Serikali ya Rais Magufuli na hesabu kichaa za fedha

Orketeemi

JF-Expert Member
Feb 12, 2013
4,315
10,017
Wanabodi,

Huu ni utafiti mdogo nilioufanya katika mwenendo wa fedha ndani ya serikali ya Rais JPM.

Ndani ya kipindi cha miaka mitatu ya mwisho, serikali ya Rais Kikwete iliajiri takribani waalimu elfu 31 kwa kila mwaka ambapo ndani ya miaka mitatu waalimu zaidi ya elfu 80 waliajiriwa.

Katika kipindi cha miaka mitatu ya kwanza ya utawala wa Rais Magufuli serikali imezibana ajira za ualimu na kumekuwa na upungufu wa takribani waalimu 40 au zaidi ukilinganisha na wale walioajiriwa katika miaka mitatu ya mwisho ya utawala wa Kikwete.

Kwa average mwalimu mmoja analipwa mshahara wa Tsh 500,000 kwa mwezi na hivyo kufanya alipwe 6,000,000 kwa mwaka.

Walimu elfu 40 ambao ajira zimefutwa ina maana serikali imeokoa takribani Tsh bilioni 720 za mishahara ambayo ilipaswa kutumika kulipa waalimu hao elfu 40 ndani ya miaka mitatu.

Hilo ni eneo moja tu la ubanaji wa matumizi.

Serikali inajitapa kujenga hospitali za wilaya 67 nchi nzima. Ambapo ukipiga hesabu ni hospitali moja imegharimu bilion 1.5 hivyo hospitali zote zimegharimu takriban billion 100 na milion 500 za Kitanzania.

Vilevile, serikali inajitapa kujenga vituo vya afya 400 nchi nzima. Wastani wa gharama za ujenzi wa kituo cha afya ni tsh milion 600 ambapo kwa vituo vyote serikali imetumia zaidi ya Tsh bilioni 240.

Ukijumlisha gharama hizo utakuta serikali imetumia si zaidi ya billion 350 katika ujenzi wa vituo vya afya na hospitali za wilaya nchi nzima.

Ninachotaka kusema ni kwamba Serikali hii ukiichunguza kwa makini ni serikali ya kifisadi maana hizo zote zilizotumika katika ujenzi huo hazizidi hata nusu ya pesa zilizookolewa kwenye eneo moja tu la mishahara ya waalimu ambao wangeajiriwa.

Zipo sehemu nyingi fedha zimeokolewa hivyo kuna walakini mkubwa katika matumizi ya fedha za umma kipindi hiki cha utawala wa Rais Magufuli.

Kuna fedha lukuki zimekopwa ambazo ni tsh trilion kadh, kuna fedha kutoka kwenye makusanyo ya kodi sekta binafsi, kuna fedha kutoka kwa wahisani n.k

mvuv
 
Umejiuliza na hii miradi ya reli ya 'standard gauge', barabara hii ya Morogoro, flyover ya Ubungo, Bwawa la 'Stieglers Gorge' n.k, bila kusahau elimu bure kwa watoto mpaka kidato cha nne zinatumika fedha gani?

Huenda ndipo zilipo unazozitilia shaka maana vitu hivi vyote vinafanyika kwa pamoja usisahau kujumlisha na manunuzi ya ndege pia.

Mi naona mnyonge mnyongeni haki yake mpeni bora ya hivi kuliko watu kuiba pesa na kwenda kuzificha nke ya nchi.
 
Bado hujapigia hesabu na yale maburungutu ya milioni tano tano na kumi kumi yanayotolewa kwa makundi mbalimbali wakati wa zile ziara zetu za kiserikali, zinazobeba sura ya kisiasa.
 
Umejiuliza na hii miradi ya reli ya 'standard gauge', barabara hii ya morogoro,flyover ya Ubungo, Bwawa la 'Stieglers gorge' n.k n.k bila kusahau elimu bure kwa watoto mpk kidato cha nne zinatumika fedha gani?

Huenda ndipo zilipo unazozitilia shaka maana vitu hivi vyote vinafanyika kwa pamoja usisahau kujumlisha na manunuzi ya ndege pia.

Mi naona mnyonge mnyongeni haki yake mpeni bora ya hivi kuliko watu kuiba pesa na kwenda kuzificha nke ya nchi.

