Siku nilipolazimishwa kutoa mchango kanisani

Siku nilipolazimishwa kutoa mchango kanisani

Desierto

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2019
Posts
852
Reaction score
2,976
Ilikuwa hivi, baada ya kupambana Dar, ili nipate nauli niende nyumbani Singida.

Nilifanikiwa kufika nyumbani ila mfukoni nikiwa nimebakiwa na 500 tu, basi jumapili nikaenda kanisani kusali baada ya ibaada kuisha kukawa na mchango wa ujenzi wa kanisa.

Ikawa kila mtu ana ahidi kiasi au kitu atakacho changia mm nikaahidi 2000 wakakataa, muda huo pesa ya sabuni naomba kwa mama kwani sikuwa na biashara yeyote,

Basi bana wakanibana wee mpaka stimu za sala zikanikata, nikakubali nitatoa 3000 nilipoondokaga sikugeuka nyuma

Hii kitu ya kulazimisha watu waahidi vitu vilivyo nje ya uwezo wao lipo mana baadhi ya Malamud.
 
Ilikuwa hivi, baada ya kupambana dar, ili nipate nauli niende nyumbani, singida

Nilifanikiwa kufika nyumbani ila .
Umenikumbusha mzee wangu alikuja dar. Sa bro wangu na mkewe ealikuwa wanasali kwa mwingira tena wanakaa seat za mbele.

Si wakaenda naye, sa sijui walikuwa wanachangisha pesa ya nini watu wanaahidi mamilioni walipofika kwa mzee, mzee akasema atatoa 50,000 maana ilikuwa wanauliza mmoja mmoja aliyekaa mbele.

Wacha mwingira amchane 😂😂 unatoaje 50,000
 
Umenikumbusha mzee wangu alikuja dar. Sa bro wangu na mkewe ealikuwa wanasali kwa mwingira tena wanakaa seat za mbele. Si wakaenda naye, sa sijui walikuwa wanachangisha pesa ya nini watu wanaahidi mamilioni walipofika kwa mzee, mzee akasema atatoa 50,000 maana ilikuwa wanauliza.mmoja.mmoja aliyekaa mbele. Wacha mwingira amchane 😂😂 unatoaje 50,000
i bet mzee hakurudi tena huko
 
Mi huwa nina tabia ya kuingia makanisa mbalimbali. Siku moja nilijikuta nabaki kwenye viti vya waumini wanaotakiwa kutoa kiasi fulani japo hicho kiasi hakikuwa cha juu. Huu mtindo wa kulazimia kutoa mchango kiasi fulani utapangwa au utaingia mwenyewe kwenye kundi la wenye fedha unaloweza kutoa hutakwepa. Sana sana utajiingiza kwenye kundi la juu, la pili au tatu, kundi la mwisho huwa ni la mwenye chochote cha kutoa. Ukitaka sifa utatoa sana tu kana kwamba unamfurahisha Mungu kumbe unamfurahisha mchungaji tu akuone ni mtoaji hodari
 
Nimejikuta nakakumbuka haka kawimbo miaka hiyoooo

"Toa ndugu, toa ndugu ulichonacho wewe...
Bwana anakuona mpaka rohoni mwako...
Wiki nzima Bwana Mungu amekulinda vyema...
Sasa nawe ndugu umtumikieee..."
Kumbuka jinsi Yesu alivyojitolea pale msalabani kwa ajili yetu
 
Ilikuwa hivi, baada ya kupambana Dar, ili nipate nauli niende nyumbani Singida.

Nilifanikiwa kufika nyumbani ila mfukoni nikiwa nimebakiwa na 500 tu, basi jumapili nikaenda kanisani kusali baada ya ibaada kuisha kukawa na mchango wa ujenzi wa kanisa.

Ikawa kila mtu ana ahidi kiasi au kitu atakacho changia mm nikaahidi 2000 wakakataa, muda huo pesa ya sabuni naomba kwa mama kwani sikuwa na biashara yeyote,

Basi bana wakanibana wee mpaka stimu za sala zikanikata, nikakubali nitatoa 3000 nilipoondokaga sikugeuka nyuma

Hii kitu ya kulazimisha watu waahidi vitu vilivyo nje ya uwezo wao lipo mana baadhi ya Malamud.
mi nilishawahi tembelea kanisa flani miaka hiyo kutembelea tu nikaambiwa niahidi afu mgeni then umri bado na hela sina sijarudi tena (yani hadi mgeni kweli ?)
 
Ndio maana nilisilimu na kuwa muislamu.

Huko kumejaa utapeli ,unafiki na maigizo ya kijinga.
huna lolote wewe Mwajuma alikwambia mi hunioi hadi uwe mwislamu leo unasema maigizo na unafiki utachomwa moto siku ya kiyama kwa kosa la kudanganya
 
Kati ya waislamu na wakristo wapi waliohalalisha ushoga?
Hakuna dini iliyohalalisha ushoga.. ila nchi zenye wa cristu wengi, ndio nchi ambazo zina uhuru kuwa unavyotaka.. mashoga huko unaruhisiwa...

Ila kwa huku africa, ukanda wa pwani, wenye waislam wengi, ndio unaongoza kuingiliana kinyume cha maumbile, ila hawataki kuitwa mashoga... Fuatilia, zenji,mombasa,tanga...
 
We kanisa hadi zinalipa namba za mitandao ya simu.

Mimi kanisani ata sadaka sitoi. Mara ya mwisho wameitwa wanaume mbele, mimi sikutoka akanifata kiongozi mbona wewe hutoki. Nikamjibu sijaja kubaguliwa kwa jinsia nipo kusali na kuondoka.
 
Wewe unakwenda kusali kwa hawa waganga wa kienyeji kisa tu wanajiita kuhani, nabii, mtume. Mtakamuliwa sana!
 
Back
Top Bottom