Serikali ya JK kuwahadaa WaTZ kwa Harakati za Vita na Malawi Uchaguzi Mkuu 2015

kanga

JF-Expert Member
Jan 13, 2011
1,025
494
Kwa wiki sasa viongozi waandamizi wa Serikali ya Tanzania wamekuwa wakitoa matamko ya kuchochea vita dhidi ya Malawi juu ya mpaka wa ziwa Nyasa/Malawi.Mbaya zaidi matamko hayo yamekuwa yakitolewa katika sehemu nyeti ya bunge la Jamhuri ya Tanzania.Mawaziri wa Serikali ya Jk Membe na Sita wametoa kauli za wazi za kuchochea vita na wakati huo huo Mwenyekiti wa kamati ya mambo ya nje,ulinzi na usalama Mh.Lowasa naye akitoa kauli ya jeuri ya kuchochea vita.
Katika haya mambo makuu yafuatayo ni dalili muhimu ambazo serikali ya JK inataka kutumia kama mwavuli wa kutowajibika kwa mambo muhimu ambayo yameikamata serikali kwa muda mrefu kama ifuatavyo.
1.Mfumuko mkubwa wa bei kwa zaidi ya 18%
2.Mahitaji ya nyongeza ya mishahara kwa watumishi wa umma
3.Ufisadi katika ofisi za Serikali.
4.Utawala mbovu wa jeshi la polisi nchini.
5.Kutotekelezwa kwa ahadi za Raisi za mwaka 2010.
6.Mgogoro ndani ya ccm na makudni yake.
7.Uongozi dhaifu wa JK
8...............................ETC.
Watanzania tuwe makini dalili za kushindwa kwa ccm na JK ndio sababu kubwa ambayo sasa inataka kupata platform la kuibukia kwenye mgogoro wa mpaka na MALAWI.Kwa ufupi kabisa wataalamu wa mambo ya migogoro ya kimataifa juu ya mipaka wanaeleza wazi kuwa mgogoro huu unaweza kusuluishwa na kamati ndogo kabisa chini hata kamati ya ujirani mwema kati ya Malawi na Tanzania bila sababbu za kuhamaki kwa serikali kuu kutoa kauli za jazbana kuchochea vita.
Ni wazi ccm na JK dhaifu wanatafuta sehemu ya kutorokea katika uchaguzi wa mwaka 2015 na kwamba sisi kama wananchi makini TUSIKUBALI KUFANYWA WAJINGA NA WATUMWA KWA JAMBO ILI KWA KISINGIZIO CHA KULINDA MIPAKA YA NCHI NA KAMA JK ATAANZISHA VITA HII YA KIJINGA APELEKE FAMILIA YAKE NA NDUGU ZAKE KUTOKA BAGAMOYO NA MSOGA AKISAIDIWA NA WANAMTANDAO WENZAKE SITA,LOWASA NA MEMBE.
 
Back
Top Bottom