Secial Thread: Bongo Lyrics And other Songs

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Apr 29, 2016
20,744
25,446
Pendekeza nyimbo yeyote ya Lyrics nami nitakukumia


1.NIITE SONGA LYRICS
[Intro]
Yeaah… Duke Tachez.. yeeah
[Ubeti wa Kwanza]
Yeah, kwa uzima nafungua kinywa nachomoa hii habari
Naisoma kwa kina vina vinatoboa ka’ bikari
Nimepima homa kwenye roho ya hii sayari
Wanasema n’na ngoma eti nakohoa mistari
Sihitaji support kupost stanza nia
Verse ni lugha mbili ka’ noti ya Tanzania
Vibaraka wana njaa, bosi anawaza mia
Ni mkosi balaa, kitaa tozi anatanga njia
Mbwiga hasifiki kwa ubingwa wa busara
Ukiona giza na jogoo haliwiki ujue mida ya kulala
MC vipi? Mbona huwakilishi shida ya fukara?
Au umeshapata tija umesahau tiba uchwara?
Mdomo… hauachi tathmini ya amani ya mswaki
Mtoa roho angepokea rushwa maskini gani angebaki?
Stuck kwenye move mi’ ni mkali kwenye flow
Na-scratch maujuzi m’ ni chaki we ni black wall
Mzungu anaiga kwenye shida ndugu Mungu
Narusha machungu zaidi ya miba ya nungunungu
Nyoa dungu huu ni msiba mbwiga tubu
Nimeshika rungu nyumbu anasinywa ka’ sungusungu!

[Kiitikio x2]

Niite SONGA!
Kanuni ya harakati
Wana haraka wapo kati nabuni sina tamati
Niite SONGA!
Thamani ya muwajibikaji
Maisha darasa huru na mi’ ndo muelimikaji

[Ubeti wa Pili]
Wazazi wanasema nimeshakua
Ina maana… vibaya na vyema nimeshajua
Jua linazama tazama inanyesha mvua
Nakesha kwa dua kumuombea anayekesha akivua
Alfajiri inafika na mwezi unazama
Jogoo la Mbishi lawika na wezi wanahama
Yamaanisha zienzi tenzi kwa ujenzi salama
Uweze chutama japo kuna washenzi wanabana
Wanasema mi’ ni mkali ila why sisikiki?
Bei ya sukari inafanya ninywe chai na pipi
Rafiki… mnafiki hanifai kwa dhiki
N’nachomshukuru Mungu tu uhai silipii
Cheza pazuri, ukiweza eneza kauli
Wajinga wanatoa macho ka’ wamepoteza nauli
Tenzi shule kwa hizi tungo nikumbuke
Hizi verse nagawa bure kwenye midundo ya Duke

[Kiitikio x2]

[Ubeti wa Tatu]
Baba ananiambia… Maneno hayavunji kuti
Sawa nachana ila mbona flow zangu hazifumi suti
Mi’ mweusi roho yangu haifugi chuki
Dada anasema usiposoma mdogo wangu utarudi bushi
Meza ukweli kwa pressure uteme uongo
Palla anasema Mhaya nd’o kauleta umeme bongo
Kama husajiliwi jitahidi uchenze ndondo
Mwema Mungu sio Said anayesema ubebe gongo
Sifuri ndio inaanza na moja ndio ya pili
Cha ajabu ya pili inaanza na kwanza inasubiri
Hoja ya kishamba haina haja ya kuijadili
Hii ni hoja ya kijanja pata stanza na akili
Hii mic ni shamba na mimi ndio mkulima
Navuna ninachopanda na ulimi ndio unalima
Hapa utaganda huu sio Umwinyi na Ujima
Mzazi mwambie mwana mjini si pa kupima…
[Kiitikio x2]


2.MANGWEA FT DARK MASTER-NIPE DILI


Cowboys in the House!
Maseeeela, {Maheeela}
Cowboys in the House!
Maseeeela, {Maheeela}
C'mon, Cowboys in the...
Maseeela!
Nipeni, nipeni dili masela,
Nipeni dili nikamate mahela, maseela
Nipeni, nipeni dili masela,
Nipeni dili nikamate mahela, maseela
Nipeni dili masela, Maheeela
Nikamate Mahela, Maseela
Nipeni, nipeni dili masela,
Nipeni dili nikamate mahela
yo!

(Ubeti wa 1)
Mtoto wa kiume najituma na nguvu tena jasiri hata shule skusoma skuwa na hela skuwa na akili so...
Nipe dili mbili kila alfajiri then. then usinipe zaidi ya wiki mbili
usiponiona ujue nishatambaa nishasafiri yaaani... niko mbele mi nasaka mahela
Nipeni, nipeni dili masela, Nipeni dili mi nikamate mahela.maheela
Nicheke, Hata bar zetu ni za vichochoroni, usishangae tukishindia komoni
tunapenda sana ma wine ma champagne, lakini ndo vile tena hatuna mahela!
Tunatamani mamisosi ya kumwaga, ni ma'Pizza ma'Burgers na Mazagamazaga, {Zaga!}
Ila ndo vile tena hatuna mahela, leo wenyewe ma'cowboy wameshindia Mapera
Tumekondeana kama miili ya Misumari, si unajua kuwa mwili huwa haujengwi kwa tofali
Bali kwa ugali wa maharage au Pizza pepperoni, au kitu cha Beef then mixer Macaroni
Inapendeza ni mambo tu ya fedha, full diet ni muhimu ipatikane kwa meza {mh!}
So, nyie mnasemaje masela, tusake dili tukamate mahela, riight
“Nipeni, nipeni dili masela,— Ngwair feat. Steve
Maseeela!
Nipeni, nipeni dili masela,
Nipeni dili nikamate mahela, maseela
Nipeni, nipeni dili masela,
Nipeni dili nikamate mahela, maseela
Nipeni dili masela, Maheeela
Nikamate Mahela, Maseela
Nipeni, nipeni dili masela,
Nipeni dili nikamate mahela
yo