Una uhakika gani kama watawala wa utawala huu hawaibi fedha kwenda kuficha nje ya nchi? Je, unajua deni la taifa limeongezeka kwa kiwango gani ndani ya awamu hii?

Hapa ndiyo ninajua kwani awamu hii imeamua kubana vyombo vya habari, wapinzani kuongea na sheria kandamizi, lengo ni kuhakikisha wananchi hawaoni nje ya box.
 
Bado hujapigia hesabu na yale maburungutu ya milioni tano tano na kumi kumi yanayotolewa kwa makundi mbalimbali wakati wa zile ziara zetu za kiserikali, zinazobeba sura ya kisiasa.
Huwa nashangaa mkuu, Mzee sijui huwa anabeba kiasi gani akiwa anaondoka hapa Dar na accounting ya hizo pesa inafanyikaje yan zikibaki anazirudisha au ni lazima maburungutu yaishe yote njiani?
 
Fedha kuibwa zinaibwa tuu , cha msingi ni kupambana kuziba mianya ya uibaji ambayo haiwez kuisha kamwe , Jambo la maana ni kufanya kinachowezekana , matumizi ya JPM yanaonekana kuliko ya maraisi wengine waliopita,....

Kwenye matumizi ya pesa Ni kweli JPM anakiuka vifungu vingi vya katiba , kwangu min yupo Sawa cse vifungu vingi vinatoa mianya ya upigaji na ni vigumu zaidi kudhibiti, na pia vinasababisha uchelewaji mkubwa wa utekelezaji wa miradi...
 
Kwani akifanya hayo na kuruhusu ukaguzi kuna ishu gani?
Fedha kuibwa zinaibwa tuu , cha msingi ni kupambana kuziba mianya ya uibaji ambayo haiwez kuisha kamwe , Jambo la maana ni kufanya kinachowezekana , matumizi ya JPM yanaonekana kuliko ya maraisi wengine waliopita,....

Kwenye matumizi ya pesa Ni kweli JPM anakiuka vifungu vingi vya katiba , kwangu min yupo Sawa cse vifungu vingi vinatoa mianya ya upigaji na ni vigumu zaidi kudhibiti, na pia vinasababisha uchelewaji mkubwa wa utekelezaji wa miradi...
 
Kuna watu wana PHD Ya unafiki

Mazuri ya JK Kama hayo ya kuajiri wahitimu wengi yalikuwa ni kama hayaonekani. Leo hii kila mtu anasifia hadi wapinzani kama Sugu na Msigwa eti wanamsifia mtawala
 
HABARI,
Ila hapo walimu so ndio wengi wao walikuwa na vyeti feki,Na Haya kipindi hicho cha JK hamkukosa LA kulaumu sasa sijui mnataka mletewe pesa milangoni kwenu.

LUMUMBA
 
HABARI,
Ila hapo walimu so ndio wengi wao walikuwa na vyeti feki,Na Haya kipindi hicho cha JK hamkukosa LA kulaumu sasa sijui mnataka mletewe pesa milangoni kwenu.

LUMUMBA

Elewa mada , toa mchango wako kuhusu mada.
 
Umejiuliza na hii miradi ya reli ya 'standard gauge', barabara hii ya morogoro,flyover ya Ubungo, Bwawa la 'Stieglers gorge' n.k n.k bila kusahau elimu bure kwa watoto mpk kidato cha nne zinatumika fedha gani?

Huenda ndipo zilipo unazozitilia shaka maana vitu hivi vyote vinafanyika kwa pamoja usisahau kujumlisha na manunuzi ya ndege pia.

Mi naona mnyonge mnyongeni haki yake mpeni bora ya hivi kuliko watu kuiba pesa na kwenda kuzificha nke ya nchi.

JK alijenga zaidi ya km 2000 za Barbara

JK alijenga UDOM ambaye hata reli yenu mnayojenga haifikii hata robo tatu ya garama ya ujenzi wa UDOM


JK alitoa ajira seckta zote

JK alianzisha mikoa mipya 5 na wilaya za kutosha

JK alitengeneza miundo mbinu ya gesi ya mtwara

Jk alitengeneza miradi mbalimbal ya umeme. Maelfu ya vijiji vilipata umeme

JK alijenga uwanja wa songwe

Jk alijenga shule za kata

Jk alitengeneza maelfu ya ajira

JK alileta hospitali za Mloganzila, Benjamin Mkapa, UDOM n.k

Uwiiii msimfananishe JK na vitu vya kijinga
 
Umejiuliza na hii miradi ya reli ya 'standard gauge', barabara hii ya morogoro,flyover ya Ubungo, Bwawa la 'Stieglers gorge' n.k n.k bila kusahau elimu bure kwa watoto mpk kidato cha nne zinatumika fedha gani?

