PostGE2025 Shida iko wapi kuunda Serikali ya mseto?

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections
Ameshauriwa hilo lakini TL amekataa. Anatarajia kupata kikubwa zaidi ya hicho, huyo ndio TL. Kashauriwa vingi ili atoke, lakini vyote kakataa. Matarajio ya TL ni makubwa sana. Anafikiri kuwa kwa sasa yeye ndio aliyeshika kwenye mpini. Hana haraka.
Ameshauriwa hilo ili atoke? Huoni kwamba huo ni uthibitisho kuwa yuko ndani kiuonevu? We Mjinga, hii hoja yako haina maashiko. Jipangeni upya.
 
Serikali ya mseto ya nini?

Itasaidia nini?

Uvhaguzi huru na wa haki ufanuike tuone nani atashinda.
 
Serikali 3 LAZIMA IJE.
YANAYOENDELEA YANASHANGAZA ULIMWENGU MZIMA!
 
Unaweza kuunda serikali ya mseto na wauuaji? Hukumbuki JK aliwasha moto AU alivyosema Kagame aongee na wale wauaji? Sasa hivi CCM ni kufutwa tu, wamemwaga da mu nyingi mno
 
Ni wazo la kipuuzi.

Serikali ya mseto wa Samia mwizi wa madaraka, aungwe mkono na wapenda haki kuhalalisha uovu aliofanya?

Mwambie aachie madaraka; iundwe serikali ya mpito kuandaa taratibu mpya za utawala wa nchi hii..

Serikali yoyote itakayomhusisha Samia Suluhu Hassan ni batili.

Huwezi kumuunganisha Tundu Lissu kwenye wazo la kipuuzi kama hilo.
 
Ameshauriwa hilo lakini TL amekataa. Anatarajia kupata kikubwa zaidi ya hicho, huyo ndio TL. Kashauriwa vingi ili atoke, lakini vyote kakataa. Matarajio ya TL ni makubwa sana. Anafikiri kuwa kwa sasa yeye ndio aliyeshika kwenye mpini. Hana haraka.
Unazo fikra za kipuuzi sana.
Matarajio aliyo nayo Lissu na waTanzania wote wapenda haki; ni kupatikana kwa HAKI katika uendeshaji wa nchi.

Hayo "matarajio makubwa" unayomtwisha Lissu umeyapata wapi wewe?
 
Serikali ya mseto ya nini?

Itasaidia nini?

Uvhaguzi huru na wa haki ufanuike tuone nani atashinda.
Ya kufanya maandalizi ya kupitisha katiba mpya na tume huru ya uchaguzi, kwa hiyo mnafikiri kuna watu wataachia madaraka kirahisi rahisi au kwa mashinikizo kama haya? Wamesha waambia "who are you"?

Aliweza kung'atuka Nyerere peke yake wengine hizo dalili hata hazipo maana wanatamani wakitoka wao waingie familia zao

Kulithibitisha hili chungulia baraza la mawaziri
 
Watu wanataka katiba itakayopunguza mamlaka kwa wanasiasa na kuwapa wananchi nguvu juu ya nchi yao na rasilimali zao namna gani watatawala uchumi wao bila kuingiliwa na external influence wewe unawaza kugawana madaraka.
 
Bangladesh wameweka serikali ya mpito hawajaweka serikali ya mseto.

Kwa hiyo si kitu ambacho hakiwezekani na hakijafanyika duniani.
 
Anaanzaje kuunda Serekali ya mseto wakati chama kikuu cha upinzani hakikushiriki uchaguzi haramu ?
Tanzania haina Rais kwa sasa kwani hakukuwa na uchaguzi mwaka huu 2025.
Katiba mpya na Serikali ya Tanganyika ndio hitaji la sasa la wananchi wa Tanzania ambao ndio waajiri wa viongozi wote wanaoaminiwa kushika madaraka na mamlaka ya kidola.
 
Aliamuru kitu cha hatari sana kwa hatma yake,naamini atakua anajutia sana maamuzi yake
 
Upande wowote unafaa bila mseto kikubwa haki, Amani, na kuondolewa Hofu ya Kutekwa ama kuuawa kwa kutoa maoni tuhakikishiwe kwa vitendo!!!!!
 
Huku tanganyika kuna manayangau yana uroho wa madaraka na yamekaa kipigaji
 
Mawazo yako mazuri tu tena yana mwelekeo wa kizalendo. Nadhani tuupe mchakato wa ICC nafasi ili tutekebishe makosa yaliyotufikisha hapa kwa kiburi tu. 🤔
 
Huwezi kuunda serikali ya mseto Kwa ajili ya WAHUNI wachache WANAOJIITA GENZ ambao wanachoma miundombinu ya wananchi.
 
Reactions: Tui
Katiba mpya itakuja na sisi tutakuwa vizuri tu lakini Lissu ni mkorofi, na asilimia kubwa yeye ndiye aliyetaka huu upumbavu utokee ili watu wakose wote.

View: https://youtu.be/Pgu4VfqBGKs?si=9ZsKGWdJTSbDLh7P
 
Reactions: Tui
Hakuna kitu kisichokuwa na maslahi ya CCM kinaweza kufanyika kwenye nchi hii
 
Kwa LIssu mwenyewe.
Ungeeleza ulichoona au kusikia toka kwa Lissu kuhusu jambo hilo ingesaidia zaidi, kuliko ulivyofanya hapa.
Lissu ni mtu wa 'principle', hayumbiyumbi tu kufurahisha kundi fulani la watu Ni mtu mwenye msimamo usiotiliwa shaka.. Ndiyo sababu unamwona akisulubiwa kama alivyo sasa.

Lisuu hawezi kuwa mshiriki katika huo ujinga wa serikali ya mseto na watu waovu hawa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…