donniebrasco
JF-Expert Member
- Aug 8, 2013
- 887
- 770
Nina Imani atapatikana,
Mfanyabiashara kijana,
Machoni hajaonekana,
Tunahuzunika sana.
Tunamuomba JALALI,
Sana kwake tunasali,
Atuoneshe hata mahali,
Tuna maumivu makali.
Polisi wetu wanajitahidi,
Na wanaongeza spidi,
Na pia raia wema ikibidi,
Watoe wao ushahidi.
Vikosi vyote viko kazini,
Vinamtafuta juu na chini,
Nchi kavu mpaka majini,
Atapatikana karibuni.
Najaribu sana kufikiri,
Wengi tu ametuajiri,
Lazima ukweli tukiri,
MWENYEZI amsitiri.
Wenzake tunasikitika,
Hatujajua nini kimemfika,
Atalindwa na malaika,
Yeye simba wa Afrika.
Tujaribu kuwa wema,
Tuache hovyo kusema,
Bado sana ni mapema,
MUNGU ni mwema.
Pole kwa wanafamilia,
Waendelee kuvumilia,
Sisi MOLA tunamlilia,
Simba na Yanga pia.
Mfanyabiashara kijana,
Machoni hajaonekana,
Tunahuzunika sana.
Tunamuomba JALALI,
Sana kwake tunasali,
Atuoneshe hata mahali,
Tuna maumivu makali.
Polisi wetu wanajitahidi,
Na wanaongeza spidi,
Na pia raia wema ikibidi,
Watoe wao ushahidi.
Vikosi vyote viko kazini,
Vinamtafuta juu na chini,
Nchi kavu mpaka majini,
Atapatikana karibuni.
Najaribu sana kufikiri,
Wengi tu ametuajiri,
Lazima ukweli tukiri,
MWENYEZI amsitiri.
Wenzake tunasikitika,
Hatujajua nini kimemfika,
Atalindwa na malaika,
Yeye simba wa Afrika.
Tujaribu kuwa wema,
Tuache hovyo kusema,
Bado sana ni mapema,
MUNGU ni mwema.
Pole kwa wanafamilia,
Waendelee kuvumilia,
Sisi MOLA tunamlilia,
Simba na Yanga pia.