Nilitabasamu kwa uchungu nikasema: yeah ni kweli
lazma makosa yote niyabebe mimi maana Yule ni
mdogo wangu na kila mtu anajifikiria kwa nini
Najma Hafi Wengine Ndo wanabaki wanakufa tu?
Zakayo Akanijibu: neno la muhimu ambalo Patrick
aliongea mara ya mwisho aliniambia Sisi tuliohai
tusijione mashujaa kwasababu hatujafa, Hapana!
Kila mtu anakufa kwa wakati wake na yote ni
mipango ya Mwenyezi Mungu.
Nikamjibu: Asante kuona hilo unalijua.
Profesa Rodrigo akauliza: tumebaki na kilometa
ngapi?
Dominic akamjibu: sio nyingi tunataka kufika.
Tulifurahi na kumuuliza: kufika?
Dominic: msipatini.
Sofia akiwa ametulia zake akasema: naskia njaa
jamani.
Nikamuambia: my dear Vumilia, hapa matunda
tunayatoa wapi?
Sofia: ukweli siwezi kupumua tena.
Dominic akasema: mnisubiri naenda kuwataftieni
chochote.
Nilishtuka na kumuuliza: utakuwa Salama kweli?
Dominic: Mungu ndie anaelinda si ndio
mlivyosema?
Niliendelea kumtazama kisha akaondoka.
Derick akiwa ametulia Nilimsogelea na kumuambia:
ukiwa kwenye Hali hio vipi kuhusu Sisi.
Derick: nahisi kitu tofauti Sana ndani ya mwili
wangu.
Nikamjibu: utakuwa ni uchovu tu we usijali.
Derick: ni kweli vipi kuhusu wewe Upo Salama
mwilini?
Nikamjibu: nipo freshi licha harufu ya mtoa roho
nabaki naisikia kila muda.
Derick alitabasamu na kusema: una maana Kifo
kipo karibu na wewe.
Nikamjibu: kipo karibu yangu kuliko moyo wangu.
Derick: usikate tamaa.
Nikamuambia: kila mtu anakuambia wewe uweze
kuwa hai.
Derick: kwasababu wanahisi mimi ni muhimu ila
wanasahau mbele ya Kifo hata uwe umehifadhi
vitabu vya kila Aina kichwani ili kusaidia watu, Kifo
kikiwa kimekulenga haijalishi, nakumbuka enzi za
zamani kuna mama flani Alikuwa ndani ya pango na
mwanae mchanga sana na pango hilo lilikuwa mbali
mno ambapo watu kufika eneo lile inachukuwa
miezi kadhaa ila huwezi kuamini Kifo kilimfikia
mama Yule akiwa yupo pangoni na mwanae
mchanga akapoteza maisha akamuacha mwanae,
jiulize Yule mama ni bora kiasi gani kwa mtoto
wake muda ule ila akachukuliwa sembuse mtu
Kama Mimi.
Nilishusha pumzi na kusema: kwa story yako
umenifanya nisiogope Kifo.
Derick: lazma uogope maana kinaogopeka sana.
Nikasema: Kitambo Sana Sijaiskia story zako hivi
Derick uliwazaje kukaa kimya bila kuongea na mimi
kipindi kile chote?
Derick alijishika masikio na kusema: Nisamee sijui
mwenyewe.
Nilitabasamu na kusema: sijui tukifa tutaonana tena.
Derick: maneno gani unaongea!
Muda Huo Dominic alifika akiwa na matunda sote
tulipomuona tulifurahi maana tulitegemea
hangeweza kurudi ndipo nikamtania: tulikuwa
tumesubiri kusikia msaaaadaaaa!!!
Wote walicheka kisha Dominic akaweka Chini
matunda Yale na kusema: Tuleni ili kesho
ikiwezekana tuanze mchaka mchaka.
Nikasema: ninavyokimbia muda mwingine nahisi
nimewekewa miguu ya bandia maana maisha yangu
ya Kawaida tu huwezi niambie kuhusu kukimbia
mimi.
