Serikali yatikiswa

Nadhani hii njia aliyoitumia JK ni ya busara sana ili kuweza kuondoa sintofahamu kwani inaelekea dhahiri wasaidizi wake wana hulka ya kufanya mambo kwa papara bila kujua adhari zake. Kauli ya wasira ilinisikitisha sana ,siku zote amekuwa kiongozi asiyetumia busara na kutoitambua nafasi yake katika kulitumikia Taifa. Ngoja tusubiri tuone nini kitajiri
 
Reactions: BAK
Mzee msolwa, makundi kwa sasa tusiyape nafasi.Kumbuka muungano wao ndiyo uliofungua njia ya majadiliano ya mezani kati yao na serikali.Acha waende kama muungano wa vyama vya upinzani na si kama chama cha upinzani ukinzani wa chama kimojakimoja ni rahisi kufutika kuliko wa muungano wa vyama vya upinzani.

 
Reactions: BAK
War-hassira bichwa chini
Chicarwe haya,anzisha ww mgogoro na bunge
 
mkuu, wananchi unaowasema ni hawa machadema ambao wanatafuna fedha za ruzuku kila kukicha na kutotoa mapato na matumizi ya fedha tunazowachangisha?

....OUT OF POINT!!. I think your brain is suffering from disease called "Wassirensis''.
The patient with this disease talks nonsense, use a lot of energy to convince people on small issues, his brain can't accept new things and believe that xmple of person with the same disease is Steven Wassira.

Pole sana, wahi hospital kabla haijawa too late!
 
Ng'wamapalala siku zote siasa ni dynamic kwahiyo usije ukadhani kwamba hawa viongozi wa vyama vya Chadema, Cuf na Nccr hawajui usanii wa Kikwete na ccm yake. Wanaujua sana lakini na wao wanajua namna ya ku deal na msanii na aina yoyote ya usanii.
Mwita Maranya , Hakuna sehemu ambayo nimesema siasa hazibadiliki. Makosa ya kisiasa yanayofanyika siyo kwa sababu siasa hazibadiliki. Moja ya makosa ya kisiasa ni pale kiongozi anaposubiri siasa zimubadilishe (out of control).

Kama waswahili wasemavyo, kutenda kosa siyo kosa bali kurudia kosa. Hiki ndicho kinachotokea kwa sasa kwa wanasiasa wa vyama vya upinzani kwenye mchakato wa katiba mpya ambapo wanasubiri Rais Kikwete na CCM yake iwabadilishe badala ya kuibadilisha.

Kwa sasa Ratiba za kisiasa zimekuwa 'pending' au go haywire kwa sababu mwenye maamuzi ni Rais Kikwete na CCM yake.
Hivi unafahamu kama CCM wako na furaha sana kuhusiana na mchakato kwenda kwa kuchechemea na hasa ikichukuliwa kuwa wanapenda 'kumuongezea' Rais Kikwete muda kisheria pamoja na kwamba wanakanusha kutokana kutokukamilika katiba mpya na pia uchaguzi wa Madiwani taifa kufanyika chini ya katiba ya 1977 "inayoipa" CCM ushindi sunami.

Kuchechemea kwa mchakato kumeifanya hata CHADEMA kushindwa kutekeleza sera yake ya majimbo Zanzibar kwa sababu haifahamu matokeo ya mchakato wa katiba yatakuwaje(serikali mbili au tatu).

Wakati CHADEMA mambo yao yamesimama au yanachechemea huku wakikabiliwa na chaguzi kuu mbili 2014, huku uchaguzi mkuu wa ndani ya chama ukiwa political hot potato. CCM wao wanajiandaa na chaguzi kuu moja huku wakizidi ku-consolidate more political and economic power.

Watu kama mimi ninaangalia kwa pembeni jinsi viongozi wa vyama vya upinzani wakikosa mwerekeo na nguzo imara katika political case yao kuhusiana na mchakato wa katiba huku Rais Kikwete na CCM yake waki-dictate terms and condition na pia mwerekeo wa upatikanaji wa katiba mpya.

