Segerea na hatma ya mabadiliko: Siasa uchwara zisitunyime kiongozi bora UKAWA

activist

Senior Member
Jan 3, 2014
151
178
Segerea Na Hatma Ya Mabadiliko: Siasa Maji Taka Zisitukwamishe.

Na Ebenezer Kwayu
Jongea Tanzania

Jimbo la Segerea (Dar es Salaam) lina watia nia zaidi ya 20 wa CHADEMA mpaka sasa. Hii ni kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na uongozi wa chama (kamati tendaji ya Jimbo) kupitia mikutano na waandishi wa habari. Ni jimbo lenye kata 13.

Kati ya hawa watia nia 20, watano (5) ni viongozi wa Jimbo ambao ni wajumbe wa Kamati tendaji ya Jimbo. Hili nililibaini baada ya kufuatilia mwenendo wa chama Segerea kutaka kudadisi sababu za msingi za kutofanyika kwa shughuli za chama.

Kazi za chama na uendeshaji wa chama Segerea umedorora na hii imetokana na uwepo wa mgongano wa maslahi (conflict of interest) miongoni mwa viongozi wa Jimbo hili.

Kutokana na uwepo wa mgongano huu wa maslahi, kumesababisha uwepo wa makundi makuu matatu (3) ya kihasimu.

Kundi la kwanza ni lile linalonasibishwa na viongozi waliopita. Mtakumbuka kwamba baada ya chaguzi za chama za kata na mitaa, uliokuwa unafuata ni uchaguzi wa Jimbo. Lakini Makao Makuu waliengua wagombea waliokuwa wanataka kugombea tena segerea kutokana na kufeli katika ngwe yao ya kwanza ya uongozi. Aliyetaka kugombea nafasi ya Mwenyekiti ni Bw. Mchele.

Bw. Mchele alienguliwa kutokana na kuwa na uhusiano uliokuwa na sura ya hatari kwa chama kati yake na Dr Makongoro Mahanga (Mb) ambaye ndiye mbunge wa sasa wa Segerea kupitia CCM pamoja na Nimrod Mkono mbunge wa Musoma.

Tuhuma alizokuwa nazo ni kuhongwa na Dr Mahanga ili akidhoofishe chama. Lakini pia alihongwa na Nimrod Mkono ili asigombee jimbo la Musoma anakotokea na ambako mbunge wake ni Mzee Nimrod. Na katika harakati zake ndani ya chama kwa sasa, Pesa anazowahonga viongozi wa kata ili wampitishe anazitoa kwa Dr Mahanga na Mzee Nimrod Mkono.

Hii ni kutokana na ukweli kwamba, Mchele ameacha ualimu alikokuwa akifundisha katika shule ya Kristo Mfalme, lakini anazo pesa za kuwahonga viongozi wetu, anayo magari mapya anayonunua mfululizo na pia nyumba amajenga. Lakini pia amejenga shule yake binafsi. Hakuna kazi wala biashara anayoifanya na hakufundisha zaidi ya miaka mitatu alipokuwa Kristo Mfalme. Wala hakuna taarifa zozote kwamba aliwahi kuokota Tanzanite, Dhahabu, almasi wala vito vingine vya thamani. Anafanya tuu hizi siasa za kuunganisha UKAWA na akina Mahanga na Nimrod.

Hisia zimeibuliwa na kumnasibisha Bw. Mchele na u-CCM kwamba anahongwa na rafiki yake Dr Makongoro Mahanga pamoja na Nimrod Mkono. Hii ni kutokana na kuwa na utajiri bila kuwa na chanzo halisi na halali cha mapato (Wealth Without Work).

Pia, Makao Makuu hawakukurupuka kumuengua huyu Bw. Mchele kwa sababu zipo tetesi (zinazoelekea kuwa ukweli) kwamba Bw. Mchele anaandaliwa na Makongoro Mahanga kugombea kupitia ACT kama hatapitishwa na UKAWA kugombea Ubunge Segerea.
Kwa kuoanisha 'dots' utapata picha kwamba huyu anatumika kudhoofisha chama na harakati za mabadilko Segerea.

Ikiwa atapitishwa na UKAWA, atasaliti, asipopata nafasi ya kusaliti, ataasi kwa kwenda ACT ili kugawa kura ambazo zingetiwa katika kapu la UKAWA.

Lakini hawa walioenguliwa ndio waliokuwa wameshasimamia chaguzi za ngazi zote za chini. Hivyo kazi ya kuwapandikiza watu watakaowasapoti ilikuwa imeshakamilika. Kwa tafasiri na kisiri ya moja kwa moja, ni kwamba hawa walioenguliwa wanayo nguvu kwa viongozi wa kata na mitaa wakiwa nje ya uongozi.

Kutokana na hali hii, viongozi wa kata na mitaa wanakahidi kwa makusudi maagizo ya uongozi uliopo kwa sasa. Wanawasikiliza walioenguliwa maana ndio waliowasimamia na pengine kuwapandikiza katika nafasi za uongozi walizonazo.

Kutokana na kasumba hii iliyojijenga na kustawi Segerea, shughuli za uendeshaji wa jimbo zimekwama.

Kundi la pili ni la viongozi waliopo madarakani kwa sasa. Katibu wa sasa (Bw. Anatropia) na Mwenyekiti wa Chama Segerea wa sasa (Bw. Kidera) hawafanyi kazi kwa pamoja. Hawaaminiani. Wote wanatafuta na kuunda mtandao wa kisiasa (polotical network) ili waweze kushinda kura za maoni. Hii imesababisha kazi na shughuli za ujenzi wa chama kusimama na kuzorota.

Lakini pia imesababisha ugomvi mkubwa na kutoelewana miongoni mwa viongozi hawa. Mathalani, katika mkutano mkuu wa kata za Vingunguti na Kiwalani, Mwenyekiti na Katibu wa chama jimbo la Segerea walionekana kugombana hadharani na kupigana mbele ya viongozi wa mitaa waliofika katika mkutano mkuu wa kata hizo uliokuwa umebeba agenda ya uchaguzi katika kata hizi. Hii ilisababisha kushindwa na kuahirisha uchaguzi na kikao kuvurugika. Mpaka ninapoandika andiko hili, chaguzi hazijafanyika katika kata hizi.

Kama hiyo haitoshi, Katibu wa sasa wa Segerea (Bw. Anatropia) ameunda na anaunda mtandao wa kikabila (tribal network aiming at political victory). Anaposimamia chaguzi katika kata kama Katibu wa Jimbo na Kiongozi wa Kamati Tendaji ya Jimbo, anahakikisha anawashawishi wapiga kura (viongozi wa wa chama wa mitaa) kuwachagua Wahaya. Katika kata ambazo uchaguzi umeshafanyika, anatumia agenda ya ukabila kuwapata wahaya wenzake katika jimbo la Segerea.

