Serikali yaruhusu matambiko hifadhi ya Katavi

Serikali yaruhusu matambiko hifadhi ya Katavi

Inside10

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2011
Posts
33,703
Reaction score
40,335
SERIKALI mkoani Katavi kuanzia sasa imeruhusu wazee wa jadi na machifu mkoani humo kufanya matambiko katika Hifadhi ya Taifa ya Katavi iliyopo wilayani Mlele ili wanyama waishio humo wasiweze kuuawa na majangili kama ilivyo katika hifadhi nyingine za taifa nchini.

Hayo yalibainishwa jana na Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Dk Rajab Rutengwe wakati akifungua mkutano wa wadau uliokuwa ukijadili kwa kina Mpango Kamambe wa Mji wa Mpanda na Mwongozo wa Ukuaji wa Mji huo 2014-34 uliofanyika mjini hapa.

Aliongeza kuwa wazee hao wa jadi pamoja na baadhi ya machifu wameruhusiwa kufanya matambiko katika Hifadhi ya Taifa ya Katavi kila mwaka ili wanyama waliomo humo waweze kuzaliana kwa wingi, lakini pia kutouawa kiholela na majingili kama ilivyo katika Hifadhi kadhaa za taifa nchini.

Baadhi ya wakazi wa kijiji cha Sitalike kilichopo karibu na hifadhi hiyo ya Katavi wakizungumza kwa masharti ya majina yao kutoandikwa gazetini, wamekiri kuwa kutokana na kutofanyika kwa matambiko ya jadi majingili sugu wamekuwa wakiua kiholela wanyama wakiwemo nyati,tembo na twiga.

source: habarileo

My take: wanajf ni kweli tambiko litazuia ujangili!?
 
Kabla ya dini hizi tulizoletewa na Wazungu na Waarabu, sisi Waafrika tulikuwa na dini zetu. Tulitambika na kutoa sadaka. Mimi nimeshiriki kwenye matambiko katika msitu wetu wa Muhunda. Matambiko yanasaidia sana, maana yote yanalengwa kumwomba Mungu asiyeonekana. Walipokuja hawa wenzetu na dini za 'kistaarabu' wakayafanya matambiko yetu eti ni dhambi na ni utii kwa shetani. Tumeingia mkenge kuitupa asili yetu, na sasa tunaona mabalaa mengi. Naipongeza Serikali kwa kuwaruhusu wananchi wa Katavi kuendelea na matambiko ndani ya Katavi. Nami naanza mipango ili yale matambiko ndani ya Muhunda yaweze kufufuliwa.
 
huu ni mwanzo mzuri kwenye jitihada za kujitambua na kufanya maendeleo kwa ushiriki wa watu wetu katika jadi zetu wenyewe; jadi ambazo kwa kweli ni nzuri sana.... nimeipenda sana hii ....

CC: Remote,
Manyerere Jackton
 
Kabla ya dini hizi tulizoletewa na Wazungu na Waarabu, sisi Waafrika tulikuwa na dini zetu. Tulitambika na kutoa sadaka. Mimi nimeshiriki kwenye matambiko katika msitu wetu wa Muhunda. Matambiko yanasaidia sana, maana yote yanalengwa kumwomba Mungu asiyeonekana. Walipokuja hawa wenzetu na dini za 'kistaarabu' wakayafanya matambiko yetu eti ni dhambi na ni utii kwa shetani. Tumeingia mkenge kuitupa asili yetu, na sasa tunaona mabalaa mengi. Naipongeza Serikali kwa kuwaruhusu wananchi wa Katavi kuendelea na matambiko ndani ya Katavi. Nami naanza mipango ili yale matambiko ndani ya Muhunda yaweze kufufuliwa.

kwa dunia ya sasa yenye sayansi na teknolojia unahisi matambiko yatasaidia kuboresha ulinzi. hivyo basi majangili yatashindwa kuendelea kuua wanyama!???
 
kwa dunia ya sasa yenye sayansi na teknolojia unahisi matambiko yatasaidia kuboresha ulinzi. hivyo basi majangili yatashindwa kuendelea kuua wanyama!???[/QUOTE


mkuu,siyo hata enzi za mababu kusema matambiko yanasaidia ila nikujenga imani na kuendeleza mila,hata hapo nyasa samaki wamekuwa wanaelea wakiwa wamekufa wazee wakiomba kufanya tambiko mi sitaona sababu ya kuwanyimwa kwakuwa kila mtu ana haki ya kufanya hvyo asipo vunja sheria ya nchi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom