Samweli Sitta live star tv

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
52,172
Reaction score
162,619
Habari wadau,

Jumapili hii tarehe 16/11/2014, kuanzia saa 4:30 asubuhi,aliekuwa Mwenyekiti wa Bunge la katiba ambae pia ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki na mbunge wa Urambo,bwana Samweli Sitta,atakuwa live star tv katika kipindi cha Medani za Siasa na Uchumi kinachorushwa na kituo hicho.

Na katika kuonyesha kuwa hajutii kitendo alichokifanya katika usimamizi wake wa kuandika katiba mpya,bwana Sitta anasikika akisema,na hapa namnukuu, "kila siku najisikia wiwa kuikamilisha kazi ile kwa uaminifu".

Hiyo na moja ya kauli zake iliyorekodiwa na inayotumika katika kukitangaza kipindi hicho cha Jumapili.

Ni nafasi nyingine ya kupima kauli,mtazamo na uwezo wa kiongozi huyu mwenye utata mkubwa.

Stay tuned.
 

Kaka yaani kabisa badala nipumzike ni mwangalie juha six, nitake radhi kwanza
 

Huyu ni Sh.t.ni tu hawezi geuka malaika hata ajitakase vp!
 
Ahsante kwa taarifa nipange ratiba mapema saa 4:30 nitoke out
 
Ni heri niangalue vipindi vya chekechea au catoon
 
Hana jipya huyu ameshuka kisiasa na hapati ubunge/uraisi 2015!
 
Jumapili tuna kazi moja tu,kumsikiliza Warioba na kumtazama live ITV na Radio one.
Sio mpuuzi huyo,kubwa jinga
 


Ana utata gani wakati hata bei yake inajulikana?
 
mke wake na familia yake ndiyo watamtizama......!
 
Inahitaji ujasiri wa hali ya juu ili kutazama kipindi cha Samuel Sitta.
 
Watamsikiliza wanafiki na wehu wenzie, wengine hatutakuwa na muda wa kupoteza kumsikiliza huyu mnafiki mkubwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…