Simba inahitaji mageuzi katika aina ya wachezaji

Simba inahitaji mageuzi katika aina ya wachezaji

Namshakende

JF-Expert Member
Joined
Sep 23, 2021
Posts
771
Reaction score
1,903
Ni dhahiri Sisi mashabiki wa Simba tuna mapenzi makubwa na timu yetu na tunatamani kuona mafanikio endelevu. Katika kutafakari mwenendo wa timu, ni muhimu kuangalia kwa jicho la tatu aina ya wachezaji ambao watatufikisha kwenye malengo yetu.

Wakati tunawashuhudia wachezaji wengi wa Simba wakitumia nguvu, kasi, na kujituma uwanjani, kuna wasiwasi kuhusu uwezo wao wa kufanya maamuzi sahihi na kuwa na ubunifu katika eneo la mwisho. Mara nyingi, tunaona juhudi kubwa zinazokosa umakini na maarifa yanayohitajika ili kuleta madhara kwa timu pinzani.

Tunahitaji kukiri kuna pengo katika akili ya soka kwa baadhi ya wachezaji wetu. Tunashuhudia wachezaji ambao wanategemea zaidi nguvu na mikimbio kuliko uwezo wa kufikiri na kupanga mashambulizi kwa ufanisi. Matokeo yake, tunajikuta tukipoteza nafasi nyingi na kushindwa kuvunja ulinzi wa wapinzani kwa urahisi.


Ni wakati sahihi kwa uongozi wa Simba kuweka mkazo katika kusajili wachezaji wenye akili kubwa ya soka, kama tunavyoona kwa Clatous Chama, Pacome, Maxi, Fabrice , e.tc . Wachezaji wenye uwezo wa kuona nafasi, kupiga pasi zenye uhakika, na kufanya maamuzi sahihi chini ya presha ndio watakaotupeleka kwenye mafanikio makubwa.

Tusipuuze umuhimu wa kuwa na wachezaji wenye uwezo wa kufikiri na kutumia akili zao uwanjani. Ni muhimu kuwekeza katika wachezaji ambao wanaweza kuleta ubunifu na mbinu mpya katika safu yetu ya ushambuliaji.

Tunahitaji timu ambayo ina mchanganyiko wa nguvu na akili. Kuwa na wachezaji wenye uwezo wa kufikiri na kutenda kwa usahihi ndio tutaweza kushinda mechi na kufikia malengo yetu.

Simba inahitaji mageuzi katika aina ya wachezaji ili kuhakikisha tunakuwa na timu imara na yenye uwezo wa kushindana katika ngazi zote(Yanga) . Ni wakati wa kuwekeza kwenye akili ya soka kwa manufaa ya timu yetu.
 
Very true. Simba hamna timu. Huwezi kuwa tegemezi wa Kibu Denga mchezaji anaefunga goli moja msimu mzima. Hamna timu pale. Fukuza wachezaji leta wengine wanaweza kutumia akili kucheza. Na kocha pia fukuza leta mwingine. Huwezi chukua Assistant Coach aje kuwa kocha mkuu Simba alafu utegemee timu ifanye vizuri Africa. Mfukuzeni akajenge CV kwanza huko KMC au Namungo
 
Ni dhahiri Sisi mashabiki wa Simba tuna mapenzi makubwa na timu yetu na tunatamani kuona mafanikio endelevu. Katika kutafakari mwenendo wa timu, ni muhimu kuangalia kwa jicho la tatu aina ya wachezaji ambao watatufikisha kwenye malengo yetu.

Wakati tunawashuhudia wachezaji wengi wa Simba wakitumia nguvu, kasi, na kujituma uwanjani, kuna wasiwasi kuhusu uwezo wao wa kufanya maamuzi sahihi na kuwa na ubunifu katika eneo la mwisho. Mara nyingi, tunaona juhudi kubwa zinazokosa umakini na maarifa yanayohitajika ili kuleta madhara kwa timu pinzani.

Tunahitaji kukiri kuna pengo katika akili ya soka kwa baadhi ya wachezaji wetu. Tunashuhudia wachezaji ambao wanategemea zaidi nguvu na mikimbio kuliko uwezo wa kufikiri na kupanga mashambulizi kwa ufanisi. Matokeo yake, tunajikuta tukipoteza nafasi nyingi na kushindwa kuvunja ulinzi wa wapinzani kwa urahisi.


Ni wakati sahihi kwa uongozi wa Simba kuweka mkazo katika kusajili wachezaji wenye akili kubwa ya soka, kama tunavyoona kwa Clatous Chama, Pacome, Maxi, Fabrice , e.tc . Wachezaji wenye uwezo wa kuona nafasi, kupiga pasi zenye uhakika, na kufanya maamuzi sahihi chini ya presha ndio watakaotupeleka kwenye mafanikio makubwa.

Tusipuuze umuhimu wa kuwa na wachezaji wenye uwezo wa kufikiri na kutumia akili zao uwanjani. Ni muhimu kuwekeza katika wachezaji ambao wanaweza kuleta ubunifu na mbinu mpya katika safu yetu ya ushambuliaji.

