Serikali Mbili ni Gharama Kubwa !

Serikali Mbili ni Gharama Kubwa !

Goodrich

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2012
Posts
2,091
Reaction score
1,179
Serikali mbili zenye marais watano ni vague na pia ni gharama kubwa.

Ni vema kuwa na serikali moja ya Tanzania.

Serikali ya Zanzibar isiwepo kama ambavyo hakuna serikali ya Tanganyika.

Hayo ndio hasa yalikuwa malengo ya waasisi wa Muungano.

Muundo wa serikali mbili haukubaliki maana ni gharama na unaifanya Tanganyika kuwa nchi isiyo na mwenyewe.

Otherwise tutaendelea kuikana nchi yetu Tanganyika kwa gharama ya Zanzibar.
 
Angalizo: Hakuna chama cha siasa, iwe ni tawala au upinzani ambao wanathubutu japo kugusia serikali moja.

Sababu ni kuwa WANAOGOPA kupoteza wafuasi au kupingwa Zanzibar.
 
ccm wanawaza pafupi sana. Naamini kama wakati huu Rais wa Tanzania angekuwa ni wa kutoka Zanzibar basi mambo yangekuwa tofauti.

Pia umepata kujiuliza ni kwanini kero za muungano ni zenye kuifavor znz tu ?
 
ccm wanawaza pafupi sana. Naamini kama wakati huu Rais wa Tanzania angekuwa ni wa kutoka Zanzibar basi mambo yangekuwa tofauti.

Pia umepata kujiuliza ni kwanini kero za muungano ni zenye kuifavor znz tu ?

Wewe ndo unamatatizo mi nafkiri kwa hili CCM wako sahihi kushinda yeyote yule serkali 2 ndo dili au moja zaidi ya hapo hamtutakii mema.
 
Unafikiri idadi ua serikali ndo tatizo??? Zimekuwepo serikali mbili znazoiwezesha zbar kuwa na madaraka yake binafsi na kufanya muungano pia uwepo.
 
Serikali mbili zenye marais watano ni vague na pia ni gharama kubwa.

Ni vema kuwa na serikali moja ya Tanzania.

Serikali ya Zanzibar isiwepo kama ambavyo hakuna serikali ya Tanganyika.

Hayo ndio hasa yalikuwa malengo ya waasisi wa Muungano.

Muundo wa serikali mbili haukubaliki maana ni gharama na unaifanya Tanganyika kuwa nchi isiyo na mwenyewe.

Otherwise tutaendelea kuikana nchi yetu Tanganyika kwa gharama ya Zanzibar.

Nani anayejuwa malengo yao? walimuuliza nani kabla ya kuungana?

Hawa tusiwafuate. Gharama ya serikali haitokani na idadi ya serikali. Tunazo mbili na bado Rais anachota anavyotaka. eti ikulu haifanyiwi audit! Ndo maana mtu anabeba tu na kufanya kila aina ya biashara.

Atanunua UDA, ataagiza mchele, Atajenga mahoteli, Ataaagiza mafuta,..... yote hakuna anayeuliza.

Tunataka Serikali tatu, hatujasema tunataka marais watatu. watu wakiona huyu anavyoiba wanadhani wakiwa watatu, wataiba mara tatu! Kumbe si hivyo. halafu eti gaharama za serikali ndo zinawafanya wachukie kiasi hicho na matusi kwa wana CCM wenzao (akina Warioba) kweli? au ni wasiwasi kupoteza madaraka!
 
Back
Top Bottom