Dominic akaniuliza: huwa haufanyi mazowezi?
Nikamjibu: ya nini sasa!
Sofia akadakia: sio wewe mwenyewe mimi hapa
nakuwaga kama kiwete Ila ninavyokimbia
mwenyewe sijiamini.
Zakayo akasema: jamani hapa Sina imani ya kuishi
tena Naomba ujumbe huu atakaefanikiwa kupona
awafikishie wazazi wangu waambieni hivi nilikuwa
kwenye harakati ya kutafuta maisha Ila Nawapenda
Sana.
Profesa Rodrigo alichukia na kusema: unaongea nini
sasa!
Nikadakia: Mwaya hata mimi atakaefanikiwa kupona
aende kuangalia hali ya mama yangu kwenye
hospitali ya vichaa Ila usimuambie chochote pili
nenda umuangalie baba yangu jela umuambie Mimi
na Latina tunamsalimia sana Ila usimuambie kuwa
nimeshakufa.
Sofia akasema: Mimi utaambia familia yangu Yule
mtoto wetu wa mwisho wamsomeshe kama Mimi ili
kesho aje kuwasaidia maana Mimi sintoweza
kufanya hivo.
Nilianza kulia nikisema: naongea hivi mpaka
uchungu nauamsha tena.
Derick: sote hapa tutapona masuala sijui ya
kumtuma mtu flani acheni.
Siku iliofuata Tulianza mchaka mchaka upya,
tulikimbia mpaka Majira ya saa tisa Mchana,
tulipunguza spidi maana tulikuwa tumechoka, tukiwa
tunazidi kusonga mbele Sofia aliona kitu mbele
Kama kisiki cha mti mkubwa akakifuata na kukaa
juu huku akisema: ngoja tupumzike kwanza.
Nilipoangalia vizuri nikakumbuka siku ile mimi
niliona kitu kama hicho nikapanda juu matokeo yake
nilichofanyiwa sintoweza kusahau, kwa sauti ya
Chini nikamuambia: toka hapo!
Sofia akaniuliza kwa sauti ya Juu: nini na wewe!
Aisee nyoka yule mwenye kichwa cha binadamu
Alimrusha juu ya miti kisha akamfuata na............
Huku Sisi tukiwa hatuelewi ni nini kinaendelea.

SEHEMU YA 19
TULIPOISHIA: Nilipoangalia vizuri nikakumbuka siku
ile mimi niliona kitu kama hicho nikapanda juu
matokeo yake nilichofanywa sintoweza kusahau,
kwa sauti ya Chini nikamuambia: toka hapo!
Sofia akaniuliza kwa sauti ya Juu: nini na wewe!
Aisee nyoka yule mwenye kichwa cha binadamu
Alimrushia juu ya miti kisha akamfuata na............
Huku Sisi tukiwa hatuelewi ni nini kinaendelea.
SONGA NAYO!
Nyoka yule mwenye kichwa cha binadamu baada ya
kumrusha juu ya miti Sofia alimfuata na kupotea nae
Huku Sisi tukiwa hatuelewi nini kinaendelea.
Macho yalitutoka tukaanza kumuita Ila haikusaidia
chochote ndipo Dominic akasema: Kumbe huyu
kiumbe ana nguvu za miujiza!
Nikasema: nahisi ukimchokoza akiwa ametulia zake
anakuua.
Derick: muonekano wake alikuwa ni mtu hatari
Sana.
Rodrigo: kwasababu anatembelea laana.
Zakayo: vipi kuhusu mwenzetu?
Rodrigo: Sofia?
Zakayo: Ndio.
Rodrigo: habari yake imeishia hapa si unakumbuka
Amanda kilichomtokea.
Zakayo: aisee Na maneno alioyaongea Jana Kumbe
alikuwa yupo serious.
Rodrigo: tunafanyaje? Kama muonapo tumebaki
wachache mno.
Dominic: hapa Hamna kurudi nyuma lazma
tupambane hata akibaki mmoja usife kizembe
Pambana ufe ukiwa upo kwenye harakati kwasababu
tukisema turudi nyuma tunasafari ndefu kuliko hii
tumebaki nayo ili kumaliza tatizo hii, pili tutakufa
wote.
Zakayo: Ni kweli maana siku ile mimi na wenzangu
tulihisi tukisema tunaachana nayo tutapona kumbe
tatizo lipo pale pale.
Nikasema: yule mzungu maskini ningemuona tena
Labda angetupa miindumbinu mingine.
Dominic: acha kumfikiria yule, kama ni Msaada
tayari ametusaidia vya kutosha hapa kilichobaki ni
Sisi wenyewe kujibeba.
Nikamuuliza: tunajisaidiaje kwa Mfano?
Dominic: tusonge mbele.
Tulianza safari tukiwa tumebaki jeshi ya watu wa
tano hali ya kuwa tulikuja tupo watu zaidi ya kumi
na 15.
Njia nzima kila mmoja alikuwa anamuomba
Muumba wake huku pia akiomba wazazi wake kwa
Hisia wamuombee msaada kwa Allah, Hofu na
uoga tuliokuwa nayo Ilikuwa sio ya Kawaida,
nilipojaribu kumkumbuka Sofia Aliposema kuwa Ana
njaa Nikakumbuka tena maneno alioyaongea kama
ujumbe kwa familia yake aisee machozi yalianza
kunitiririka mashavuni.
Majira ya usiku tuliweza kupumzika Kwa Muda,
Usingizi Hakuna alieweza kuupata ndipo nikasema:
muda kama huu huu ndugu yetu Sofia tulikuwa nae.
Zakayo Akanijibu: unajua Najma Tukifanikiwa kutoka
hapa wengi tutapata maradhi mengi sana.
Nikamjibu: sometimes nafikiria kwa nini Nilikuja
huku nakosa majibu yake.
Zakayo: Ni kweli Ukiona nchi za ulaya na ndo watu
wanajifanya viherehere kwa maswala kama haya
wapo zao kimya wala hawataki kufuatilia, Ila Sisi
toka nchi yetu iumbwe Hakuna mtanzania aliewahi
kuvumbua kitu chochote kupitia Utafiti wa
kuzunguka eneo hatari kama hii ili basi Na Sisi
tuseme tumekuja huku kwasababu mtafiti flani
aliwahi kwenda sehemu flani akafanya hivi akarudi
Salama Hakuna ndo tunategemea tutapona kweli!
hili tayari limeshakuwa tatizo ndoto za watu 16 wote
zimepotea kirahisi rahisi kweli?
Nikamuuliza: wewe kama vile hauamini
kinachoendelea?
Zakayo: naamini sana sema tu najilazimisha
kutokuamini.
Nikamuuliza: kwanza nimekumbuka kuna Jambo
flani silielewi, hivi muda ule ili mti umdondokee
marehemu Patrick ilikuwaje?
Zakayo: mwenyewe sielewi, ila nahisi nilivyokuwa
nakimbia kuna sehemu nilifinyaga nahisi ule Mti
ulikuwa mbovu kutokana Chini ulikuwa kama vile
umeoza.
Ndo nikapata picha na kusema: Ndo maana
ulikatika hii ardhi nahisi sio nzuri.
Zakayo: Ipo baadhi ya miti hukuwa vizuri kutokana
na hii Mvua ya kila siku ndo maana unaona ni
mirefu sana na mingine ili iweze kuwa na hafya
nzuri yahitaji Mvua na jua, mambo hayo mawili moja
ikikosekana matokea yake ni Yale.
Nikamjibu: wewe mambo mengi unayaelewa sana.
Zakayo: Nina Jamaa yangu Anaitwa Philip maswala
ya Utafiti ni namba one, lugha anazozijua kingereza,
kiswahili, kifaransa, kichina na huku Kongo anajua
lugha Kama Sita za kabila tofauti.
Nilishangaa na kumuuliza: Yeye ni kabila gani?
Zakayo: nimkongo ila kabila yake Mbembe.
Nikasema: Oohh kabila moja na Yule mama nyoka.
Zakayo: eeehh ila anaishi dar es salam.
Nikamuuliza: anasoma chuo gani?
Zakayo: amehitimu, nimtafiti mzuri sana Mara nyingi
anatembea nchi mbali mbali.
Nikamuuliza: Kumbe tajiri!
Zakayo: Hana hela nyingi Ila ni mtu mwenye hakili
nyingi, si Unajuwa ukiwa mwenye hakili huwezi kufa
na njaa.
Nikakubali na kumuuliza: Kwa nini hakuungana na
sisi kwa hii inshu?
Zakayo: Alikataa.
Nikamuuliza: au anajua kilichomo humu?
Zakayo: may be! ila sina uhakika.
Nikamuuliza: ulimjuaje?
Zakayo: mwanafunzi mwenzangu tulikutania mwaka
wa pili university ya Uganda.
Nikamuuliza: ulisoma international university
Makerere?
Zakayo: yeah! Mwaka wa kwanza na wa pili.
Nikasema: Oohh! naona wote wamesinzia.
Zakayo: wataamshwa na kelele zetu wasubiri tu.
Nikamjibu: Natamani tuliobaki hapa tufanikiwe
kutoka Salama.
Zakayo: sio wewe tu hata mimi pia.
Nikasema: muda ule tupo kwenye kile kimbunga
cha wale pygmy si Unajuwa tulikuwa tupo juu ya
msitu wote!
Zakayo: Eeeee.
Nikamjibu: nilitamani kupiga kelele ikiwezekana
Tanzania wasikie.
Zakayo: ungesemaje?
Niliweka mikono yangu kwenye mdomo kisha
nikasema: jamani msaada tumekwama hukuuuuuu!!
Zakayo alicheka huku akiendelea kuniangalia.
Baada ya muda tuliamshwa asubuhi na sauti za
ndege tukaamka kila mmoja akiwa anajishangaa
kulala muda mrefu namna ile, maana ilikuwa tayari
saa 2 asubuhi.
Dominic alinipa mkono nikamshika kisha akaniinua
na safari ikaanza.
Mchaka mchaka kama Kawaida yetu tulikuwa
tunakimbia, njiani nguvu ziliniishia nikasema huku
nikikimbia: pumzi inakata.
Derick ambae alikuwa karibu yangu akaniambia:
jikaze muda si mrefu tunafika.
Tukiwa tunazidi kusonga mbele aisee huwezi
kuamini Latina alipita karibu na zakayo kama radi
aka............... Zakayo akapiga kelele kwa maumivu
makali.

SEHEMU YA MWISHO YA 20
TULIPOISHIA: Mchaka mchaka kama Kawaida yetu
tulikuwa tunakimbia, njiani nguvu ziliniishia
nikasema huku nikikimbia: pumzi inakata.
Derick ambae alikuwa karibu yangu akaniambia:
jikaze muda si mrefu tunafika.
Tukiwa tunazidi kusonga mbele aisee huwezi
kuamini Latina alipita karibu na Zakayo kama radi
aka............... Zakayo akapiga kelele kwa maumivu
makali.
SONGA NAYO!
Latina alipita karibu na Zakayo kama radi akamkata
mkono akaenda nao, Zakayo akapiga kelele kwa
maumivu makali.
Tulimuwahi mwenzetu tukamshika huku tukimuuliza
hali yake, maskini Zakayo alilia mno kwa maumivu
huku akisema: Kwa nini asingeniua tu.
Nilimziba mdomo na kumuambia: usiseme hivo
jitahidi twende.
Zakayo: Naumia Sana dada yangu mwenzio siwezi
kuyavumilia haya maumivu.
Nilianza kulia huku nikizidi kumpa moyo.
Baada ya muda Nilimpa profesa Rodrigo kasimu
kale kabatani nilikopewa na Dominic ndipo profesa
akaniuliza: Unaogopa?
