Simba Chawene mwenyekiti kila mahali

fikirini

Senior Member
May 24, 2011
114
22
Nipo ndani ya ukumbi wa chuo cha ualimu mpwapwa, kuna kongamano la miaka 50 ya uhuru kwa wilaya ya mpwapwa. watoa mada ni ndugu Chiwanga ambaye ni askofu mstaafu kanisa la anglican hapa mpwapwa. Na pia wadau kibao wa siasa wapo hapa, ila kilichovutia zaidi ni kiuwasili kwa Mbunge Simba Chawene ambaye amepewa uenyekiti wa kongamono.

Yupo pia naibu waziri wa fedha ndgu Gregory teu ambaye ni mbunge wa Mpwapwa, mjadala umepamba moto. Ila wakati wa hotuba ya ufunguzi naibu waziri wa fedha amesema kuna mchakato wa kukipandisha hadhi chuo cha ualimu Mpwapwa kuwa chuo kikuu kishiriki cha Dodoma. Na pia chuo cha mifugo liti kuwa chuo kikuu kishiriki cha SUA.
 
Back
Top Bottom