Huenda ndipo zilipo unazozitilia shaka maana vitu hivi vyote vinafanyika kwa pamoja usisahau kujumlisha na manunuzi ya ndege pia.

Mi naona mnyonge mnyongeni haki yake mpeni bora ya hivi kuliko watu kuiba pesa na kwenda kuzificha nke ya nchi.
Hapo mdau hajagusia kwenye deni la taifa ambalo kwa miaka hii minne tu, ni balaa!! Yaani kama haya anayoyafanya angekuwa ameweza kuyafanya na mengi ya watangulizi wake, yangekuwa maajabu, mfano angeweza kuongeza kuajiri kila mwaka, kama JK, angeweza kuongeza mishahara ya watumishi, kila mwaka, akalipa madeni hasa ya wakandarasi wa ndani, thamani ya shilingi yetu ikawa vizuri, angalau maisha ya wananchi nayo yakawa na unafuu kidogo, hapo kweli. Lakini ukiangalia ni kama yale yale tu.
 
mvuv,

Kuna kitu sijakielewa kwenye utawala huu mpaka sasa hivi.

Vitu vingine karibu vyote tunatajiwa kwa majina na sehemu zilipo, lakini cha ajabu tunaambiwa tu kuna vituo vya Afya 352 lakin sijaona vimetajwa kwa majina popote, pia tunaambiwa Hospitali za Wilaya basi wangetaja hata 30 zipo kwenye wilaya zipi, isije kuwa kama Daraja la Kigamboni limejengwa enzi za Kikwete ila tunatangaziwa ni la awamu ya 5.

Cha ajabu kuliko vyote, kuna wahudumu wa afya wengi waliondolewa kwa vyeti feki, sasa je hizi hospitali 67 na vituo vya afya 352 ni akina nani wanafanya kazi?
 
Kuna kitu sijakielewa kwenye utawala huu mpaka sasa hivi.

Vitu vingine karibu vyote tunatajiwa kwa majina na sehemu zilipo, lakin cha ajabu tunaambiwa tu kuna vituo vya Afya 352 lakin sijaona vimetajwa kwa majina popote, pia tunaambiwa Hospitali za Wilaya basi wangetaja hata 30 zipo kwenye wilaya zipi, isije kuwa kama Daraja la Kigamboni limejengwa enzi za Kikwete ila tunatangaziwa ni la awamu ya 5.

Cha ajabu kuliko vyote, kuna wahudumu wa afya wengi waliondolewa kwa vyeti feki, sasa je hizi hospitali 67 na vituo vya afya 352 ni akina nani wanafanya kazi?

Viwanda 5,000
 
Kuna kitu sijakielewa kwenye utawala huu mpaka sasa hivi.

Vitu vingine karibu vyote tunatajiwa kwa majina na sehemu zilipo, lakin cha ajabu tunaambiwa tu kuna vituo vya Afya 352 lakin sijaona vimetajwa kwa majina popote, pia tunaambiwa Hospitali za Wilaya basi wangetaja hata 30 zipo kwenye wilaya zipi, isije kuwa kama Daraja la Kigamboni limejengwa enzi za Kikwete ila tunatangaziwa ni la awamu ya 5.

Cha ajabu kuliko vyote, kuna wahudumu wa afya wengi waliondolewa kwa vyeti feki, sasa je hizi hospitali 67 na vituo vya afya 352 ni akina nani wanafanya kazi?

Hufahamu lolote kwenye sekta ya afya na bora umekiri hujaelewa. Vituo vya afya na hospitali za wilaya zimejengwa kwenye wilaya zilizokuwa hazina hospitali ya wilaya. Mfano hai ni wilaya ya Kilolo Iringa wanamalizia na kuhusu kuajiri sekta ya afya wanaajiri manesi, doctor, wauguzi, watu wa pharmacy n.k Tena ajira zinatoka ukimaliza Chuo tu. Mfano hai ni mimi ni pharmacist nipo Iringa hospitali ya mkoa.
 
Back
Top Bottom