Samwel John Sitta: Nyota iliyozimika

MTK

JF-Expert Member
Joined
Apr 19, 2012
Posts
8,920
Reaction score
6,859
Wahenga walisema; "Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni"; Ni ukweli usiopingika; labda kwa wale wenye bifu zao binafsi!! kwamba Mh Samwel John Sitta; kupitia falsafa yake ya "Kasi na Viwango" alilisimamia Bunge la 9 la jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa weledi; umahiri na ufanisi mkubwa sana na hivyo kufaulu kujijengea heshima isiyo na kifani nchini na kwa hiyo kuwa tumaini kubwa la watanzania wengi kwake kuchukua nafasi katika ngazi kubwa katika uongozi wa taifa letu.

Moja ya mambo makubwa aliyoyasimamia akiwa Spika wa bunge la tisa ni uchunguzi wa kashfa ya "Rich-Monduli" iliyohusu mkataba tata wa kufua nishati ya umeme, ambayo ilipelekea kuzuka kwa moja ya matetemeko makubwa kabisa ya kisiasa katika historia ya Tanzania baada ya uchunguzi huo kusababisha kujiuzulu kwa Waziri mkuu wa JMT Mh Edward Ngoyai Lowassa.

Mara tu Baada ya tetemeko hilo kuu, ndipo nyota ya kisiasa ya Mh Sitta ilipoanza kufifia alipochukua hatua isiyotarajiwa na wengi ya kuuzima ghafla na bila maelezo ya kina mjadala wa kashfa ya Rich-Monduli; sina uhakika kama hatua hiyo ilitokana na kutishiwa maisha au kisiasa; kwa vyovyote vile kwa maoni yangu alifanya makosa makubwa sana kwa kuamua kuiponya ama roho yake au nafasi yake baada ya kuwa amechukua hatua za kuichunguza kashfa hiyo ambayo tayari ilishamgharimu sana mwenzie Mh Edward Lowassa! ni bora angeendeleza alichokianzisha mpaka hitimisho kamili;("logical conclusion"). Wengi wetu tulivunjika moyo na kuanza kupoteza imani kwa kasi sana kwa Mh Sitta; kumbe tulikuwa tunastaajabu ya Musa kabla ya kuyaona ya "farahani"!!

Hata hivyo Mh Sitta alifanikiwa kuiokoa nyota yake isizimike kabisa pale alipoamua kuendeleza mapambano dhidi ya ufisadi na rushwa nje ya bunge kupitia vyombo vya habari, makongamano na makanisani japo alishapoteza "moral authority" ya kukemea maovu hayo baada ya kuuzima mjadala wa moja ya kashfa kubwa zaidi za ufisadi zilizowahi kutokea nchini; Rich-monduli!

Madhara yalishafanyika kwa hiyo kelele za Mh Six dhidi ya ufisadi hazikumsaidia kutetea nafasi yake ya Uspika baada ya kutengenezewa Zengwe la kimataifa ambalo asingeweza kulikwepa kwamba wakati ulikuwa muafaka kuwa na Spika mwanamke; Zengwe ambalo lilimfikisha Mh Anne makinda katika ofisi ya Spika akiwa mwanamke wa kwanza nchini kushika wadhifa huo adhimu.

Kwa bahati nzuri rekodi nzuri ya Bwana Sitta katika bunge la 9 na mapambano yake ya hadharani dhidi ya ufisadi na rushwa vilimsaidia Mh Sitta kubakiza matumaini miongoni mwa baadhi ya watanzania ambao walimuona kwamba alikuwa bado ni Kiongozi bora kuliko wenzie wengi katika chama tawala na kwa hiyo alipojitokeza kugombea uenyekiti wa Bunge maalumu la katiba watanzania wengi waliweka matumaini yao kwake kwamba angesaidia kuliongoza BMK kwa ufanisi kama alivyofanya katika bunge la 9 na kwa hiyo kupelekea kutuwezesha kupata sio tu katiba mpya bali KATIBA BORA kwa kurejea falsafa yake ya kasi na viwango;

Lo salalalah; maajabu ya 8 ya dunia yalikuwa yanatungojea!! mara tu baada ya Mzee Six kuukwaa ueneyekiti wa BMK; kufumba na kufumbua akabadilika "kwa kasi na viwango" vya kutisha kabisa! wengi wetu mpaka leo hii hatujaweza kuelewa ni nini kilichomsibu Mzee huyo mnyamwezi wa Urambo; hatujui kama kilichombadilisha ghafla kilikuwa ni vitisho vya kisiasa au dhidi maisha yake au haja ya kuwafurahisha mahafidhina ndani ya CCM aliowaudhi kutokana uendeshaji wake wa bunge la 9!?

Ghafla bin vuu! Mzee Six akaanza ubabe, kuchakachua kanuni za BMK, akaweka misimamo ya kuegemea matakwa ya chama chake badala ya taifa kisha akatuangushia bomu la Hiroshima kwa kutaka kuwaziba midomo wananchi; Tume ya mabadiliko ya Katiba na vyombo vya habari wasijadili jambo linalohusu mustakabali wao na taifa lao!!

Na hapo ndipo utabiri wa Mh godbless Lema mbunge wa Arusha mjini ulipoanza kutimia; Mh. Lema aliwahi kumwambiua Mh Six katika ukumbi wa BMK mara baada ya kuchaguliwa kuwa mwenyekiti kwamba nafasi aliyoipata ilikuwa ni kitanzi cha kujinyongea mwenyewe kwani kama angefanikiwa kulipatia taifa katiba mpya na bora basi ndoto yake kuelekea kugombea Urais 2015 ingeimarika; vinginevyo isipopatika katiba mpya na bora; basi ndoto hiyo atakuwa ameinyonga kwa mikono yake mweyewe!

