SIMIYU: “USIONE VYAELEA UJUE VIMEUNDWA.”
Na Donald Bakari.
Mnamo tarehe 13 Machi 2016 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli alimteua kijana mwerevu, mnyenyekevu na asiye na mihemko mwenye umri wa miaka 33 Anthony Mtaka kuwa Mkuu wa mkoa wa Simiyu. Mtaka akaingia katika vitabu vya kihistoria na kuwa mmoja wa wakuu wa mikoa wenye umri mdogo kuwahi kutokea nchini.
Hakutaka kiki, aliitazama ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya 2015 – 2020, kwa upole, busara, hekima na maarifa akaianza kazi na kututimizia maneno ya wahenga yanayosema “Usione vyaelea ujue vimeundwa”.
JPM leo (04/09/2020) atakuwa pale mkoani Simiyu kunadi sera za CCM na kuomba ridhaa ya kuchaguliwa kwa kipindi cha pili katika nafasi ya urais. Kazi yake itakuwa nyepesi sana kwa sababu Mtaka na watendaji kazi wengine walishaviunda na sasa vinaelea.
Yafuatayo ni baadhi ya mafanikio yaliyopatikana katika Mkoa wa Simiyu.
- Uzinduzi wa muongozo wa uwekezaji umebaini na kunadi fursa za uwekezaji katika mkoa wa Simiyu.
Mtaka ameutendea kazi muongozo huu, mkoa wa Simiyu umefungua fursa za uwekezaji na kunufaika nao. Katika hili JPM ataomba kura bila jasho.
- Kujengwa kwa hospitali ya rufaa katika mkoa mpya wa Simiyu.
Simiyu ni moja ya mikoa michanga, Serikali ya awamu ya tano ikaamua kujenga hospitali ya rufaa ya Simiyu kwa lengo la kusogeza huduma za rufaa karibu na wananchi kwa sababu Simiyu ni mkoa mchanga kwa namba za kuanzishwa ila sio kwa kuweza kujitegemea. Hapa Chama Cha Mapinduzi na JPM wataomba kura kwa lugha nyepesi sana.
- Utekelezaji wa mradi mkubwa wa maji na wa kimkakati wa kukabiliana na athari za mabadiliko ya mazingira mkoani Simiyu (Simiyu Climate Resilience Water Project).
Mradi huu una thamani ya shilingi bilioni 400, ukigharamiwa na Serikali ya Tanzania, Shirika la GCF na Serikali ya Ujerumani. Mtaka ameusimamia barabara, ameshaunda JPM ataomba kura na kuondoka kwa furaha.
- Ujenzi wa mahakama ya Hakimu Mkazi wa Simiyu umekamilika.
Chama cha Mapinduzi kinazingatia utoaji wa haki, Ujenzi wa mahakama ya hakimu mkazi umetimiza azma ya wengi ya kuona huduma za kimahakama zinapatikana kwa ubora na wakati. JPM atawapungia mkono wananchi wa Simiyu, nao watampa kura bila kinyongo.
- Ujenzi wa nyumba ya mkuu wa mkoa wa Simiyu na katibu tawala wa mkoa wa Simiyu umekamilika.
Serikali ilihakikisha watendaji hawa wa mkoa wanakuwa na makazi bora, unajua nini kilifuata? Mtaka na wenzake wakaiongoza Simiyu katika kuhakisha wanafunzi pale Simiyu wanafaulu. Walipigana kufa na kupona kuhakisha Simiyu inapaa katika elimu.
Ukienda pale NECTA watakuambia Simiyu huwa haikosi kumi bora katika matokeo. JPM akifika atawaeleza kuhusu elimu bure, wananachi watasema watoto wetu wanasonga mbele kielimu kura zote Kwako JPM mzalendo wa nchi.
- Kuongeza uwezo wa kuhifadhi mazao kwa kujenga ghala lenye uwezo wa kuhifadhi tani 34,000.
Usichukulie poa, Serikali iliamua. Pamba ni dhahabu nyeupe inatakiwa kuhifadhiwa vema. Mtaka alisimamia vema, JPM atasisitiza juu ya kujenga viwanda vya kutengeneza nguo zetu wenyewe na kuachana na mitumba, atafunga na kuondoka na kura zake kedekede.
Tuendelee kufurahia mafanikio makubwa na yenye tija yaliyopatikana katika Serikali ya awamu ya tano na tuwasisitize watanzania kuendelea kufanya kazi kwa bidii. “Kwa pamoja tumekeleza kwa kishido, tunasonga mbele pamoja” kura kwa JPM na Chama Cha Mapinduzi.
Wenu Donald Bakari
Email:
donaldbakari4@gmail.com