Shukrani ndugu zangu, natafuta kazi ya unganishaji wa umeme level one

Kijana Jr

JF-Expert Member
May 12, 2016
560
838
Habari zenu wakuu,

Mrejesho;

Ni mimi mdogo wenu, kaka yenu, mjomba wenu, baba mdogo wenu, mwanenu n.k. Mwaka jana nilikuja hapa ndani na thread ya kukata tamaa kwa kukosa mpenzi, rafiki kwa tatizo la usikivu(deaf) wangu na mambo yangu kwenda vibaya sana.

Wakuu asanteni sana kwa kunipa moyo wa ujasiri wa kupambana na kutokuwa na mtazamo wa kushindwa na kutoji -richard kwa sababu zisizo na umuhimu zaidi ya utu wangu nilionao ni bora zaidi.


Wana JF, Tatizo hili hapa wadau, ningependa kwa yoyote mwenye uwezo wakunipatia au kuniunganisha na kampuni au mtu yoyote nikapata kazi katika taaluma yangu ya unganishaji wa umeme level one ili niweze kumudu hali ya maisha hapa mjini maana nakufaa njaa.

Sio siri mficha maradhi kifo humuhumbua jamani nakufa njaa nashindia uji, nahitaji kazi kwa yoyote, mwenye uwezo wa kuniunganisha na kampuni za umeme kama TANESCO, TEMESA na kampuni nyengine ani PM niko vizuri sana katika hii fani ni great thinker, nipo tayari kufanya kazi katika mazingira yoyote.

Asanteni.
 
Unajua Fanya VP, jiajiri, weka tangazo humu humu JF kwenye jukwaa la matangazo madogo, hautokosa watu nakuhakikishia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom