Serikali Msaidieni Mwekezaji Asifunge Kiwanda

Serikali Msaidieni Mwekezaji Asifunge Kiwanda

mwanamichakato

JF-Expert Member
Joined
Mar 20, 2015
Posts
1,208
Reaction score
1,109
Ninapongeza kwa dhati juhudi kubwa za kukomboa wananchi toka katika lindi la umaskini,maladhi,ufukara,shida na tabu.Napongeza utendaji wa kasi wa serikali ya awamu ya tano katika kurejesha nidhamu ya juu/maadiri na uwajibikaji katika utumishi wa umma.Nina kila sababu ya kushiriki kuiunga Mkono serikali sikivu na yenye uzalendo wa kweli chini ya His Excellency JPM,PM {MKM}..

Kwa unyenyekevu mkubwa nawakirisha hili ili hekima itumike kuendelea kulijenga taifa letu kwa kuokoa ajira,mapato,na kuepuka kukimbiza baadhi ya wawekezaji ambao ni chachu kwa tulio wengi kuifinyanga Tanzania mpya ya viwanda vikubwa vya vyenye kukidhi mahitaji ya wananchi wetu katika nyanja mtambuka hivyo kuepuka uagizaji usio na tija ktk uchumi kama toothpick,karatasi,furniture,stapler pins,matairi,vipuri,nguo,n.k.

Kuna kampuni ya kimataifa {toka thailand yenye viwanda takribani 15 katika nchi mbalimbali Duniani} iliowekeza katika utengenezaji wa chakula cha kuku/mifugo takribani miaka 3 hapa nchini..Kiwanda cha kampuni hii kipo maeneo ya chang'ombe,jirani na kiwanda cha konyagi.Kiwanda hiki kimeajiri zaidi ya watanzania 50 wenye elimu ya juu na kati wakiwemo {Mechanical engineers,chemical engineers,Food engineers,etc etc},Kiwanda hiki ni mnunuaji mzuri wa nishati ya umeme;malighafi mbalimbali za kilimo {mafuta ya alizeti,mahindi,madawa,pembejeo,] hivyo kuchangia kwa namna moja ukuaji wa uchumi wetu,pato la taifa hata kwa kiwango kidogo.

Kiwanda hiki kimesimamisha na kufunga uzalishaji kwa zaidi ya miezi miwili sasa na kwa sasa wapo katika mchakato wa kuuza mitambo yao yenye thamani ya zaidi ya shilingi za kitanzania bilioni tatu {3} sababu kubwa ni kodi ya VAT {Value Added Tax} katika bidhaa zinazozalishwa..Kilio cha wawekezaji hawa ni soko kuwa dogo na linalobembelezwa kukua ili kukidhi mapana ya uwekezaji katika sekta ya ufugaji..VAT inafanya bidhaa kuwa na bei kubwa ukilinganisha na bidhaa zinazoagizwa toka katika mataifa yasiochaji VAT.

Kilimo ni uti wa mgongo wa taifa letu ,wakati huo huo ni ngumu sana kutenganisha kilimo na mifugo katika muktadha wa maendeleo ya taifa letu tukufu..Ufugaji umekuwa ukifanywa kwa miaka nenda rudi na kaya za kipato cha chini,kati na juu..Ufugaji wa kisasa umekuwa chachu ya wafugaji kukidhi soko la bidhaa za ufugaji kama maziwa,mayai,nyama,asali,n.k.

Nina amini kwa dhati kabisa serikali yetu italifuatilia hili,pata taarifa za kina na kulipatia ufumbuzi makini kwa manufaa mapana ya taifa letu sasa na baadae kwani Mh. Rais wetu na serikali ni wasikivu sana,wenye ufahamu mkubwa sana,wenye hekima sana,na busara nyingi.

Mungu Ibariki Afrika,Mungu Ibariki Tanzania bara na Tanzania Visiwani {Zanzibar}.

CC:Wizara Ya Kilimo na Mifugo
CC:Wizara ya Viwanda na Biashara
CC:TIC
 
Mh Rais alisema kuwa watu kama hawa wanapaswa wajiongeze na watumie akili za ziada....

Wanashindwaje kuendesha shughuli za uzalishaji kwa VAT ndogo kiasi hiki? Au wanataka kumlingia Rais kwa hako kakiwanda kao? Serikali imeongeza tozo ipi ijenge viwanda vingine, mbona mamlaka ya Bandari hailalamiki kwa ongezeko la tozo?


Wasiijaribu kabisa serikali ya Magufuli, kama hawataki warudi kwao Thailand, huenda wakawa marafiki wa Lowassa hawa.

