Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Kikosi cha Simba kilichopo Misri, katika maandalizi ya msimu mpya wa NBC Premier League na mashindano ya kimataifa, kimecheza mchezo wa kwanza wa kirafiki wa kujipima nguvu na timu ya Carabat FC, ambapo Mnyama ameshinda magoli 2-0.
Bao la Mohamed Bajaber katika mechi ya kirafiki dhidi ya Kahraba Ismailia katika uwanja wa Suez Canal Authority.
Kahraba Ismailia SC, inacheza Ligi Kuu ya Egypt na imeshacheza mchezo mmoja wa ligi ya Egypt dhidi ya El Gouna ambayo walifungwa pia bao 1-0.
Goli la kwanza lilifungwa kipindi cha kwanza na mchezaji Mohammed Bajaber huku goli la pili likifugwa kipindi cha pili na Jonathan Sowah.
Jonathan Sowah akifunga bao la pili katika mechi ya kirafiki dhidi ya Kahraba Ismailia
Wikiendi ijayo Kikosi cha Simba SC kitahamisha kambi yao kutoka Ismailia kwenda Cairo ambako watacheza michezo mingine ya kirafiki kabla ya kurejea Tanzania.