Albert Msando
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 1,019
- 171
Wasalaam,
Kumekuwa na wimbi la uundwaji wa serikali za Umoja wa Kitaifa kwa nchi za Afrika siku za karibuni. Serikali ya Umoja wa Kitaifa siyo kitu kigeni ila kilicho kigeni ni sababu mpya ya uundwaji wake. Sababu kuu iliyokuwa inasababisha uundwaji huo inapatikana katika maneno yafuatayo;
.....Here the opinion has taken root that in times of crisis - political, military or economic - we must unite under such a government. The argument is that in times like these, there is no room for petty political differences and we must all make a common effort to overcome the causes of the crisis.......
"Tough opposition is vital to democracy" By Hillel Schocken.
Kwa maneno hayo ni kwamba Serikali ya Umoja wa Kitaifa muundo wake unazaliwa wakati wa crisis it be political, military or economic.
Kwa sasa hivi Serikali hizo zinaundwa wakati wa crisis za uchaguzi zinazosababishwa na walioshindwa kupinga matokeo au waliokuwa madarakani (Kenya na Zanzibar) kukataa kuachia madaraka (angalia Zimbabwe na mawazo ya wachache kuhusu suluhu ya Ivory Coast). Pia vilevile uundwaji wake unaweza ukapangwa way before the crisis kama ilivyo Zanzibar. Kwa Zanzibar makubaliano yalifikiwa wakati ambao crisis 'ilishamalizika' kwa lengo la kuzuia machafuko baada ya uchaguzi wa 2010!! Mtu utajiuliza, je uchaguzi ule ulikuwa na maana gani? Lengo lilikuwa ni kushiriki kukamilisha utaratibu au ni kutoa nafasi ya demokrasia ya kweli? Hilo naaliachia hapo kuzua mjadala endelevu.
Matunda ya muundo huo sio lazima yawe umoja wa kitaifa (angalia Kenya). Hillel Schocken anasema "one must distinguish between the concept of "national unity" and a national unity government. A national unity government is no guarantee of national unity"
Leo asubuhi nimesikia Tunisia wataunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa ndipo nikajiuliza, je CHADEMA na wao wanataka Serikali ya Umoja wa Kitaifa? Ndio kilichochochea uamuzi wa kuandamana Arusha ili kucreate crisis?
Je ni faida zipi zipatikanazo kwa uundwaji wa Serikali za Umoja wa Kitaifa? Serikali hizo ni kwa manufaa ya viongozi au wananchi? Ni yapi wananchi wa Zimbabwe, Kenya, Zanzibar n.k wanaweza kufurahia kwamba yameletwa na Serikali za Umoja wa Kitaifa?
Je ni mfumo ambao Tanganyika tunaweza kuufuata hivyo CHADEMA waanzishe vurugu CCM wakatae kuachia madaraka. Wengine wachochee udini na ukabila ili tuvurugane mwishoni tuunde Serikali ya Umoja wa Kitaifa???
Nawasilisha!!:sing:
Kumekuwa na wimbi la uundwaji wa serikali za Umoja wa Kitaifa kwa nchi za Afrika siku za karibuni. Serikali ya Umoja wa Kitaifa siyo kitu kigeni ila kilicho kigeni ni sababu mpya ya uundwaji wake. Sababu kuu iliyokuwa inasababisha uundwaji huo inapatikana katika maneno yafuatayo;
.....Here the opinion has taken root that in times of crisis - political, military or economic - we must unite under such a government. The argument is that in times like these, there is no room for petty political differences and we must all make a common effort to overcome the causes of the crisis.......
"Tough opposition is vital to democracy" By Hillel Schocken.
Kwa maneno hayo ni kwamba Serikali ya Umoja wa Kitaifa muundo wake unazaliwa wakati wa crisis it be political, military or economic.
Kwa sasa hivi Serikali hizo zinaundwa wakati wa crisis za uchaguzi zinazosababishwa na walioshindwa kupinga matokeo au waliokuwa madarakani (Kenya na Zanzibar) kukataa kuachia madaraka (angalia Zimbabwe na mawazo ya wachache kuhusu suluhu ya Ivory Coast). Pia vilevile uundwaji wake unaweza ukapangwa way before the crisis kama ilivyo Zanzibar. Kwa Zanzibar makubaliano yalifikiwa wakati ambao crisis 'ilishamalizika' kwa lengo la kuzuia machafuko baada ya uchaguzi wa 2010!! Mtu utajiuliza, je uchaguzi ule ulikuwa na maana gani? Lengo lilikuwa ni kushiriki kukamilisha utaratibu au ni kutoa nafasi ya demokrasia ya kweli? Hilo naaliachia hapo kuzua mjadala endelevu.
Matunda ya muundo huo sio lazima yawe umoja wa kitaifa (angalia Kenya). Hillel Schocken anasema "one must distinguish between the concept of "national unity" and a national unity government. A national unity government is no guarantee of national unity"
Leo asubuhi nimesikia Tunisia wataunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa ndipo nikajiuliza, je CHADEMA na wao wanataka Serikali ya Umoja wa Kitaifa? Ndio kilichochochea uamuzi wa kuandamana Arusha ili kucreate crisis?
Je ni faida zipi zipatikanazo kwa uundwaji wa Serikali za Umoja wa Kitaifa? Serikali hizo ni kwa manufaa ya viongozi au wananchi? Ni yapi wananchi wa Zimbabwe, Kenya, Zanzibar n.k wanaweza kufurahia kwamba yameletwa na Serikali za Umoja wa Kitaifa?
Je ni mfumo ambao Tanganyika tunaweza kuufuata hivyo CHADEMA waanzishe vurugu CCM wakatae kuachia madaraka. Wengine wachochee udini na ukabila ili tuvurugane mwishoni tuunde Serikali ya Umoja wa Kitaifa???
Nawasilisha!!:sing: