Eng. Y. Bihagaze
JF-Expert Member
- Sep 8, 2011
- 1,488
- 908
Wakati mzimu hatari wa mgongano wa ki- utu na maslahi kati ya serikali na madaktari ukiwa kwenye wakati wa joto kali ukifanyika kwenye shingo tepetevu ya raia asiye na hatia yoyote, mapambano yakiendelea kwa ari na kasi zaidi kiasi cha kutekana na kushambuliana kihasimu, kimaudhi na kiuzembe zaidi, Duru za wachunguzi wa kimtazamo zinavuja kwamba haya YANATOA TAFSIRI KWAMBA SERIKALI INAIPINDUA NCHI KIJESHI.
Katika tafsiri nyepesi ya kawaida JESHI ni Kikundi cha watu waliojiunga ili kukamilisha kusudio maalum. Kwenye jamii ya watu wanaoikalia dunia wanatafsiri kwamba jeshi ni kikundi cha watu –wenye zana zinazoweza kuleta maangamizi kwa mwanadamu-waliojiunga kwa kusudio maalum. Na hapo ndipo tunayakuta majeshi mawilii ambayo yote yana lengo moja kumlinda au kumdhuru raia. Jeshi Lenye silaha za moto na Jeshi lenye silaha za madawa(madaktari na fani nzima ya uuguzi).
Nachelea kuweka Petroli kwenye Moto unaowaka lakini pia sitaki kuwa mzembe wa kuweka mtazamo wa wazi wa hiki kinachoendelea. Kama raia wa kawaida Tunaamini Madaktari ni binaadam ambao wanabeba vichwa vinavyofikiri lakini pia serikali ina watu wanaofikiri on this basis hakuna mwenye hoja nyepesi hapa, kila mmoja ana hoja nzito na hoja yake lazima ifikie makamo stahilivu. Nataka niseme bila kulegeza semi, HILI NI JANGA LA KITAIFA..
Unapotembelea baadhi ya Hospitali zetu, watoto wanavyoteketea kwa kukosa matibabu, wagonjwa wanavyohangaika kujipanga ili wajitibu, wananchi wanavyotafuta wataalam wa mitishamba kama tiba mbadala na huku wanapata madhara mengi zaidi, sasa hata wauza maduka ya dawa wamegeuka madaktari kwenye vitengo vyao ili wanufaike na sakata hili kwa kuwatibu wagonjwa kinyume na fani inavyotaka, na hapo haitoshi jibini la majadiliano linatiwa doa kwa kumshambulia kiini wa majadiliano Dr. Ulimboka, na hali kuwa tete zaidi kwetu wananchi maskini ya mungu sisi tusiojua lolote..Ni tafsiri gani ya maneno utayaweka hapa kama sio JANGA la kitaifa?
Nirudi Duruni, Serikali inaipindua nchi kijeshi, serikali ikiwa ni kikundi kidogo sana cha watu waliokasmiwa dhamana ya uongozi wa nchi, na nchi ikiwa ndio umati wa raia wenyewe wenye nchi. Serikali ikiwa ni pamoja na Rais na vyombo vyote vya ulinzi na usalama, Bunge, Baraza la mawaziri, watumishi wa serikali wakiwemo na madaktari wenyewe, ambao wamekuwa kwenye mzozo, migongano na kero kwa Muda sasa. Huku Nchi, yaani sisi raia tukiwa watazamaji na waathirika wakuu wa kadhia hii. Kumekuwa na kero kati ya wabunge na posho zao, wizi wa wanyamapori, maandamano ya kupinga muungano, Vurugu za Zanzibar, Mauaji ya walemavu wa ngozi, ujambazi na ujangili uliokithiri, wizi wa waziwazi na ufisadi wa kutisha ambayo yote haya hayajapatiwa majibu toshelezi kwa raia, lakini mwananchi mtanzania ametulia tuli kama mjinga vile, sasa chokochoko hii imefikia hatua ambayo haiwezi KUVUMILIKA, inapogusa eneo la uhai wa raia..TIBA.
Kuifatakua kadhia hii, tunajua wazi jeshi la kwanza yaani Vyombo vyote vya ulinzi na usalama ikiwemo Polisi, magereza, jeshi la wananchi nk, wana uwezo wa kuua kwa makusudi au bahati mbaya na jamii ikafichwa taarifa lakini vile vile Jeshi linalotumia madawa yani madaktari na Wauguzi nao pia wana uwezo huo huo wa kuua kwa bahati mbaya au makusudi na jamii sisi wananchi tukafichwa. Sasa inapofikia mishale jeshi mojawapo kati ya haya linapoanza kuua raia kwa makusudi, WAZIWAZI na Serikali Ikiwepo HAYA NI MAPINDUZI MAKUBWA.
Madaktari wanapogoma kutoa tiba, ni tafsiri ya wazi kwamba wameamua kuua raia. Na kwa Kuwa Kuna Viongozi waliokasmiwa madaraka kuhakikisha hili lisitokee, ama kwa uzembe wao, ama kwa kushindwa kuongoza vema, ama kwa makusudi yao tu na chuki zao kwetu sisi raia maskini tusio na mtetezi wameamua kuruhusu janga hili litokee, hatuoni sababu ya ushawishi ya wao kuendelea kuhodhi madaraka hayo. WATOKE HARAKA SANA KABLA HALI HAIJAWA MBAYA ZAIDI.
Wananchi hatuwajibiki kujua kiini cha tatizo –HAISAIDII, nani anaongoza vuguvugu hili-HAISAIDII, Ugomvi wa kimaslahi na kimapato hata kama serikali itatuelezea kiini cha ugonvi huu hadi mtondogoo haitasaidia lolote ilihali madhara ya kadhia hii yakiendelea kuwepo na kuleta balaa kila sekunde inayoondoka, tunachojua serikali ingekeketa mbivu na mbovu kwa uwezo ilionao na kuidhibiti hali hii isitokee.. kwa hiyo hatuzuiliki kabisa kuamini kwamba sasa VIONGOZI WETU UWEZO WAO WA UONGOZI NA KIFIKRA UMEKOMEA HAPO, TAFADHALI WAJIUZULU KUPISHA KADA NYINGINE YA SAFU YA WATUMISHI NAO WASHIKE USUKANI WA UONGOZI WA NCHI HII.
Mweshimiwa Rais, Hivi kweli Unapata hamu ya Kula, Kulala, Na Kuburudika na Familia Yako Ilihali kuna watu ndani ya nchi yako Unayoiongoza wanateketea kwa kukosa Huduma muhimu kabisa ya kijamii ambayo ni TIBA!!.. unalala na Kuamka kabisaa.. Moyo wako Uko mweupe kabisaa. Aise haya kwanini yasiwe maajabu ya Nchi.. Mwenyezi Mungu amekupa Uwezo wa Kutamka neno kudhibiti hali hii lakini Umewaachia watoto huku wanavunjana mbavu na kutengeneza propaganda za kipumbavu kila mchao na kuzunguka kwenye vyombo vya habari kupika majungu, uchonganishi na Fitna na wewe upo kimya ukiangalia Mchezo huu unavyokwenda? Juzi Mganga mkuu wa Serikali na Timu ya watu watatu wamening'inia TBC wakisambaza umbea na chuki kwa watanzania. Unapoiambia jamii kwamba Daktari nayeanza ajira analipwa mshahara wa laki nane na nusu wakati MhandisiAnayeanza kazi analipwa laki nne, huu ni uchonganishi wa chuki. Kwamba sasa serikali inataka sisi wahandisi tuwachukie Madakrati kwa sababu kwanini wao wanapendelewa na serikali na bado hawatosheki wanataka serikali iwapendelee zaidi? Wakati shule yao ni Ngumu pia Shule ya Uhandisi ni Ngumu vilevile, Top brain Layers za Hesabu huenda Uhandisi na Top brain Layers za bailojia huenda kwenye fani ya matibabu, kwa hiyo mnataka wahandisi na kada nyingine waingie kwenye ugomvi na madaktari? Hii ni akili kweli au matope? Mtu ananing'inia kabisa kwenye TV ya kitaifa anamwaga Majungu haya.. na Bado yupo kwenye kiti anaendelea kula bata.. watu wanakufa huku.. huu si moyo wa uzalendo hata kidogo.. tumewakosea nini.. mtunyime matibabu na kutuchonganisha pia?
Viongozi wengine wa serikali wako kukusaidia wewe kutuongoza sisi, sasa tunapoona viongozi hao uliowaweka wewe wakusaidie kutuongoza sisi leo wanagombana na madhara tunaathirika sisi, na wewe uko kimywa hutaki kumuwajibisha yeyote ni tafsiri gani sisi raia maskini ya Mungu Tunaipata? Tukisema Umewatuma Watutendee Hivi Utasema Tunakosea mweshimiwa?
Ni baba gani asiye na uwezo wa kuadabisha familia yake mbele ya jamii??. Kwamba kuna mahakama ya Kazi, kwamba kuna kosa la kinidhamu mambo yote hayo hayasaidii baba Riz, Tunachotaka ni Huduma kwa jamii ziwepo na ziendelee.. Ila pia elewa kwamba sisi sote ni binaadam, tunatofautiana kifikra na kiuongozi, kama Mwenyezi Mungu hakukujaalia kipaji cha kuongoza matukio kama haya ya binaadam ni vema ama Ukakubali kizalendo kwamba Uongozi wa hili kibinaadam siuwezi, unang'atuka na mwingine anaendelea naye akishindwa vilevile anang'atuka. Au wajibisha uliowakasmia madaraka husika haraka ili kunusuru balaa zaidi ambalo sasa hasira ya mwananchi ikishaiva haitadhibitika.
Kumwongoza binaadam ni Kazi Ngumu.
Wanajeshi wana Umoja wa kitaifa ila madaktari wana umoja wa Kimataifa. Tunakoelekea sasa watu hawa kila mmoja kwa nafasi yake ataanza kutumia nafasi yake kumdhuru mwenzie kwa siri. Hata kama mtu atakimbilia Kutibiwa Nchi za nje, Madaktari watasema huyu ndiye yule kiongozi anayetoka kwenye nchi wanayodhalilisha fani yetu, watamtengeneza wanavyotaka kwa sababu uwezo huo wanao, watampeleka kwenye "Mabwepande" za kikwao..
Amka kwenye kiti Mheshimiwa, wajibika kwenye Hili sakata sasa. INATOSHA.