(Ubeti wa 2)
Sjui hata nifanye dili ipi, naona kama vile zote hazilipi yaani...
Nishaamua mi kufanya muziki, kuja 41 nae eti anataka mahela
nimeshachoka haya maisha ya mtaani, ofisi maskani, breakfast mjani {of course yes}
wakati kichwa kinawaza mamilion, vipi nita'ride na marque stallion {check bling bling}
So kila kona ya mtaa kujimix, figure dili one two, one two the five six
ikiwezekana unapiga hata fix, so acha uoga wa kulala sjui kituo cha polisi
bila mapene jua mengi utamiss, achia mbali lazima wajinga wata diss
mi mwenyewe mtu fulani wa ma'chicks, vipi nitaopoa miss bila ya kuwa na mahela?
sio visenti kama fifty fifty, kutembea mfukoni mchizi sina hata jiti
so, nyie mnasemaje masela tusake dili tutadaka mahela, yeaaaaaah!
Maseeela!
Nipeni, nipeni dili masela,
Nipeni dili nikamate mahela, maseela
Nipeni, nipeni dili masela,
Nipeni dili nikamate mahela, maseela
Nipeni dili masela, Maheeela
Nikamate Mahela, Maseela
Nipeni, nipeni dili masela,
Nipeni dili nikamate mahela
na, na

(Ubeti wa 3)
sjui nimcheki freddy, bob waziri au mwanangu zizzou sjui nani anipe dili
tena iwe moja tu yenye akili, ile ya kulala maskini na kuamka tajiri
nipeni dili nami nitoe mashairi yenye akili ili wenye sigiri wote wakiri
na kabla ya vocals ni smoke up bob marley kisha nitoe rhymes zenye sumu kali ka rift valley
na burn copy ka ice cream za Bakhresa, ni'make more money, more dough more pesa {cash}
Na waliozusha, {majombaz wawe teja!} kesha wapange foleni kuja kugombea umeneja {haha}
na wasionipenda ndo wazidi nichukia, ila dada zao kwenye kona sitoacha kuwabambia hola!
au mnasemaje masela na dawa yao ni kupata mahela, nipeni dili
Maseeela!
Nipeni, nipeni dili masela,
Nipeni dili nikamate mahela, maseela
Nipeni, nipeni dili masela,
Nipeni dili nikamate mahela, maseela
Nipeni dili masela, Maheeela
Nikamate Mahela, Maseela
Nipeni, nipeni dili masela,
Nipeni dili nikamate mahela
Maseela, maheeela
Maseela, maheeela C'mon
Maseela, maheeela Cowboy
Maseela, maheeela
Maseela, maheeela

3.T.I.D FT JAY MO-GIRLFRIEND

I: (Jay Moe)
More techniques
Ah Top In Dar yoh
Ah P Funk yoh
Ahaa (ahaa)
Ukimwona utamwona nakshi
Sio mpenda makuu
Ni mwenye tofauti kubwa
Kuanzia chini mpaka juu
Mtoto ana mapozi
Kiboko ya masister duh
Na kila nikimtazama
Nazidi kumpenda tu
Ah sisemi mengi
Bali i wanna be your boyfriend
Hakuna zaidi yako please be my girlfriend
Uwe wangu wa kufa na kuzikana mama
Unachotaka ntakupa (twende angaza tukapime)
Napenda kua na girlfriend
Mwenye kucha za kung'aa
Pamba za kuvaa awe na mimi
Napenda kua na girlfriend
Kwenye shida na balaa
Anitoe mashakani
Napenda kua na girlfriend
Mwenye pozi na nasaa
Anipende masikini
Napenda kua na girlfriend, girlfriend, girlfriend

II: (T.I.D)
Yani picha limeanza
Top in Dar nimepigika
Kwa kifupi natafuta
Dada mwenye vyangu vigezo
Kwanza akitembea kama kinyonga
Pili awe anaringa kama twiga
Nadhani hapo umenipata
Msela wako nakupa da, da, da, daata
Napenda kua na girlfriend
Mwenye kucha za kung'aa
Pamba za kuvaa awe na mimi
Napenda kua na girlfriend
Kwenye shida na balaa
Anitoe mashakani
Napenda kua na girlfriend
Mwenye pozi na nasaa
Anipende masikini
Napenda kua na girlfriend, girlfriend, girlfriend
Ukimwona utamwona nakshi
Sio mpenda makuu
Ni mwenye tofauti kubwa
Kiboko ya masister du
Mtoto ana mapozi
Mcheni chini mpaka juu
Nawaeleza washkaji
Sisemi mengi
Bali i wanna be your boyfriend
Hakuna zaidi yako
Please be my girlfriend
Kwenye shida na balaa
Nakupenda we ba, ba, ba, ba, baby
Napenda kua na girlfriend
Mwenye kucha za kung'aa
Pamba za kuvaa awe na mimi
Napenda kua na girlfriend
Kwenye shida na balaa
Anitoe mashakani
Napenda kua na girlfriend
Mwenye pozi na nasaa
Anipende masikini
Napenda kua na girlfriend, girlfriend, girlfriend
Ah
Ushindi upo lakini hauji papo kwa papo
Bora kula kiapo sihitaji tena milupo
Come here ma
Najua we kifaa haswa
Nakuahidi tutafunga ndoa
Na ili tuzae watoto ma
Ukinimwaga mawazo
Nitavunjika guu
Twende nyumbani love
Tukapate raha tu
Ni wewe tu pekee simhitaji mwingine aisee
Nawe nakuomba usipagawe na mapedeshee
Ah mwenye pamba za kuvaa
Kucha za kung'aa
Hakuna mwingine (napenda kua na girlfriend)
Ah pozi kali za kukaa
Wazushi wanashangaa
Wanavyoona napenda (kua na girlfriend)
Ndani ya moyo wangu una nafasi dunia nzima
Muziki wako mnene
Kila nikiimba wanasema

Jay Moe na TID
Girlfriend ndo soundtrack
Nawe ndo barafu wa moyo
Napenda kua na girlfriend
Mwenye kucha za kung'aa
Pamba za kuvaa awe na mimi
Napenda kua na girlfriend
Kwenye shida na balaa
Anitoe mashakani
Napenda kua na girlfriend
Mwenye pozi na nasaa
Anipende masikini
Napenda kua na girlfriend, girlfriend, girlfriend
No no no

4.PROF JAY FT JUMA NATURE-ZALI LA MENTALI

Ubet wa 1.
Naamka asubuhi nipo chwiri tena mapema
Nautoa mkeka sakafuni kisha naukunja vyema
Nawaza nitakula nini mentali kisha naguna
Naanza kujikongoja kichwa chini mikono nyuma
Naelekea kilingeni nilikopaki mkokoteni
Nasaga na rumba kimshazali nyie acheni
Nawapa 'Hi' machizi wananipa peace tunafurahi
Tunapiga stori nyingi walah bila maslahi
Mara napata zali napeleka kago uswahili
Wananipa bukumbili dangaa chee nazisunda chini
Wakati natoka huku kijasho chembamba kikinitoka
Nikaona toto ya nguvu nikajikuta nimeropoka
"Dada habari samahani naomba niulize swali"
Akajibu "maskini koma tafadhali hii ngoma ya gari"
"Ehee unajua dada", "we vipi hebu nipishe"
"Dada mbona mkali", "wee kinyago kubali yaishe"
Nikasema Inshala sawa hiyo yote kwa sababu ya fukara
Nisije nikakubaka nitupwe selo nikawe kafara
Nikaachana nae sehemu za nyuma akizitingsha
Nilikula kwa macho hali yangu haikuridhisha
Nageuza mkokoteni nakuelekea maskani
Nikawapa stori machizi wakanicheka ikawa utani
Siku moja nililemaa maskani sikuwa na tenda
Na nilikuwa nikitafakari ni vipi siku itakwenda
Kumbe kuna gari ilikuja na kupaki karibu yangu
Sikuweza kuisikia labda sababu ya njaa yangu
Nilishtushwa ghafla na mlio mkali wa honi
Nilipatwa na mshtuko na hofu kubwa moyoni
Kuangalia pembeni ilikuwa imepaki Toyota Surf
Kulikuwa na sura ngeni ya malaika akaomba tafu
Nilisita kunyanyuka kwa sababu nilikuwa mchafu
Na alitoa elfu kumi na alikuwa akitaka dafu
Nilipokea hela alichotaka nilimletea akakipokea
Tabasamu zito akanitolea nilimpa chenji
"Ohh no keep chenji, una mawazo mengi itakufariji week end"
Alikunywa maji ya dafu alitupa na kunikonyeza
Niliganda kama nyamafu nikahisi alinibeza
Alinipa busu la huba shavuni akanichombeza
"I love You"
Akawasha gari akateleza


Chorus - Kiitikio
Zali la mentali limetokea wakati mimi n'njaa
Nikapendwa na demu mkali
Na kuwaacha watu wote wakinishangaa 'katika mitaaa'


Verse 2
Zilipita siku mbili nikiwaza kilichotokea
Nikawaza yule ni mtu au jini amenitokea
Potelea mbali uchawi hauendi kwa mentali
Narudi nanyonya napuliza mentali nakuwa shwari
Nabeba rumbesa nakatiza Samora Avenue
Mara kwa ghafla mbele yangu inapaki Toyota mark II
Ohh napata ghadhabu mara nyingi sipendi dharau
Naifuata gari kuanza kupaka mara nahema juu juuu "Aaa" ni yule mrembo"
"Maskini pole sana mzigo mbona mzito kweli utafika nao salama"
Natabasamu "Oh nimeshazoea mama na namshukuru Mwenyezi Mungu kwani hii ni kama karama"
Anakuwa mnyonge anakata kucha anantazama anaaza kulia anatoa leso anainama
"Namwambia bibie ni mara ya pili tunaonana
na sidhani kama ni mbaya iwapo tutafahamiana"
"Naitwa Vicki, nina miaka 22 ni mtoto wa kipekee kwenye familia ya kitajiri"
'Oh naitwa Jay ukiniita fukara haukosei
Na naishi kwa nguvu za macho siku zenyewe hazisogei
Alishuka toka garini na kusema
"Jay nakupenda"
Akaruka kwangu mdomoni nakuanza kupata denda
Nilichomoka kwake na kuanza kurudi nyuma
"Tafadhali mpenzi Jay jamani nionee huruma
Acha kubeba mizigo panda ndani kwenye mchuna
Twende Mbezi Beach kwangu upepo unapovuma"
Sikiliza Vick napenda tuwe marafiki
Lakini hadhi yako hutakiwi kuwa na mtu wa dhiki
Hata wazazi wako naaamini hawataafiki
Tajiri na tajiri maskini sithaminiki
Tafuta kibopa mwenzio ili usishushe hadhi yako
Mimi sistahili hata kuwa kijakazi wako
"Tafadhali Jay usitamke maneno hayo
Naomba unielewe haya machache niyasemayo
Hadi huu wakati mimi nimekupenda kwa dhati
Ukikubali niwe wako nitajiita mwenye bahati"
Nimeelewa Vicki naomba niwahishe mzigo
Tajiri ni mkorofi anan'subiri migomigo
Na kila nikichelewa mwenzako napata kipigo
Nasaga na rumba jua na mvua kwa mpigo
Tuliongea mengi akanipa hela za matumizi
Sikuwahi hata kuziona nilikuwa kama chizi
Niliacha kubeba mizigo penzi letu likaota mizizi
Watu wa uswahili wakasema natumia kizizi


Rudia Kiitikio

Verse 3.
Baada ya miezi mitano Vick alipata ujauzito
Tulifurahi sana mambo yakawa mpwito-mpwito
Swala la kwenda kwa wazazi wake halikuwa zito
Walifurahi sana kuniona tukafanya tambiko
Walisema Jay maisha ya Vick yapo chini yako
Tumefurahi mmpendana kumlea ni jukumu lako
Ilipangwa mikakati kamambe ya kufunga ndoa
Watu hawakuamini kama mimi vipi nitamuoa
Ilifika siku ya siku mentali Jay ndani ya jumba
Na Vick ndani ya shela hakuna uchawi wala ndumba
Tulishikana mikono ni nderemo na vifijo
Tukafunga pingu za maisha kanisani bila ya fujo
Furaha isiyo kifani lilifanyika bonge la party
Watoto wa uswahili walibeba wali kwenye mashati (du)
Zawadi zilizagaa zilikuwa nyingi tena kemkem
Baba mkwe alitupa benzi, kiwanda nyumba na bm
Acha zawadi nyingi kutoka kila sehemu
Nilikumbuka nikacheka nilivyoteswa na wale mademu
Mambo swadakta nipo na Vick ndio my wife
Kidume nang'aa wanajigonga shenzi tipe (shenzi tipe)
Nilipokuwa arosto mlinikwepa kama ukoma
Mambo juu ya mstari kunisalimu mnaona noma
Sasa hivi napeta nabadili gari full kipupwe
Mlio nicheka wanataka ardhi ipasuke
Naelekea kilingeni kuwapa dili machizi wangu
Tena mara kwa mara siwezi kuwacha asili yangu
Vick ni Jay, Jay ni Vick mustarehe kutoka ndani ya dhiki
Sasa kila siku sherehe ahaaaa!

5.MWANA FA FT LINAH-YALAITI

keeping good music alive that is my job
My sunshine my moonlight and everything i dream about
Linah let's go
(Chorus)
Yalaiti napenda pasi kifani,
Tofauti sikutilii moyoni
Sikuachi leo na kesho peponi
Aaa aaa aa i love you (repeat chorus)

(Verse:1)
Sambaza love kama dawa sikuachi mpaka napagawa
Wakisema me siwagusi natingisha kichwa
Mapenzi yako yanielemea kama chupa nzima ya tequilla
Si ulishasomw nakupenda acha masihara
Kuna aja gani nikushikie fimbo ili nikusikilza kama gorrila
me mtu na mapenz yangu nmeshaaja zaman usela
Una matatizo yako najua
Na me yangu boo
With together from this moment
We will sue them through
Nikukosea nisute,nipige vibao nizodoe,
Ninunie kwa siku kadhaa ila nachokuomba usinikimbie
Mapenzi hatamu me kwangu hadithi mambo ya kizamani hayo
Ukiniudhi ntakupiga kwa kanga ndo nilivyofunzwa Tanga ivyo
Toaga mabusu nikufute kwa kumbatio mpk tamu kwa kiss ya pili
Ukinikumbuka iwe kilio
Sipendi mapenzi napenda mapenzi nawe usinikatae utaniumiza me na
biashara na wewe


repeat(chorus)


(Verse2)
Nshasema Sipendi mapenzi napenda mapenzi nawe
Usinikatae utaniumiza me na biashara na wewe
Ushaangaliwa niunge tela
Usingoje mpaka uambiwe
ushaangukiwa anguka nawe usizubae mpaka irejewe
Kwako ntakuwa Bushoke sitajiulza ka zezeta
Yatoe mahaba mapenzi amani tumepita
Me sakafuni we ukingoni mbio zangu haziendi mbali
Na moyo wangu nitapenda bila kujali
Hata marefa wana timu zao mama
Hupanga matokeo
pambano lianze
washajua goli ngapi ngapi leo
Husiache kuvaa nguo ndefu hivi vimini waachie vicheche
Mwanamke kwetu staa hatuna tupendao sio wote
Akili haziwezi moyo na wenyewe una ubongo pia hauwezi kufuata fuata
kila utakachouambia
Nahitaji yako mapenzi
Napata picha yako kwanza
Natamani upate yangu nayo iwe inakuliwaza


(Bridge)
Linah:toa shaka na wasiwasi moyoni*2
Kukuepuka ilo haliwezekani
ntakushika leo na kesho peponi
repeat(Chorus)

6.AFANDE SELE-DARUBINI KALI

[Chorus – Ditto]
Mimi ni msanii, mimi ni msanii Kioo cha jamii (kioo cha jamii)
Mimi naona mbali, mimi naona mbali Kwa darubini kali (kwa darubini kali)

[Verse 1 – Afande Sele]
Afande anasema wote (wote kimya) Ntakayo nena hapa yatamgusa mwenye hekima
(Hapo!) hapo ulipo Kama waipenda pepo kwanini uogope kifo?
(Eehee) unachekesha
(Aah) wanipa raha
Unafikiri mbinguni utakwenda kwa motor car eh?
(Ama utapata zali kama Yesu alivyopaa?)
Acha kujidanganya, kwa Mungu si kwa mzungu Unapokwenda kwa pipa ikibidi kwa njia za panya
(Loo) haiwezekani
(Hasa?) bila ya imani Unaelipiza baya kwa jema…
(We ni shetani) Haufai kanisani, haufai msikitini Na hutufai kwenye fani Take care utapotea (Aliwazalo mjinga ndilo litalomtokea) Na hii ndo darubini (darubini) Wasanii muweke akilini, hasa kwa mtu makini Makini kiusanii Ila kama mtalii (no sweat, tupa kapuni) Watakuokota chini Unafanya mziki Bongo unaekti kama matoni (Ya nini?!) Bora kuimba katuni Lugha ngeni za nini kwenye mziki wa nyumbani? (Wakati Bongo Flava inapeta zaidi uswahilini) Mi n’nacheka sana (hee) Kuna vitu vya kuimba vyenye maana kila kona (Sasa?) Inakuwa vipi unataja taja majina tu, nyimbo nzima (Tena) kwa mistari isiyo na vina!


[Chorus – Ditto]
Mimi ni msanii, mimi ni msanii Kioo cha jamii (kioo cha jamii) Mimi naona mbali, mimi naona mbali Kwa darubini kali (kwa darubini kali)


[Verse 2 – Afande Sele]
Yes, naona mbali, kwa darubini kali Ndo maana mziki wangu unaegemea kwenye ukweli Kwa mfano… (Labda ungewapo mfano kabla hujashusha kibano) Nasema rap ni ukweli mtupu, rap jasiri Rap si kuimba uongo (kama siasa za bongo) Useme kwenu una Benz wakati jumba la udongo!Mh! Bwa’ mdogo acha upambe, unavyopelekwa tu Unakwenda kama ling’ombe (Simama utupe ujumbe) Kama huwezi unyamaze Nasema mara ya mwisho… (Sio lazima wote tuimbe) Watu wanataka ujumbe, sio majigambo tu (Mnasifu ngono na pombe) Pumbavu hamna soni eh, kwenye zama za ukimwi Kwenye nchi masikini, ya pili kutoka chini Afande nashangaa (hata Mungu anakataa) Kwa msanii wa nchi hii Kuimba nyimbo za furaha, kila saa (Wakati huko kijijini watu wanakufa kwa njaa) Haipendezi, kutomjali mwenzako eti kwa ajili yamavazi (haipendezi) Ama kujiona bora eti kwa ajili ya makazi (haipendezi) Kuna tofauti gani kati ya Temeke na Mbezi? Au labda ukiishi Mbezi utakapokufa hauozi? (twashangaa) Eti Majani vipi? Kwanza stopisha beat Nimuulize kijana alichokipata ni kipi Aliponyoosha miguu wakati blanketi ni fupi (Aling’atwa na mbu kwenye visigino huyo)

[Chorus – Ditto]
Mimi ni msanii, mimi ni msanii Kioo cha jamii (kioo cha jamii) Mimi naona mbali, mimi naona mbali Kwa darubini kali (kwa darubini kali)


[Verse 3 – Afande Sele]
Na bado tu, mwaka huu haki ya nani Mamluki kwenye game mtatoka taka msitake (Na hii ndo maanake) Mwanamke kama hataki basi muache aende zake (usimbake) Kulazimisha penzi ni hatari sawa na kulazimishafani (Kisha unaleta utani) Mpumbavu, hilo ni kosa kama padri kubaka muumini (Au kama ticha mkuu kumbaka denti ofisini) Utafungwa! (arabuni utanyongwa) Bwa’ mdogo, ndani ya shamba la miwa hauwezi ukavuna miogo (Kuna tofauti kubwa kati ya wivu na usongo) Sahau superstar, superstar Kujifanya msanii ndani ya jumba la sanaa (Wasanii tunashangaa) unashuka si tunapaa (Unainuka si tunakaa) Ukipotea? (Kwetu furaha) Adui? (Muombee njaa) Ntanyoosha mikono juu hata kama alikuwa shujaa
[Chorus – Ditto] x2 Mimi ni msanii, mimi ni msanii Kioo cha jamii (kioo cha jamii) Mimi naona mbali, mimi naona mbali Kwa darubini kali (kwa darubini kali)


7.NUH MZIWANDA FT ALI KIBA-JIKE SHUPA

Verse 1 – Nuh Mziwanda
Nipeleke kwa muganga
Na mimi nataka wanga
Maana mapenzi yamenikoroga kinoma
Anichanje chale mwili muzima
Nisimkumbuke hata jina
Yule asidi, gaidi wa moyo wangu
Anichanje chale mwili muzima
Nisimkumbuke hata jina
Yule asidi, gaidi wa moyo wangu


Bridge – Nuh Mziwanda
Haya mapenzi basi
Nimeyavulia shati
Kupendwa ni ajira
Na mimi sina vyeti
Haya mapenzi basi
Nimeyavulia shati
Kupendwa ni ajira
Na mimi sina vyeti


Hook - Nuh Mziwanda
Kule kukusifia
Mabaya kukufichia
Mbele ya mama, oh baba, oh lala
Mapenzi si ubondia
Najikaza huku nateketea
Bora nijivue, nisijisumbue
Mapenzi si ubondia
Najikaza huku nateketea
Bora nijivue, nisijisumbue

Chorus – Alikiba
Sasa basi (sasa basi)
Inatosha, nimekopesha mwili wangu
Bila kuogopa
Kumbe jike shupa (shupa)
Hata kwenye karata haupo
Unaruka kila sehemu umeshapita
Sasa basi


Verse 2 – Nuh Mziwanda
Ulijidai kunipima akili kwa mizani
Kuniendesha kama toy, kukosa nuru kisa kizani
Ukanikinai aibu kunitia hadharani
Kuniona sifai, masikini nimekosa nini?!
Bridge – Nuh Mziwanda
Haya mapenzi basi
Nimeyavulia shati
Kupendwa ni ajira
Na mimi sina vyeti
Haya mapenzi basi
Nimeyavulia shati
Kupendwa ni ajira
Na mimi sina vyeti
Hook - Nuh Mziwanda
Kule kukusifia
Mabaya kukufichia
Mbele ya mama, oh baba, oh lala
Mapenzi si ubondia
Najikaza huku nateketea
Bora nijivue, nisijisumbue
Mapenzi si ubondia
Najikaza huku nateketea
Bora nijivue, nisijisumbue


Chorus – Alikiba
Sasa basi (sasa basi)
Inatosha, nimekopesha mwili wangu
Bila kuogopa
Kumbe jike shupa (shupa)
Hata kwenye karata haupo
Unaruka kila sehemu umeshapita
Outro – Alikiba & Nuh Mziwanda
Yeap!
What goes around, comes around baby
Mr T-Touch
Nuh Mziwanda, we pop, anhaa
Mr T-Touch, pop it
K Zone
You know how it is always and always
Anhaa hey, yeap
Mziwanda!
Inauma, inauma (x4)

8.BEN POL-MOYO MASHINE

[Verse 1]
Najua kukikucha ntajuta kama nikikuta unanitania
Maana moyo wangu nimekupa uweke
Mimi ni mfungwa tena ni mjinga
Nimejileta gerezani
Tena sikuwaza ntakuwa mateka
Mmh

[Pre-Chorus]
Najua ulinizungusha sana
Sijali huwa ni mambo ya ujana
Kukupenda wewe sijuti
Maneno yalisemwa mengi sana
Kuna wakati nilikata tamaa
Kukupenda wewe sichoki

[Chorus]
(Moyo mashine)
Ila majibu ya upendo ulishakosa
(Acha waseme)
Nimekupendea nini
(Moyo mashine)
Ila majibu ya upendo ulishakosaga
(Wacha waseme)
Nimekupendea nini

[Verse 2]
Nafsi inanituma upendo uko nje ya maneno
Ila vitendo
Kama bubu akipenda atanena vipi kwa maneno
Pasina vitendo?
Kiziwi, hata ukimwambia “nakupenda” wata hasikii
Ila vitendo oh
Wewe sijui sababu za kukupenda
Siwezi sema, ila utaona ah

[Pre-Chorus]
Najua ulinizungusha sana
Sijali huwa ni mambo ya ujana
Kukupenda wewe sijuti
Maneno yalisemwa mengi sana
Kuna wakati nilikata tamaa
Kukupenda wewe sichoki

[Chorus]
(Moyo mashine)
Ila majibu ya upendo ulishakosa
(Acha waseme)
Nimekupendea nini
(Moyo mashine)
Ila majibu ya upendo ulishakosaga
(Wacha waseme)
Nimekupendea nini

[Bridge]
Oh kama moyo ulisimama nlipokuona
Hukuongea, hukucheka, nilikuona tu
Na tabia sikufahamu, labda niache mwanadamu
Ukipenda usishangae ni upofu wa moyo
Kumbe moyo ulinirubuni, hukusema umependa nini

[Chorus]
(Moyo mashine)
Ila majibu ya upendo ulishakosa
(Acha waseme)
Nimekupendea nini
(Moyo mashine)
Ila majibu ya upendo ulishakosaga
(Wacha waseme)
Nimekupendea nini

9.NANDY-WASIKUDANGANYE

Ubeti wa 1.
Wasikuambie kwamba mimi eti sina lolote
Labda wakuambie sina ujanja juu yako
Wasikudanganye watakupa utakacho chochote
Wataitoa wapi furaha yako
Maana wabaya hawatoki mbali
Jirani yako we ndio anapenda usile
Hawatokubali kuona bendera ya penzi lako inapepea
Hawatokujali kipindi ambacho mawazo
Yanafanya usile watakutupia mbali
Si ulisema unataka gari na nimekubali kuenyeka mie
Tule mbegu na ugali kesho tutapata kipenzi nivumilie
Ukinitema itakuwa ni hatari utanipa na ajali kitanzi
Kuninginia si tumetoka mbali
Mazoea na ushakuwa maua
Moyo moyo wangu mimi
Unauendesha moyo moyo
Funga macho na masikio Ziba moyo moyo
Usiwasikie usiwaone pia moyo moyo
Umegota kwako moyo wangu moyo moyo
Auuu uuh moyo moyo Usiwaone pia

Uneti wa 2.
Kukosa majaribu moyo usije
Tia donda ukauchubua maumivu yani adhibu
Kisa upendo furaha kuichua
Kwenye kosa niadhibu nami mwanadamu
Siku ntakosea kukuacha
Sijaribu wapi niende nami kwako nishajifia
Ila usifanye kama fimbo
Ufanane na tindo ukashindwa kujali maumivu yangu
Si ulisema unataka gari na nimekubali kuenyeka mie
Tule mbegu na ugali kesho tutapata kipenzi nivumilie
Ukinitema itakuwa ni hatari utanipa na ajali kitanzi
Kuninginia si tumetoka mbali
Mazoea na ushakuwa maua
Moyo moyo wangu mimi
Unauendesha moyo moyo
Funga macho na masikio Ziba moyo moyo
Usiwasikie usiwaone pia moyo moyo
Umegota kwako moyo wangu moyo moyo
Auuu uuh moyo moyo Usiwaone pia
Ouuhh moyo moyoo huu moyo
Moooooyo heyyyy huu moyooo oh moyooo wangu
Mimi ah moyo moyo funga macho moyo moyo uuh baby


9.DIAMOND-I MISS YOU

Hello hapo vipi sijui unanisikia
Hello nnamaneno natamani kukwambia
Hello tafadhari usije nikatia
Hello ona mpaka nasaau kusalimia
Habari ghani leo nmekukumba sana
Na mama yangu twakuwazagaa
Vipi nyumbani hali ya mumeo na wana
Na aunty shani wa chimwagaa ah ah
Kile kidonda changu cha roho bado kinatia tabu
Nnajitaidi kukaza roho ila nadhidisha adhabu
Tena silali oh nasubiri maajabu
Maumivu yangu ayajapata dawa
… I miss you nakukumbuka iye iyeh
I miss you nakukumbuka iye iyeh
… I miss you nakukumbuka iye iyeh
I miss you nakukumbuka iye iyeh
Na roho yangu mama bingili bingili
Ah nikikuwaza bingili bingili
Nikisinzia bingili bingili bayoyo
Oh nikilala bingili bingili
Ih inama inuka uwoh bingili bingili
Uku sina raha bingili bingili bingili bayoyo
Ah iyeeeh ah iyeeeh
Tatizo kwetu sijui nini kosa langu
Mpaka nikawa adui ghafla ukanichukiaga
Nawaza ila siambui ama shida zangu
Simba nikawa chui mi roho inaniumaga
Yawezekana ahadi zangu zisizotimia
Ndio maana haukutaka kusubiria
Nasema nyama mwisho wa siku naleta bamia
Chai mchana usiku dona kurumaghia
Nilitamani sana ila wangu vyangu palinishia
Ningalikua na uwezo ningekutimizia
Mingali unafuraha haya maumivu ntayavumilia
Ila japo nambie ivi unanifikiria maana eh eeh

Nakumkumbuka iyeeh iyeh nakumkumbuka sana ooh
… I miss you nakukumbuka iye iyeh
I miss you nakukumbuka iye iyeh
… I miss you nakukumbuka iye iyeh
I miss you nakukumbuka iye iyeh
Ah na roho yangu mama bingili bingili
Ah nikikuwaza bingili bingili
Nikisinzia bingili bingili bayoyo
Oh nikilala bingili bingili
Ih inama inuka uwoh bingili bingili
Uku sina raha bingili bingili bingili bayoyo
Ata nikila bingili bingili
Nikikuwa bingili bingili
Nikilala heeh bingili bingili bayoyo
Ooh ona roho mama bingili bingili
Ah nikikuwaza bingili bingili
Nikisinzia bingili bingili bayoyo
Heeeh! Roho yangu mama bingili bingili
Heh heh heeh! Bingili bingili
Heh heh heeh! Bingili bingili bayoyo
Oooh roho yangu mama bingili bingili
Ih inama inuka uwoh bingili bingili
Ajabu sina raha bingili bingili bayoyo
Ah ata nikila!

10.ALI KIBA-SEDUCE ME


Chorus
Do not do like that i'm too smart dada
Seduce me like what a hell (ah hold up)
What the hell
Don’t do like that I’m too smart dada
Seduce me like what a hell (ah hold up)
What a hell

Verse 1
Nakuona unakata be careful sister
Na kama unataka they call me heart breaker (breaker)
Nina majina mapya kila mmoja amenipa
Wananiita kipusa ooh pasua kichwa
Mi ninamajina mapya kila kona wamenipa
Wananiita kipusa ooh pasua kichwa

Chorus
Do not do like that I’m too smart dada
Seduce me like what a hell (ah hold up)
What the hell
Don’t do like that I’m too smart dada
Seduce me like what a hell (ah hold up)
What a hell

Verse 2
Eh Najua kupenda nagawa mavumba
Na kama unataka they call me kiba Rockstar
Nina mandinga mapya kila mmoja nampa
Wananiita misifa ooh pasua kichwa
Nina mandinga mapya kila mmoja nampa
Wananiita misifa ooh pasua kichwa ona

Chorus
Do not do like that I’m too smart dada
Seduce me like what a hell (ah hold up)
What the hell
Don’t do like that I’m too smart dada
Seduce me like what a hell (ah hold up)
What a hell

Outro
Yup You know me girl I go by the name Alikiba
Unstopable what the…
Bambamba lailalaila bamba Despacito
Despacito cheza kidogo
Zungusha kiuno chako unionyeshe


Weka wa kwako
 
JIDENNA-BAMBI

[Chorus]
Bambi Bambi (Ahh Bam-Bambi)
My dear, my dear, my dear (Ahh Bam-Bambi)
My dear I want you here (Ahh Bam-Bambi)
But don't get too near for there’s lions beware (Ahh Bam-Bambi)
[Verse 2]

[Chorus]
Bambi Bambi (Ahh Bam-Bambi)
My dear, my dear, my dear (Ahh Bam-Bambi)
My dear I want you here (Ahh Bam-Bambi)
But don't get too near for there’s lions beware (Ahh Bam-Bambi)

[Verse 3]
No one can take you from me Bambi
No one can take you from me Bambi
No one can take you from me Bambi

[Chorus]
Bambi Bambi (Ahh Bam-Bambi)
My dear, my dear, my dear (Ahh Bam-Bambi)
My dear I want you here (Ahh Bam-Bambi)
But don't get too near for there’s lions beware (Ahh Bam-Bambi)
I just wanna see my baby, that's my Bambi, that's my dear
I just wanna see my baby, that's my Bambi, that's my dear
I just wanna see my baby, that's my Bambi, that's my dear
I just wanna see my baby, that's my Bambi, that's my dear
 
nyimbo ya NASTY C
" hello naw "
Nasty C Lyrics
"HellNaw"
Am I ever gonna quit? (Hell Naw) Will I dumb itdown a bit? (Hell Naw) Am I runningwith the shit? Fuckinright I bringthe levelsto this bitch You knowyouright mynigga Am I ever gonna quit?(hellnaw) (Hell Naw) Will Idumb it down a bit? (hellnaw) (Hell Naw) Am Irunning withthe shit? (I really am) Fuckinright I bringthe levelsto this bitch (itsall done) Youknowyou right
I'mmakingmusicfor niggasin suits & ties They all got a"money& evil"smile That'sendingconversations withthe "I'll letmypeople call yourpeople" line I rap forthe ones still in highschool Probably my age andtheythink I'm cool For the little ones calling me uncle Shit youknowI do thisforthe dimes too I'mtrynafind out where mind at Idon't think I'mcrazy I'mbeyond that EverygirlI'mwithis either blessed or obsessed with dressing and lookinglike Beyoncé AndI'ma jiggyjigga, yea I'mon that There's not a thingIhate morethan acontract I been killingniggas since I was the kidthat rushes homejustto go play mortal combat I'mtooWAVylike format Icould really bringitto your doormat I don't thinkyou wannaget embarrassed by the young king aaah-aah Noor man I'mthe leader, now justget behind me Youknowyou like my shit, you can't deny it Bro, I cameup like BOOM BOOM BOOM,dead silence. Someone get the bodies, get the
Am I ever gonna quit? (Hell Naw) Will I dumb itdown a bit? (Hell Naw) Am I runningwith the shit? Fuckinright I bringthe levelsto this bitch You knowyouright mynigga Am I ever gonna quit?(hellnaw) (Hell Naw) Will Idumb it down a bit? (hellnaw) (Hell Naw) Am Irunning withthe shit? (I really am) Fuckinright I bringthe levelsto this bitch (itsall done) Youknowyou right
Thereal ones listento me when Itell my story Thefakes ones always wanna writeit forme I never wanted torain on your parade I started doing all of thisforwhite Jordan's Now I madeit.Clear.. to the store managerI wantthe shitdelivered to me It's like..All the niggas that youall praise.Arejustsome other niggasto me Dumbing down is a motherfuckn mission forme I knowa couplethat could usea couplelyricsfromme I makeall ofmy womenmirror for me And then I tell em wouldyouplease pick apillowfor me Aaahnigga wouldyou pleasecrya river forme Put a pistolto yourhead andpull the triggerforme Tellmedo youwant a kidney or a liverfromme? If youhate me then why do you loginto Twitter forme Isn't thisa biiiitchtho A shortnigga cameandhit a swiiish hoe I'mdoing every Day andnightshift Justto get itcoz youain'treally hot untilyour wristcold Can somebodyorder mesome chill tho.. I really neverever hadno chill,bro But I'm really givingeverybodychills. Niggachill chill chill,can somebody get the window. Damncan somebody get the window
Am I ever gonna quit? (Hell Naw) Will I dumb itdown a bit? (Hell Naw) Am I runningwith the shit? Fuckinright I bringthe levelsto this bitch You knowyouright mynigga Am I ever gonna quit?(hellnaw) (Hell Naw) Will Idumb it down a bit? (hellnaw) (Hell Naw) Am Irunning withthe shit? (I really am) Fuckinright I bringthe levelsto this bitch (itsall done) Youknowyou right
 
Nasty C Lyrics
"HellNaw"
Am I ever gonna quit? (Hell Naw) Will I dumb itdown a bit? (Hell Naw) Am I runningwith the shit? Fuckinright I bringthe levelsto this bitch You knowyouright mynigga Am I ever gonna quit?(hellnaw) (Hell Naw) Will Idumb it down a bit? (hellnaw) (Hell Naw) Am Irunning withthe shit? (I really am) Fuckinright I bringthe levelsto this bitch (itsall done) Youknowyou right
I'mmakingmusicfor niggasin suits & ties They all got a"money& evil"smile That'sendingconversations withthe "I'll letmypeople call yourpeople" line I rap forthe ones still in highschool Probably my age andtheythink I'm cool For the little ones calling me uncle Shit youknowI do thisforthe dimes too I'mtrynafind out where mind at Idon't think I'mcrazy I'mbeyond that EverygirlI'mwithis either blessed or obsessed with dressing and lookinglike Beyoncé AndI'ma jiggyjigga, yea I'mon that There's not a thingIhate morethan acontract I been killingniggas since I was the kidthat rushes homejustto go play mortal combat I'mtooWAVylike format Icould really bringitto your doormat I don't thinkyou wannaget embarrassed by the young king aaah-aah Noor man I'mthe leader, now justget behind me Youknowyou like my shit, you can't deny it Bro, I cameup like BOOM BOOM BOOM,dead silence. Someone get the bodies, get the
Am I ever gonna quit? (Hell Naw) Will I dumb itdown a bit? (Hell Naw) Am I runningwith the shit? Fuckinright I bringthe levelsto this bitch You knowyouright mynigga Am I ever gonna quit?(hellnaw) (Hell Naw) Will Idumb it down a bit? (hellnaw) (Hell Naw) Am Irunning withthe shit? (I really am) Fuckinright I bringthe levelsto this bitch (itsall done) Youknowyou right
Thereal ones listento me when Itell my story Thefakes ones always wanna writeit forme I never wanted torain on your parade I started doing all of thisforwhite Jordan's Now I madeit.Clear.. to the store managerI wantthe shitdelivered to me It's like..All the niggas that youall praise.Arejustsome other niggasto me Dumbing down is a motherfuckn mission forme I knowa couplethat could usea couplelyricsfromme I makeall ofmy womenmirror for me And then I tell em wouldyouplease pick apillowfor me Aaahnigga wouldyou pleasecrya river forme Put a pistolto yourhead andpull the triggerforme Tellmedo youwant a kidney or a liverfromme? If youhate me then why do you loginto Twitter forme Isn't thisa biiiitchtho A shortnigga cameandhit a swiiish hoe I'mdoing every Day andnightshift Justto get itcoz youain'treally hot untilyour wristcold Can somebodyorder mesome chill tho.. I really neverever hadno chill,bro But I'm really givingeverybodychills. Niggachill chill chill,can somebody get the window. Damncan somebody get the window
Am I ever gonna quit? (Hell Naw) Will I dumb itdown a bit? (Hell Naw) Am I runningwith the shit? Fuckinright I bringthe levelsto this bitch You knowyouright mynigga Am I ever gonna quit?(hellnaw) (Hell Naw) Will Idumb it down a bit? (hellnaw) (Hell Naw) Am Irunning withthe shit? (I really am) Fuckinright I bringthe levelsto this bitch (itsall done) Youknowyou right
Oyooooo thanks you sana..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom