Serikali inawaharibu watumishi

Serikali inawaharibu watumishi

East Zoo

Member
Joined
Mar 12, 2015
Posts
63
Reaction score
14
Katika kufanya kazi, unatakiwa utoe result na pia ufanye kazi kwa weledi, katika utafiti wangu mdogo nimegundua mfanyakazi wa private sector anafanya kazi kwa ufanisi na kwa taaluma yake tofauti na serikalini kwa sababu zifuatazo:

1. Ukifanya kazi Serikalini hata kama result yako haitakuwa nzuri sio tatizo mfano bwana shamba wa Serikali na bwana shamba wa kibena estate au TPC uwezo wao wa kutoa matokeo ni tofauti kabisa,hii ni kwa sababu serikalini kazi zinafanyika kimazoea na watu hata hawapo serious.

2. Imekuwa ni kasumba kwa huduma za private kuwa bora kuliko serikalini mfano afya, elimu, nk kwa sababu private unajituma mpaka kujisomea ili kazi yako iwe safi lakini kule ukifika job yatosha huwezi kupimwa kazi uliofanya na ufanisi wake, hii imewafanya wafanyakazi Serikalini kubweteka na kuwa mizigo.

Chukua mchumi mwenye uzoefu wa miaka 3 Serikalini na private utagundua wa private ana vitu vipya vingi tofauti na alivyopata shule kwa sababu kutafuta ziada ni kawaida, but mwalimu wa serikalini hata kama anafundisha advance yeye anaweza kutumia notice miaka kumi zilezile hata kama haziendani na wakati.


3. Serikalini huogopi kwa sababu system ya Serikali haifanyi kazi vizuri na hakuna jipya watu wanapishana tu kama wako busy lakini baadhi ni mizigo, hii ni kutokana na siasa mpaka kwenye taaluma na kazini.

Naombeni mjadili kwa hoja, note wafanyakazi Serikalini wanaofanya kazi sawasawa ni wachache sana scientificaly is like nothing.

Asanteni.
 
Ukiwa Serikalini una uhakika wa mshahara kila mwezi kwani hautegemei uzalishaji. Hivyo, baadhi ya wafanyakazi wachache hawajitumi!
 
East Zoo

Suluhisho ni kutoa welfare kwa wananchi, ndio wafanyekazi kwa weredi.

Mimi nimekuelewa sana.
Tatizo ni siasa, Wanasiasa wanabaki kutetea wabaki pale walipo. Nchi za ulaya zinautaratibu wa kujali watu wao, kwa utaratibu wa welfare system.

Kitu kinachoitwa ruzuku, welfare kwa wenzetu inajenga imani na watu, kazi na kila kitu, wenzetu hakuna fujofujo na vita kwa sabb ya imani.

leo hii mtanzania ndio wa kwanzs kufanya deal na mgeni kuiibia nchi. Wasomali,wakongo,waganda,wakenya wanatanua nchini kama njia panda vile, yaan ni ujinga ujinga


Katika hoja yako hii, kipengele cha 2, wanasoma katika vyuo vikuu kozi ya públic administration, wote wanasoma, hays mambo kw tz tutaita, is too late. Sio rahis kurejesha imani, labda kwa mishahara, na maslah muhm kwa wafanykazi. zaid ya hapo inabaki rushwa, fujo, ufisadi na vita
 
Last edited by a moderator:
naunga mkono hoja. Nini kifanyike basi ni kupangua mfumo woooote huo na kuanza upya kwa kufuatiliana, kukumbushana na kuonyana bila kuogopana. Maana sisi wabongo hatuna tabia ya kusema/kukemea maovu ya wenzetu badala ake tumekuwa watu wakuongelea chinichini tu.
FUNGUA KINYWA CHAKO PALE UNAPOONA MAMBO HAYAENDI SAWASAWA ILI KULETA UFANISI KATIKA UTENDAJI
 
very true, huko watu wanaenda kupumzika sio kufanya kazi.
 
mazoea yameharbu sana nchi yangu ya tz.

watu wanafanya kazi kwa mazoea sana.

na tatizo kubwa uongozi mbaya wa baadh ya masisiem yan wananiboa mno!

wafanyakazi wananyanyaswa na uongoz wa juu kutokana na wao kutojua haki zao. na kushndwa kufwatilia kutokana weng wao wapenda rushwa wamebebana sana..
ndio maana utakuta sekta muhimu ka afya na elimu znaenda ovyo sana.

