Mwanagandila
Senior Member
- Oct 9, 2011
- 182
- 100
Timu ya Simba Sports Club jana usiku imeshindwa kutamba mbele ya timu ya Miembeni United inayomilikiwa na Aman Makungu.
Katika mchezo wa jana usiku katika uwanja wa Amani mpaka dakika ya 90 timu zote zilikuwa 3-3 hali iliyomfanya mmiliki wa timu ya Miembeni ashuke chini kwenye benchi la ufundi kwenda kumuambia kocha awaambie wachezaji wawaachie Simba wapate bao la nne.
Dakika moja baada ya kutoa maagizo hayo baadhi ya wachezaji wa Miembeni waliendelea kuwa imara na hasa golikipa wao Abbas alikuwa kikwazo kwao, dakika ya 92 Kocha wa Miembeni alimuita Uhuru Selemani wa Simba na kumuambia mbona hamfungi wewe ingia mpaka golini mabeki hawatakukaba, na sekende baadaye Uhuru alifanya hivyo mabeki hawakumkaba na kwenda kufunga bao la nne na ushindi, baada ya kufunga bao hilo tu refarii alimaliza mchezo.
Mashabiki wa soka mjini hapa walikerwa na kitendo cha Amani Makungu kuwaambia timu yake iwaachie bao Simba amabapo washabiki hao walipokwenda kumuuliza kwa nini amefanya hivyo akasema Simba ingetoka yeye atakosa hela!
Hayo ndo mambo ya soka la Tanzania mwenye timu ana amri
Hongera Simba kwa kubebwa
Katika mchezo wa jana usiku katika uwanja wa Amani mpaka dakika ya 90 timu zote zilikuwa 3-3 hali iliyomfanya mmiliki wa timu ya Miembeni ashuke chini kwenye benchi la ufundi kwenda kumuambia kocha awaambie wachezaji wawaachie Simba wapate bao la nne.
Dakika moja baada ya kutoa maagizo hayo baadhi ya wachezaji wa Miembeni waliendelea kuwa imara na hasa golikipa wao Abbas alikuwa kikwazo kwao, dakika ya 92 Kocha wa Miembeni alimuita Uhuru Selemani wa Simba na kumuambia mbona hamfungi wewe ingia mpaka golini mabeki hawatakukaba, na sekende baadaye Uhuru alifanya hivyo mabeki hawakumkaba na kwenda kufunga bao la nne na ushindi, baada ya kufunga bao hilo tu refarii alimaliza mchezo.
Mashabiki wa soka mjini hapa walikerwa na kitendo cha Amani Makungu kuwaambia timu yake iwaachie bao Simba amabapo washabiki hao walipokwenda kumuuliza kwa nini amefanya hivyo akasema Simba ingetoka yeye atakosa hela!
Hayo ndo mambo ya soka la Tanzania mwenye timu ana amri
Hongera Simba kwa kubebwa