Sauti ya nyikani
Member
- Jan 24, 2015
- 29
- 20
Asantee
Tunda hukukuta chini, liangani ukalidaka!
Tunda tamu kama nini, midenda inakutoka!
Tunda lafichwa porini, kwenye nyasi na vichaka!!!
Tunda hili la ajabu!!!!!!
Tunda hukukuta chini, liangani ukalidaka!
Tunda tamu kama nini, midenda inakutoka!
Tunda lafichwa porini, kwenye nyasi na vichaka!!!
Tunda hili la ajabu!!!!!!
Zingatia vina na mizani tafadhali
Zingatia vina na mizani tafadhali
Andanenga malenga wetu.
Kwa kweli tunda ni tamu, kama umejitwalia,
Sukariye ni adimu, adhimu wengine hulia,
Si mithili kujikimu, pspf chungulia,
Tunda lina baraka, haulipati kondeni.
Ndugu yangu Jogi hata wewe kwenye ubeti wako katika mshororo ( mataeri) wa pili umeweka mizani 9 badala ya 8? pale ulipo andika "adhimu wengine hulia". Hakuna mkamilifu sote hughafirika kama alivyo kosea kwa bahati mbaya Mzee Raza.
Ila wote ni wazuri nipenda tungo zenu.
Kwa mujibu wa wanafasihi mambo leo, shairi si lazima lizingatie urari wa vina na mizani mkuu,
Sijivunii kukosea, nasikitika lakini sitaacha kuhimiza ukamilifu.
NAPENDA MASHAIRI
Ndugu yangu Jogi hata wewe kwenye ubeti wako katika mshororo ( mataeri) wa pili umeweka mizani 9 badala ya 8? pale ulipo andika "adhimu wengine hulia". Hakuna mkamilifu sote hughafirika kama alivyo kosea kwa bahati mbaya Mzee Raza.
Ila wote ni wazuri nipenda tungo zenu.
Pia uzuri wake hili ni jukwaa la mahuaiano, mapenz nk. si jukwaa la lugha tunalenga kuburudisha na kufundisha yanayohusiana na jukwaa husika ili hata asie mshairi achangie.
Sijivunii kukosea, nasikitika lakini sitaacha kuhimiza ukamilifu.
NAPENDA MASHAIRI
1) Kutunga nlivokumisi,
mwishoni nitaugua,
Mtima wangu yabisi,
nawe ndio lake jua,
Ya moyoni warahisi,
walimwengu kuyajua,
Kutunga sitokudisi,
amani waniletea.
2) Wafanya kwa ufanisi,
jukumu walichukua,
Wawapita wahandisi,
mabonde kuyafukia,
Wafundisha kirahisi,
vipofu wawafungua,
Kutunga sitokudisi,
amani waniletea.
3) Usiku wa alhamisi,
kwa kazi mejichokea,
Bado kelele za bosi,
mambo yananilemea,
Kwa yote sitokuasi,
na moyo ukatulia,
Kutunga sitokudisi,
amani waniletea.
4) Kama mfupa na fisi,
mfano kichulia,
Muda wangu we filisi,
milele sitojutia,
Hatutengi ibilisi,
damu tulishangia,
Kutunga sitokudisi,
amani waniletea.