Labda niwape kisa hiki cha kweli, kitawasaidia ndugu zangu Waislamu.
Juzi Kanisa katoliki Jimbo la Arusha lilipata dili ya kununua Shule ya Arusha Modern(Ni shule kubwa ya kuanzia Primary hadi A-Level inayokwenda kwa mfumo wa ENGLISH medium) kutoka kwa mmiliki ambaye ni Mwislamu (Wakatoliki wa Arusha wote mnalijua jambo hili kwa usahihi)!
Jamaa akawa anataka Bilioni 4 kama bei, ambapo ni majengo yaliyoko katika space ya eka 9, na eneo la eka 15 open space ambayo haijajengwa, jumla ya eneo ni eka 25.
Walichofanya Mapadre na Askofu Lebulu ni kuitisha sensa ya Wakatoliki wa jimbo la Arusha. Taarifa zikashuka hadi kwenye Jumuia ndogondogo ambapo ndiko ilikoanzia sensa.
Kila paroko akapata idadi ya watu walio katika Parokia yake kutokea kwenye jumuia, na parokia zikawasilisha kwa Askofu, akajumlisha na kujua kwa usahihi kabisa Idadi ya Wakatoliki Jimboni, zoezi lililochukua siku 3 tu.
Baada ya hapo wakagawa hiyo 4bn kwa idadi ya wakatoliki. na kutuletea hesabu kuwa kila mtu achange kiasi gani...kimsingi kila mtu mzima mkatoliki wa Arusha aanachanga elfu 10 kwa mwaka, na mtoto anachanga elfu 5 tu, na ndani ya miaka 2 tutakuwa tumemeliza deni tayari!....ha ha haaa, rahisi mno!
Waislamu mnataka nini zaidi kama si kusababisha machafuko na kuipima nguvu serikali?
OK, Mnataka kujuaidadi yenu, KUNA JAMBO LA MAENDELEO MNATAKA KUFANYA, kama mfano wa hapo juu niliowaletea?