Na kwanini walalamikie udogo wa soko la bidhaa zao.?
Rais alishatoa ushauri, kama umekosa soko la bidhaa zako yakupasa kujiongeza na kutumia akili zaidi... Wahakikishe wanapaki hizo bidhaa zao kwenye maBaiskeli wakauze kule Dodoma.

"Wasimjaribu na kumuudhi rais, yuko busy kuandaa Tanzania ya viwanda."
 
Duh hii inatisha, the same applies kwenye zile ICDs ambazo zilikua zimeajiri vijana wengi sana, walikua wanalipa kodi hawa vijana yaani PAYE, Mifuko ya hifadhi ya Jamii lakini pia pamoja na kwamba huenda mshahara yao ilikua midogo bado walikua wanasaidia Sana kuiweka fedha kwenye mzunguko! Achilia umeme unaolipiwa, kodi ya Ardhi na majengo, Mapato, etc!!

Tumekwisha
 
Hali si mbaya,
Wana wa Israel walipotoka Misri Mwenyezi Mungu aliwapitisha Jangwani {Kwa miaka takribani 40} kwa makusudi maalumu kabla ya kufikia nchi ya ahadi iliojaa maziwa na asali...

Tupo katika mapito kuelekea neema kubwa ,Nchi yetu ni tajiri sana ina kila aina ya vinono,vitamu,ving'aavyo,madini na vito vya thamani sana..

Ushupavu/ujasiri wa viongozi wetu awamu kutufikisha tuendako/ kufika tuendako upo katika hali kubwa,nia kubwa,kasi kubwa na dhamili ya wazi..tuwasaidie,tuliombee taifa,tushiriki kuwa chachu ya maendeleo tunayoyaota..

Viva Tanzania Mpya
 
Umeandika vibaya sana mwanzo wa uzi wako.
Huwezi kujikomba kiasi hicho kwa watu wasiojiombea wao kwa mungu bali wanategemea kuombewa.

Ombi langu kwao:-
NAO WAKATWE KODI.
Kikevi kitumie mshahara wake kutunzia my wife wake,
Nao pension mpaka miaka inayoainishwa na mifuko ya jamii.
Kwa uchache nimeyaandika.
 
Ninapongeza kwa dhati juhudi kubwa za kukomboa wananchi toka katika lindi la umaskini,maladhi,ufukara,shida na tabu.Napongeza utendaji wa kasi wa serikali ya awamu ya tano katika kurejesha nidhamu ya juu/maadiri na uwajibikaji katika utumishi wa umma.Nina kila sababu ya kushiriki kuiunga Mkono serikali sikivu na yenye uzalendo wa kweli chini ya His Excellency JPM,PM {MKM}..

Kwa unyenyekevu mkubwa nawakirisha hili ili hekima itumike kuendelea kulijenga taifa letu kwa kuokoa ajira,mapato,na kuepuka kukimbiza baadhi ya wawekezaji ambao ni chachu kwa tulio wengi kuifinyanga Tanzania mpya ya viwanda vikubwa vya vyenye kukidhi mahitaji ya wananchi wetu katika nyanja mtambuka hivyo kuepuka uagizaji usio na tija ktk uchumi kama toothpick,karatasi,furniture,stapler pins,matairi,vipuri,nguo,n.k.

Kuna kampuni ya kimataifa {toka thailand yenye viwanda takribani 15 katika nchi mbalimbali Duniani} iliowekeza katika utengenezaji wa chakula cha kuku/mifugo takribani miaka 3 hapa nchini..Kiwanda cha kampuni hii kipo maeneo ya chang'ombe,jirani na kiwanda cha konyagi.Kiwanda hiki kimeajiri zaidi ya watanzania 50 wenye elimu ya juu na kati wakiwemo {Mechanical engineers,chemical engineers,Food engineers,etc etc},Kiwanda hiki ni mnunuaji mzuri wa nishati ya umeme;malighafi mbalimbali za kilimo {mafuta ya alizeti,mahindi,madawa,pembejeo,] hivyo kuchangia kwa namna moja ukuaji wa uchumi wetu,pato la taifa hata kwa kiwango kidogo.

Kiwanda hiki kimesimamisha na kufunga uzalishaji kwa zaidi ya miezi miwili sasa na kwa sasa wapo katika mchakato wa kuuza mitambo yao yenye thamani ya zaidi ya shilingi za kitanzania bilioni tatu {3} sababu kubwa ni kodi ya VAT {Value Added Tax} katika bidhaa zinazozalishwa..Kilio cha wawekezaji hawa ni soko kuwa dogo na linalobembelezwa kukua ili kukidhi mapana ya uwekezaji katika sekta ya ufugaji..VAT inafanya bidhaa kuwa na bei kubwa ukilinganisha na bidhaa zinazoagizwa toka katika mataifa yasiochaji VAT.

Kilimo ni uti wa mgongo wa taifa letu ,wakati huo huo ni ngumu sana kutenganisha kilimo na mifugo katika muktadha wa maendeleo ya taifa letu tukufu..Ufugaji umekuwa ukifanywa kwa miaka nenda rudi na kaya za kipato cha chini,kati na juu..Ufugaji wa kisasa umekuwa chachu ya wafugaji kukidhi soko la bidhaa za ufugaji kama maziwa,mayai,nyama,asali,n.k.

Nina amini kwa dhati kabisa serikali yetu italifuatilia hili,pata taarifa za kina na kulipatia ufumbuzi makini kwa manufaa mapana ya taifa letu sasa na baadae kwani Mh. Rais wetu na serikali ni wasikivu sana,wenye ufahamu mkubwa sana,wenye hekima sana,na busara nyingi.

Mungu Ibariki Afrika,Mungu Ibariki Tanzania bara na Tanzania Visiwani {Zanzibar}.

CC:Wizara Ya Kilimo na Mifugo
CC:Wizara ya Viwanda na Biashara
CC:TIC
 
Inabidi ijulikane ni VAT ipi inayodaiwa!au km ni mzigo haununuliki
 
Wazo ni zuri na natumaini ujumbe wako utafanyiwa kazi na viongozi husika katika serikali yetu.Tanzania haiwezi kujengwa na mtu mmoja bali ni ushirikiano wa nguvu kazi pamoja na mawazo mazuri kama haya kwa wananchi pamoja na viongozi.
 
Siku hizi imekuwa ni "fashion" mtu biashara ikimdodea tu na kuashiria kufilisika anasingizia "VAT"
 
Mh Rais alisema kuwa watu kama hawa wanapaswa wajiongeze na watumie akili za ziada....

Wanashindwaje kuendesha shughuli za uzalishaji kwa VAT ndogo kiasi hiki? Au wanataka kumlingia Rais kwa hako kakiwanda kao? Serikali imeongeza tozo ipi ijenge viwanda vingine, mbona mamlaka ya Bandari hailalamiki kwa ongezeko la tozo?


Wasiijaribu kabisa serikali ya Magufuli, kama hawataki warudi kwao Thailand, huenda wakawa marafiki wa Lowassa hawa.

Na kwanini walalamikie udogo wa soko la bidhaa zao.?
Rais alishatoa ushauri, kama umekosa soko la bidhaa zako yakupasa kujiongeza na kutumia akili zaidi... Wahakikishe wanapaki hizo bidhaa zao kwenye maBaiskeli wakauze kule Dodoma.

"Wasimjaribu na kumuudhi rais, yuko busy kuandaa Tanzania ya viwanda."
kama washauri wote wa Rais wako kama wewe,kwa heri Tanzania ya viwanda.
 
Watakuja wengine watakao kubaliana na VAT ila itachukua muda sana...
Tunarudi kulekule kuwa Uzalendo ni kitu muhimu sana kutegemea wawekezaji watufanyie kila kitu ni hatari kwa afya ya uchumi wa nchi sana ona hawa wanaondoka kwa kuangalia maslahi yao.
Hakuna mwekezaji anaekuja kuuza sura huku wore hawa ni wanjonyaji tu...
 
Ninapongeza kwa dhati juhudi kubwa za kukomboa wananchi toka katika lindi la umaskini,maladhi,ufukara,shida na tabu.Napongeza utendaji wa kasi wa serikali ya awamu ya tano katika kurejesha nidhamu ya juu/maadiri na uwajibikaji katika utumishi wa umma.Nina kila sababu ya kushiriki kuiunga Mkono serikali sikivu na yenye uzalendo wa kweli chini ya His Excellency JPM,PM {MKM}..

Kwa unyenyekevu mkubwa nawakirisha hili ili hekima itumike kuendelea kulijenga taifa letu kwa kuokoa ajira,mapato,na kuepuka kukimbiza baadhi ya wawekezaji ambao ni chachu kwa tulio wengi kuifinyanga Tanzania mpya ya viwanda vikubwa vya vyenye kukidhi mahitaji ya wananchi wetu katika nyanja mtambuka hivyo kuepuka uagizaji usio na tija ktk uchumi kama toothpick,karatasi,furniture,stapler pins,matairi,vipuri,nguo,n.k.

Kuna kampuni ya kimataifa {toka thailand yenye viwanda takribani 15 katika nchi mbalimbali Duniani} iliowekeza katika utengenezaji wa chakula cha kuku/mifugo takribani miaka 3 hapa nchini..Kiwanda cha kampuni hii kipo maeneo ya chang'ombe,jirani na kiwanda cha konyagi.Kiwanda hiki kimeajiri zaidi ya watanzania 50 wenye elimu ya juu na kati wakiwemo {Mechanical engineers,chemical engineers,Food engineers,etc etc},Kiwanda hiki ni mnunuaji mzuri wa nishati ya umeme;malighafi mbalimbali za kilimo {mafuta ya alizeti,mahindi,madawa,pembejeo,] hivyo kuchangia kwa namna moja ukuaji wa uchumi wetu,pato la taifa hata kwa kiwango kidogo.

Kiwanda hiki kimesimamisha na kufunga uzalishaji kwa zaidi ya miezi miwili sasa na kwa sasa wapo katika mchakato wa kuuza mitambo yao yenye thamani ya zaidi ya shilingi za kitanzania bilioni tatu {3} sababu kubwa ni kodi ya VAT {Value Added Tax} katika bidhaa zinazozalishwa..Kilio cha wawekezaji hawa ni soko kuwa dogo na linalobembelezwa kukua ili kukidhi mapana ya uwekezaji katika sekta ya ufugaji..VAT inafanya bidhaa kuwa na bei kubwa ukilinganisha na bidhaa zinazoagizwa toka katika mataifa yasiochaji VAT.

Kilimo ni uti wa mgongo wa taifa letu ,wakati huo huo ni ngumu sana kutenganisha kilimo na mifugo katika muktadha wa maendeleo ya taifa letu tukufu..Ufugaji umekuwa ukifanywa kwa miaka nenda rudi na kaya za kipato cha chini,kati na juu..Ufugaji wa kisasa umekuwa chachu ya wafugaji kukidhi soko la bidhaa za ufugaji kama maziwa,mayai,nyama,asali,n.k.

Nina amini kwa dhati kabisa serikali yetu italifuatilia hili,pata taarifa za kina na kulipatia ufumbuzi makini kwa manufaa mapana ya taifa letu sasa na baadae kwani Mh. Rais wetu na serikali ni wasikivu sana,wenye ufahamu mkubwa sana,wenye hekima sana,na busara nyingi.

Mungu Ibariki Afrika,Mungu Ibariki Tanzania bara na Tanzania Visiwani {Zanzibar}.

CC:Wizara Ya Kilimo na Mifugo
CC:Wizara ya Viwanda na Biashara
CC:TIC
Nakifahamu hicho kiwanda lakini chakula chao cha kuku ni bei mkomoto.
 
Naamini miaka michache ijayo hatutawahitaji sana wawekezaji toka nje hata kufikia kuwabembeleza lakini kwa sasa inatubidi hata ikibidi kwa shingo upande ..nadhani ni bora tupate kidogo vijana wetu wakapata ajira na kusaidia ndugu zao huku serikali ikipata walau kidogo na kuwezesha utoaji wa huduma mbalimbali kwa ufanisi {Elimu,Afya,Miundombinu,ulinzi,Usalama}..
 
Hali si mbaya,
Wana wa Israel walipotoka Misri Mwenyezi Mungu aliwapitisha Jangwani {Kwa miaka takribani 40} kwa makusudi maalumu kabla ya kufikia nchi ya ahadi iliojaa maziwa na asali...

Tupo katika mapito kuelekea neema kubwa ,Nchi yetu ni tajiri sana ina kila aina ya vinono,vitamu,ving'aavyo,madini na vito vya thamani sana..

Ushupavu/ujasiri wa viongozi wetu awamu kutufikisha tuendako/ kufika tuendako upo katika hali kubwa,nia kubwa,kasi kubwa na dhamili ya wazi..tuwasaidie,tuliombee taifa,tushiriki kuwa chachu ya maendeleo tunayoyaota..

Viva Tanzania Mpya
Wana wa Israel walitoka utumwani Misri, sisi (Tz) tunatoka ktk utumwa wa nani?
 
Wana wa Israel walitoka utumwani Misri, sisi (Tz) tunatoka ktk utumwa wa nani?

Utumwa wa umaskini japo tumezungukwa na utajiri,ujinga,maradhi {kiroho,kimwili,kiufahamu},matumizi mabaya ya madaraka,ufisadi,uvivu,upigaji dili kila kona...uchakachuaji mambo..michakato hewa..
 
Utumwa wa umaskini japo tumezungukwa na utajiri,
Utumwa wa ujinga,
Utumwa wa maradhi {kiroho,kimwili,kiufahamu},
Utumwa wa matumizi mabaya ya madaraka,
Utumwa wa ufisadi,uvivu,upigaji dili kila kona...
uchakachuaji mambo..michakato hewa..
 
Back
Top Bottom