Shairi: Mtatiro..

Dotto C. Rangimoto

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2012
Posts
1,985
Reaction score
1,286
Wajomba na mashangazi,wazee mabarobaro,
Pana fungu la ghawazi, latumiwa na kigaro,
Hununua waziwazi, wanati kama nduaro.

Yale yake maongezi, yamejaa chinjarero,
Kanaswa na hajiwezi, kama nswi kwenye vyero,
Ni wa hovyo utetezi, amefanywa nini sero?

Jamani ndarama hizi, zilizo fungasha ziro,
Zimewatia uchizi, Mwikabe na Mtatiro,
Wameushiriki wizi, Buyungu na Simanjiro.

Huyafungua maozi, aone yenye kasoro,
Ni sifa ya kiongozi, kutatua migogoro,
Hakimbii kama bozi, kutafuta kichochoro.

Kiongozi mfumbuzi, katu haleti uchuro,
Hutafuta utatuzi, wala hatafuti guro,
Ila wapo wapuuzi, hununuliwa kwa yuro.

MISAMIATI
Ghawazi...........fedha
Kigaro...............kikundi
Nduaro...........samaki
Nimekishufu.....nimekitazama
Chinjarero......hofu
Nswi.............samaki
Ndarama.......pesa
Maozi............macho
Bozi...............mpumbavu
Katwa...........katu
Vyero.............mtego wa kunasa samaki
Guro.............uhamaji wa sehemu nyingine
Yuro.............fedha ya umoja wa Ulaya.

18 Agosti 2018 Alhamis 18:31

Jina la Mtunzi Dotto Rangimoto
Jina La Utunzi Jini Kinyonga
Simu +255762845394 Morogoro.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni jambo la kushangaza pumba siku hizi zina picha contact number
 
Ni jambo la kushangaza pumba siku hizi zina picha contact number
Shukuru kwa kupata uzi wa kucomment! Wewe chenga zako zi wapi kama siyo kushika simu muda wote kukodolea nyuzi za wenye busara na hekima?
 
Mkuu Dotto
1. Mtamlaumu bure, kuhama halali yake,
Kujiunga ni kwa bure, kuhama ni haki yake,
Ukizoea vya bure, tavunja heshima yake,
Mtatiro amehama, sababu ya matatizo,

2. Sababu ya matatizo, Mtatiro amehama,
Upinzani ni tatizo, na wengine watahama,
Wapinzani matatizo, wote watakuja hama,
Mtatiro amehama, sababu ya matatizo.

3. Nchi yetu ni tatizo, watu wetu matatizo,
Viongozi ni tatizo, wananchi matatizo,
Vyama vyetu ni tatizo, serikali matatizo,
Mtatiro amehama, sababu ya matatizo.

4. CUF ina matatizo, CCM ni tatizo,
Amehama matatizo, amehamia tatizo,
Chama chenye matatizo, ameongeza tatizo,
Mtatiro amehama, sababu ya matatizo.

5. Chadema ni matatizo, viongozi ni tatizo,
Sera zake matatizo, na misingi ni tatizo,
Wakimbia matatizo, waenda kwenye tatizo,
Mtatiro amehama, sababu ya matatizo.

P.
 
Hata nyumbani kwangu pia TATIZO sijuwi nihamiye wapi miye??? kweli ni haki yake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata nyumbani kwangu pia TATIZO sijuwi nihamiye wapi miye??? kweli ni haki yake.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kwako tatizo linafahamika, pole, huna pa kuhamia kwa sababu kote ni matatizo tupu, ila when you have to choose in between two devils, choose the lesser, tangaza tuu kuhamia, ukavute mpunga, ujilie tuu kivulini kusubiria teuzi!.

P.
 
Kwako tatizo linafahamika, pole, huna pa kuhamia kwa sababu kote ni matatizo tupu, ila when you have to choose in between two devils, choose the lesser, tangaza tuu kuhamia, ukavute mpunga, ujilie tuu kivulini kusubiria teuzi!.

P.
sina bei,,hapana, sina soko, ningekuwa diwani au kigogo ningekuwa na soko na dhahiri ningekuwa na bei pia.... mm kama kwenda nende kwa mkopo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa mara ya kwanza nakupongeza baada ya kukuponda kipindi kirefu lkn umeonyesha uvumilivu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyo mtatiro kiufupi ni njaa naamini moyoni bado ni mpinzani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyo mtatiro kiufupi ni njaa naamini moyoni bado ni mpinzani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama upinzani ni tatizo ndo mana amehama, mbona unasema pia nchi yetu ni tatizo na bwana paskali hauhami?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…