barafu
JF-Expert Member
- Apr 28, 2013
- 6,726
- 32,818
Shule ya Sekondari Isimani imefungwa,hapa ndipo yalipo makao makuu ya Tarafa ya Isimani na ilipokuwa ngome ya Chama cha Mapinduzi.Uchaguzi huu na wimbi la mabadiliko limeipitia mpaka Isimani, Upinzani dhidi ya CCM na makuwadi wake umeshika hatamu.
Mbunge wa miaka 20 mfululizo toka mwaka 1995 anayetafuta ridhaa ya kwenda mwaka wa 25 anakabiliwa na upinzani mkubwa sana.Hali ni tete kwa #WilliamLukuvi na chama cha Mapinduzi.
Wiki iliyopita Lukuvi ameamua kuishinikiza Serikali na mamlaka husika kuifunga Shule ya Sekondari Isimani baada ya walimu na mkuu wake wa shule kukataa kutumika kisiasa kwa kuibeba CCM na walimu wake kutumika kuipigia chapuo CCM na wagombea wake wa ngazi ya Jimbo.Walimu wamekataa kutumika kugawa kofia na T-shirt ili kuhudhuria mikutano ya CCM na kujaza "nyomi" mahali Lukuvi anapohutubia.
Hali hii imefanya mkuu wa Shule ya Sekondari Isimani ndugu AIDAN KAPINGA kuvuliwa ukuu wa shule na "kutupwa" kuwa mwalimu wa kawaida katika shule ya Sekondari LYANDEMBELE huko Ifunda Iringa Vijijini.
Baada ya tukio hilo walimu na wanafunzi waligoma kwa siku kadhaa kushinikiza mwalimu wao mkuu arudishwe sbb anaonewa na hana makosa,hali hiyo ikalazimu Lukuvi aamrishe shule hiyo kufungwa na watoto warudishwe nyumbani bila kujali kuwa Vijana wa kidato cha nne wapo ktk maandalizi ya Mitihani yao ya mwisho ya Taifa.
Mpaka sasa hali si shwari katika eneo la Isimani na Vitongoji vyake.Serikali ya CCM na Lukuvi wasiingize "siasa" katika mambo ya elimu na uhuru wa watu kujiamlia mambo yao,Wananchi wa Isimani wanakabiliwa na matatizo mengi sana. watatumia tukio hili la watoto wao kunyimwa nafasi ya kujiandaa na mitihani kuiadabisha Serikali na chama chake.
William Lukuvi asitumie nguvu kuyazuia mabadiliko bali atumie nguvu kuonyesha maendeleo.Bring back our Children to School
Mbunge wa miaka 20 mfululizo toka mwaka 1995 anayetafuta ridhaa ya kwenda mwaka wa 25 anakabiliwa na upinzani mkubwa sana.Hali ni tete kwa #WilliamLukuvi na chama cha Mapinduzi.
Wiki iliyopita Lukuvi ameamua kuishinikiza Serikali na mamlaka husika kuifunga Shule ya Sekondari Isimani baada ya walimu na mkuu wake wa shule kukataa kutumika kisiasa kwa kuibeba CCM na walimu wake kutumika kuipigia chapuo CCM na wagombea wake wa ngazi ya Jimbo.Walimu wamekataa kutumika kugawa kofia na T-shirt ili kuhudhuria mikutano ya CCM na kujaza "nyomi" mahali Lukuvi anapohutubia.
Hali hii imefanya mkuu wa Shule ya Sekondari Isimani ndugu AIDAN KAPINGA kuvuliwa ukuu wa shule na "kutupwa" kuwa mwalimu wa kawaida katika shule ya Sekondari LYANDEMBELE huko Ifunda Iringa Vijijini.
Baada ya tukio hilo walimu na wanafunzi waligoma kwa siku kadhaa kushinikiza mwalimu wao mkuu arudishwe sbb anaonewa na hana makosa,hali hiyo ikalazimu Lukuvi aamrishe shule hiyo kufungwa na watoto warudishwe nyumbani bila kujali kuwa Vijana wa kidato cha nne wapo ktk maandalizi ya Mitihani yao ya mwisho ya Taifa.
Mpaka sasa hali si shwari katika eneo la Isimani na Vitongoji vyake.Serikali ya CCM na Lukuvi wasiingize "siasa" katika mambo ya elimu na uhuru wa watu kujiamlia mambo yao,Wananchi wa Isimani wanakabiliwa na matatizo mengi sana. watatumia tukio hili la watoto wao kunyimwa nafasi ya kujiandaa na mitihani kuiadabisha Serikali na chama chake.
William Lukuvi asitumie nguvu kuyazuia mabadiliko bali atumie nguvu kuonyesha maendeleo.Bring back our Children to School