Sheria ya Habari 2016: Pongezi kwa JPM toka kwa waandishi Arusha

kunena

JF-Expert Member
Nov 29, 2016
506
719
Umoja wa waandishi wa habari mkoani Arusha umeipongeza serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mh John Pombe Magufuli kwa kuupitisha muswada wa sheria ya vyombo vya habari ya mwaka 2016 kwani utaleta heshima kwa tasnia ya habari nchini.
"At least sasa sheria hii inamtambua mwandishi ni nani kwani fani hii imevamiwa" alinukuliwa mwenyekiti wa Arusha Press Club Ndg Cloud Gwando wakati wa kongamano la waandishi wa habari na sekretarieti ya mkoa kufanya tathmini ya mafanikio na changamoto kwa kipindi cha nusu mwaka Juni -Desemba 2016.
Pia waandishi hao wamemshukuru mkuu wa mkoa Ndg Mrisho Gambo kwa kutambua mchango wa waandishi kwa maendeleo ya mkoa kiujumla, ambapo Mh Gambo aliwaasa waandishi wafanye kazi zao kwa weledi na kutanguliza uzalendo mbele kwa kuandika habari ambazo zitaonyesha vipaumbele gani serikali ivifanyie kazi kwa maslahi mapana ya taifa.
fad6e608dbf25d7383315952b37a1412.jpg

Mkuu wa mkoa wa Arusha Ndg Mrisho Gambo
7c86c3cbb5f5cb60f20fe2c81107b5c1.jpg

Mwenyekiti wa Arusha Press Club Ndg Cloud Gwando akitoa hotuba ya waandishi wa habari mkoani Arusha
f6ea2227fb9fab09dc92c31ef0d7e07f.jpg

Mmoja wa waandishi akichangia mada katika kongamano hilo
a4d26ce5aa8ed2ecc85d8d46de78fb4e.jpg

Picha ya pamoja, mkuu wa mkoa wa Arusha,sekreteriet ya mkoa,mkurugenzi wa Jiji la Arusha na wadau wa habari mkoa wa Arusha.
 
Daaah kitu kimetokea miezi sasa mnatoa pongezi leo, au ndo kujipendekeza? Mlikuwa wapi wakato ule. Hapa kazi tu pongezi baadaye na mkalime sasa mvua zimeshaanza kunyesha na mwaka kesho kama mvua zitanyesha msitegemee serikali kuwapa chakula bure
 
Daaah kitu kimetokea miezi sasa mnatoa pongezi leo, au ndo kujipendekeza? Mlikuwa wapi wakato ule. Hapa kazi tu pongezi baadaye na mkalime sasa mvua zimeshaanza kunyesha na mwaka kesho kama mvua zitanyesha msitegemee serikali kuwapa chakula bure
Mkuu acha kujitoa fahamu basi, mi sijaona tatizo kwa waandishi kutoa pongezi zao leo sabau labda ndio mahali leo wamepata jukwaa rasmi la kusemea yanayowagusa, nadhani wamesikia pia wito wako wa kwenda kulima....no hard feelings kiongozi pamoja sana.
 
Bila kusahau kauli mbiu ya [HASHTAG]#UongoziUnaoachaAlama[/HASHTAG]
 
nimegundua pale panaposemekana kuna nafasi fulani ipo wazi inahitaji uteuzi.... post nyingi za kusifia zinaongezeka mtandaoni hivi kwa nini?
 
nimegundua pale panaposemekana kuna nafasi fulani ipo wazi inahitaji uteuzi.... post nyingi za kusifia zinaongezeka mtandaoni hivi kwa nini?
Hahaha sasa mkuu hayo yamesemwa na mwenyekiti wa Arusha Press Club je na yeye anatafuta kuteuliwa??
 
Safi sana waandishi, msiwasikilize chadema ambao wanalipwa na mafisadi kupinga kila kitu


Tokea wasafishe fisadi lowasa, akili zao zimefyatuka
 
Hahaha sasa mkuu hayo yamesemwa na mwenyekiti wa Arusha Press Club je na yeye anatafuta kuteuliwa??
Hujasikia nimejiuzulu ukuu wa wilaya .....si lazima ijazwe? Hivi Gondwe mbona hasomi taarifa ya habari ITV? au amehama?
 
Back
Top Bottom