Simba SC Tusimkufuru Mungu

Linguistic

JF-Expert Member
Mar 16, 2021
3,671
8,237
Unapokuwa mwamba wa soka nchini kwa miaka minne mfululizo, na unapojenga sifa na heshima Afrika kwa miaka mitano, na kuwa timu pekee ya Tanzania inayojulikana huko duniani, unapokuja mwaka mmoja ukajikwaa ukihuzunika unamkufuru Mungu.

Kwa Ligi yenye figisu na siasa za “ku-balance” kati ya watani wa jadi, kuchukua ubingwa kwa miaka minne mfululizo na Kombe la FA kwa miaka mitatu mfululizo ni jambo lisilowezekana. Bayern Munich ni timu inayotamba Ujerumani lakini kuna miaka wanakosa Kombe. Tukubali kwa roho safi kwamba mwaka huu haukuwa wetu. Sababu:
.
1. Tumekumbwa na jinamizi la majeruhi kuliko ilivyo kawaida, kwani hakuna mchezaji hata mmoja ambaye hakukaa nje ya uwanja;

2. Tumebadilisha makocha katikati ya misimu mara mbili mfululizo.

3. Tumekuwa kwenye kipindi cha mpito kwa kuingiza wachezaji wapya vijana kwa mpigo.

4. Huku tukiwa na majeruhi, timu yetu imecheza mechi 12 zaidi ya timu nyingine za Ligi Kuu (mechi za Confederation na Mapinduzi).

5. Wenzetu waliutaka Ubingwa kwa kufa na kupona kuliko sisi. Kwa tajiri wa Yanga, ubingwa wa Yanga ni shughuli ya kujijenga kwenye jamii. Kwa tajiri yetu, mpira ni hobby

6. Viongozi wa soka na Bodi ya Ligi walikuwa kwenye vita dhidi yetu kutokana na siasa za “ku-balance”.

Tufanyeje kuanzia hapa tulipo?

1. Tutulie. Tusipaniki. Tutataniwa sana na watani wetu na wanayo haki kwani kukosa Ubingwa kwa muda mrefu ukiupata lazima ukimbie uchi mji mzima kwa furara. Lakini tuvumilie. Masikini akipata matako hulia mbwata.

2. Tuachane na benchi la sasa la ufundi. Kocha tuliye naye hatoshi. Hajaleta falsafa mpya ya uchezaji. Fitness coach hatoshi kwani majeraha mengi ni ya misuli ambayo chanzo ni fitness. Physio wa timu hatoshi. Tusitafute kocha wa muda mfupi mfupi.

3. Tuachane na wachezaji wazee wasioongeza chochote kwenye timu. Tuangalie mbele badala ya kuangalia nyuma. Future ya Simba ni Mwinuke, Israel Mwenda, Peter Banda, Sakho, Kanute, Kibu, Duchu (arudishwe kutoka kwenye mkopo). Wana umri mzuri. Waaminiwe na wapewe nafasi. Tusijenge timu ya msimu mmoja au miwili kama wenzetu.

4. Msimu ujao tutacheza round moja kabla ya kuingia group stage ya Klabu Bingwa Afrika, na tutapangiwa timu ndogo. Watani zetu watalazimika kucheza round mbili na watapangiwa timu ngumu. Wao watabaki, sisi tutavuka. Tusajili kwa ajili ya Klabu Bingwa Afrika. Hiyo ndio Ligi yetu kila mwaka inayotutambulisha duniani. Mchezaji yoyote mzuri Afrika atapenda kuchezea Simba. Tunayo sifa na uwezo wa kuvutia wachezaji bora kabisa kwenye Bara hili.

5. Tukamilishe miradi ya kuendeleza timu tuliyoipanga…kituo cha mazoezi, uwanja na masuala mengine ya mapato kwa Klabu.

Simba bado ni timu bora Tanzania. Ni timu inayocheza mpira bora zaidi. Ni timu iliyo na mafanikio zaidi kwa miaka ya karibuni.

Ni timu inayoibeba nchi barani Afrika kwa kuitangaza nchi lakini pia kwa kuifanya ipeleke timu nne kwenye mashindano ya Afrika kila mwaka.

Ni timu inayoongozwa kwa weledi zaidi. Tusimkufuru Mungu kwa kuhuzunika sana na matokeo ya mwaka huu.

Tuwapongeze na kuwatia moyo wachezaji na viongozi kwa jitihada waliyoiweka mwaka huu. Simba Nguvu Moja.

Ndimi

Edwin Silayo
Moshi

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Makolo mnajisahaulisha sana. Mliusotea ubingwa miaka 5 mfululizo bika kufanyiwa figisu yyte kutoka kwa wanasiasa. Yanga kausotea ubingwa miaka 4 kutokana na figisu za akina bashite.

Mnasema bodi ya ligi na tff kubalance, mbona ngao ya jamii mlipigwa kidude mkapoteana? Ukaenda mara uka draw, dodoma ukapata ushindi kwa taaabu, polisi nao pia. Na baadae mkala kipigo kwa mbeya city na hamisi kiiza akawamalizia?!

Tuambieni ni magoli mangapi mlifunga yakakataliwa. Tena nyie ushindi huo mmeupata kwa penalti na red card laa sivyo mngekua na point 36 mpaka sasa.

Mnawalalaimikiaje bodi ilhali ushindi wenu ulighubikwa na mizengwe na kuibua mijadala mikubwa sana kitaifa. Au mmesahau?

Yanga kwamba sio timu ya makombe, nani ana trophies nyingi kati yenu na yanga? Na huko Africa kwani yanga hajawahi kufika makundi?
 
Makolo mnajisahaulisha sana. Mliusotea ubingwa miaka 5 mfululizo bika kufanyiwa figisu yyte kutoka kwa wanasiasa. Yanga kausotea ubingwa miaka 4 kutokana na figisu za akina bashite...
simba tulisota miaka 5 utopolo mkachukua mara 3 na azam mara 1. Utopox mmesota miaka 5 wanaume tumebeba mara 4 zote huku tukitamba huko africa.

UTOPWINYO TUNASUBIRI AIBU KWA TAIFA ILA KWA KUWA MTETEZI SIMBA YU HAI WALA HATUTAWAZINGATIA SANA VYURA UTOPOLO KUBWA JINGA SHWAIN.
 
simba tulisota miaka 5 utopolo mkachukua mara 3 na azam mara 1. Utopox mmesota miaka 5 wanaume tumebeba mara 4 zote huku tukitamba huko africa. UTOPWINYO TUNASUBIRI AIBU KWA TAIFA ILA KWA KUWA MTETEZI SIMBA YU HAI WALA HATUTAWAZINGATIA SANA VYURA UTOPOLO KUBWA JINGA SHWAIN.
3+1=5?
Shida yenu mnajilinganisha, hoja ni kwamba ww umeka miaka mingapi bila kombe?

Tafuta historia, Yanga imebeba ubingwa back to back mara 5 na zaidi. Kolo sio wa kwanza kufanya hivo.

Saivi huku ligi kuu hakuna chenu 10 seasons consecutively.maana akina bashite tena wamebaki historia. Kalogeni huko mnakologa ili mshinde.
 
simba tulisota miaka 5 utopolo mkachukua mara 3 na azam mara 1. Utopox mmesota miaka 5 wanaume tumebeba mara 4 zote huku tukitamba huko africa. UTOPWINYO TUNASUBIRI AIBU KWA TAIFA ILA KWA KUWA MTETEZI SIMBA YU HAI WALA HATUTAWAZINGATIA SANA VYURA UTOPOLO KUBWA JINGA SHWAIN.
Dogo hebu relax
 
3+1=5?
Shida yenu mnajilinganisha, hoja ni kwamba ww umeka miaka mingapi bila kombe?

Tafuta historia, Yanga imebeba ubingwa back to back mara 5 na zaidi. Kolo sio wa kwanza kufanya hivo.

Saivi huku ligi kuu hakuna chenu 10 seasons consecutively.maana akina bashite tena wamebaki historia. Kalogeni huko mnakologa ili mshinde.
nimesema sisi ndani ya miaka 5 tumebeba 4 mfululizo. Nyie mapunguwan enzi za teja manji mlibeba 3 ndani ya miaka mitano na azam 1. Sasa wewe chura wa pale jangwani hujui simba alibeba mara 6 mfululizo kwa miaka hiyo unayodai wewe!? UTOPOX JUHA MKUBWA.
 
3+1=5?
Shida yenu mnajilinganisha, hoja ni kwamba ww umeka miaka mingapi bila kombe?

Tafuta historia, Yanga imebeba ubingwa back to back mara 5 na zaidi. Kolo sio wa kwanza kufanya hivo.

Saivi huku ligi kuu hakuna chenu 10 seasons consecutively.maana akina bashite tena wamebaki historia. Kalogeni huko mnakologa ili mshinde.


Naomba unitajie hiyo misimu ambayo Yanga alibeba ubingwa mara 5 back to back
 
Mwenye Uzi ungeeleweka Sana bila kuitaja Yanga. Kuiweka Yanga kwenye Uzi huu inaonyesha na kudhihirisha ulivyopewa Msongo wa mawazo na vipigo mfululizo toka kwa wananchi. Mawazo mengine ukiondoa hii ya kuitaja Yanga huko sahihi.
 
Mwenye Uzi ungeeleweka Sana bila kuitaja Yanga. Kuiweka Yanga kwenye Uzi huu inaonyesha na kudhihirisha ulivyopewa Msongo wa mawazo na vipigo mfululizo toka kwa wananchi. Mawazo mengine ukiondoa hii ya kuitaja Yanga huko sahihi.
Eti anataka kuaminisha ya kwamba Yanga itakuwa bingwa msimu huu kwa sababu ya "kubalance"!!!

Na siyo kwa sababu ya mipango kabambe waliyo jiwekea tangu msimu unaanza, huku ikichagizwa na uwepo wa kikosi kizuri, benchi bora kabisa la ufundi, na udhamini mzuri kutoka GSM!
 
Makolo mnajisahaulisha sana. Mliusotea ubingwa miaka 5 mfululizo bika kufanyiwa figisu yyte kutoka kwa wanasiasa. Yanga kausotea ubingwa miaka 4 kutokana na figisu za akina bashite.

Mnasema bodi ya ligi na tff kubalance, mbona ngao ya jamii mlipigwa kidude mkapoteana? Ukaenda mara uka draw, dodoma ukapata ushindi kwa taaabu, polisi nao pia. Na baadae mkala kipigo kwa mbeya city na hamisi kiiza akawamalizia?!

Tuambieni ni magoli mangapi mlifunga yakakataliwa. Tena nyie ushindi huo mmeupata kwa penalti na red card laa sivyo mngekua na point 36 mpaka sasa.

Mnawalalaimikiaje bodi ilhali ushindi wenu ulighubikwa na mizengwe na kuibua mijadala mikubwa sana kitaifa. Au mmesahau?

Yanga kwamba sio timu ya makombe, nani ana trophies nyingi kati yenu na yanga? Na huko Africa kwani yanga hajawahi kufika makundi?
Kama simba haikufanyiwa figisu na Wana siasa basi ilifanyiwa figisu na Jamal Malinzi utopolo wa kutupwa
 
Unapokuwa mwamba wa soka nchini kwa miaka minne mfululizo, na unapojenga sifa na heshima Afrika kwa miaka mitano, na kuwa timu pekee ya Tanzania inayojulikana huko duniani, unapokuja mwaka mmoja ukajikwaa ukihuzunika unamkufuru Mungu.

Kwa Ligi yenye figisu na siasa za “ku-balance” kati ya watani wa jadi, kuchukua ubingwa kwa miaka minne mfululizo na Kombe la FA kwa miaka mitatu mfululizo ni jambo lisilowezekana. Bayern Munich ni timu inayotamba Ujerumani lakini kuna miaka wanakosa Kombe. Tukubali kwa roho safi kwamba mwaka huu haukuwa wetu. Sababu:
.
1. Tumekumbwa na jinamizi la majeruhi kuliko ilivyo kawaida, kwani hakuna mchezaji hata mmoja ambaye hakukaa nje ya uwanja;

2. Tumebadilisha makocha katikati ya misimu mara mbili mfululizo.

3. Tumekuwa kwenye kipindi cha mpito kwa kuingiza wachezaji wapya vijana kwa mpigo.

4. Huku tukiwa na majeruhi, timu yetu imecheza mechi 12 zaidi ya timu nyingine za Ligi Kuu (mechi za Confederation na Mapinduzi).

5. Wenzetu waliutaka Ubingwa kwa kufa na kupona kuliko sisi. Kwa tajiri wa Yanga, ubingwa wa Yanga ni shughuli ya kujijenga kwenye jamii. Kwa tajiri yetu, mpira ni hobby

6. Viongozi wa soka na Bodi ya Ligi walikuwa kwenye vita dhidi yetu kutokana na siasa za “ku-balance”.

Tufanyeje kuanzia hapa tulipo?

1. Tutulie. Tusipaniki. Tutataniwa sana na watani wetu na wanayo haki kwani kukosa Ubingwa kwa muda mrefu ukiupata lazima ukimbie uchi mji mzima kwa furara. Lakini tuvumilie. Masikini akipata matako hulia mbwata.

2. Tuachane na benchi la sasa la ufundi. Kocha tuliye naye hatoshi. Hajaleta falsafa mpya ya uchezaji. Fitness coach hatoshi kwani majeraha mengi ni ya misuli ambayo chanzo ni fitness. Physio wa timu hatoshi. Tusitafute kocha wa muda mfupi mfupi.

3. Tuachane na wachezaji wazee wasioongeza chochote kwenye timu. Tuangalie mbele badala ya kuangalia nyuma. Future ya Simba ni Mwinuke, Israel Mwenda, Peter Banda, Sakho, Kanute, Kibu, Duchu (arudishwe kutoka kwenye mkopo). Wana umri mzuri. Waaminiwe na wapewe nafasi. Tusijenge timu ya msimu mmoja au miwili kama wenzetu.

4. Msimu ujao tutacheza round moja kabla ya kuingia group stage ya Klabu Bingwa Afrika, na tutapangiwa timu ndogo. Watani zetu watalazimika kucheza round mbili na watapangiwa timu ngumu. Wao watabaki, sisi tutavuka. Tusajili kwa ajili ya Klabu Bingwa Afrika. Hiyo ndio Ligi yetu kila mwaka inayotutambulisha duniani. Mchezaji yoyote mzuri Afrika atapenda kuchezea Simba. Tunayo sifa na uwezo wa kuvutia wachezaji bora kabisa kwenye Bara hili.

5. Tukamilishe miradi ya kuendeleza timu tuliyoipanga…kituo cha mazoezi, uwanja na masuala mengine ya mapato kwa Klabu.

Simba bado ni timu bora Tanzania. Ni timu inayocheza mpira bora zaidi. Ni timu iliyo na mafanikio zaidi kwa miaka ya karibuni.

Ni timu inayoibeba nchi barani Afrika kwa kuitangaza nchi lakini pia kwa kuifanya ipeleke timu nne kwenye mashindano ya Afrika kila mwaka.

Ni timu inayoongozwa kwa weledi zaidi. Tusimkufuru Mungu kwa kuhuzunika sana na matokeo ya mwaka huu.

Tuwapongeze na kuwatia moyo wachezaji na viongozi kwa jitihada waliyoiweka mwaka huu. Simba Nguvu Moja.

Ndimi

Edwin Silayo
Moshi

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
makolo nguvu moyaaaa
 
Eti anataka kuaminisha ya kwamba Yanga itakiwa bingwa msimu huu kwa sababu ya "kubalance"!!!

Na siyo kwa sababu ya mipango kabambe waliyo jiwekea tangu msimu unaanza, huku ikichagizwa na uwepo wa kikosi kizuri, benchi bora kabisa la ufundi, na udhamini mzuri kutoka GSM!
Jamaa mjinga sana. Et kubalance.
 
Makolo mnajisahaulisha sana. Mliusotea ubingwa miaka 5 mfululizo bika kufanyiwa figisu yyte kutoka kwa wanasiasa. Yanga kausotea ubingwa miaka 4 kutokana na figisu za akina bashite.

Mnasema bodi ya ligi na tff kubalance, mbona ngao ya jamii mlipigwa kidude mkapoteana? Ukaenda mara uka draw, dodoma ukapata ushindi kwa taaabu, polisi nao pia. Na baadae mkala kipigo kwa mbeya city na hamisi kiiza akawamalizia?!

Tuambieni ni magoli mangapi mlifunga yakakataliwa. Tena nyie ushindi huo mmeupata kwa penalti na red card laa sivyo mngekua na point 36 mpaka sasa.

Mnawalalaimikiaje bodi ilhali ushindi wenu ulighubikwa na mizengwe na kuibua mijadala mikubwa sana kitaifa. Au mmesahau?

Yanga kwamba sio timu ya makombe, nani ana trophies nyingi kati yenu na yanga? Na huko Africa kwani yanga hajawahi kufika makundi?
We topolo ushawahi kufika robo fainali au makundi si ulishika mkia
 
Unapokuwa mwamba wa soka nchini kwa miaka minne mfululizo, na unapojenga sifa na heshima Afrika kwa miaka mitano, na kuwa timu pekee ya Tanzania inayojulikana huko duniani, unapokuja mwaka mmoja ukajikwaa ukihuzunika unamkufuru Mungu.

