Serukamba alikuwa anamaanisha type ya kina Nape?

kipuyo

JF-Expert Member
Jul 30, 2009
1,785
1,464
Mijadala ya makadirio ya bajeti ya wizara ya Elimu na mafunzo ya ufundi inaendelea kwa siku ya pili hii leo.

Wabunge wengi waliopata nafasi ya kuchangia kwenye bajeti hii wameona kuna haja ya tume kuundwa itakayoangalia mustabali wa elimu yetu kwa ujumla kwani kutokana na mfumo wa elimu tulionao kwa sasa ni dhahiri kuwa tunawandaa wataalam feki wa kisasi kijacho.

Wengi walipendekeza maslahi ya waalimu yaboreshwe ili wale wanafunzi wanaofanya vizuri zaidi wapelekwe kwenye vitivo vya elimu ili wawe waalimu tofauti na sasa ambapo wanaoonekana kuwa na ufaulu wa chini ndio wanaopelekwa kwenye vitivo vya elimu. Akionyesha jinsi elimu yetu ilivyokuwa mbovu kwa sasa mbunge wa jimbo la Kigoma mjini ndugu Peter Serukamba alisema wakati wa mchango wake bungeni jana kuwa asilimia zaidi ya 60 ya wanafunzi wanaosoma shahada ya pili hapa nchini wanaandikiwa 'thesis' kwa maana ya kuwa hawana uwezo kabisa.

Niliposikia hivyo nikakumbuka madai ya watu wengi kwenye mitandao ya kijamii kuwa mheshimiwa mmoja mwenezi wa chama cha zamani amemaliza shahada yake ya pili mzumbe kwa kusaidiwa kuandikiwa dissertation yake.
 
aliowamaanisha siwajui ila kuhusu uheshimiwa inategemea na qualifications za chama, kama ni elimu ya kidato cha nne hata kufikaMzumbe ameovaqulify.
 
Niliposikia hivyo nikakumbuka madai ya watu wengi kwenye mitandao ya kijamii kuwa mheshimiwa mmoja mwenezi wa chama cha zamani amemaliza shahada yake ya pili mzumbe kwa kusaidiwa kuandikiwa dissertation yake.
BE STRYT DOUBLE K....SEMA NAPE NDYE TUNAJUA CV YAKE ALIFELI FORM 2,AKABADILI JINA AKAFELI TENA FORM FOUR AKARUKIA DPLOMA DN MASTERS MZUMBE AKASAIDIWA DISERTION
 
Mijadala ya makadirio ya bajeti ya wizara ya Elimu na mafunzo ya ufundi inaendelea kwa siku ya pili hii leo.

Wabunge wengi waliopata nafasi ya kuchangia kwenye bajeti hii wameona kuna haja ya tume kuundwa itakayoangalia mustabali wa elimu yetu kwa ujumla kwani kutokana na mfumo wa elimu tulionao kwa sasa ni dhahiri kuwa tunawandaa wataalam feki wa kisasi kijacho.

Wengi walipendekeza maslahi ya waalimu yaboreshwe ili wale wanafunzi wanaofanya vizuri zaidi wapelekwe kwenye vitivo vya elimu ili wawe waalimu tofauti na sasa ambapo wanaoonekana kuwa na ufaulu wa chini ndio wanaopelekwa kwenye vitivo vya elimu. Akionyesha jinsi elimu yetu ilivyokuwa mbovu kwa sasa mbunge wa jimbo la Kigoma mjini ndugu Peter Serukamba alisema wakati wa mchango wake bungeni jana kuwa asilimia zaidi ya 60 ya wanafunzi wanaosoma shahada ya pili hapa nchini wanaandikiwa 'thesis' kwa maana ya kuwa hawana uwezo kabisa.

Niliposikia hivyo nikakumbuka madai ya watu wengi kwenye mitandao ya kijamii kuwa mheshimiwa mmoja mwenezi wa chama cha zamani amemaliza shahada yake ya pili mzumbe kwa kusaidiwa kuandikiwa dissertation yake.

Alichokizungumza Serukamba ni kweli kabisa kwani hata mimi aliwahi kufuata mtu mmoja ambaye ni wakala wa kutafutia wanafunzi watu wa kuwaandikia dissertation kwa malipo ya laki 2. Nilimkatalia nikamwambia mimi ni maskini jeuri. kwa hiyo wapo watu wanaishi kwa kuwaandikia wenzao dissertation. Wanaoandikiwa wakishahitimu hawawezi kuandika barua ya kuomba kazi. Sasa hawa watashindanishwa na wenzao wa EAC? Hii ni hatari. Na bado tunaendelea kuwaongezea marks ili waonekane wamefaulu. Haya bhana.
 
Siamini kama ameropoka ni lazima ana uhakika. Kwa maana hiyo tuna wasomi wengi wa cheti sio wa taaluma
 
Back
Top Bottom