matokeo yake ni huduma mbaya kwa raia, ndo mana takuta shulen michango ming wakat walisema wamefuta- hospital ukiwa na mkono wa birika hatar.

na sio kwamba hawajui wanajua.. kwa sababu wenyewe wanaenda tibiwa aghakan na watoto wao wanaenda soma escrow fedha boys and girls, na usafir awang'ang'anian kama sie wa mbagara ad twaingilia mlango wa dereva.

pamoja we can kuleta mabadiliko kuwachagua viongoz wataotujal jamani
 
......Serikali hii ya CCM naona inazorotesha uwezo wangu wa kiutendaji na kugaragaza taaluma yangu nilikifananisha na miaka kadhaa iliyopita wakati nipo katika Private sector.

Hawa wanaojiita Waheshimiwa nao ni kikwazo kikubwa sana katika kufanikisha utoaji huduma zilizokusudiwa kwa Wananchi halafu hao hao wanajifanya wanawapenda wananchi kwa Propaganda zao uchwara.

Sio siri, tunahitaji mabadiliko makubwa sana katika mifumo yetu ya kiutendaji serikalini vinginevyo wananchi wataendelea kulalamika kila siku na Watumishi wataendelea kuwa mizigo maana wengi wao huwaza posho za vikao muda mwingi.
 
Muda mwingine dawa ni privatisation tu....

Ipe kampuni A bandari ya Dar na ipe kampuni B bandari ya Tanga na mpe kampuni C bandari ya Mtwara halafu tuone kama muda wa mizigo haujapungua.
 
Tatizo kubwa ni siasa kuingilia utendaji, wacha watu wapumzike bwana tumechoka sisi! Chukulia mfano huku kwetu Afisa kilimo akitaka kuwaweka wananchi vizuri ili wafuate masharti ya KILIMO bora madiwani wanakuja juu eti watu wangu! Ukisema ufuate sheria za kuwawajibisha wakulima wanaokiuka misingi ya KILIMO bora unakutana na kigingi cha madiwani mwisho Wa siku unajikuta umejengewa uhasama na wananchi kiasi cha mpaka kukutishia maisha!

Kikwazo kingine ni maslahi, huwezi kulinganisha mshahara Wa serikalini na sekta binafsi, serikalini ni wizi mtupu!! Ndo maana raia wanafanya bora liende!! Serikali ifanye majaribio ya kubinafsisha halmashauri moja ione kama hakutakuwa na mabadiliko!
 
Katika kufanya kazi, unatakiwa utoe result na pia ufanye kazi kwa weledi, katika utafiti wangu mdogo nimegundua mfanyakazi wa private sector anafanya kazi kwa ufanisi na kwa taaluma yake tofauti na serikalini kwa sababu zifuatazo:

1. Ukifanya kazi Serikalini hata kama result yako haitakuwa nzuri sio tatizo mfano bwana shamba wa Serikali na bwana shamba wa kibena estate au TPC uwezo wao wa kutoa matokeo ni tofauti kabisa,hii ni kwa sababu serikalini kazi zinafanyika kimazoea na watu hata hawapo serious.

2. Imekuwa ni kasumba kwa huduma za private kuwa bora kuliko serikalini mfano afya, elimu, nk kwa sababu private unajituma mpaka kujisomea ili kazi yako iwe safi lakini kule ukifika job yatosha huwezi kupimwa kazi uliofanya na ufanisi wake, hii imewafanya wafanyakazi Serikalini kubweteka na kuwa mizigo.

Chukua mchumi mwenye uzoefu wa miaka 3 Serikalini na private utagundua wa private ana vitu vipya vingi tofauti na alivyopata shule kwa sababu kutafuta ziada ni kawaida, but mwalimu wa serikalini hata kama anafundisha advance yeye anaweza kutumia notice miaka kumi zilezile hata kama haziendani na wakati.


3. Serikalini huogopi kwa sababu system ya Serikali haifanyi kazi vizuri na hakuna jipya watu wanapishana tu kama wako busy lakini baadhi ni mizigo, hii ni kutokana na siasa mpaka kwenye taaluma na kazini.

Naombeni mjadili kwa hoja, note wafanyakazi Serikalini wanaofanya kazi sawasawa ni wachache sana scientificaly is like
 
Back
Top Bottom