PreGE2025 Shinyanga: Wasira atahadharisha wanaotaka kununua nafasi za ubunge, watumie pesa hizo kufungua biashara maana hawawezi kuhonga wajumbe wote 4,800

PreGE2025 Shinyanga: Wasira atahadharisha wanaotaka kununua nafasi za ubunge, watumie pesa hizo kufungua biashara maana hawawezi kuhonga wajumbe wote 4,800

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Mwizukulu wa Buganda

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2024
Posts
638
Reaction score
1,771
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira, ameonya vikali dhidi ya wale wanaotaka kununua nafasi za ubunge, akisisitiza kuwa kitendo hicho ni ukiukaji wa maadili ya chama na hakitavumiliwa. Badala yake, amewashauri kutumia fedha hizo kuanzisha biashara kama maduka.

Wasira alitoa kauli hiyo jana wakati akizungumza na wanachama wa CCM pamoja na makundi mbalimbali ya wananchi katika mkutano uliofanyika mjini Shinyanga.

Alieleza kuwa CCM imebadilisha mfumo wa upatikanaji wa wagombea wa ubunge kwa kura za maoni, ambapo idadi ya wajumbe wa kupiga kura imeongezeka kutoka 400 hadi 4,800. Lengo la mabadiliko hayo ni kuhakikisha mgombea anayepatikana ni chaguo halisi la wananchi.

"Zamani mlikuwa mkiwahonga shilingi laki moja moja kwa wajumbe 400. Sasa hivi wapo 4,800; kwa kiwango hicho hicho cha hongo, ni sawa na shilingi milioni 400. Si bora fedha hizo ufungue duka? Unanunua ubunge wa nini wakati mshahara wa mbunge ni shilingi milioni nne tu?" alisema Wasira.
Aliongeza kuwa hata kwa kiwango hicho cha fedha, mgombea hatoweza kutoa rushwa ya kutosha kwa kila mjumbe, akisema:

"Huwezi kutoa milioni 400, utawapa tu shilingi elfu kumi kila mmoja, lakini sisi tutakushughulikia kimaadili. Tunataka mtu achaguliwe kwa hiari ya wapiga kura, si kwa kununua ubunge. Lazima turudishe nidhamu ya chama."

Chanzo: Nipashe
 
Tangu lini CCM na maadili vikawa pamoja? CCM rafiki yake ni wizi, ufisadi, rushwa. Hata wakiweka wajumbe 10,000 wapige kura, akiamua mwenyekiti kuwa fulani apite kinyume na kura za wajumbe watakataa? Kama goli la mkono lilitumika uchaguzi wa serikali za mitaa, penye wapiga kura wengi zaidi ya hao 4,800; hiyo idadi haitasaidia kitu.

Halafu mzee hapo kwenye mshahara wa mbunge eti ni 4M! Asituone wajinga.
 
Back
Top Bottom