Simba itaifunga Stellenbosch kwao?

Simba itaifunga Stellenbosch kwao?

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
16,252
Reaction score
16,171
Kuna watu wanafurahia na kusema kuwa Simba ina mashabiki wengi sana South Afrika kuliko Stellenbosch; hivyo kuwa kama sababu ya Simba kufanya vizuri kule dhidi ya Stelle

Simba walifanya vitu vingi sana nyumbani ikiwemo uwepo wa mashabiki wengi uwanjani lakini waliambulia goli moja tu. Hii inaonyesha kuwa kuwa na mashabiki wengi uwanjani halikuwa tatizo kubwa sana kwa Stellenbosch.
Je, kama Stellenbosch wakiwafanyia japo nusu tu ya mambo waliofanyiwa na Simba kule kwao Simba watatoboa? Nguvu ya simba kule itakuwa iko sehemu ipi?
 
Jambo linalolengwa sana ni Simba kuitoa Stellenbosch kwa sare, kushinda au kufungwa ila aggregate iibebe Simba. Kama Zamalek alitolewa 2003 kwanini ishindikane kwa hawa vijakazi wa Makaburu?
 
Kuna watu wanafurahia na kusema kuwa Simba ina mashabiki wengi sana South Afrika kuliko Stellenbosch; hivyo kuwa kama sababu ya Simba kufanya vizuri kule dhidi ya Stelle

Simba walifanya vitu vingi sana nyumbani ikiwemo uwepo wa mashabiki wengi uwanjani lakini waliambulia goli moja tu. Hii inaonyesha kuwa kuwa na mashabiki wengi uwanjani halikuwa tatizo kubwa sana kwa Stellenbosch.
Je, kama Stellenbosch wakiwafanyia japo nusu tu ya mambo waliofanyiwa na Simba kule kwao Simba watatoboa? Nguvu ya simba kule itakuwa iko sehemu ipi?
Simba umeshatoa timu ngumu na kongwe kuliko stelle
Timu imejulikana miaka hii ta karibuni
Simba ni lidude likubwa sana africa
 
Rai yangu kwao, wasichome tu moto uwanja wa watu!
 
Jambo linalolengwa sana ni Simba kuitoa Stellenbosch kwa sare, kushinda au kufungwa ila aggregate iibebe Simba. Kama Zamalek alitolewa 2003 kwanini ishindikane kwa hawa vijakazi wa Makaburu?
Tuombe Mungu, lakini haitakuwa kazi rahisi aisei!!! mbwa mkali kwao.
 
Yanga walicheza na MC Alger wakafanya vitu vingi sana nyumbani lakini hawakuambulia goli lolote
Tofautisha kati ya Champions and confederation' ni mbingu na ardhi. Yanga ilibakia kiduchu tu irejee nyumbani na tukombe hutu twa confederation kama isingekuwa figisu za timu mwenyeji na kanuni ya bao la ugenini. Hakuna cha ajabu hapo!!!!
 
Simba umeshatoa timu ngumu na kongwe kuliko stelle
Timu imejulikana miaka hii ta karibuni
Simba ni lidude likubwa sana africa
Simba sio lidude, haina kikombe cha CAF hata kimoja, hata hii nusu finali imepatikana kwa mbinde na tumba.
 
Tofautisha kati ya Champions and confederation' ni mbingu na ardhi.
Pia tofautisha kati ya wanaoshiriki Champions League (Ahly, Mamelodi, Pirates na Pyramids) na wanaoshabikia Champions League (utopolo, Vital'O, CBE na Zalan).
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom