Stabilaiza
JF-Expert Member
- Jul 11, 2012
- 1,843
- 1,143
Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania inatamka wazi kuwa mamlaka yote katika nchi yanatoka kwa wananchi. Hivyo sera ya majimbo ya CHADEMA inatekeleza kwa vitendo ushiriki wa wananchi katika utawala.
Kwa kupitia sera ya majimbo ambayo lengo lake ni kuongeza madaraka kwa wananchi katika kusimamia wawakilishi wao na kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo katika eneo husika. Ni vigumu kuona matatizo kwa ukaribu kwa kuongoza kutokea Dar es Slaam. Usimamizi wa raslimali na shughuli za maendelo utakuwa rahisi na hivyo kuimarisha katika yetu ya nchi.
Sera hii ya majimbo pia itaimarisha local governments kwa vile usimamizi wake utakuwa karibu zaidi kuliko kutokea Dar es Salaam. Taasisi mbalimbali katika nchi hii zimegawanya katika maeneo madogo ili kuleta ufanisi na kufanya utekelezaji kuwa rahisi. Mfano wa Taasisi hizi ni Radio Tanzania. Radio Tanzania wana kanda ya mashariki, kanda ya kati, kanda ya kusini, kanda ya magharibi ili kuleta huduma wanazotoa ziwe karibu zaidi na wananchi.
Pia TANESCO imegawanywa katika kanda mbalimbali ziitazo mikoa, ambayo ni tofauti na mikoa ya nchi. Hivyo sera ya majimbo ya CHADEMA inatekeleza kikamilifu matakwa ya katiba ya Tanzania inayohimiza madaraka ya nchi kuwa mikononi mwa umma.
Kwa kupitia sera ya majimbo ambayo lengo lake ni kuongeza madaraka kwa wananchi katika kusimamia wawakilishi wao na kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo katika eneo husika. Ni vigumu kuona matatizo kwa ukaribu kwa kuongoza kutokea Dar es Slaam. Usimamizi wa raslimali na shughuli za maendelo utakuwa rahisi na hivyo kuimarisha katika yetu ya nchi.
Sera hii ya majimbo pia itaimarisha local governments kwa vile usimamizi wake utakuwa karibu zaidi kuliko kutokea Dar es Salaam. Taasisi mbalimbali katika nchi hii zimegawanya katika maeneo madogo ili kuleta ufanisi na kufanya utekelezaji kuwa rahisi. Mfano wa Taasisi hizi ni Radio Tanzania. Radio Tanzania wana kanda ya mashariki, kanda ya kati, kanda ya kusini, kanda ya magharibi ili kuleta huduma wanazotoa ziwe karibu zaidi na wananchi.
Pia TANESCO imegawanywa katika kanda mbalimbali ziitazo mikoa, ambayo ni tofauti na mikoa ya nchi. Hivyo sera ya majimbo ya CHADEMA inatekeleza kikamilifu matakwa ya katiba ya Tanzania inayohimiza madaraka ya nchi kuwa mikononi mwa umma.