Toosweet
JF-Expert Member
- May 27, 2012
- 2,140
- 1,982
Salaam
Siasa za vyama vingi zilirejea Tanzania mwaka1992.Kabla ya hapo ilikuwa ni chama kimoja.Wanajeshi walikuwa makada wa chama. (Wah.Kikwete,Kinana,Moses Nnauye nk. Wakati tupo jeshini, ilikuwa mtu akiona muda wa ruhusa umeisha anakimbilia kwa mkuu wa wilaya kuongeza kibali. Akirudi kambini haguswi kwa kuwa 'afande' ameongeza kibali
Siasa za vyama vingi ziliondoa siasa jeshini lakini ni kwa nadharia tu. Katika awamu hii kuna wakuu wa wilaya na mikoa ambao ni wanajeshi na wana magwanda. Wako pia makatibu wakuu. Walikuwa 'wamehifadhi'kadi zao. Ni watiifu kwa chama.
CCM wanaweza kumpa cheo chochote ofisa wa jeshi na asiwakatalie ingawa ni kinyume cha taratibu. Majeshi bado ni jumuiya za Chama Cha Mapinduzi.
CCM imepiga marufuku vyama vya upinzani visifanye siasa, yenyewe inafanya mikutano ipendavyo, tena kwa rasilimali,miundombinu na muda wa serikali.
CCM na Magufuli hawawezi kufanya siasa za ushindani. Wanategemea jeshi la polisi kuwasaidia. Ukiondoa dola, CCM ni chama dhaifu sana.
Opposition wanasakwa na polisi na kufunguliwa mashtaka. Zamani waliambiwa ni vyama vya msimu,ha wana anuani,wanafanya siasa wakati wa uchaguzi. Sasa hivi wakifanya siasa wanaambiwa wanamzuia Rais kuleta maendeleo. Wakifanya CCM hawazuii maendeleo.
Siku mbili zilizopita Rais alifanya kikao na wakuu wa majeshi wastaafu. Alisema anabadilishana nao uzoefu. Nadhani ni zaidi ya hapo. Alitaka wa-plead allegiance. Si angewaita kina Mkapa, Kikwete na wengine wa kisiasa?
Kutumia majeshi yakusaidie kwenye siasa ni woga. Woga unazaa maamuzi yenye utata. Hii ni tabia halisi ya madikteta. CCM haiwezi kukamilika bila majeshi.
Ukiondoa majeshi/dola inakiua.
Hiki si chama cha siasa kwa kuwa hakikubaliki kwa kuuza sera na kujenga hoja, kinatumia, vitisho na ulaghai.
Sent using Jamii Forums mobile app
Siasa za vyama vingi zilirejea Tanzania mwaka1992.Kabla ya hapo ilikuwa ni chama kimoja.Wanajeshi walikuwa makada wa chama. (Wah.Kikwete,Kinana,Moses Nnauye nk. Wakati tupo jeshini, ilikuwa mtu akiona muda wa ruhusa umeisha anakimbilia kwa mkuu wa wilaya kuongeza kibali. Akirudi kambini haguswi kwa kuwa 'afande' ameongeza kibali
Siasa za vyama vingi ziliondoa siasa jeshini lakini ni kwa nadharia tu. Katika awamu hii kuna wakuu wa wilaya na mikoa ambao ni wanajeshi na wana magwanda. Wako pia makatibu wakuu. Walikuwa 'wamehifadhi'kadi zao. Ni watiifu kwa chama.
CCM wanaweza kumpa cheo chochote ofisa wa jeshi na asiwakatalie ingawa ni kinyume cha taratibu. Majeshi bado ni jumuiya za Chama Cha Mapinduzi.
CCM imepiga marufuku vyama vya upinzani visifanye siasa, yenyewe inafanya mikutano ipendavyo, tena kwa rasilimali,miundombinu na muda wa serikali.
CCM na Magufuli hawawezi kufanya siasa za ushindani. Wanategemea jeshi la polisi kuwasaidia. Ukiondoa dola, CCM ni chama dhaifu sana.
Opposition wanasakwa na polisi na kufunguliwa mashtaka. Zamani waliambiwa ni vyama vya msimu,ha wana anuani,wanafanya siasa wakati wa uchaguzi. Sasa hivi wakifanya siasa wanaambiwa wanamzuia Rais kuleta maendeleo. Wakifanya CCM hawazuii maendeleo.
Siku mbili zilizopita Rais alifanya kikao na wakuu wa majeshi wastaafu. Alisema anabadilishana nao uzoefu. Nadhani ni zaidi ya hapo. Alitaka wa-plead allegiance. Si angewaita kina Mkapa, Kikwete na wengine wa kisiasa?
Kutumia majeshi yakusaidie kwenye siasa ni woga. Woga unazaa maamuzi yenye utata. Hii ni tabia halisi ya madikteta. CCM haiwezi kukamilika bila majeshi.
Ukiondoa majeshi/dola inakiua.
Hiki si chama cha siasa kwa kuwa hakikubaliki kwa kuuza sera na kujenga hoja, kinatumia, vitisho na ulaghai.
Sent using Jamii Forums mobile app