Shule za serikali zaanza kuikumbatia CHADEMA

Shule za serikali zaanza kuikumbatia CHADEMA

belin

Member
Joined
Jan 9, 2012
Posts
21
Reaction score
8
Katika Kile kinachoonyesha kuwa CHADEMA inakwenda kuchukua dola 2015, Shule za sekondari zinazomilikiwa na Serikali zimeanza kuikumbatia CHADEMA.

Katika hali isyotarajiwa, kamati ya shule ya Sekondari ya Minaki imempitisha Mbunge wa Mbozi Magharibi kuwa Mgeni rasmi wa mahafali ya hamsini na nne yaliyofanyika leo shuleni hapo. Ikumbukwe kuwa Shule ya Minaki ni miongoni mwa shule kubwa Tanzania iliyotoa viongozi wengi wa serikali na CCM. Akihutubia Shuleni hapo, david Silinde alisema kuwa kuna haja ya kubadilisha mfumo wa elimu uliopo. licha ya shule hiyo kuwa kongwe hapa nchini, imebakia kuwa magofu ya wakoloni huku ikitelekezwa na Serikali ya CCM. Mbunge wa Kisarawe amehahidi maji ya uhakika chuoni hapo, huku Mgeni rasmi Mh. David Silinde akichangia fedha taslimu shlingi Milioni mbili pamoja na mambo mengine.

Huku akishangiliwa na wanafunzi hao, amesema kuwa wasubiri neema zaidi mwaka 2015 punde CHADEMA itakapochukua dola. hata hvivyo amehahidi kufikisha kilio chao katika kambi rasmi ya upinzania pamoja na kikao cha Bunge kinachokuja. katika hali ya kushangaza, Mbunge wa Kisarawe alizomewa na wanfunzi hao hali iliyomlazimu kuondoka haraka sana akisingizia kuwa ana vikao vya halmashauri. hata hivyo, Afisa Elimu wa Wilaya aiyekuwa mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaaya ya Kisarawe alisema kuwa leo hakuna kikao chochote cha Halmashauri, hajui kwanini Mbunge huyo aliamua kuwadanganya umati hwote huo.
 
Mkutano wa hadhara wa CCM uliofanyika mwishoni mwa week iliyopita katika viwanja vya Nyamagana kule MZA. Mwenyekiti wa CCM wa mkoa wa Mwanza Mh. Antony Diallo alisikika Ch 10 TV akisema kwamba CCM ndiyo yenye dola, na watendaji wake wote wa serikali wanatekeleza sera za CCM.

Akaendelea kuonya kwamba mfanyakazi yeyote yule wa SERIKALI awe Mwalimu, Daktari etc atakayeonekana anashabikia chama chochote cha cha UPINZANI, CCM itamshughulikia kwa kumfukuza kazi. Hivyo wafanyakazi wote wa Serikali wanatakiwa kushabakia chama tawala.

Kumbuka huyu Diallo alishawahi kuwa WAZIRI kwenye serikali za awamu ya 3 na 4. Ngoja tuone huo uongozi wa Minaki Sekondari CCM utaifanya nini??!!, maana alitoa kauli hiyo mbele ya Philip Mangula Makamu M/kiti wa CCM (T). Na mpaka leo haijakanushwa popote kuashiria kwamba CCM wanakubaliana na kauli ya Antony Diallo.
 
Kwa kutekeleza hilo la Dialo TV yake jana imeonyesha jinsi walivyowahamisha waalimu wakuu na kuwashusha vyeo na wengine kuwastaafisha CCM inatafuta kifo kitakatifu wanadhani waalimu hawana alliance au wamesahau methali ya ukiona mwenzio ananyolewa na wewe tia maji kichwa,walimu watageuka rebelious,mwanza ufaulu utashuka kwa kasi ya ajabu ,Dialo alikuwa kati ya watu waliofodge vyeti waliotajwa na Msema kweli na mimi naamini anaelimu ya kupepea,huwezi kusema maneno hayo kwenye chombo cha habari na waalimu kwa wingi wao wakasikia nchi nzima halafu Mangula hakurekebisha usemi
 
Dialo yuko ccm kwa ajili ya wizi na kukwepa kodi.
 
Kualikwa mbunge wa upinzani kwenye shule ya umma sio kosa,pia silinde amesoma hapo. Ccm ni vihiyo kwenye mambo mengi ya taifa letu! Hongera kamanda silinde.
 
natamani ningekuwapo kwenye mahafali hiyo Leo, lakini wapi? ila nitajua.... mimi .ni mkazi pale
 
Mkutano wa hadhara wa CCM uliofanyika mwishoni mwa week iliyopita katika viwanja vya Nyamagana kule MZA. Mwenyekiti wa CCM wa mkoa wa Mwanza Mh. Antony Diallo alisikika Ch 10 TV akisema kwamba CCM ndiyo yenye dola, na watendaji wake wote wa serikali wanatekeleza sera za CCM.

Akaendelea kuonya kwamba mfanyakazi yeyote yule wa SERIKALI awe Mwalimu, Daktari etc atakayeonekana anashabikia chama chochote cha cha UPINZANI, CCM itamshughulikia kwa kumfukuza kazi. Hivyo wafanyakazi wote wa Serikali wanatakiwa kushabakia chama tawala.

Kumbuka huyu Diallo alishawahi kuwa WAZIRI kwenye serikali za awamu ya 3 na 4. Ngoja tuone huo uongozi wa Minaki Sekondari CCM utaifanya nini??!!, maana alitoa kauli hiyo mbele ya Philip Mangula Makamu M/kiti wa CCM (T). Na mpaka leo haijakanushwa popote kuashiria kwamba CCM wanakubaliana na kauli ya Antony Diallo.
ukisikia taifa letu limevurugika ujue ni sababu ya ulevi wa madaraka wa ccm.
 
Diallo anauelewa finyu sana kuhusu taratibu na kanuni za utumishi serekalini. Yeye anafikiri anavyowapelekesha watumishi wake kule RFA na StarTV ndivyo hata watumishi wa serikali na mashirika yake wanavyoweza kuhenyeshwa.
Baada ya uchaguzi 2010 na yeye kutangazwa kashindwa Ilemela,alimsimamisha mtangazaji mmoja( kwa kumlinda na madhila mengine hatumtaji) kwa muda mrefu kisa eti aliposikia kapigwa chini aliangua kicheko.
Diallo atazidi kuididimiza CCM Mwanza kuliko anavyodhani
 
Huku kwetu mwenyekiti wa bodi ni chadema na mkuu watu amepewa jukumu la kusimamia shule mpya inayotarajiwa kufunguliwa hii karibu,hvyo maranyingi mkuu huambatana na mwenyekiti wa bodi ambaye ni cdm kwenda kukagua shule hyo,hvyo baadhi ya wanaccm humwambia mkuu amfukuze kwani wanadai yy amekwenda kuangalia mapungufu.mkuu huwaabia kuwa huyu ni mwenyekit wa bodi lazma ajue misaada ninayotoa kwny shule hii.
 
kumbe ndio maana walimu wa muce wameamua kujiunga kwa kuchukua kadi kabisa za CCM kisa ini wafanya kazi wa UMMA
 
RFA & Star TV walishabikia ushundi wa CDM pale Arumeru Mashariki na pia walikuwa wanaonyesha ushabiki wao kwa CDM wakati wa kutangazwa kwa matakeo ya Igunga. Nchi hii ni CDM mtindo mmoja. Walimu, Media, Madaktari, Watoto wa Mtaani, Wanavyuo, Makandarasi,,,, hata wafanyabiashara wakubwa soon wataonyesha ushabiki wao kwa CDM. Mjinga sana. Nani asiyeona hali ilivyo? Ni nani hasa asiyependa kupata maendeleo? Nimesoma kidogo pale School Of Medicine lakini siwezi kuendesha familia. No money... Miaka 51 huru! Sasa ni uhuru gani usioambatana na mabadiliko katika nyanja zakijamii? Kwenda zako Diallo. Tuache sisi waajiriwa na CDM yetu... The country of Democracy...the freedom of choice.

"I'll die fighting for the better future of Orphans, 'so called street children; but not real because they have are once upon the time they had parents', and my fellow poor men of my lovely country; Tanzania."
 
Tulianza na mungu,tutaendelea na mungu,tutamaliza na mungu
 
Back
Top Bottom