ostrichegg
JF-Expert Member
- Jun 30, 2013
- 12,048
- 6,199
Kweli corona imekita, kudanganya haifai.
Dunia yote walia, hata wenye utajiri.
Wenzetu wanapambana, Siye bado hatujali.
Pazuri pakipotea, tuje kumlaumu nani?
Mlioshika madaraka, hivi mwatupelekapi?
Misingi tumeitoka, twayahama maadili.
Mema tulioachiwa, yanarithiwa na chuki.
Pazuri pakipotea, tuje kumlaumu nani?
Kwa kuringia umwamba, tumesha poteza vingi.
Umoja ulotulea, umekwisha tupwa mbali.
Sasa wapima corona, nao eti wahaini.
Pazuri pakipotea, tuje kumlaumu nani?
Fikra zilizowajaa, kutishana kwa visasi.
Wengine kuwakataa, na kuwazushia uchawi.
Mwanzo wa kushindwa vita, ni dhahiri uko nanyi.
Pazuri pakipotea, tuje kumlaumu nani?
Dunia yote walia, hata wenye utajiri.
Wenzetu wanapambana, Siye bado hatujali.
Pazuri pakipotea, tuje kumlaumu nani?
Mlioshika madaraka, hivi mwatupelekapi?
Misingi tumeitoka, twayahama maadili.
Mema tulioachiwa, yanarithiwa na chuki.
Pazuri pakipotea, tuje kumlaumu nani?
Kwa kuringia umwamba, tumesha poteza vingi.
Umoja ulotulea, umekwisha tupwa mbali.
Sasa wapima corona, nao eti wahaini.
Pazuri pakipotea, tuje kumlaumu nani?
Fikra zilizowajaa, kutishana kwa visasi.
Wengine kuwakataa, na kuwazushia uchawi.
Mwanzo wa kushindwa vita, ni dhahiri uko nanyi.
Pazuri pakipotea, tuje kumlaumu nani?