Serikari iboreshe stendi ya Makumbusho

MLUGURU

JF-Expert Member
Mar 30, 2012
2,836
3,539
Hii stand ya makumbusho imekuwa ni kiungo muhimu cha usafiri kuelekea sehemu mbalimbali za mji huu Dar es Salaam.

Lakini kinyume na umuhimu wake naona imesahauliwa kabisa kwani maendeleo ya miundombinu ndani ya jiji hili ni tofauti kabisa na miundombinu ndani ya stand hii muhimu.

Mashimo makubwa yaliyo ndani ya stand hii ni hatarishi kwa usalama wa magari ya wafanyabiashara mbalimbali ambao kwa sasa ndio walipakodi wakubwa katika serikali hii ya awamu ya tano.

Madereva wa mabasi makubwa aina ya Tata na eicher imekuwa mtihani mkubwa kwao kutoka na abiria salama bila kupata hitilafu yoyote katika magari hayo.

Leo nimekuwa shuhuda wa basi aina ya tata linalofanya safari zake Mbagala- Makumbusho likivunja sijui ni spring au kitu gani na hatimaye kushusha abiria wake.

Ombi kwa serikali hii ya sasa iangalie kwa jicho la tatu hii stand kuanzia waliosimamia ujenzi wa stand watuambie imekuwaje stand hata miaka 5 haijafika imechoka hivi?

Kifupi leo nimewaonea huruma sana wafanyakazi kwenye lile basi.
 
Kiukweli vituo vya daladala vingi ambavyo vimewekewa matofali madogomadogo hua havimalizi hata mwaka bila ku haribika sijui wawekaji hawashindilii vizuri au hua havina ubora kwenye sehemu hizo.
Ningekua naweza kuwasahauri wakanielewa bora hata zege angalau
 
Stendi ya Makumbusho ni mradi Kati ya mtu binafsi na Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam.

Bahati mbaya Mwenye stendi mungu alishamchukua mzee Maganga wa BOT. Lazima kimkataba kutakuwa na mapungufu ikiwemo ukarabati.
 
Halafu kungekuwa na mpaka wa wafanya biashara wanao jenga vibanda magari hayana pa kupaki mfn ya mbweni nafasi imejazwa na mabanda ya popcorn juisi ya miwa mishikaki mara viatu hata eleo la watembea kwa miguu au kusimama abiria hakuna
 
Kiukweli vituo vya daladala vingi ambavyo vimewekewa matofali madogomadogo hua havimalizi hata mwaka bila ku haribika sijui wawekaji hawashindilii vizuri au hua havina ubora kwenye sehemu hizo.
Ningekua naweza kuwasahauri wakanielewa bora hata zege angalau
Mkuu nadhani shida ni usimamizi mathubuti kipindi cha ujenzi....stand ya msamvu nayo ina vitofali lakini nakumbuka ilivyoanza kutumika vitofali vikaanza kudidimia mapema tu wahusika wakachukua hatua na sasa hali ni shwali kabisa.
 
Kiukweli vituo vya daladala vingi ambavyo vimewekewa matofali madogomadogo hua havimalizi hata mwaka bila ku haribika sijui wawekaji hawashindilii vizuri au hua havina ubora kwenye sehemu hizo.
Ningekua naweza kuwasahauri wakanielewa bora hata zege angalau
Zege si angalau mkuu,. Hiyo ndo kiwango bora zaidi kuliko hata rami na ni gharama sana kwa square metre moja ya mraba au kwa kilometre moja.
 
Cha ajabu ni kuwa barabara zinazozunguka stand ni imara na mathubuti na za kupendeza kweli.Ukarabati wa stand ndio umekuwa ishu kabisa.
Stand ya makumbusho ni mradi Kati ya mtu binafsi na Halmashauri ya jiji la dsm.

Bahati mbaya Mwenye stendi mungu alishamchukua mzee Maganga wa BOT. Lazima kimkataba kutakuwa na mapungufu ikiwemo ukarabati.
 
Aisee mkandarasi aliyeweka pavement pale makumbusho ni mtu wa hovyo sana sijui kwann manispaa hawaweki zege pale hata lile jengo ukiingia ndani halijamalizika pale wahusila walikula pesa kabisa.
 
Back
Top Bottom