Tunahitaji timu ambayo ina mchanganyiko wa nguvu na akili. Kuwa na wachezaji wenye uwezo wa kufikiri na kutenda kwa usahihi ndio tutaweza kushinda mechi na kufikia malengo yetu.

Simba inahitaji mageuzi katika aina ya wachezaji ili kuhakikisha tunakuwa na timu imara na yenye uwezo wa kushindana katika ngazi zote(Yanga) . Ni wakati wa kuwekeza kwenye akili ya soka kwa manufaa ya timu yetu.
Hapa ni unamsema Ateba, Kibu, Mukwala na yule Mwanariadha wa DRC (Mpanzu).
 
Unashinda JF kuandika utumbo tu.
UNASIKITISHA SANA.
Sijui nikujibu wewe mwendawazimu unayefahamika na kila mtu humu jukwaani! Sijui ni kupotezee tu!

Ila kwa taarifa yako mimi nipo humu jukwaani kwa ajili ya ku refresh tu akili yangu! Na siyo kupunguza msongo wa mawazo unaotokana na maisha magumu kama ilivyo kwako wewe. Sawa. So relax, ok?
 
kutwa Kushinda jf kuandika pumba tu.
Inaonekana Maisha yangu unayajua kuliko hata mimi mwenyewe ???

Sipendi kuandika matusi na Upumbavu kama wewe usiye na Akili wala Elimu.

Idiot.
 
No reforms. No election.

Twende na hili kwanza. Mengine yatafuata, yanazungumzika
 
Nadhani Kuna haja ya Kubadili mfumo wa Usajili wa Simba umo umekaa kiwizi na utapeli Mwingi.

1. Nashauri apatikane Mkurugenzi wa Ufundi afanye hii kazi. Au wamtafute mtu maalum kwaajili ya kazi ya Usajili na sio medo.

2. Wachezaji wote wanaosajiliwa wawe angalau wamewahi kuitwa au wanaitwa timu za Taifa.

3. Mchezaji wa kigeni hatakiwi kupigwa benchi na Mzawa nk
 
kutwa Kushinda jf kuandika pumba tu.
Inaonekana Maisha yangu unayajua kuliko hata mimi mwenyewe ???

Sipendi kuandika matusi na Upumbavu kama wewe usiye na Akili wala Elimu.

Idiot.
Dogo una msongo wa mawazo uliopitiliza! Na haihitaji mtu awe na elimu kubwa kukutambua kama dishi lako kichwani limeyumba kutokana tu na msongo mkubwa wa mawazo ulio nao.

Inaonekana bado unaishi maisha magumu kwa wazazi/walezi wako, kutokana tu na huu ukosefu mkubwa wa ajira. Na ndiyo maana unawachukia watu kama mimi tunaoshinda muda wote humu jukwaani, na huku maisha yakiendelea kama kawaida.
 
Sijui nikujibu wewe mwendawazimu unayefahamika na kila mtu humu jukwaani! Sijui ni kupotezee tu!

Ila kwa taarifa yako mimi nipo humu jukwaani kwa ajili ya ku refresh tu akili yangu! Na siyo kupunguza msongo wa mawazo unaotokana na maisha magumu kama ilivyo kwako wewe. Sawa. So relax, ok?
IMG_20241231_164052_104.jpg
 
Simba kwa sasa imejipata mnoo, tukianza na safu ya ulinzi unakutana na Pinpin Camara, Nyau kabisaa hii.

Pale safu ya ulinzi hakuna shaka, kina chamou, zimbwe, spear JR, na Malone, hakika huna Cha kuhofia .

Viungo tunao kina Kagoma hachomoki Mtu, ngoma Mzee wa pass mpenyezo, Sema Mavamboww, budo, asee hii ndio timu sasa,

Safu ya ushambuliaji ndio tishio kwa sasa NBC, unakutana na Ateba, mukwala, na Manpower Rasta man, wakichagizwa na mafundi Ahua na mpanzu, hakika hakuna tunachowadai.

Wacha wauawe kiume.
 
Ndugu zangu wa simba, shida siyo wachezaji! Shida ni GSM anatuharibia ligi yetu. Hata kule kufungwa na Al Masry, chanzo ni GSM! Hili jambo hatutakiwi kulisahau hata sekunde moja. GSM anadhamini timu 7 kwenye ligi yetu.
Kabisa ujue sisi Simba ni Mbumbumbu na tunawahi kusahau sana ukiangalia Yanga Ina wachezaji waliojichokea kama Pacome , mzize na Dube hata kupiga shuti hawawezi lakini bado wanashinda kwa kuhonga marefa..

Fikiria sisi tuna majembe kina Mukwala, Ateba na Mutale lakini tunafungwa na vibonde kwa sababu GSM anaharibu sana ligi yetu.. baba yetu Karia inabidi amtimue kabisa kwenye mpira
 
Back
Top Bottom