Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 19,768
- 49,940
Kuna pesa nyingi za umma na za mikopo zimewekezwa kwenye usafiri wa mwendokasi Dar lakini ubora wa usafiri ni duni sana na unazidi kuwa duni zaidi kutokana na kutokuwepo kwa mabasi ya kutosha kunakosababishwa na kuharibika na kufa kwa mabasi kwa mara kwa mara.
Duniani kote inafahamika kuwa bidhaa za China ni aghali kuliko za Taifa lolote ingawa unaponunua zinaonekana ni za bei nafuu kuliko za Taifa lolote.
Mathalani, gari la Mchina linauzwa dola 45,000 lakini linalofanana na hilo la Mjapani au lililotengenezwa Ulaya, linauzwa dola 90,000. Gari hilo la Mchina quarenteed life expectancy yake ni miaka 3 wakati la Mjapani au Mjerumani ni miaka 12.
Hii ina maana annual ownership cost ya gari la Mchina ni dola 15,000 na lile la Mjapani, Mjerumani au Mbelgiji ni dola 7,500. Hapa umeangalia ununuzi pekee, hujajumuisha matatizo mengine kwa gari hilo la Mchina ikiwemo kukosekana kwa huduma kutokana na kuharibika kwa mara kwa mara, gharama za Kisaikolojia, gharama zinazopunguza uzalishaji kutokana na watu kukaa kwa muda mrefu vituoni, usalama wa watu (ukweli ni kuwa mabasi haya ya Mchina usalama wake huwa ni mdogo kutokana na tekinolojia iliyotumika. Tuombe isitokee ajali, ni kama karatasi). Ubora mdogo wa kiusalama ndiyo sababu ya baadhi ya mataifa kuzuia mabasi ya Mchina kutumika kwenye safari ndefu.
Kwa miradi mikubwa ya Serikali, kama mradi wa mabasi yaendayo kasi, ni vema kila kitu kikawa katika viwango vya ubora unaotakiwa, yaani kuanzia mabasi yanayotumika mpaka mpangilio wa utoaji wa huduma yenyewe.
Ni vema kila njia ikawa na kampuni inayojitegemea, Serikali iwe mwangalizi wa ubora huduma wa kila kampuni itakayokuwa imewekeza kwenye kila njia ili pesa hizi za wananchi na mikopo, ziwe na ubora. Serikali itoe mwongozo wa mabasi yanayotakiwa kutumika kwenye njia hizi, na wawekezaji wenye uwezo wajitokeze. Zinatumika pesa nyingi ili kupunguza msongamano wa mabasi lakini uduni wa huduma huleta matokeo hafifu.
Siku za huko nyuma, ilikuwa inajulikana kuwa Serikali hununua wakati wote vifaa vyenye ubora wa hali ya juu. Dar iliwahi kuwa na mabasi maakum ya usafiri wa mjini, mabasi yale ya Ikarus. Hata kwa mwonekano tu yalikuwa ni mabasi yenye ubora wa hali ya juu. Ikarus ilikuwa kampuni ya Hungary, ilikuwa ndiyo kampuni kubwa na bira kuliko zote za magari kwa nchi za Ulaya Mashariki. Yaani hapo zamani, Serikali wakati wote ilikuwa inatafuta kilicho the best.
Ikarus was a bus manufacturer based in Budapest and Székesfehérvár, Hungary. It was established in 1895 as Imre Uhry's Blacksmith Workshop and Coach Factory and during the Communist era in Hungary it dominated bus markets of the entire Eastern Bloc and its allies. Wikipedia
Leo, Serikali nayo inaangukia kwenye ununuzi wa bidhaa hafifu!
Duniani kote inafahamika kuwa bidhaa za China ni aghali kuliko za Taifa lolote ingawa unaponunua zinaonekana ni za bei nafuu kuliko za Taifa lolote.
Mathalani, gari la Mchina linauzwa dola 45,000 lakini linalofanana na hilo la Mjapani au lililotengenezwa Ulaya, linauzwa dola 90,000. Gari hilo la Mchina quarenteed life expectancy yake ni miaka 3 wakati la Mjapani au Mjerumani ni miaka 12.
Hii ina maana annual ownership cost ya gari la Mchina ni dola 15,000 na lile la Mjapani, Mjerumani au Mbelgiji ni dola 7,500. Hapa umeangalia ununuzi pekee, hujajumuisha matatizo mengine kwa gari hilo la Mchina ikiwemo kukosekana kwa huduma kutokana na kuharibika kwa mara kwa mara, gharama za Kisaikolojia, gharama zinazopunguza uzalishaji kutokana na watu kukaa kwa muda mrefu vituoni, usalama wa watu (ukweli ni kuwa mabasi haya ya Mchina usalama wake huwa ni mdogo kutokana na tekinolojia iliyotumika. Tuombe isitokee ajali, ni kama karatasi). Ubora mdogo wa kiusalama ndiyo sababu ya baadhi ya mataifa kuzuia mabasi ya Mchina kutumika kwenye safari ndefu.
Kwa miradi mikubwa ya Serikali, kama mradi wa mabasi yaendayo kasi, ni vema kila kitu kikawa katika viwango vya ubora unaotakiwa, yaani kuanzia mabasi yanayotumika mpaka mpangilio wa utoaji wa huduma yenyewe.
Ni vema kila njia ikawa na kampuni inayojitegemea, Serikali iwe mwangalizi wa ubora huduma wa kila kampuni itakayokuwa imewekeza kwenye kila njia ili pesa hizi za wananchi na mikopo, ziwe na ubora. Serikali itoe mwongozo wa mabasi yanayotakiwa kutumika kwenye njia hizi, na wawekezaji wenye uwezo wajitokeze. Zinatumika pesa nyingi ili kupunguza msongamano wa mabasi lakini uduni wa huduma huleta matokeo hafifu.
Siku za huko nyuma, ilikuwa inajulikana kuwa Serikali hununua wakati wote vifaa vyenye ubora wa hali ya juu. Dar iliwahi kuwa na mabasi maakum ya usafiri wa mjini, mabasi yale ya Ikarus. Hata kwa mwonekano tu yalikuwa ni mabasi yenye ubora wa hali ya juu. Ikarus ilikuwa kampuni ya Hungary, ilikuwa ndiyo kampuni kubwa na bira kuliko zote za magari kwa nchi za Ulaya Mashariki. Yaani hapo zamani, Serikali wakati wote ilikuwa inatafuta kilicho the best.
Ikarus was a bus manufacturer based in Budapest and Székesfehérvár, Hungary. It was established in 1895 as Imre Uhry's Blacksmith Workshop and Coach Factory and during the Communist era in Hungary it dominated bus markets of the entire Eastern Bloc and its allies. Wikipedia
Leo, Serikali nayo inaangukia kwenye ununuzi wa bidhaa hafifu!