Siasa na Dini: Mitume na Manabii mbona suala la kuombea mvua mmemwachia Mufti peke yake?

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
91,116
158,380
Ni kawaida panapokuwa na matukio ya kitaifa ya kisiasa viongozi wetu wa dini hukusanyika pamoja na wanasiasa na kufanya dua.

Sasa watanzania wote tunajua kuwa Maji ni uhai na kwamba katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu mvua haijanyesha. Mpaka sasa nilitegemea wale mitume na manabii wa nchi hii walau wangetukusanya pale uwanja wa taifa kwa ajili ya maombi kama wafanyavyo nyakati za mwaka mpya.

Nimpongeze Mufti Abubakar Zuber kwa kuitangaza jumapili hii kuwa ni siku ya kuombea mvua za heri, nami naahidi kuwa pamoja nao katika maombi hayo kiroho.

Mitume na manabii nanyi hamuoni umuhimu wa kutenda kama Mufti na kama mmebanwa na ratiba zenu tujulisheni ili tuangalie namna nzuri ya kushirikiana na Mufti siku ya jumapili.

Niendelee kuwatakia Kwaresma yenye baraka!
 
Hivi huyo Mufti ndo rafikiye Bashite?maana haya majina ya Alhad Musa na Abubaker Zubeir yananichanganya.

Kama ni yeye basi Allah hatayasikia maombi yake.Huwezi kushirikiana na Bar-shite halafu Mwenyezi Mungu akuhesabie haki au ajibu maombi yako.

Lakini kama si yeye,Allah atasikia maombi hayo na kuyajibu kwa kadri ya rehma zake.
 
Hii dhana ya kumuomba Mungu inanichanganya sana maana yeye ndiye aliyetuumba na anajua mahitaji yetu ya kila siku tena sio ya leo tu bali hata siku ijayo sasa ni vipi tena katika kututengenezea mustakabali wetu hadi tumuombe?
Alituumba ili tusitende dhambi usisahau hilo mkuu!
 
Hii dhana ya kumuomba Mungu inanichanganya sana maana yeye ndiye aliyetuumba na anajua mahitaji yetu ya kila siku tena sio ya leo tu bali hata siku ijayo sasa ni vipi tena katika kututengenezea mustakabali wetu hadi tumuombe?
Wewe kama mzazi una watoto ina maana wanapokuomba mahitaji sisi wazazi hatujui mahitaji yao?Au wewe hukuwahi kuwaomba wazazi wako kitu ulichokuwa unakihitaji? Kama uliomba au unaombwa mahitaji umewazaa wa nini?
 
Hii dhana ya kumuomba Mungu inanichanganya sana maana yeye ndiye aliyetuumba na anajua mahitaji yetu ya kila siku tena sio ya leo tu bali hata siku ijayo sasa ni vipi tena katika kututengenezea mustakabali wetu hadi tumuombe?
Ina maana hukubaliani nalo? Umeshawahi kujiuliza ni kwa nini mabaya hayo yanatokea? Au huelewi maana ya maombi hayo?
 
Hao maaskofu na manabii wa chini ya miti waombe mvua ije dhubutu labda maaskofu wa katoliki ,Anglikana ,waluteli ,lakini hawa akina lusekelo Gwajima ,Kakobe hata wamalize miaka wanaomba mvua haishuki .Halafu kwa nini toka Jiwe aingie madarakani hii nchi hajawahi kupata mvua za kutosha kama zamani ,maana yake hakubaliki ,mbingu zimemkataa ,atakuwa aliingia kimagumashi Hakuna aliyemchagua sasa Mungu ndio ana muonyesha .
 
Kwa kweli najiuliza sana lakini sipati jibu maana tunaelezwa heri na shari zimeumbwa na Mungu sasa najiuliza aliumba shari kwa madhumuni gani?
Shari imekuja baada ya uasi. Dunia iko mikononi mwa muasi (shetani). Yeye mkakati wake mkuu ni kuvuruga kazi za Mungu. Kila aliyeko duniani ana hiari ya ama kukubaliana na muasi au kumpinga. Njia pekee ya kumpinga ni maombi na kumcha Mungu. Ukielewa hayo hutashangaa.
 
Ni kawaida panapokuwa na matukio ya kitaifa ya kisiasa viongozi wetu wa dini hukusanyika pamoja na wanasiasa na kufanya dua.

Sasa watanzania wote tunajua kuwa Maji ni uhai na kwamba katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu mvua haijanyesha. Mpaka sasa nilitegemea wale mitume na manabii wa nchi hii walau wangetukusanya pale uwanja wa taifa kwa ajili ya maombi kama wafanyavyo nyakati za mwaka mpya.

Nimpongeze Mufti Abubakar Zuber kwa kuitangaza jumapili hii kuwa ni siku ya kuombea mvua za heri, nami naahidi kuwa pamoja nao katika maombi hayo kiroho.

Mitume na manabii nanyi hamuoni umuhimu wa kutenda kama Mufti na kama mmebanwa na ratiba zenu tujulisheni ili tuangalie namna nzuri ya kushirikiana na Mufti siku ya jumapili.

Niendelee kuwatakia Kwaresma yenye baraka!
Mufti wetu anapita katika njia ya sawa: Allah amuongoze katika kheri.
 
Kwanini basi Mungu amemuacha huyo shetani aendelee kutamba na kuwapoteza waja wake ilhali ana uwezo wa kumdhibiti ili ulimwengu uwe mahala salama kwa waja wake?

Shetani hana mamlaka kwa waja wa Mwenyezi Mungu: Jifunze sifa za waja.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom