Mwanaukweli
JF-Expert Member
- May 18, 2007
- 4,789
- 1,732
Rais wa Zanzibar Dr. Ali Mohamed Shein jana alikemea vikali vitendo vya ubakaji na udhalilishaji wa Jinsia, alipokuwa akihutubia Baraza la Idd. Baraza hilo lilifanyika kwenye Ukumbi wa Salama katika Hoteli ya Bwawani mjini Unguja.
Dkt. Shein alinukuu taarifa ya Waziri wa Ustawi wa Jamii, Maendeleo ya Vijana, wanawake na watoto, ambayo inasema kuwa jumla ya watoto wa kike 480 wamebakwa Unguja na Pemba katika kipindi cha tangu Julai 2012 hadi April 2013, wastani wa matukio 48 kwa mwezi, au 12 kwa wiki.
Alifafanua kuwa watoto 53 wameharibiwa katika kipindi hicho na wanawake 273 kudhalilishwa.
Alisema ni jambo la kusikitisha sana kuona kwamba silka, ustaarabu na mila za Kizanzibari zinapotea kwa nguvu huku vitendo vya ubakaji na udhalilishaji vikishamiri.
Dkt. Shein alikumbusha wazazi, walezi, wazee na viongozi mballmbali kutimiza wajibu wao wa kulea pamoja na kusimamia na kuendeleza maadili mema.
Kwa namna ya pekee aliwaomba viongozi wa dini waendelee kukemea maovu na kuamrisha matendo mema, na kuepuka mizozano na migogoro ya kidini. Aliwasihi viongozi hao wa dini wawe mfano wa kuönesha subira na kufuata misingi ya dini kusuluhisha tofauti. Aliwaomba viongozi hao wa dini wasichochee waumini kuvunja amani.
Dkt. Shein alinukuu taarifa ya Waziri wa Ustawi wa Jamii, Maendeleo ya Vijana, wanawake na watoto, ambayo inasema kuwa jumla ya watoto wa kike 480 wamebakwa Unguja na Pemba katika kipindi cha tangu Julai 2012 hadi April 2013, wastani wa matukio 48 kwa mwezi, au 12 kwa wiki.
Alifafanua kuwa watoto 53 wameharibiwa katika kipindi hicho na wanawake 273 kudhalilishwa.
Alisema ni jambo la kusikitisha sana kuona kwamba silka, ustaarabu na mila za Kizanzibari zinapotea kwa nguvu huku vitendo vya ubakaji na udhalilishaji vikishamiri.
Dkt. Shein alikumbusha wazazi, walezi, wazee na viongozi mballmbali kutimiza wajibu wao wa kulea pamoja na kusimamia na kuendeleza maadili mema.
Kwa namna ya pekee aliwaomba viongozi wa dini waendelee kukemea maovu na kuamrisha matendo mema, na kuepuka mizozano na migogoro ya kidini. Aliwasihi viongozi hao wa dini wawe mfano wa kuönesha subira na kufuata misingi ya dini kusuluhisha tofauti. Aliwaomba viongozi hao wa dini wasichochee waumini kuvunja amani.