Ni viongozi hawa hawa walisema hawaweI tena kwenda kuonana na Rais kuhusiana na swala la katiba mpya kwa sababu ni "msanii" na katika masaa 24, walichokisema kikawa ni useless baada ya hotuba ya Rais.

Yangu macho na masikio.
 
Kiukweli rais kikwete anapaswa kuwa makini sana kwa sasa,achague kati ya chama au taifa.
s
Hapo hakuna suala la Chama au Taifa ila kilichopo hapo ni kikundi cha manyang'au wachache wanatokata kutumbukiza nchi kwenye matatizo wakijua wazi kuwa wao wana mahali pa kukimbilia. Hebu fikiri mtu anateuliwa na kupewa mkate wake wa kila siku anafika mahali anasema rais hana muda wa kukutana na wapinzani waliokuwa na hamu ya kwenda kunywa juisi Ikulu kwa maneno mengine ni kuwa milango ya Ikulu imefungwa! Huyo anayesema hivyo siyo Rais wa nchi ni mteule tu wa Rais, anajipachika madaraka makubwa hivyo ya kusema Rais hana muda! Rais hana muda! Rais hana muda wa kushughulikia jambo linalopasua nchi! Rais hana muda wa kukutana na kushughulikia kero za wananchi! Kweli aliyesema sentensi hiyo anapaswa kujiuzulu haraka kwa kujivika madaraka ya kumsemea Rais tena vibaya.

Wako manyang'au wachache ndani ya CCM ambao ukiangali utaona wazi wana mpango wa kuhujumu mchakato wa Katiba mpya. Wengine wamekemewa waziwazi na Mwenyekiti wa Tume ya Katiba na tumewasikia. Sasa hao ndio wanaomshinikiza Rais wa nchi kwa kigezo tu kuwa ni mwenyekiti wa CCM. Tukiangalia maslahi mapana ya Taifa ambayo mimi ninaamini wako watu ndani ya CCM wenye uwezo wa kuona maslahi hayo mapana ya Taifa wakiongozwa na Mwenyekiti wao hao ni wakati wao kujibainisha na kumtia nguvu Mwenyekiti wao ili afanye lile ambalo litajali maslahi ya Taifa hili kwa miaka zaidi ya hamsini ijayo. Manyang'au hawa wanaobweka bila kuwaza wala kupewa ruhusua ya kubweka wakipewa nafasi watalichanachana hili taifa. Na hilo likitokea wao watakua wa kwanza kwenda ughaibuni kwa kuwa tayari wamejiwekea mazingira huko.
 
siasa za tanzania unapaswa kuzifatilia kwa styl hii,hazina maana wala heshima
 
Nakuheshimu hivyo nisingependa kujibu hili bandiko lako kisha hitimisho lako likawa, nimekuvunjia heshima yako. Uwe na mchana mwema.

[B BAK bado sana kwa upinzani kupewa nchi;
bado hamjakomaa kuweza kuongoza nchi BAK[/B]
 
Kikwete hana pa kujificha ni ama afanye kazi ya wananchi au awafurahishe watu wake akina ndio sasa amezingirwa na saikolojia ya kumkoroga watu wamemtangalia hatua mia mbele yeye anadhani ujanja ujanja utamsaidia , ni bora akatulia na kuanza kuhakikisha wananchi tunapata katiba nzuri ya kutmika miaka mingi ijayo badala ya kujitegesha kusikilizia upepo halafu ndio atoe maamuzi manake sikio moja liko kwa mACCM aliowatuma kukanusha na kutoa kashifa linguine liko kwa wananchi wanaotaka akome kuendesha mchakato wa katiba kwa njia ya usanii
 
Impact ya Rais kukutana na viongozi wa upinzani itakuwa kubwa kwa upande wa CCM sababu walijiapiza hakuna nafasi ya kukutana na Rais au kuwa na majadiliano tena.Kunaweza kukawa na kutokuelewana kati ya pande mbili za wahafidhina ndani ya CCM na wale wenye mlengo wa kati.Imani kwa mwenyekiti wao na viongozi wa serikali itashuka pia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…