Kwa Ligi yenye figisu na siasa za “ku-balance” kati ya watani wa jadi, kuchukua ubingwa kwa miaka minne mfululizo na Kombe la FA kwa miaka mitatu mfululizo ni jambo lisilowezekana. Bayern Munich ni timu inayotamba Ujerumani lakini kuna miaka wanakosa Kombe. Tukubali kwa roho safi kwamba mwaka huu haukuwa wetu. Sababu:
.
1. Tumekumbwa na jinamizi la majeruhi kuliko ilivyo kawaida, kwani hakuna mchezaji hata mmoja ambaye hakukaa nje ya uwanja;

2. Tumebadilisha makocha katikati ya misimu mara mbili mfululizo.

3. Tumekuwa kwenye kipindi cha mpito kwa kuingiza wachezaji wapya vijana kwa mpigo.

4. Huku tukiwa na majeruhi, timu yetu imecheza mechi 12 zaidi ya timu nyingine za Ligi Kuu (mechi za Confederation na Mapinduzi).

5. Wenzetu waliutaka Ubingwa kwa kufa na kupona kuliko sisi. Kwa tajiri wa Yanga, ubingwa wa Yanga ni shughuli ya kujijenga kwenye jamii. Kwa tajiri yetu, mpira ni hobby

6. Viongozi wa soka na Bodi ya Ligi walikuwa kwenye vita dhidi yetu kutokana na siasa za “ku-balance”.

Tufanyeje kuanzia hapa tulipo?

1. Tutulie. Tusipaniki. Tutataniwa sana na watani wetu na wanayo haki kwani kukosa Ubingwa kwa muda mrefu ukiupata lazima ukimbie uchi mji mzima kwa furara. Lakini tuvumilie. Masikini akipata matako hulia mbwata.

2. Tuachane na benchi la sasa la ufundi. Kocha tuliye naye hatoshi. Hajaleta falsafa mpya ya uchezaji. Fitness coach hatoshi kwani majeraha mengi ni ya misuli ambayo chanzo ni fitness. Physio wa timu hatoshi. Tusitafute kocha wa muda mfupi mfupi.

3. Tuachane na wachezaji wazee wasioongeza chochote kwenye timu. Tuangalie mbele badala ya kuangalia nyuma. Future ya Simba ni Mwinuke, Israel Mwenda, Peter Banda, Sakho, Kanute, Kibu, Duchu (arudishwe kutoka kwenye mkopo). Wana umri mzuri. Waaminiwe na wapewe nafasi. Tusijenge timu ya msimu mmoja au miwili kama wenzetu.

4. Msimu ujao tutacheza round moja kabla ya kuingia group stage ya Klabu Bingwa Afrika, na tutapangiwa timu ndogo. Watani zetu watalazimika kucheza round mbili na watapangiwa timu ngumu. Wao watabaki, sisi tutavuka. Tusajili kwa ajili ya Klabu Bingwa Afrika. Hiyo ndio Ligi yetu kila mwaka inayotutambulisha duniani. Mchezaji yoyote mzuri Afrika atapenda kuchezea Simba. Tunayo sifa na uwezo wa kuvutia wachezaji bora kabisa kwenye Bara hili.

5. Tukamilishe miradi ya kuendeleza timu tuliyoipanga…kituo cha mazoezi, uwanja na masuala mengine ya mapato kwa Klabu.

Simba bado ni timu bora Tanzania. Ni timu inayocheza mpira bora zaidi. Ni timu iliyo na mafanikio zaidi kwa miaka ya karibuni.

Ni timu inayoibeba nchi barani Afrika kwa kuitangaza nchi lakini pia kwa kuifanya ipeleke timu nne kwenye mashindano ya Afrika kila mwaka.

Ni timu inayoongozwa kwa weledi zaidi. Tusimkufuru Mungu kwa kuhuzunika sana na matokeo ya mwaka huu.

Tuwapongeze na kuwatia moyo wachezaji na viongozi kwa jitihada waliyoiweka mwaka huu. Simba Nguvu Moja.

Ndimi

Edwin Silayo
Moshi

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
hamna jipya
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom