Baraka Kasinge
Member
- Apr 4, 2016
- 68
- 81
MWAIKENDA
Salaam Bwana Kasinge, nimefika kukuona,
Machache nawe tubonge, mawazo badilishana,
Vipi taifa lisonge? Vijana kibaguana?
Aliyetuloga kafa, vijana twaangamia.
KASINGE
Nami ninakusalimu, karibu wangu rafiki,
Yako mada ni muhimu, tukikwacha unafiki,
Kibaya kwetu na sumu, vijana kwishi kwa chuki,
Mwaikenda wakosea, alotuloga hajafa.
MWAIKENDA
Nelewe yangu kauli, kusema mlozi kafa,
Tupishanapo kauli, sicho kisa maarifa,
Ni misimamo mikali, mapenzi chama ya kufa,
Kasinge unielewe, aliyetuloga kafa.
Kwa nini alishakufa, vibaya twachukiana,
Mtu sipatwe maafa, peana pole hakuna,
Licha sawia taifa, peke vyama vyatukuna,
Kasinge unielewe, aliyetuloga kafa.
Hatunayo maendeleo, uvyama ndiye mchawi,
Chekecha wako upeo, ushirika haukuwi,
Mahasimu kila leo, na matusi yapunguwi,
Maisha pasi umoja, aliyetuloga kafa.
KASINGE
Sana ninakuelewa, hitimisho nabishia,
Mchawi kujielewa, kichwani kwatupungua,
Ushabiki twazidiwa, twafwa pasi kujua,
Alotuloga hajafa, wenyewe hatujelewi.
Mwitwao wakereketwa, hamwezi kubaliana,
Mezani mada kiletwa, lenu kubwa kushindana,
Nzito hoja zikikitwa, mwishoni kutukanana,
Mwaikenda nielewe, alotuloga hajafa.
Haijalishi ni wapi, hata kiwa fesibuku,
Mtaonana makapi, vile mwewe naye kuku,
Shikana kono sa ngapi? Mwekeana marufuku,
Alotuloga hajafa, ni ubongo kutulegea.
Mwenyewe ufikirie, chako chama licho nacho,
Wangapi nihesabie, wasosema kwa kificho,
Mwenyekiti wasijalie, kikovu akiwa nacho,
Alotuloga hajafa, akili haturefushi.
Na matokeo ukada, kilo kwenu kutetea,
Bichwa lajaa husuda, upande ule chukia,
Utegeshi misaada, yenu kesho kuhofia,
Alotuloga hajafa, ufungi ndoa na vyama.
Wale utawasikia, magamba wote kijani,
Na kijani hujibia, lenu chama ukandani,
Vijana mwajimezea, sumu pasi kubaini,
Alotuloga hajafa, wazalendo tubakie.
MWAIKENDA
Yako jamali mawazo, Kasinge nayasikia,
Kile naweka katazo, vyama kujikosea,
Sioni pote katazo, katibani na sheria,
Alotuloga kafa, Kasinge usikatae.
Kimoja nikuulize, karibu ninakuaga,
Zetu kadi tuunguze, ndo wazalendo huwaga?
Na uhuru nieleze, si vyama viliutega?
Kubali ama kataa, aliyetuloga kafa.
KASINGE
Sisemi kadi mchane, si dhambi wala miiko,
Nashauri muungane, kwa ajenda za mashiko,
Mabaya yaonekane, mazuri nayo yaweko,
Aliyetuloga hajafa, tena tunamjua.
Akishaitwa fisadi, sijalishe chako chama,
Mwenyekiti kikaidi, simumunye kumsema,
Kuwasifu huna budi, na wale kifanya vyema,
Alotuloga hajafa, akili zinatupwaya.
Vijana tunatumika, kila panapo umoja,
Kwako kikivurugika, malipo laki moja,
Wona maisha hakika, hujui kesho yangoja,
Alotuloga hajafa, yu hai twaishi naye.
Umoja imara kosa, chama kinakutuma,
Gombea twakupa pesa, kushinda ni lazima,
Usije macho pepesa, wavuruge kundi zima,
Alotuloga hajafa, tumezidi kutumika.
Wenu uchumi kujenga, vyama kando wekeni,
Kasinge yule atunga, nami mwimbaji kwayani,
Pamoja tukijiunga, umasikini kapuni,
Uchumi ushirikyano, alotuloga hajafa.
MWAIKENDA
Huishi katu kunena, Kasinge hapo ishia,
Mekwelewa kwa mapana, tutaja kuendelea,
Naona yawezekana, vijana kubadilikia,
Alotuloga kafa, Kasinge usiku mwema.
KASINGE
Zangu pongezi za dhati, kwako pia Mwaikenda,
Vijana tukaze buti, vyawezekana viwanda,
Serikali yekwe kati, wapi mitaji na randa?
Alotuloga hajafa, usiku mwema bradha.
©2017
barakakasinge@gmail.com
Salaam Bwana Kasinge, nimefika kukuona,
Machache nawe tubonge, mawazo badilishana,
Vipi taifa lisonge? Vijana kibaguana?
Aliyetuloga kafa, vijana twaangamia.
KASINGE
Nami ninakusalimu, karibu wangu rafiki,
Yako mada ni muhimu, tukikwacha unafiki,
Kibaya kwetu na sumu, vijana kwishi kwa chuki,
Mwaikenda wakosea, alotuloga hajafa.
MWAIKENDA
Nelewe yangu kauli, kusema mlozi kafa,
Tupishanapo kauli, sicho kisa maarifa,
Ni misimamo mikali, mapenzi chama ya kufa,
Kasinge unielewe, aliyetuloga kafa.
Kwa nini alishakufa, vibaya twachukiana,
Mtu sipatwe maafa, peana pole hakuna,
Licha sawia taifa, peke vyama vyatukuna,
Kasinge unielewe, aliyetuloga kafa.
Hatunayo maendeleo, uvyama ndiye mchawi,
Chekecha wako upeo, ushirika haukuwi,
Mahasimu kila leo, na matusi yapunguwi,
Maisha pasi umoja, aliyetuloga kafa.
KASINGE
Sana ninakuelewa, hitimisho nabishia,
Mchawi kujielewa, kichwani kwatupungua,
Ushabiki twazidiwa, twafwa pasi kujua,
Alotuloga hajafa, wenyewe hatujelewi.
Mwitwao wakereketwa, hamwezi kubaliana,
Mezani mada kiletwa, lenu kubwa kushindana,
Nzito hoja zikikitwa, mwishoni kutukanana,
Mwaikenda nielewe, alotuloga hajafa.
Haijalishi ni wapi, hata kiwa fesibuku,
Mtaonana makapi, vile mwewe naye kuku,
Shikana kono sa ngapi? Mwekeana marufuku,
Alotuloga hajafa, ni ubongo kutulegea.
Mwenyewe ufikirie, chako chama licho nacho,
Wangapi nihesabie, wasosema kwa kificho,
Mwenyekiti wasijalie, kikovu akiwa nacho,
Alotuloga hajafa, akili haturefushi.
Na matokeo ukada, kilo kwenu kutetea,
Bichwa lajaa husuda, upande ule chukia,
Utegeshi misaada, yenu kesho kuhofia,
Alotuloga hajafa, ufungi ndoa na vyama.
Wale utawasikia, magamba wote kijani,
Na kijani hujibia, lenu chama ukandani,
Vijana mwajimezea, sumu pasi kubaini,
Alotuloga hajafa, wazalendo tubakie.
MWAIKENDA
Yako jamali mawazo, Kasinge nayasikia,
Kile naweka katazo, vyama kujikosea,
Sioni pote katazo, katibani na sheria,
Alotuloga kafa, Kasinge usikatae.
Kimoja nikuulize, karibu ninakuaga,
Zetu kadi tuunguze, ndo wazalendo huwaga?
Na uhuru nieleze, si vyama viliutega?
Kubali ama kataa, aliyetuloga kafa.
KASINGE
Sisemi kadi mchane, si dhambi wala miiko,
Nashauri muungane, kwa ajenda za mashiko,
Mabaya yaonekane, mazuri nayo yaweko,
Aliyetuloga hajafa, tena tunamjua.
Akishaitwa fisadi, sijalishe chako chama,
Mwenyekiti kikaidi, simumunye kumsema,
Kuwasifu huna budi, na wale kifanya vyema,
Alotuloga hajafa, akili zinatupwaya.
Vijana tunatumika, kila panapo umoja,
Kwako kikivurugika, malipo laki moja,
Wona maisha hakika, hujui kesho yangoja,
Alotuloga hajafa, yu hai twaishi naye.
Umoja imara kosa, chama kinakutuma,
Gombea twakupa pesa, kushinda ni lazima,
Usije macho pepesa, wavuruge kundi zima,
Alotuloga hajafa, tumezidi kutumika.
Wenu uchumi kujenga, vyama kando wekeni,
Kasinge yule atunga, nami mwimbaji kwayani,
Pamoja tukijiunga, umasikini kapuni,
Uchumi ushirikyano, alotuloga hajafa.
MWAIKENDA
Huishi katu kunena, Kasinge hapo ishia,
Mekwelewa kwa mapana, tutaja kuendelea,
Naona yawezekana, vijana kubadilikia,
Alotuloga kafa, Kasinge usiku mwema.
KASINGE
Zangu pongezi za dhati, kwako pia Mwaikenda,
Vijana tukaze buti, vyawezekana viwanda,
Serikali yekwe kati, wapi mitaji na randa?
Alotuloga hajafa, usiku mwema bradha.
©2017
barakakasinge@gmail.com