Nikamjibu: wewe utapona.
Rodrigo: kwasababu unaona sifi?
Nikamjibu: nahisi tu wewe utaishi.
hatukuchoka kukimbia tulizidi kusonga mbele licha
Zakayo alikuwa na maumivu makali nae pia
alijikaza.
Baada ya muda Latina alianza kutusumbua Mara
apite mara apotee, haikuchukuwa dakika mbili
kilikuja kimbunga kikali kikaturusha kila mmoja
akaenda sehemu yake.
Muda Huo mimi na Dominic tulienda sehemu yetu.
tukiwa tumeanguka kifudi fudi kuna nyoka mdogo
alimdondokea mgongoni Dominic, akaanza
kujikunguta na Mimi huku nikiwa namuangalia.
Ile Hali Dominic anarusha rusha mikono huku akirudi
nyuma huwezi kuamini alifika mwisho sehemu flani
kulikuwa na korongo ndefu mno na Chini
yalikuwepo maji ambayo hayateremki wala kupanda,
aisee mguu wa kushoto wa Dominic uliteleza
kwenye jiwe flani akateremka Ila kwa bahati nzuri
akashikilia kwenye mawe flani huku akiwa
ananing'inia.
Maskini Dominic alipoangalia Chini aisee Kina
kilikuwa kirefu mno hali ya kwamba akidondokea
mule Hawezi kupona.
Nikiwa najiuliza Dominic kapatwa na nini aliniita
niende kumsaidia, bila kupoteza muda nikawahi
aisee kuangalia Chini tu nilisikia kizungu zungu,
nikamuangalia Dominic na kumuambia: sasa hivi
nakutoa.
Dominic alitabasamu ishara ananiamini.
Pembeni kulikuwepo mti flani ulio imara nikaushika
kisha nikampa mkono wangu wa kulia, alinishika
freshi nikaanza kumvuta kwa nguvu.
Ukweli tumaini ya kumtoa eneo lile ilikuwepo Ila
huwezi kuamini tatizo lingine lilijitokeza pale pale.
Dominic akiwa bado hajapanda juu alishtuka na
kuniambia: angalia nyuma yako.
Niligeuka fasta aisee Sikuamini kukutanisha macho
na Latina akiwa yupo karibu yangu, maskini ya
Mungu kutokana na mshtuko uliochanganya na
uoga ndani yake nilijikuta naishiwa nguvu bila
kujielewa nikamuachia Dominic, kwa mbali sauti
yake Nikaisikia akipiga kelele, nguvu ziliniishia
machozi yakaanza kuniteremka maana moja
nimemuua mwenzangu pili muda si mrefu na Mimi
naenda kufa.
Taratibu Nilinyanyuka huku nikiwa nimejiandalia
Kifo, ile Latina analeta kucha zake karibu na kifua
changu ili kuchomoa moyo wangu huwezi kuamini
Zakayo alijitokeza na kunizuwia mimi kisha yeye
akaingizwa kucha zile ndani ya kifuata chake, nikiwa
nashangaa shangaa Zakayo Aliniambia kwa sauti ya
maumivu makali: wahi profesa Rodrigo ameona
Yale maji.
Nilishtuka kuondoka nikashindwa Zakayo akazidi
kunisisitiza, nikiwa nalia nilimuambia: Asante
zakayo please usinisamehe kwa hili.
Nilianza kukimbia, zakayo akauwawa papo hapo.
Spidi niliokuwa nayo Ilikuwa sio ya Kawaida, njia
nzima nilikuwa siamini kama nimemuua mwenyewe
mwanajeshi Dominic, machozi yalizi kunibubujika
huku nikizidi kukumbuka tulioyafanya Mimi na
Dominic, Kumbukumbu zilinirudisha nyuma
nikakumbuka Zakayo alivyokuja kujitolea akafa Yeye
ili mimi niweze kupona, aisee nilikimbia nikiwa nalia
kwa kupaza sauti.
Ile mkukimbia Kimbia tuligongana na profesa
Rodrigo kila mmoja akaangukia pembeni.
Derick alifika akiwa anachechemea kwa maumivu
ndipo Nikamuuliza: kuna nini kwenye mguu wako?
Derick hakutaka kunijibu kuhusu mguu wake
akatuambia: nyanyukeni tuwahi ni pale vile
tumefika.
Alinyoosha mkono akatuonesha aisee ishara tu
ilikuwa inaonesha ndio sehemu husika, nikawaambia
kwa sauti ya maumivu: Dominic na Zakayo hatupo
nao tena.
Walisikitika kwa Muda Huo, bila kupoteza muda
nikanyanyuka na kumpa mkono profesa Rodrigo ili
kumuinua, kabla hajainuka huwezi kuamini Latina
alifika akiwa amechukia mno, tukajuwa basi Ndo
tumekwisha sote, Derick akiwa anachechemea
akaanza kurudi nyuma akielekea kule kule sehemu
husika, hakutaka kuniacha akanishika mkono huku
akimuangalia Latina.
Kwa sauti ya Juu Nikamuuliza profesa Rodrigo:
huwezi kunyanyuka?
Profesa: acheni niwe chambo tu! ili Ninyi muweze
kupata nafasi, Nyie nendeni, kwanza siwezi
kutembea maana miguu yangu imevimba haiwezi
kufanya kazi tena.
Tukiwa tunamsikiliza Latina alimuwahi profesa
Rodrigo akaingiza kucha kwenye koo ya profesa
wetu huku Sisi tukiwa hatuamini.
Derick alianza kunivuta kwa uchungu nikaendelea
kumtazama profesa wetu.
Profesa Rodrigo kwa ushujaa aliokuwa nao aliingiza
mkono wake ndani ya mfuko wa suruwali yake kisha
Akachomoa kale kasimu kadogo na kunirushia.
Papo hapo Latina akavuta koo ya profesa Rodrigo
akapoteza maisha hapo hapo.
Sasa kimbembe kikabaki kwetu, mguu wa Derick
ulikuwa mbovu, Mimi tena ndo Yale Yale, na kizuri
mto ulikuwa nyuma yetu Kidogo, taratibu Latina
akaanza kutufuata huku Sisi tukiwa tunarudi nyuma
taratibu, kasimu kale kadogo nilikawasha huku
nikiwa namuangalia usoni Latina anavyonisogelea,
nikafanikiwa ku play muziki wa diamond na Inno's
B, huwezi kuamini Latina alianza kucheza Jambo
ambalo lilitupa tumaini ya kuweza kufanikiwa
zowezi lile.
Derick kwa nyuma akaanza kutabasamu ishara ya
Ushindi, sekunde Kama mbili aisee betri ya simu
ikadondoka Chini maana mfunikio wa simu ile
ulikuwa umepotea toka Dominic anaimiliki, hapo
hapo muziki ukakata.
Nyuso zetu zilijikunja kwa kusubiria Kifo.
Latina alisimamisha kucheza kisha akaanza
kutufuata taratibu, siku zote wanasema Allah akitaka
kukusaidia hata uwe kwenye mdomo wa mamba
utatoka tu, tena ukiwa ni mzima.
Kama bahati nikaanza kuimba nyimbo ile tena vile
vile Kama nimemezeshwa sidi aisee huwezi kuamini
Latina akaanza kucheza, Derick alipoona hivo nae
akaanza kunisaidia tukapaza sauti ili kumlewesha
kabisa, nyimbo ile nilikuwa Naijuwa kuiimba kwa
kubabaisha ila siku hio nilijishangaa niliimba vizuri
kuliko hata mwenye nayo.
Kuimba kwetu huku tukirudi nyuma na Latina alizidi
kutufuata maana alifuata muziki unapoelekea.