Kundi la tatu linalohasimiana na makundi mengine ni kundi la watia nia wasiokuwa na Kundi. Hili nalo ni kundi. Hawa wapo katika hawa waliobaki wasiokuwa na hila wala mauzauza ndani ya chama. Hawa wanapata changamoto moja kubwa.

Hawaruhusiwi na uongozi uliopo (Bw. Kidera na Bw. Anatropia) kufanya kazi za chama. Hawashirikishwi katika kazi yoyote kwa hofu ya kueleweka kwa wapiga kura kuliko wao, (ikitokea kazi ya chama mara moja moja).
Hawa wapo zaidi ya 15. Si viongozi wa Jimbo. Wengine katika hawa pia si viongozi kabisa ndani ya Chama.
Ninaamini hapa ndipo alipo Mbunge wa Segerea mwenye uwezo kusimama kidete dhidi ya huu mfumo wa CCM wa 'Mangi meza'. Wanaopambana na kupigana hadharani mbele ya wanachama na wananchi hawatapewa ridhaa kuongoza Segerea na kuiwakilisha mjini Dodoma.

Wakati Makao Makuu wakitoa tamko na kupuliza kipenga cha kuchukua fomu za kuwania udiwani na Ubunge katika ngazi za kata na Majimbo mbalimbali nchini kuanzia tarehe 18.05.2015 hadi tarehe 20.06.2015, Uongozi wa Jimbo la Segerea haujafanya chaguzi za viongozi wa kata katika kata Sita (6) mpaka sasa ninapoandika makala haya.

Sababu kuu za msingi ziko mbili, kwanza ni uwepo wa makundi haya ya akina Bw. Mchele, Bw. Kidera na Bw. Anatropia. Msuguano unasababisha shuguli za ujenzi wa chama kusimama. Mlolongo (bureaucracy) wa kufanya uchaguzi umefanywa mgumu (complicated) kutokana na mgongano wa maslahi.

Kutokana na kutoaminiana kwa hawa 'mafahali walio hodhi chama', Kwa sasa hakuna mjumbe wa kamati tendaji anayeruhusiwa kwenda peke yake au wawili, watatu katika kata kusimamia uchaguzi wa Viongozi kule. Wanakwenda wajumbe wote wa kamati tendaji ya jimbo. Akikosekana mmoja au wawili (bahati mbaya awe ni mtia nia), kazi zinasimama.

Mwenyekiti wa sasa wa Jimbo (Bw. Kidera) anatuhumiwa kutumia mabavu, akili ndogo na hamasa za lazima kuwaongoza viongozi wenzake wa Kamati Tendaji na Kata za Jimbo. Ugomvi usioisha katika jimbo baina ya viongozi, ngumi mkononi ni tabia ya kipekee ya Mwenyekiti wetu Bw. Kidera.

Kuthibitisha hili, katika chaguzi katika kata za Bonyokwa, Kinyerezi na Kisukuru (anakotokea Bw. Kidera), Kidera alipigana ngumi katika chaguzi hizi kutokana na mgongano wa maslahi miongoni mwa kundi lake na 'Mabwana wakubwa' wengine.

Sababu ya pili ya kushindwa (fail) au kuchelewa kwenye sura ya kushindwa (delay) kufanya chaguzi katika kata hizi sita ni Kufutwa kwa chaguzi zilizofanyika katika baadhi ya kata.

Hii ni kutokana na kambi za viongozi wa sasa kushindwa katika chaguzi hizo. Kata za Liwiti na Kiwalani (ambako ngumi zilipigwa kama nilivyoeleza awali kabisa kati ya katibu na Mwenyekiti ) ni miongoni mwa kata ambazo matokeo yake yamefutwa kutokana na kushindwa kwa kambi hizi mbili zinazohodhi kamati tendaji ya Jimbo la Segerea. Kambi iliyokuwa imeshinda ni ya Mwenyekiti wa Zamani Bw. Mchele kutokana na rushwa kuzidi akina Kidera.

Jimbo la Segera lina kata kumi na tatu (13). Katika kata hizi, ni kata saba (7) tu zimekwisha fanya chaguzi za uongozzli wa chama. Kata sita (6) hazijafanya chaguzi. Kwa tafsiri hiyo, hatuna kamati tendaji katika Kata sita. Hatuna viongozi wa kusimamia mchakato wa upatikanaji wa madiwani.katika kata sita.

Kwa kunasibisha hoja hii na hatma ya chama na matamanio yake, kitakwimu, ni kwamba 46.2% ya kata za Jimbo la Segerea haina uongozi, 53.8% ya kata za jimbo ndiyo yenye uongozi kamili wa chama. Kiulinganishi, nusu ya jimbo haina uongozi. Kwa hoja hii, hata viongozi wa Jimbo walioko hawana sifa za kikatiba (katiba ya chama) za kuendelea kuwa viongozi.

Ni vizuri sasa Kamanda Mabere Marando (Mwenyekiti Wa CHADEMA Kanda) ukajiridhisha mwenyewe kwa uozo ulioko Segerea na umazwazwa unaoendelea kufanyika. Wananchi wa Segerea wako tayari kwa mabadiliko. Wako tayari kuyafanya na kuyagharamia. Tusiwakatishe tamaa watu hawa. Tuwape kiongozi anaefaa. Tuwape mtetezi wa Maslahi, haki na matamanio yao ambaye wamekuwa wakimsubiri kwa zaidi ya nusu karne sasa.

Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki UKAWA, Ibariki CHADEMA.

Nawasilisha.

Cc:
1. Mabere Marando - Mwenyekiti Kanda

2. Dr Willbroad Slaa -Katibu Mkuu Taifa

3. Kamati Tendaji Segerea - Kwa Taarifa.
 
Segerea Na Hatma Ya Mabadiliko: Siasa Maji Taka Zisitukwamishe.

Na Ebenezer Kwayu
Jongea Tanzania

Jimbo la Segerea (Dar es Salaam) lina watia nia zaidi ya 20 wa CHADEMA mpaka sasa. Hii ni kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na uongozi wa chama (kamati tendaji ya Jimbo) kupitia mikutano na waandishi wa habari. Ni jimbo lenye kata 13.

Kati ya hawa watia nia 20, watano (5) ni viongozi wa Jimbo ambao ni wajumbe wa Kamati tendaji ya Jimbo. Hili nililibaini baada ya kufuatilia mwenendo wa chama Segerea kutaka kudadisi sababu za msingi za kutofanyika kwa shughuli za chama.

Kazi za chama na uendeshaji wa chama Segerea umedorora na hii imetokana na uwepo wa mgongano wa maslahi (conflict of interest) miongoni mwa viongozi wa Jimbo hili.

Kutokana na uwepo wa mgongano huu wa maslahi, kumesababisha uwepo wa makundi makuu matatu (3) ya kihasimu.

Kundi la kwanza ni lile linalonasibishwa na viongozi waliopita. Mtakumbuka kwamba baada ya chaguzi za chama za kata na mitaa, uliokuwa unafuata ni uchaguzi wa Jimbo. Lakini Makao Makuu waliengua wagombea waliokuwa wanataka kugombea tena segerea kutokana na kufeli katika ngwe yao ya kwanza ya uongozi. Aliyetaka kugombea nafasi ya Mwenyekiti ni Bw. Mchele.

Bw. Mchele alienguliwa kutokana na kuwa na uhusiano uliokuwa na sura ya hatari kwa chama kati yake na Dr Makongoro Mahanga (Mb) ambaye ndiye mbunge wa sasa wa Segerea kupitia CCM pamoja na Nimrod Mkono mbunge wa Musoma.

Tuhuma alizokuwa nazo ni kuhongwa na Dr Mahanga ili akidhoofishe chama. Lakini pia alihongwa na Nimrod Mkono ili asigombee jimbo la Musoma anakotokea na ambako mbunge wake ni Mzee Nimrod. Na katika harakati zake ndani ya chama kwa sasa, Pesa anazowahonga viongozi wa kata ili wampitishe anazitoa kwa Dr Mahanga na Mzee Nimrod Mkono.

Hii ni kutokana na ukweli kwamba, Mchele ameacha ualimu alikokuwa akifundisha katika shule ya Kristo Mfalme, lakini anazo pesa za kuwahonga viongozi wetu, anayo magari mapya anayonunua mfululizo na pia nyumba amajenga. Lakini pia amejenga shule yake binafsi. Hakuna kazi wala biashara anayoifanya na hakufundisha zaidi ya miaka mitatu alipokuwa Kristo Mfalme. Wala hakuna taarifa zozote kwamba aliwahi kuokota Tanzanite, Dhahabu, almasi wala vito vingine vya thamani. Anafanya tuu hizi siasa za kuunganisha UKAWA na akina Mahanga na Nimrod.

Hisia zimeibuliwa na kumnasibisha Bw. Mchele na u-CCM kwamba anahongwa na rafiki yake Dr Makongoro Mahanga pamoja na Nimrod Mkono. Hii ni kutokana na kuwa na utajiri bila kuwa na chanzo halisi na halali cha mapato (Wealth Without Work).

Pia, Makao Makuu hawakukurupuka kumuengua huyu Bw. Mchele kwa sababu zipo tetesi (zinazoelekea kuwa ukweli) kwamba Bw. Mchele anaandaliwa na Makongoro Mahanga kugombea kupitia ACT kama hatapitishwa na UKAWA kugombea Ubunge Segerea.
Kwa kuoanisha 'dots' utapata picha kwamba huyu anatumika kudhoofisha chama na harakati za mabadilko Segerea.

Ikiwa atapitishwa na UKAWA, atasaliti, asipopata nafasi ya kusaliti, ataasi kwa kwenda ACT ili kugawa kura ambazo zingetiwa katika kapu la UKAWA.

Lakini hawa walioenguliwa ndio waliokuwa wameshasimamia chaguzi za ngazi zote za chini. Hivyo kazi ya kuwapandikiza watu watakaowasapoti ilikuwa imeshakamilika. Kwa tafasiri na kisiri ya moja kwa moja, ni kwamba hawa walioenguliwa wanayo nguvu kwa viongozi wa kata na mitaa wakiwa nje ya uongozi.

Kutokana na hali hii, viongozi wa kata na mitaa wanakahidi kwa makusudi maagizo ya uongozi uliopo kwa sasa. Wanawasikiliza walioenguliwa maana ndio waliowasimamia na pengine kuwapandikiza katika nafasi za uongozi walizonazo.

Kutokana na kasumba hii iliyojijenga na kustawi Segerea, shughuli za uendeshaji wa jimbo zimekwama.

Kundi la pili ni la viongozi waliopo madarakani kwa sasa. Katibu wa sasa (Bw. Anatropia) na Mwenyekiti wa Chama Segerea wa sasa (Bw. Kidera) hawafanyi kazi kwa pamoja. Hawaaminiani. Wote wanatafuta na kuunda mtandao wa kisiasa (polotical network) ili waweze kushinda kura za maoni. Hii imesababisha kazi na shughuli za ujenzi wa chama kusimama na kuzorota.

Lakini pia imesababisha ugomvi mkubwa na kutoelewana miongoni mwa viongozi hawa. Mathalani, katika mkutano mkuu wa kata za Vingunguti na Kiwalani, Mwenyekiti na Katibu wa chama jimbo la Segerea walionekana kugombana hadharani na kupigana mbele ya viongozi wa mitaa waliofika katika mkutano mkuu wa kata hizo uliokuwa umebeba agenda ya uchaguzi katika kata hizi. Hii ilisababisha kushindwa na kuahirisha uchaguzi na kikao kuvurugika. Mpaka ninapoandika andiko hili, chaguzi hazijafanyika katika kata hizi.

Kama hiyo haitoshi, Katibu wa sasa wa Segerea (Bw. Anatropia) ameunda na anaunda mtandao wa kikabila (tribal network aiming at political victory). Anaposimamia chaguzi katika kata kama Katibu wa Jimbo na Kiongozi wa Kamati Tendaji ya Jimbo, anahakikisha anawashawishi wapiga kura (viongozi wa wa chama wa mitaa) kuwachagua Wahaya. Katika kata ambazo uchaguzi umeshafanyika, anatumia agenda ya ukabila kuwapata wahaya wenzake katika jimbo la Segerea.

Kundi la tatu linalohasimiana na makundi mengine ni kundi la watia nia wasiokuwa na Kundi. Hili nalo ni kundi. Hawa wapo katika hawa waliobaki wasiokuwa na hila wala mauzauza ndani ya chama. Hawa wanapata changamoto moja kubwa.

Hawaruhusiwi na uongozi uliopo (Bw. Kidera na Bw. Anatropia) kufanya kazi za chama. Hawashirikishwi katika kazi yoyote kwa hofu ya kueleweka kwa wapiga kura kuliko wao, (ikitokea kazi ya chama mara moja moja).
Hawa wapo zaidi ya 15. Si viongozi wa Jimbo. Wengine katika hawa pia si viongozi kabisa ndani ya Chama.
Ninaamini hapa ndipo alipo Mbunge wa Segerea mwenye uwezo kusimama kidete dhidi ya huu mfumo wa CCM wa 'Mangi meza'. Wanaopambana na kupigana hadharani mbele ya wanachama na wananchi hawatapewa ridhaa kuongoza Segerea na kuiwakilisha mjini Dodoma.

Wakati Makao Makuu wakitoa tamko na kupuliza kipenga cha kuchukua fomu za kuwania udiwani na Ubunge katika ngazi za kata na Majimbo mbalimbali nchini kuanzia tarehe 18.05.2015 hadi tarehe 20.06.2015, Uongozi wa Jimbo la Segerea haujafanya chaguzi za viongozi wa kata katika kata Sita (6) mpaka sasa ninapoandika makala haya.

Sababu kuu za msingi ziko mbili, kwanza ni uwepo wa makundi haya ya akina Bw. Mchele, Bw. Kidera na Bw. Anatropia. Msuguano unasababisha shuguli za ujenzi wa chama kusimama. Mlolongo (bureaucracy) wa kufanya uchaguzi umefanywa mgumu (complicated) kutokana na mgongano wa maslahi.

Kutokana na kutoaminiana kwa hawa 'mafahali walio hodhi chama', Kwa sasa hakuna mjumbe wa kamati tendaji anayeruhusiwa kwenda peke yake au wawili, watatu katika kata kusimamia uchaguzi wa Viongozi kule. Wanakwenda wajumbe wote wa kamati tendaji ya jimbo. Akikosekana mmoja au wawili (bahati mbaya awe ni mtia nia), kazi zinasimama.

Mwenyekiti wa sasa wa Jimbo (Bw. Kidera) anatuhumiwa kutumia mabavu, akili ndogo na hamasa za lazima kuwaongoza viongozi wenzake wa Kamati Tendaji na Kata za Jimbo. Ugomvi usioisha katika jimbo baina ya viongozi, ngumi mkononi ni tabia ya kipekee ya Mwenyekiti wetu Bw. Kidera.

Kuthibitisha hili, katika chaguzi katika kata za Bonyokwa, Kinyerezi na Kisukuru (anakotokea Bw. Kidera), Kidera alipigana ngumi katika chaguzi hizi kutokana na mgongano wa maslahi miongoni mwa kundi lake na 'Mabwana wakubwa' wengine.

Sababu ya pili ya kushindwa (fail) au kuchelewa kwenye sura ya kushindwa (delay) kufanya chaguzi katika kata hizi sita ni Kufutwa kwa chaguzi zilizofanyika katika baadhi ya kata.

Hii ni kutokana na kambi za viongozi wa sasa kushindwa katika chaguzi hizo. Kata za Liwiti na Kiwalani (ambako ngumi zilipigwa kama nilivyoeleza awali kabisa kati ya katibu na Mwenyekiti ) ni miongoni mwa kata ambazo matokeo yake yamefutwa kutokana na kushindwa kwa kambi hizi mbili zinazohodhi kamati tendaji ya Jimbo la Segerea. Kambi iliyokuwa imeshinda ni ya Mwenyekiti wa Zamani Bw. Mchele kutokana na rushwa kuzidi akina Kidera.

Jimbo la Segera lina kata kumi na tatu (13). Katika kata hizi, ni kata saba (7) tu zimekwisha fanya chaguzi za uongozzli wa chama. Kata sita (6) hazijafanya chaguzi. Kwa tafsiri hiyo, hatuna kamati tendaji katika Kata sita. Hatuna viongozi wa kusimamia mchakato wa upatikanaji wa madiwani.katika kata sita.

Kwa kunasibisha hoja hii na hatma ya chama na matamanio yake, kitakwimu, ni kwamba 46.2% ya kata za Jimbo la Segerea haina uongozi, 53.8% ya kata za jimbo ndiyo yenye uongozi kamili wa chama. Kiulinganishi, nusu ya jimbo haina uongozi. Kwa hoja hii, hata viongozi wa Jimbo walioko hawana sifa za kikatiba (katiba ya chama) za kuendelea kuwa viongozi.

Ni vizuri sasa Kamanda Mabere Marando (Mwenyekiti Wa CHADEMA Kanda) ukajiridhisha mwenyewe kwa uozo ulioko Segerea na umazwazwa unaoendelea kufanyika. Wananchi wa Segerea wako tayari kwa mabadiliko. Wako tayari kuyafanya na kuyagharamia. Tusiwakatishe tamaa watu hawa. Tuwape kiongozi anaefaa. Tuwape mtetezi wa Maslahi, haki na matamanio yao ambaye wamekuwa wakimsubiri kwa zaidi ya nusu karne sasa.

Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki UKAWA, Ibariki CHADEMA.

Nawasilisha.

Cc:
1. Mabere Marando - Mwenyekiti Kanda

2. Dr Willbroad Slaa -Katibu Mkuu Taifa

3. Kamati Tendaji Segerea - Kwa Taarifa.

sio siri segerea ni shidaa, viongozi wa cdm segerea wana uchu wa madaraka kazi kutengeneza makundi ndani ya chama, halafu hata chama chenyewe hawajakipigania kivilee kazi kuvaa magwanda tu na kuja kwenye vikao na kusema peopleees wkt mzigo wa kuimarisha chama hawafanyi. Hakuna mikutano ya kuhamasisha wanachi yaani mpaka uje uchaguzi.
 
sio siri segerea ni shidaa, viongozi wa cdm segerea wana uchu wa madaraka kazi kutengeneza makundi ndani ya chama, halafu hata chama chenyewe hawajakipigania kivilee kazi kuvaa magwanda tu na kuja kwenye vikao na kusema peopleees wkt mzigo wa kuimarisha chama hawafanyi. Hakuna mikutano ya kuhamasisha wanachi yaani mpaka uje uchaguzi.
wasegerea wanajuta kuchezea kura zao
 
SEGEREA NA HATMA YA MABADILIKO:- SIASA MAJI ZISITUKWAMISHE.

Na Ebenezer Kwayu+255764013330

Jimbo la Segerea (Dar esSalaam) lina watia nia zaidi ya 20 wa CHADEMA mpaka sasa. Hii ni kwa mujibu watakwimu zilizotolewa na uongozi wa chama (kamati tendaji ya Jimbo) kupitiamikutano na waandishi wa habari. Ni jimbo lenye kata 13.

Kati ya hawa watia nia 20,watano (5) ni viongozi wa Jimbo ambao ni wajumbe wa Kamati tendaji ya Jimbo.Hili nililibaini baada ya kufuatilia mwenendo wa chama Segerea kutaka kudadisisababu za msingi za kutofanyika kwa shughuli za chama.

Kazi za chama na uendeshaji wa chama Segereaumedorora na hii imetokana na uwepo wa mgongano wa maslahi (conflict ofinterest) miongoni mwa viongozi wa Jimbo hili.

Kutokana na uwepo wa mgonganohuu wa maslahi, kumesababisha uwepo wa makundi makuu matatu (3) ya kihasimu.

Kundi la kwanza ni lilelinalonasibishwa na viongozi waliopita. Mtakumbuka kwamba baada ya chaguzi zachama za kata na mitaa, uliokuwa unafuata ni uchaguzi wa Jimbo. Lakini MakaoMakuu waliengua wagombea waliokuwa wanataka kugombea tena segerea kutokana nakufeli katika ngwe yao ya kwanza ya uongozi. Aliyetaka kugombea nafasi yaMwenyekiti ni Bw. Mchele.

Bw. Mchele alienguliwakutokana na kuwa na uhusiano uliokuwa na sura ya hatari kwa chama kati yake naDr Makongoro Mahanga (Mb) ambaye ndiye mbunge wa sasa wa Segerea kupitia CCMpamoja na Nimrod Mkono mbunge wa Musoma.

Tuhuma alizokuwa nazo nikuhongwa na Dr Mahanga ili akidhoofishechama. Lakini pia alihongwa na Nimrod Mkono ili asigombee jimbo la Musomaanakotokea na ambako mbunge wake ni Mzee Nimrod. Na katika harakati zake ndaniya chama kwasasa, Pesa anazowahongaviongozi wa kata ili wampitishe anazitoa kwa Dr Mahanga na Mzee Nimrod Mkono.

Hii ni kutokana na ukweli kwamba, Mcheleameacha ualimu alikokuwa akifundisha katika shule ya Kristo Mfalme, lakinianazo pesa za kuwahonga viongozi wetu, anayo magari mapya anayonunua mfululizona pia nyumba amajenga. Lakini pia amejenga shule yake binafsi. Hakuna kaziwala biashara anayoifanya na hakufundisha zaidi ya miaka mitatu alipokuwaKristo Mfalme. Wala hakuna taarifa zozote kwamba aliwahi kuokota Tanzanite,Dhahabu, almasi wala vito vingine vya thamani. Anafanya tuu hizi siasa zakuunganisha UKAWA na akina Mahanga na Nimrod.

Hisia zimeibuliwa nakumnasibisha Bw. Mchele na u-CCM kwamba anahongwa na rafiki yake Dr MakongoroMahanga pamoja na Nimrod Mkono. Hii ni kutokana na kuwa na utajiri bila kuwa nachanzo halisi na halali cha mapato (Wealth Without Work).

Pia, Makao Makuuhawakukurupuka kumuengua huyu Bw. Mchele kwa sababu zipo tetesi (zinazoelekeakuwa ukweli) kwamba Bw. Mchele anaandaliwa na Makongoro Mahanga kugombeakupitia ACT kama hatapitishwa na UKAWA kugombea Ubunge Segerea.
Kwa kuoanisha 'dots' utapatapicha kwamba huyu anatumika kudhoofisha chama na harakati za mabadilko Segerea.

Ikiwa atapitishwa na UKAWA, atasaliti,asipopata nafasi ya kusaliti, ataasi kwa kwenda ACT ili kugawa kura ambazozingetiwa katika kapu la UKAWA.

Lakini hawa walioenguliwandio waliokuwa wameshasimamia chaguzi za ngazi zote za chini. Hivyo kazi yakuwapandikiza watu watakaowasapoti ilikuwa imeshakamilika. Kwa tafasiri nakisiri ya moja kwa moja, ni kwamba hawa walioenguliwa wanayo nguvu kwa viongoziwa kata na mitaawakiwa nje ya uongozi.

Kutokana na hali hii,viongozi wa kata na mitaa wanakahidi kwa makusudi maagizo ya uongozi uliopo kwasasa. Wanawasikiliza walioenguliwa maana ndio waliowasimamia na penginekuwapandikiza katika nafasi za uongozi walizonazo.

Kutokana na kasumba hiiiliyojijenga na kustawi Segerea, shughuli za uendeshaji wa jimbo zimekwama.

Kundi la pili ni la viongoziwaliopo madarakani kwa sasa. Katibu wa sasa (Bw. Anatropia)na Mwenyekiti wa Chama Segerea wa sasa (Bw.Kidera) hawafanyi kazi kwa pamoja. Hawaaminiani. Wote wanatafuta na kuundamtandao wa kisiasa (polotical network) ili waweze kushinda kura za maoni. Hiiimesababisha kazi na shughuli za ujenzi wa chama kusimama na kuzorota.

Lakini pia imesababishaugomvi mkubwa na kutoelewana miongoni mwa viongozi hawa. Mathalani, katikamkutano mkuu wa kata za Vingunguti na Kiwalani, Mwenyekiti na Katibu wa chamajimbo la Segereawalionekana kugombanahadharani na kupigana mbele ya viongozi wa mitaa waliofika katika mkutano mkuuwa kata hizo uliokuwa umebeba agenda ya uchaguzi katika kata hizi. Hiiilisababisha kushindwa na kuahirisha uchaguzi na kikao kuvurugika. Mpakaninapoandika andiko hili, chaguzi hazijafanyika katika kata hizi.

Kama hiyo haitoshi, Katibu wasasa wa Segerea (Bw. Anatropia) ameunda na anaunda mtandao wa kikabila (tribalnetwork aiming at political victory). Anaposimamia chaguzi katika kata kamaKatibu wa Jimbo na Kiongozi wa Kamati Tendaji ya Jimbo, anahakikishaanawashawishi wapiga kura (viongozi wa wa chama wa mitaa) kuwachagua Wahaya.Katika kata ambazo uchaguzi umeshafanyika, anatumia agenda ya ukabila kuwapatawahaya wenzake katika jimbo la Segerea.

Kundi la tatu linalohasimianana makundi mengine ni kundi la watia nia wasiokuwa na Kundi. Hili nalo ni kundi.Hawa wapo katika hawa waliobaki wasiokuwa na hila wala mauzauza ndani ya chama.Hawa wanapata changamoto moja kubwa.

Hawaruhusiwi na uongoziuliopo (Bw. Kidera na Bw. Anatropia) kufanya kazi za chama. Hawashirikishwikatika kazi yoyote kwa hofu ya kueleweka kwa wapiga kura kuliko wao, (ikitokeakazi ya chamamara moja moja).
Hawa wapo zaidi ya 15. Siviongozi wa Jimbo. Wengine katika hawa pia si viongozi kabisa ndani ya Chama.
Ninaamini hapa ndipo alipoMbunge wa Segerea mwenye uwezo kusimama kidete dhidi ya huu mfumo wa CCM wa'Mangi meza'. Wanaopambana na kupigana hadharani mbele ya wanachama na wananchihawatapewa ridhaa kuongoza Segerea na kuiwakilisha mjini Dodoma.

Wakati Makao Makuu wakitoatamko na kupuliza kipenga cha kuchukua fomu za kuwania udiwani na Ubunge katikangazi za kata na Majimbo mbalimbali nchini kuanzia tarehe 18.05.2015 haditarehe 20.06.2015, Uongozi wa Jimbo la Segerea haujafanya chaguzi za viongoziwa kata katika kata Sita (6) mpaka sasa ninapoandika makala haya.

Sababu kuu za msingi zikombili, kwanza ni uwepo wa makundi haya ya akina Bw. Mchele, Bw. Kidera na Bw.Anatropia. Msuguano unasababisha shuguli za ujenzi wa chama kusimama. Mlolongo(bureaucracy) wa kufanya uchaguzi umefanywa mgumu (complicated) kutokana namgongano wa maslahi.

Kutokana na kutoaminiana kwa hawa 'mafahaliwalio hodhi chama', Kwa sasahakunamjumbe wa kamati tendaji anayeruhusiwa kwenda peke yake au wawili, watatukatika kata kusimamia uchaguzi wa Viongozi kule. Wanakwenda wajumbe wotewakamati tendaji ya jimbo. Akikosekanammoja au wawili (bahati mbaya awe ni mtia nia), kazi zinasimama.

Mwenyekiti wa sasa wa Jimbo(Bw. Kidera) anatuhumiwa kutumia mabavu, akili ndogo na hamasa za lazimakuwaongoza viongozi wenzake wa Kamati Tendaji na Kata za Jimbo. Ugomvi usioishakatika jimbo baina ya viongozi, ngumi mkononi ni tabia ya kipekee ya Mwenyekitiwetu Bw. Kidera.

Kuthibitisha hili, katikachaguzi katika kata za Bonyokwa, Kinyerezi na Kisukuru (anakotokea Bw. Kidera),Kidera alipigana ngumi katika chaguzi hizi kutokana na mgongano wa maslahimiongoni mwa kundi lake na 'Mabwana wakubwa'wengine.

Sababu ya pili ya kushindwa(fail) au kuchelewa kwenye sura ya kushindwa (delay) kufanya chaguzi katikakata hizi sita ni Kufutwa kwa chaguzi zilizofanyika katika baadhi ya kata.

Hii ni kutokana na kambi zaviongozi wa sasa kushindwa katika chaguzi hizo. Kata za Liwiti na Kiwalani(ambako ngumi zilipigwa kama nilivyoeleza awali kabisa kati ya katibu naMwenyekiti ) ni miongoni mwa kata ambazo matokeo yake yamefutwa kutokana nakushindwa kwa kambi hizi mbili zinazohodhi kamati tendaji ya Jimbo la Segerea.Kambi iliyokuwa imeshinda ni ya Mwenyekiti wa Zamani Bw. Mchele kutokana narushwa kuzidi akina Kidera.

Jimbo la Segera lina katakumi na tatu (13). Katika kata hizi, ni kata saba (7) tu zimekwisha fanyachaguzi za uongozzli wa chama. Kata sita (6) hazijafanya chaguzi. Kwa tafsirihiyo, hatuna kamati tendaji katika Kata sita. Hatuna viongozi wa kusimamiamchakato wa upatikanaji wa madiwani.katika kata sita.

Kwa kunasibisha hoja hii nahatma ya chama na matamanio yake, kitakwimu, ni kwamba 46.2% ya kata za Jimbola Segerea haina uongozi, 53.8% ya kata za jimbo ndiyo yenye uongozi kamili wachama. Kiulinganishi, nusu ya jimbo haina uongozi. Kwa hoja hii, hata viongoziwa Jimbo walioko hawana sifa za kikatiba (katiba ya chama) za kuendelea kuwaviongozi.

Ni vizuri sasa Kamanda MabereMarando (Mwenyekiti Wa CHADEMA Kanda) ukajiridhisha mwenyewe kwa uozo uliokoSegerea na umazwazwa unaoendelea kufanyika. Wananchi wa Segerea wako tayari kwamabadiliko. Wako tayari kuyafanya na kuyagharamia. Tusiwakatishe tamaa watuhawa. Tuwape kiongozi anaefaa. Tuwape mtetezi wa Maslahi, haki na matamanio yaoambaye wamekuwa wakimsubiri kwa zaidi ya nusu karne sasa.

Mungu Ibariki Tanzania, MunguIbariki UKAWA, Ibariki CHADEMA.

Nawasilisha.

Cc:
1. Mabere Marando -Mwenyekiti Kanda

2. Dr Willbroad Slaa -KatibuMkuu Taifa

3. Kamati Tendaji Segerea -Kwa Taarifa.
 
SEGEREA NA HATMA YA MABADILIKO:- SIASA MAJI ZISITUKWAMISHE.

Na Ebenezer Kwayu+255764013330

Jimbo la Segerea (Dar esSalaam) lina watia nia zaidi ya 20 wa CHADEMA mpaka sasa. Hii ni kwa mujibu watakwimu zilizotolewa na uongozi wa chama (kamati tendaji ya Jimbo) kupitiamikutano na waandishi wa habari. Ni jimbo lenye kata 13.

Kati ya hawa watia nia 20,watano (5) ni viongozi wa Jimbo ambao ni wajumbe wa Kamati tendaji ya Jimbo.Hili nililibaini baada ya kufuatilia mwenendo wa chama Segerea kutaka kudadisisababu za msingi za kutofanyika kwa shughuli za chama.

Kazi za chama na uendeshaji wa chama Segereaumedorora na hii imetokana na uwepo wa mgongano wa maslahi (conflict ofinterest) miongoni mwa viongozi wa Jimbo hili.

Kutokana na uwepo wa mgonganohuu wa maslahi, kumesababisha uwepo wa makundi makuu matatu (3) ya kihasimu.

Kundi la kwanza ni lilelinalonasibishwa na viongozi waliopita. Mtakumbuka kwamba baada ya chaguzi zachama za kata na mitaa, uliokuwa unafuata ni uchaguzi wa Jimbo. Lakini MakaoMakuu waliengua wagombea waliokuwa wanataka kugombea tena segerea kutokana nakufeli katika ngwe yao ya kwanza ya uongozi. Aliyetaka kugombea nafasi yaMwenyekiti ni Bw. Mchele.

Bw. Mchele alienguliwakutokana na kuwa na uhusiano uliokuwa na sura ya hatari kwa chama kati yake naDr Makongoro Mahanga (Mb) ambaye ndiye mbunge wa sasa wa Segerea kupitia CCMpamoja na Nimrod Mkono mbunge wa Musoma.

Tuhuma alizokuwa nazo nikuhongwa na Dr Mahanga ili akidhoofishechama. Lakini pia alihongwa na Nimrod Mkono ili asigombee jimbo la Musomaanakotokea na ambako mbunge wake ni Mzee Nimrod. Na katika harakati zake ndaniya chama kwasasa, Pesa anazowahongaviongozi wa kata ili wampitishe anazitoa kwa Dr Mahanga na Mzee Nimrod Mkono.

Hii ni kutokana na ukweli kwamba, Mcheleameacha ualimu alikokuwa akifundisha katika shule ya Kristo Mfalme, lakinianazo pesa za kuwahonga viongozi wetu, anayo magari mapya anayonunua mfululizona pia nyumba amajenga. Lakini pia amejenga shule yake binafsi. Hakuna kaziwala biashara anayoifanya na hakufundisha zaidi ya miaka mitatu alipokuwaKristo Mfalme. Wala hakuna taarifa zozote kwamba aliwahi kuokota Tanzanite,Dhahabu, almasi wala vito vingine vya thamani. Anafanya tuu hizi siasa zakuunganisha UKAWA na akina Mahanga na Nimrod.

Hisia zimeibuliwa nakumnasibisha Bw. Mchele na u-CCM kwamba anahongwa na rafiki yake Dr MakongoroMahanga pamoja na Nimrod Mkono. Hii ni kutokana na kuwa na utajiri bila kuwa nachanzo halisi na halali cha mapato (Wealth Without Work).

Pia, Makao Makuuhawakukurupuka kumuengua huyu Bw. Mchele kwa sababu zipo tetesi (zinazoelekeakuwa ukweli) kwamba Bw. Mchele anaandaliwa na Makongoro Mahanga kugombeakupitia ACT kama hatapitishwa na UKAWA kugombea Ubunge Segerea.
Kwa kuoanisha 'dots' utapatapicha kwamba huyu anatumika kudhoofisha chama na harakati za mabadilko Segerea.

Ikiwa atapitishwa na UKAWA, atasaliti,asipopata nafasi ya kusaliti, ataasi kwa kwenda ACT ili kugawa kura ambazozingetiwa katika kapu la UKAWA.

Lakini hawa walioenguliwandio waliokuwa wameshasimamia chaguzi za ngazi zote za chini. Hivyo kazi yakuwapandikiza watu watakaowasapoti ilikuwa imeshakamilika. Kwa tafasiri nakisiri ya moja kwa moja, ni kwamba hawa walioenguliwa wanayo nguvu kwa viongoziwa kata na mitaawakiwa nje ya uongozi.

Kutokana na hali hii,viongozi wa kata na mitaa wanakahidi kwa makusudi maagizo ya uongozi uliopo kwasasa. Wanawasikiliza walioenguliwa maana ndio waliowasimamia na penginekuwapandikiza katika nafasi za uongozi walizonazo.

Kutokana na kasumba hiiiliyojijenga na kustawi Segerea, shughuli za uendeshaji wa jimbo zimekwama.

Kundi la pili ni la viongoziwaliopo madarakani kwa sasa. Katibu wa sasa (Bw. Anatropia)na Mwenyekiti wa Chama Segerea wa sasa (Bw.Kidera) hawafanyi kazi kwa pamoja. Hawaaminiani. Wote wanatafuta na kuundamtandao wa kisiasa (polotical network) ili waweze kushinda kura za maoni. Hiiimesababisha kazi na shughuli za ujenzi wa chama kusimama na kuzorota.

Lakini pia imesababishaugomvi mkubwa na kutoelewana miongoni mwa viongozi hawa. Mathalani, katikamkutano mkuu wa kata za Vingunguti na Kiwalani, Mwenyekiti na Katibu wa chamajimbo la Segereawalionekana kugombanahadharani na kupigana mbele ya viongozi wa mitaa waliofika katika mkutano mkuuwa kata hizo uliokuwa umebeba agenda ya uchaguzi katika kata hizi. Hiiilisababisha kushindwa na kuahirisha uchaguzi na kikao kuvurugika. Mpakaninapoandika andiko hili, chaguzi hazijafanyika katika kata hizi.

Kama hiyo haitoshi, Katibu wasasa wa Segerea (Bw. Anatropia) ameunda na anaunda mtandao wa kikabila (tribalnetwork aiming at political victory). Anaposimamia chaguzi katika kata kamaKatibu wa Jimbo na Kiongozi wa Kamati Tendaji ya Jimbo, anahakikishaanawashawishi wapiga kura (viongozi wa wa chama wa mitaa) kuwachagua Wahaya.Katika kata ambazo uchaguzi umeshafanyika, anatumia agenda ya ukabila kuwapatawahaya wenzake katika jimbo la Segerea.

Kundi la tatu linalohasimianana makundi mengine ni kundi la watia nia wasiokuwa na Kundi. Hili nalo ni kundi.Hawa wapo katika hawa waliobaki wasiokuwa na hila wala mauzauza ndani ya chama.Hawa wanapata changamoto moja kubwa.

Hawaruhusiwi na uongoziuliopo (Bw. Kidera na Bw. Anatropia) kufanya kazi za chama. Hawashirikishwikatika kazi yoyote kwa hofu ya kueleweka kwa wapiga kura kuliko wao, (ikitokeakazi ya chamamara moja moja).
Hawa wapo zaidi ya 15. Siviongozi wa Jimbo. Wengine katika hawa pia si viongozi kabisa ndani ya Chama.
Ninaamini hapa ndipo alipoMbunge wa Segerea mwenye uwezo kusimama kidete dhidi ya huu mfumo wa CCM wa'Mangi meza'. Wanaopambana na kupigana hadharani mbele ya wanachama na wananchihawatapewa ridhaa kuongoza Segerea na kuiwakilisha mjini Dodoma.

Wakati Makao Makuu wakitoatamko na kupuliza kipenga cha kuchukua fomu za kuwania udiwani na Ubunge katikangazi za kata na Majimbo mbalimbali nchini kuanzia tarehe 18.05.2015 haditarehe 20.06.2015, Uongozi wa Jimbo la Segerea haujafanya chaguzi za viongoziwa kata katika kata Sita (6) mpaka sasa ninapoandika makala haya.

Sababu kuu za msingi zikombili, kwanza ni uwepo wa makundi haya ya akina Bw. Mchele, Bw. Kidera na Bw.Anatropia. Msuguano unasababisha shuguli za ujenzi wa chama kusimama. Mlolongo(bureaucracy) wa kufanya uchaguzi umefanywa mgumu (complicated) kutokana namgongano wa maslahi.

Kutokana na kutoaminiana kwa hawa 'mafahaliwalio hodhi chama', Kwa sasahakunamjumbe wa kamati tendaji anayeruhusiwa kwenda peke yake au wawili, watatukatika kata kusimamia uchaguzi wa Viongozi kule. Wanakwenda wajumbe wotewakamati tendaji ya jimbo. Akikosekanammoja au wawili (bahati mbaya awe ni mtia nia), kazi zinasimama.

Mwenyekiti wa sasa wa Jimbo(Bw. Kidera) anatuhumiwa kutumia mabavu, akili ndogo na hamasa za lazimakuwaongoza viongozi wenzake wa Kamati Tendaji na Kata za Jimbo. Ugomvi usioishakatika jimbo baina ya viongozi, ngumi mkononi ni tabia ya kipekee ya Mwenyekitiwetu Bw. Kidera.

Kuthibitisha hili, katikachaguzi katika kata za Bonyokwa, Kinyerezi na Kisukuru (anakotokea Bw. Kidera),Kidera alipigana ngumi katika chaguzi hizi kutokana na mgongano wa maslahimiongoni mwa kundi lake na 'Mabwana wakubwa'wengine.

Sababu ya pili ya kushindwa(fail) au kuchelewa kwenye sura ya kushindwa (delay) kufanya chaguzi katikakata hizi sita ni Kufutwa kwa chaguzi zilizofanyika katika baadhi ya kata.

Hii ni kutokana na kambi zaviongozi wa sasa kushindwa katika chaguzi hizo. Kata za Liwiti na Kiwalani(ambako ngumi zilipigwa kama nilivyoeleza awali kabisa kati ya katibu naMwenyekiti ) ni miongoni mwa kata ambazo matokeo yake yamefutwa kutokana nakushindwa kwa kambi hizi mbili zinazohodhi kamati tendaji ya Jimbo la Segerea.Kambi iliyokuwa imeshinda ni ya Mwenyekiti wa Zamani Bw. Mchele kutokana narushwa kuzidi akina Kidera.

Jimbo la Segera lina katakumi na tatu (13). Katika kata hizi, ni kata saba (7) tu zimekwisha fanyachaguzi za uongozzli wa chama. Kata sita (6) hazijafanya chaguzi. Kwa tafsirihiyo, hatuna kamati tendaji katika Kata sita. Hatuna viongozi wa kusimamiamchakato wa upatikanaji wa madiwani.katika kata sita.

Kwa kunasibisha hoja hii nahatma ya chama na matamanio yake, kitakwimu, ni kwamba 46.2% ya kata za Jimbola Segerea haina uongozi, 53.8% ya kata za jimbo ndiyo yenye uongozi kamili wachama. Kiulinganishi, nusu ya jimbo haina uongozi. Kwa hoja hii, hata viongoziwa Jimbo walioko hawana sifa za kikatiba (katiba ya chama) za kuendelea kuwaviongozi.

Ni vizuri sasa Kamanda MabereMarando (Mwenyekiti Wa CHADEMA Kanda) ukajiridhisha mwenyewe kwa uozo uliokoSegerea na umazwazwa unaoendelea kufanyika. Wananchi wa Segerea wako tayari kwamabadiliko. Wako tayari kuyafanya na kuyagharamia. Tusiwakatishe tamaa watuhawa. Tuwape kiongozi anaefaa. Tuwape mtetezi wa Maslahi, haki na matamanio yaoambaye wamekuwa wakimsubiri kwa zaidi ya nusu karne sasa.

Mungu Ibariki Tanzania, MunguIbariki UKAWA, Ibariki CHADEMA.

Nawasilisha.

Cc:
1. Mabere Marando -Mwenyekiti Kanda

2. Dr Willbroad Slaa -KatibuMkuu Taifa

3. Kamati Tendaji Segerea -Kwa Taarifa.


Ndugu yangu kwa kusoma tu ulichoadika inanysha wewe ni mtia nia na Mchele anakusumbu sana Penda usipdende km CDM whats 2 win Mchele is the bst choice
 
Kilasiku tunasema hapa ndani, hivi vilio mnavyolia hapa Jf kwa chama havina msingi wowote.

Hivi kwanini mnashindwa kuelewa?

Sasa unatuma kopi kwa Marando, Ofisi ya Marando iko hapa Jf? Nani kakwambia Marando huwa anapita hapa? Unatuma kopi kwa Dr Slaa, nani kakwambia ofisi za Dr Slaa ziko hapa Jf? Sawa, hata kama Dr huwa anapita hapa, hivi unaweza kutuambia kwanini asiuchukulie huu upuuzi wako kama ni takataka zingine tu zinazotupwa jalalani? Wewe umeshindwa hata kujishughulisha angalau hata kidogo ujue anuani iwe ya Posta au Email ya Dr Slaa au chama kwa ujumla ili kupeleka malalamiko yako haya??

Unaweza kuwa na hoja nzuri, lakini utaratibu unaoutumia siyo ndugu. Hata baamedi wenyewe wanautaratibu wao wa kufuata seuze chama kubwa kama Chadema? Tamaa yako ya kugombea nafasi moja wapo kati ya Ubunge na Udiwani isikukengeushe kiasi cha kushindwa kufuata taratibu za chama.

Jifunze kufuata taratibu kila kitu kitakwenda sawasawa alalahhhhhhh..!!!!

BACK TANGANYIKA
 
aliye post huu uzi anafanya makosa makubwa ya kukianika chama hazarani kwa mambo yasiyothibitishwa, labda ni jabza zake kwa kuwa ni mtia nia .ulitakiwa upeleke waraka kwa katibu wa kanda kama umeona hapa jimbo kuna migogoro na haijapatiwa muafaka (suluhisho) vikao halali ndivyo vitatatua mizozo iliopo tunatambua matatizo yaliopo kwenye uongozi majimboni ila hii si njia sahihi ya kuyakabili .
 
Back
Top Bottom