Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 43,037
- 34,741
Leo naishika tama, nikijikuna kichwani,
Dunia sasa zahama, imejaa hamkani ,
Sungura kaila nyama, akayawacha majani,
Shangaa nikushangae, watushangae malenga.
Mwiko kukoroga chai, mwenzenu ninauliza,
Na bubu kuwa laghai, hili linanitatiza,
Lagombaniwa papai , uwa halijachomoza,
Shangaa nikushangae, watushangae malenga.
Dagaa linafukizwa, harufu lisijetoa,
Hili nalo lashangaza, pele kuitwa churua,
Na eda hajamaliza , posa keshaipokea ,
Shangaa nikushangae, watushangae malenga.
Ana upara kichwani , kitana cha kazi gani?
Papa kakutwa mtoni, na makaziye ni pwani,
Huyu kavaa miwani , kuficha tongo machoni,
Shangaa nikushangae, watushangae malenga.
Dunia sasa zahama, imejaa hamkani ,
Sungura kaila nyama, akayawacha majani,
Shangaa nikushangae, watushangae malenga.
Mwiko kukoroga chai, mwenzenu ninauliza,
Na bubu kuwa laghai, hili linanitatiza,
Lagombaniwa papai , uwa halijachomoza,
Shangaa nikushangae, watushangae malenga.
Dagaa linafukizwa, harufu lisijetoa,
Hili nalo lashangaza, pele kuitwa churua,
Na eda hajamaliza , posa keshaipokea ,
Shangaa nikushangae, watushangae malenga.
Ana upara kichwani , kitana cha kazi gani?
Papa kakutwa mtoni, na makaziye ni pwani,
Huyu kavaa miwani , kuficha tongo machoni,
Shangaa nikushangae, watushangae malenga.