Moja kwa moja ndani ya mto ule, tukazidi kusonga
Latina nae akaingia ndani ya maji Yale, nilipoona
anacheza taratibu aisee huwezi kuamini lingala
ilipanda kichwani kama mtoto aliekulia Kinshasa
nikaanza Kuimba nyimbo flani ya Fally pupa Inaitwa
Original, aisee Latina alikata mauoni kwa furaha
Baada ya kuskia nyimbo ile.
Derick alipoona nazidi kumlewesha yeye aliniacha
pale akasogea mpaka pale kunako kile kibuyu
akakichukuwa kwa umakini mkubwa, Derick
alipoyaangalia Yale maji alikubali kuwa ndio
yenyewe maana yalikuwa ya kijani mno.
Muda Huo Nyani juu ya mti ule walikuwa wanakula
Yale matunda taratibu huku wakitushangaa
tunachokifanya.
Derick aliponifikia uzalendo ulinishinda Baada ya
kuona kitu ambacho siku nyingi tumekitafuta na
kimeweza kuwauwisha watu wengi aisee
nilistopisha kuimba nikamshika mkono Derick ili
kushilikiana nae kuweza kuangamiza kiumbe kile, ile
Kuacha kuimba tu, kiumbe kile ambacho kipo ndani
ya mwili wa Latina kilichukia baada ya kuona
tumeshika kitu chake cha thamani, kikapandisha
Mzuka ili kutuua sote ila kilikuwa kimechelewa
maana tulikimwagia maji Yale ya ajabu yote huku
tukipumua kwa kasi.
Kilianza kuwaka moto huku Sisi tukiwa tunashuhudia
wenyewe, vitu kama mfuke vikaanza kumtoka Latina
na kupanda Juu huku kikipiga kelele kwa sauti ya
Juu mno iliowafanya Nyani wale watoke eneo lile.
Maajabu fuvu lile kwa Muda wote lilikuwa likiishi
ndani ya mwili wa mdogo wangu Latina lilitoka
ndani ya mwili wake likasimama pembeni, macho
kwa macho na kipenzi changu Latina Ila huwezi
kuamini Latina alipeperushwa na upepo akatoweka
eneo lile.
Macho yalinitoka mbele yangu fuvu lile lilikuwa
linawaka moto kwa macho yetu tukalishuhudia, fuvu
lile liliweza kutema sumu ile ambayo ni maji ya
ajabu yakaenda kuangukia kwenye mti ule ule
unaotoaga matunda ambayo Nyani wanapenda sana,
maji Yale yakapotelea ndani ya majani Yale ya ule
mti.
baada ya hapo fuvu lile liliteketea tukiwa
tunashuhudia kwa macho yetu
Nilimuangalia Derick, furaha, huzuni vilitawala ndani
ya nyoyo zetu tukakumbatiana kwa nguvu kuashilia
Ushindi.
Maana kubwa ya Yule kiumbe wa ajabu (fuvu)
kupuliza dawa ile inamaanisha hivi: ugonjwa wa
Ebola upo pale pale hata Mti ule ukikatwa Baada ya
mwaka mmoja au zaidi lazma utaota na majani
yake ndio yanasumu ile, hivo Jani moja ikidondokea
ndani ya maji Yale virus ya Ebola itasambaa na
maradhi yataendelea kuzunguka miaka yote hapa
Duniani kupitia Nyani kunywa maji ya ule mto
uitwao kwasasa Ebola.
+****************************************+
Huu ndio mwisho wa simulizi yetu nzuri sana
iitwayo Equatorial forest

Safi sana... Simulizi nzuri sana...

Chapter Closed...



Cc: mahondaw
 
Habari mambo naitwa Mr Equator Nimeandika ujumbe huu kuku omba swala moja tu!
Mimi nimetengeza website ya ku share story ambayo ni http://www.equatorstory.com/
Je umekuwa ukipata tabu kupost story zako hapa?
Hili ndo suluhisho lako.
Mimi nataka nkupe nafasi ya kuwa mmoja wapo wa kwanza kutumia hii website
unda account yako na uweze kupost story yako mpya.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom