Sera ya elimu bure imechangia wanachuo kukosa mkopo

Naja naja

JF-Expert Member
Sep 13, 2016
747
1,452
Sera ya elimu bure kuanzia darasa la kwanza mpaka kidato cha nne imechangia kwa kiasi kikubwa kwa wanavyuo kukosa mkopo

Pesa ambazo zingetumika kugawa mikopo ndo hizo hizo zimegharamia elimu bure ,we jaribu kufikiria mwenyewe Magu ameingia madarakani mwezi November halafu January elimu bure ikaanza rasmi jiulize hizo pesa zimepatikana wapi kama sio hizi hizi za wanavyuo vikuu

Yani ni bora turudi kulekule tulipotoka ambapo elimu ya msingi na sekondari tulikuwa tunalipia lakini wakati huohuo wanafunzi wa vyuo wanapata mkopo kuliko kuwanyima mkopo wanafunzi wa chuo na kuifanya elimu ya msingi na sekondari bure

Gharama za kulipia elimu ya msingi na sekondari ni ndogo kulinganisha na gharama ya chuo

Kutokana na watu kutomudu gharama za chuo wengi wao wanakimbilia kozi za bei rahisi na zenye vipaumbele ya mikopo

Kwa hiyo basi wengi wao wanalazimisha kusoma vitu wasivyoviweza mwisho wa siku wanakuwa watu wa kukariri sana kuliko kuelewa madhara yake inapelekea kuzalisha watalamu feki

Ombi/ushauri:naiomba serikali mara moja waliangalie suala hili kwa jicho la tatu nikimaanisha wafute sera yao ya elimu bure ili ile pesa ambayo ingetumika kugharamia elimu bure wapewe wanafunzi wa vyuo vikuu

Nasema haya kwa kuwa wanafunzi wa vyuo wengi wao hawapati muda wa kukisoma kitu kwa undani kwa kuwa wengi wao wanajigawa nikimaanisha wanasoma wakati huo huo wanatafuta pesa kwa hiyo kwa kuwasaidia kupata pesa inayotosheleza ,itasaidia kuokoa ule muda ambao wangetumia kutafuta pesa kutulia darasani na kusoma

Wengi chuo wanadisco kwa sababu ya mahudhurio afifu yanayosababishwa na utafutaji wa pesa ambao kwa kiasi kikubwa unachangia mtu kukwepa vipindi ili aelekeze nguvu zake kwenye kutafuta pesa
 
ungekuwa ww ungeweza kubadili gia angani au unashauri vitu ambavyo hata kama ungekuwa ww huwez kujaribu
 
Hata sijui sera ya serikali ni ipi sasa na kama ipo je inafuatwa? Mwaka huu tumeona vigezo vya ufaulu vikibadilishwa, vikafuatia vigezo vya kudahiliwa na sasa vigezo vya mikopo. Navigezo vyote hivyo vimebadilishwa wakati michakato ya mitihani, kudahili na sasa kutoa mikopo ikiwa imeanza. Kwa vijana wanasema gia imebadilishwa wakati chombo kiko angani. Kwa style hii huwezi kujua kipi kitatokea kesho-namba inaelekea tumeisoma vibaya na inabidi tuisome tena tuielewe. Nasikia kuna mzee alisema kila mtu abebe mzigo wake-lakini sitaki kuamini kama tumefikia hapo. Wabunge, wanafunzi, wazazi inabidi tupaze sauti vigezo muhimu kwa taifa si haki kuwekwa na watu wachache bila kushirikisha wengine. Huu utembo udhibitiwe.
 
Hata sijui sera ya serikali ni ipi sasa na kama ipo je inafuatwa? Mwaka huu tumeona vigezo vya ufaulu vikibadilishwa, vikafuatia vigezo vya kudahiliwa na sasa vigezo vya mikopo. Navigezo vyote hivyo vimebadilishwa wakati michakato ya mitihani, kudahili na sasa kutoa mikopo ikiwa imeanza. Kwa vijana wanasema gia imebadilishwa wakati chombo kiko angani. Kwa style hii huwezi kujua kipi kitatokea kesho-namba inaelekea tumeisoma vibaya na inabidi tuisome tena tuielewe. Nasikia kuna mzee alisema kila mtu abebe mzigo wake-lakini sitaki kuamini kama tumefikia hapo. Wabunge, wanafunzi, wazazi inabidi tupaze sauti vigezo muhimu kwa taifa si haki kuwekwa na watu wachache bila kushirikisha wengine. Huu utembo udhibitiwe.
nimekuelewa sana, ila c unajua hii ni mahakama ya chui???
 
Back
Top Bottom