Serikali ya Saudia imesimamisha urushaji matangazo na kufunga ofisi za kanali ya televishani ya al-Jazira inayomilikiwa na Qatar nchini humo.
Taarifa iliyotangazwa leo na viongozi wa Saudia imewataka wafanyakazi wote na waandishi wa habari wa kanali hiyo ya Qatar wenye uraia wa Saudia ambao wanaishi nje ya nchi, kurejea nyumbani haraka iwezekanavyo. Kufuatia hali hiyo, serikali ya Qatar nayo imejibu mapigo kwa kusimamisha safari za Shirika la Ndege la Qatar Airways kwenda nchini Saudia, sambamba na kuwataka raia wanaoishi nchini Saudia kurejea nchini.
Kadhalika Wizara ya Mambo ya Nje ya Qatar imetangaza kuwa, uamuzi wa Saudia, Imarat, Bahrain, Misri na Libya wa kukata mahusiano na Doha, kamwe hautoathiri kwa namna yoyote maisha ya kawaida ya raia wake au watu wanaoishi ndani ya ardhi hiyo (Qatar.) Kauli hiyo imetolewa kufuatia uamuzi wa nchi hizo za Kiarabu kutangaza mapema leo kukata mahusiano yao na Qatar ambapo serikali ya Doha imesema kuwa, uamuzi huo umechukuliwa kwa pupa na kwamba madai yaliyochukuliwa na Saudia dhidi yake hayana msingi wowote.
Source: Parstoday.sw
Serikali ya Saudia imesimamisha urushaji matangazo na kufunga ofisi za kanali ya televishani ya al-Jazira inayomilikiwa na Qatar nchini humo.
Taarifa iliyotangazwa leo na viongozi wa Saudia imewataka wafanyakazi wote na waandishi wa habari wa kanali hiyo ya Qatar wenye uraia wa Saudia ambao wanaishi nje ya nchi, kurejea nyumbani haraka iwezekanavyo. Kufuatia hali hiyo, serikali ya Qatar nayo imejibu mapigo kwa kusimamisha safari za Shirika la Ndege la Qatar Airways kwenda nchini Saudia, sambamba na kuwataka raia wanaoishi nchini Saudia kurejea nchini.
Kadhalika Wizara ya Mambo ya Nje ya Qatar imetangaza kuwa, uamuzi wa Saudia, Imarat, Bahrain, Misri na Libya wa kukata mahusiano na Doha, kamwe hautoathiri kwa namna yoyote maisha ya kawaida ya raia wake au watu wanaoishi ndani ya ardhi hiyo (Qatar.) Kauli hiyo imetolewa kufuatia uamuzi wa nchi hizo za Kiarabu kutangaza mapema leo kukata mahusiano yao na Qatar ambapo serikali ya Doha imesema kuwa, uamuzi huo umechukuliwa kwa pupa na kwamba madai yaliyochukuliwa na Saudia dhidi yake hayana msingi wowote.
Source: Parstoday.sw
Hapo wanawakomoa wananchi wake wenyeweHilo swala la kuifungia aljazeera Saudia ndio kulikua kifungua kinywa cha hivi vikwazo vyote nakumbuka walifungia aljazeera hii ni week sasa hakuna access yao Saudia.
[emoji23] [emoji23] [emoji38]Haha Trump signed $350B weapons deal with Saud ...sasa we unazan zitatumika wapi?
Hapana, aljazeera ndio inaumia kukosa coverage ya Saudia maana yake yameshuka kwenye ukubwa wa masafa na kuna matangazo watayakosa kutoka Saudia, commercials.Hapo wanawakomoa wananchi wake wenyewe