JMF
JF-Expert Member
- Jun 29, 2013
- 1,782
- 2,836
Umofia kwenu wana JF,
1. Kwa siku za karibuni kumekua na utaratibu mpya ambao ajira nyingi za serikali na taasisi zake zinahitaji kigezo cha cheti cha JKT. Hii imepelekea vijana wengi kukosa sifa za kulitumikia taifa kisa tuu hawakupitia JKT aidha kwa hiari yao wenyewe au kwakukosa nafasi za kujiunga na JKT. Mfano: kuna vijana walishindwa kujiunga na jkt kutokana na sababu za kiafya hivyo wakalazimika kuendelea na elimu ya juu. Leo wamehitimu na zinatoka nafasi za kazi ambazo zinalazimu muombaji awe na cheti cha jkt. Hili naiomba serikali iliangalie upya.
2. Kwenye ajiraportal nako kuna kasoro au tatizo la kimfumo ambalo linazuia watu kuomba kazi hata kama wanasifa zinazotakiwa au linganishi. Mfano: Zinatoka nafasi znazohitaji mtu aliye na diploma ya IT au sifa zinazoendana. Unakuta kwenye web wameandika kabisa equivalent qualification lakini mtu mwenye shahada ya IT hawezikuomba. Hata yule mwenye shahada ambae alianzia diploma nae hawezi kuomba, mfumo unakataa. Nimetolea mfano wa IT lakini kuna shida kubwa vijana tunakumbana nazo katika kuomba ajira serikalini. Hata ikitoka nafasi ya udereva na bachelor holder anayo, mfumo unakataa. Kuna watakaojiuliza kwanini mtu mwenye degree aombe udereva. Jibu utalipata kwenye aya inayofuata.
3. Nafasi za upendeleo kwa walio tayari serikalini. Hili linatufanya vijana tulio nje ya system tuendelee kubakia nje wakati waliopo wakihama toka idara moja kwenda nyingine kiulani tuu. Unakuta zinatangazwa nafasi za ajira na kigezo kinakuwa ni lazima uwe umeajiriwa serikalini, uombe kwa kupitisha barua kwa mwajiri wako ya kuomba kuhama idara. Kwanini isiwe fair play kwamba hata ambao hawapo kwenye mfumo nao waombe tuu? Inaumiza sana vijana.
4. Kigezo cha umri. Jamani kuna waliosoma kwa kuunga unga na hata ku disco chuo. Unakuta mtu unasoma maisha yanakuwa magumu una drop chuo au hata secondary kwenda kupambana na maisha hasa sisi tuliotoka kwenye familia duni. Unarudi chuoni unasoma na kuhitimu, hapo umri umeshasonga. Unarudi mtaani ajira hakuna, unakaa tokea mwaka 2015 hadi leo ndipo inatoka ajira zenye vigezo vya umri eti mwisho miaka30. Wakati mwingine wanaandika kabisa kigezo ni kwa waliohitimu labda kuanzia mwaka 2017 kuja juu. Hao wa chini wasubirie serikali yao wenyewe? kama siyo hii tunayoijua?
5. Utaratibu wa kuita watu kwenye usahili wa post chache Dodoma au Dar. Hivi haiwezekani usahili ukafanyika kikanda ili ku balance? Unakuta nafasi zimetangazwa 5 halafu wanaitwa watu 200 kwenda kufanya interview Dar bila kujali watu wanaoomba hizo nafasi wanatoka kila kona ya nchi hii. Wengine wanatokea mikoa ya mbali na Dar kama Kigoma, Mtwara, Mara, Mbeya n.k, unawaita Dar bila kujali nauli, malazi chakula na dharura wanapata wapi ukizingatia wengi ni jobless na wanatokea familia za maisha ya kuunga unga.
Yapo mengine ambayo wadau wanaweza kuongezea. Lengo ni serikali ielewe kuwa kwa hili tatizo la ajira nchini, wasilitumie vigezo vigumu ili tuu kupunguza idadi ya waombaji.
Nawasilisha.
1. Kwa siku za karibuni kumekua na utaratibu mpya ambao ajira nyingi za serikali na taasisi zake zinahitaji kigezo cha cheti cha JKT. Hii imepelekea vijana wengi kukosa sifa za kulitumikia taifa kisa tuu hawakupitia JKT aidha kwa hiari yao wenyewe au kwakukosa nafasi za kujiunga na JKT. Mfano: kuna vijana walishindwa kujiunga na jkt kutokana na sababu za kiafya hivyo wakalazimika kuendelea na elimu ya juu. Leo wamehitimu na zinatoka nafasi za kazi ambazo zinalazimu muombaji awe na cheti cha jkt. Hili naiomba serikali iliangalie upya.
2. Kwenye ajiraportal nako kuna kasoro au tatizo la kimfumo ambalo linazuia watu kuomba kazi hata kama wanasifa zinazotakiwa au linganishi. Mfano: Zinatoka nafasi znazohitaji mtu aliye na diploma ya IT au sifa zinazoendana. Unakuta kwenye web wameandika kabisa equivalent qualification lakini mtu mwenye shahada ya IT hawezikuomba. Hata yule mwenye shahada ambae alianzia diploma nae hawezi kuomba, mfumo unakataa. Nimetolea mfano wa IT lakini kuna shida kubwa vijana tunakumbana nazo katika kuomba ajira serikalini. Hata ikitoka nafasi ya udereva na bachelor holder anayo, mfumo unakataa. Kuna watakaojiuliza kwanini mtu mwenye degree aombe udereva. Jibu utalipata kwenye aya inayofuata.
3. Nafasi za upendeleo kwa walio tayari serikalini. Hili linatufanya vijana tulio nje ya system tuendelee kubakia nje wakati waliopo wakihama toka idara moja kwenda nyingine kiulani tuu. Unakuta zinatangazwa nafasi za ajira na kigezo kinakuwa ni lazima uwe umeajiriwa serikalini, uombe kwa kupitisha barua kwa mwajiri wako ya kuomba kuhama idara. Kwanini isiwe fair play kwamba hata ambao hawapo kwenye mfumo nao waombe tuu? Inaumiza sana vijana.
4. Kigezo cha umri. Jamani kuna waliosoma kwa kuunga unga na hata ku disco chuo. Unakuta mtu unasoma maisha yanakuwa magumu una drop chuo au hata secondary kwenda kupambana na maisha hasa sisi tuliotoka kwenye familia duni. Unarudi chuoni unasoma na kuhitimu, hapo umri umeshasonga. Unarudi mtaani ajira hakuna, unakaa tokea mwaka 2015 hadi leo ndipo inatoka ajira zenye vigezo vya umri eti mwisho miaka30. Wakati mwingine wanaandika kabisa kigezo ni kwa waliohitimu labda kuanzia mwaka 2017 kuja juu. Hao wa chini wasubirie serikali yao wenyewe? kama siyo hii tunayoijua?
5. Utaratibu wa kuita watu kwenye usahili wa post chache Dodoma au Dar. Hivi haiwezekani usahili ukafanyika kikanda ili ku balance? Unakuta nafasi zimetangazwa 5 halafu wanaitwa watu 200 kwenda kufanya interview Dar bila kujali watu wanaoomba hizo nafasi wanatoka kila kona ya nchi hii. Wengine wanatokea mikoa ya mbali na Dar kama Kigoma, Mtwara, Mara, Mbeya n.k, unawaita Dar bila kujali nauli, malazi chakula na dharura wanapata wapi ukizingatia wengi ni jobless na wanatokea familia za maisha ya kuunga unga.
Yapo mengine ambayo wadau wanaweza kuongezea. Lengo ni serikali ielewe kuwa kwa hili tatizo la ajira nchini, wasilitumie vigezo vigumu ili tuu kupunguza idadi ya waombaji.
Nawasilisha.