Sidhani kama shisha ni miongoni mwa matatizo hapa nchini

THEBLACKPEARL

Member
Jun 11, 2015
69
46
Yaani hii nchi bwana kweli, eti matatzo makubwa katika jamii ya watanzania sio ishu tena.Yaani kabisa na tai yangu na suti yangu naacha changamoto zote za wananchi wangu nakaa mbele ya camera nazungumzia shisha?

Hivi shisha ina percentage ngapi ya madhara ya kiuchumi na kijamii kwa mamilioni ya vijana wa Tanzania? Hili ndilo tatizo kubwa kabisa kwa vijana kuliko mengine? Huu mchezo wenu wa kutusahaulisha madai yetu ya msingi kwenu viongozi tumeugundua.

Shisha waachieni wazazi watashughulika nao,vipi ajira?Vipi ile mikopo?Vipi ubora wa elimu?Vipi pembejeo? Vipi uhaba wa waalimu? Vipi thamani ya shilingi?Vipi afya?Vipi michezo? Kuna mambo ya msingi hatutayasahau, nyie zungukeni wee,mkija tutawauliza haya haya, kwanini viongozi mwatugeuza watanzania wajinga? Hakuna cha shisha wala nini hapa, kodi mnazokusanya tunataka tuone maendeleo.

MWANAHARAKATI
 
Watumiaji wa Shisha hawafiki ata 1% ya watanzania.
Hakukuwa na haja ya marufuku.Yangetengwa maeneo maalumu ya uvutaji na watu waelimishwe madhara ya Shisha.

Tuna changamoto nyingine tu kubwa zaidi.
 
Hilo chichi hata silifahamu linafananaje, wangezuia bange at least
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom