Zifuatazo ni sifa za Mbunge wa jimbo la Bahi ambazo tunataka mwakilishi watu ajaye awe nazo,sifa hizi zimetokana na mapungufu ya Mbunge aliyopo ambayo tumeyaona nahatutaki mapungufu hayo yawepo kwa mbunge ajae.
Kwa kuwa mbunge aliyopo Mh Omary Badwel teyari tuimeisha mpa pongezi kwa kazi nzuri aliyoisha ifanya kwa kipindi cha miaka 5 na kwamba tumeisha mwambia akatafute kazi ingine basi tunahitaji mwakilishi mwenye sifa zifuatazo:-
INTERVIEW PANEL YA CHAMA CHOCHOTE HAIWEZI KUFANYA UPENDELEO WOWOTE
Karibuni.
Kwa kuwa mbunge aliyopo Mh Omary Badwel teyari tuimeisha mpa pongezi kwa kazi nzuri aliyoisha ifanya kwa kipindi cha miaka 5 na kwamba tumeisha mwambia akatafute kazi ingine basi tunahitaji mwakilishi mwenye sifa zifuatazo:-
- Awe na umri wa miaka 25 nakuendelea,miaka 18 kama katiba inavyosema asigombee hatutamchagua.
- Awe mgogo halisi kwa maana wazazi wake wote wawe wagogo, asiwe chotala, na ajue kuzungumza kigogo (chinyambwa)kwa ufasaha.
- Awe mkazi wa Bahi mwanachugu wa Bahi sokoni na kwingine wasiombe hatuwezi kuwachagua
- Awe na elimu ya juu Diploma holder na zaidi
- Awe na uwezo wa kujenga hoja ili aweze kupambana na wabunge machachari kama Tundu Lissu au John Mnyika au KangiLugola.
- Asiwe na tabia ya kuomba au kupokea rushwa,mwakilishi wa safari hii hatutaki mwenye tabia hiyo kwani tumejionea wenyewe mwakilishi wetu aliyopo alivyokuwa anatumia mda mwingi mahakamani na sisi kukosa mwakilishi.
- Awe na shamba la mpunga au mtama
- Awe na uwezo wa kulima au kuchunga ng`ombe kutwa(mgulo), kuchimba kisima, kujenga mlambo na kuesea.
- Awe na uwezo wa kupiga uwele au Lugugu au mpunga sinda moja kwa kutumia mikotya bila kusaidiwa
- Asiwe mlevi wa kupindukia, ambaye hanywi pombe ana sifa za ziada
- Awe mwanachama wa chama cha siasa kilicho na usajili wa kudumu, asiwe mtu wa kuhama hama vyama, na awe mwanachama wa chama atakachogombea siyo chini ya miaka 5
- Awe mcha mungu awe na dini inayoelewekana ucha mungu wake usiwe wa kutilia mashaka , kama mpagani asiombe hatuwezikumchagua
- Awe na DHIMA (mission) na MAONO(vision), ajue kwenye jimbo kuna matatizo gani na namna gani ataweza kuyatatua
- Asiwe mshirikina na asijihusishe na vitendo vya kishirikina kabisa, asiwe mtu wa kupiga ramli chonganishi kama mbunge Fulani wa Tanga, wenye sifa kama mbunge Fulani wa Tanga wasikanyage kwenye jimbo letu.
- Awe ameowa au ameolewa ili tumpime uwezo wake katika kutunza familia yake sifa ambayo itaturidhisha kuwa na uwezo wa kututunza sisi wana jamii.
INTERVIEW PANEL YA CHAMA CHOCHOTE HAIWEZI KUFANYA UPENDELEO WOWOTE
Karibuni.