Tatizo mambo mengi Tanzania bado yanafanyika kama enzi za Chama Kimeshika hatamu ........ No wonder Rais anadai TLS ni mali ya umma!! Kuwa mwanachama kwenye vyama vya wafanyakazi inatakiwa kuwa kwa hiari na matatizo yao walitakiwa wayamalize wao wenyewe kupitia vyombo vya kiresheri kama other NGOs au Private companies.
Haya mambo ya vyama vya wafanyakazi hayakutakiwa kabisa yawe chini ya serikali. CAG wala hakutakiwa kuwa na uezo wa kuwaingilia au kukagua mali au matumizi yao. Wao walitakiwa watumie mashirika binafsi kama KPMG, PWC, EY .... au other local accounting and audit firms.
Kwa kuendeleza kuwa chini ya ule mfumo wa kijamaa ......... ni bora visiwepo, kwa kuwa vinaendela kutetea maslahi ya serikali badala ya wafanyakazi.
Utasikia jinsi watakavyokuwa wanajikomba komba huko Iringa hiyo Mei 1 ..............!!
HII NDIO CWT USIYOIJUA.
Na Thadei Ole Mushi
[HASHTAG]#Tarehe[/HASHTAG] 27/3/2017 Katibu mkuu kiongozi alimuomba CAG afanye ukaguzi kwenye chama cha Waalimu CWT.
[HASHTAG]#Ukaguzi[/HASHTAG] ulijikita katika tuhuma dhidi ya Uongozi wa chama cha waalimu zinazohisu ubadhirifu wa fedha na mali za chama.
[HASHTAG]#Ukaguzi[/HASHTAG] maalumu ulikagua taarifa za mapato na matumizi ya Chama, Uliangalia uhusiano uliopo kati ya Benki ya waalimu na waalimu wenyewe, uhusiano uliopo kati ya Mwalimu haouse na mwalimu mwenyewe.
YALIYOBAINIKA.
1.Hakuna mfumo mzuri wa wanachama unaoonyesha kumbukumbu za wanachama. Katiba ya CWT inaeleza kuwa kunatakiwa kuwe na aina nne za wanachama lakini CWT hawaonyeshi aina hizo za wanachama hivyo haijulikani CWT ina wanachama wangapi.
Pia katika swala la wanachama hakuna taarifa zinazoonyesha wanachama walijiunga lini, mishahara yao kwa mwezi, namba ya uanachama, kiwango anachochangia kwa mwezi nk. Jambo hili CAG anasema kuna uwezekano kuna fedha nyingi zinaliwa kutokana na kutokuwepo kwa taarifa hizo.
2.Malipo ya shilingi 11,924,250,620.13 yakifanyika bila viambatanisho vyovyote. Hii ina maana hakuna nyaraka zinazoonyesha matumizi sahihi ya fedha hizo.
3. Shilingi 3,287,708,358 zilipwa bila kuidhinishwa na katibu mkuu au mweka hazina wa Chama na pia hakuna viambatanisho.
4. Shilingi 11,924,250,620.13 zililipwa bila kuzingatia makisio. Hii ina maana fedha hizi zilitumika bila kuzingatia bajeti ya CWT.CAG anasema viongozi wanakosa nidhamu ya matumizi ya fedha hivyo kuna fedha hapa zilitumika bila wanachama kujua zimekwenda wapi.
5. Hakuna nyaraka zinazoonyesha umiliki wa moja kwa moja wa CWT na miradi yake.
6. Hakuna nyaraka zinazoonyesha mtiririko wa mapato wa vitega uchumi vya chama toka CWT kianzishwe.
7.Mwalimu House imesajiliwa Brela kwa jina lingine la Teachers Development kupitia usajili wa Brea 45719 Badala ya TDCL. Na CAG amebaini kuwa kampuni hilo la Teachers Development hakijawahi kufanya kazi toka kuanzishwa kwake. Kwa hiyo mapato yake hayaonekani.
[HASHTAG]#Hii[/HASHTAG] ndio CWT ambayo huijui