Mpaka hapa tulipo hakuna mwenye shaka kwamba Mzee six amesha inyonga ndoto yake kwa mikono yake mwenyewe; kwa sasa wengi wetu tunamuona kama NYOTA ILIYOZIMIKA; Msaliti aliyenyonga matumaini ya watanzania; kwa sababu sasa tunajua fika kwamba hatuna matumaini tena ya kupata Katiba mpya wachilia mbali katiba bora!

Kwa bahati mbaya sana; kulingana na hulka za wanasiasa wa NJI hii sitashangaa kumuona na kumsikia Mh Six akijitoa akili na kuendelea kuusaka Urais 2015.
Ushauri wangu wa bure Mzee Six ajitafakari kwa kina kisha achukue hatua inayofaa; afungashe virago vyake arudi Urambo akalee wajukuu na kuanzisha kilimo cha Asali; Kura ya Urais ni ndoto ya mbali sana kwake kwa sasa!

Kwa baadhi yetu rambi rambi za maisha Mh Sitta kisiasa imeshaandikwa inasubiri tu kuchapishwa; swali sio kama itachapishwa bali lini itachapishwa?! it is only a matter of time; and that time is rapidly winding down on him;
Kwa heri ya kuonana Mzee Samwel John Sitta; asante kwa utumishi wako wa umma wa muda mrefu. Tutakukumbuka kwa jinsi ulivyoendesha Bunge la 9 la JMT; kule CDA huna la kujivunia na pale kituo cha Uwekezaji; TIC yule kijana wa Kimasai Ole naiko alikupiku ukafutika kabisa kama hukuwahi kuwepo! na sasa huu utendaji kazi wako katika BMK ni sura inayostahili kufutwa kabisa kutoka katika historia ya nchi yetu.
Adieu Sitta; Good riddance & GOD SPEED.
 
Heading ingekuwa hivi
Zitto Zuberi Kabwe: Nyota iliyofifia na kuzimika
 
Last edited by a moderator:
Katiba mpya itapatikna kwa Bunge linaloendelea Dodoma, ila nasikitika haitakuwa ya wananchi. Jamaa hawa walivyo mabingwa wa kuchakachua na kununua watu, unadhani watashindwa kununua wajumbe 16 tu wa kufanya katiba yao ipite??? Unadhani wao ni wajinga kuendelea na mjadala huo huku wakijua fika kuwa ni feki kama hawajawajaza wahusika na minoti? Unaweza kunibishia lakini tusubiri. Time will tell!
 
Huyu ni saws na ugonjwa Wa sukari. Anakufa taratibuuu.
 
Aksante Mungu kwa mchakato huu wa Katiba.Umetuonesha kuwa ccm kwa sasa hakuna mtu anayefaa si kanisani wala msikitini.wote wapo kwa ajiri ya matumbo yao si Tanzania
 
Mkuu watanzania tumekuwa wapole sana.why kila kitu tuamuliwe na watu wasiozidi milioni sita.Kukataa maoni yetu ni dharau kubwa kwetu.
 
Mh Sitta

Tungekushauri upite Nakummat na maduka mengine kutafuta madoli na toys zitakazokusaidia ukicheza na wajukuu zako.

Safari yako kisiasa imeshakamilika na historia imejiandika. Huna wa kumlaumu bali wewe mwenyewe.

Wenzako wametafuta mbuyu, nawe ukayatumia meno yako kuzitafuna.

Aliyekurushia tambara la moto siku ya ufunguzi wa bunge kakaa pembeni akikuangalia unavyoungua na kuteketea.

Ulikubali kubeba mzigo huo ukiamini una mabega ya kutosha.
Wale usalama na FFU uliowaita kutuliza hali usikikilizwe wamerudi kambini na kukuacha mwenyewe.

Kwetu sisi Watanzania tunashukuru sana kwa yaliyotokea. Bila hayo, tungejikuta tunanunua mbuzi ndani ya gunia.

Huu ni upendo mkubwa wa manani kwa taifa hili masikini.
Tunazidi kuomba ili waliobaki wavue ngozi za kondoo tuwabaini kama chui au fisi.

Mheshimiwa Sitta
Hakika ukiwa na zizi la ng'ombe kuna uwezekano jirani yako asijue unao wangapi.
Siku utakapotembea na kilo moja ya nyama iliyooza ndiyo hadithi ya mtaani na mjini.

Leo Sitta umebeba kilo ya nyama iliyooza, walikabidhi wakisifia ushujaa wako na ubabe wa kutamba mitaani. Wamekaa pembeni wanakucheka , nzi wakivuvuta kwa bidii kinywani na machoni mwako.

Safari yako kisiasa imefika ukomo.
Hakuna mahali katika taifa hili unapoweza kubadili mawazo ya wananchi juu yako.

Historia imejiandika na haitafutwa daima dawamu.
Utaishi nayo hadi siku tutakaposikia mwenyezi ameamua apendavyo.

Tunakutakia safari njema Urambo, na tusingependa kuchafua vitabu vingine vya historia kwa kuendelea kulisikia jina lako.

Tutapata habari tu siku nyingine historia itakapokoma kujiandika.

Ni vema ukashauriana na familia njia bora ya kuanza maisha mapya ya ulezi wa wajukuu.

Tungekushauri usizungumzie siasa kabisa maana hiyo ni thing of past.

Ni history tunayoweza kuipata maktaba wakati wowote.

Huna sababu za kuhangaika tena na hilo.
Google na you tube watatusaidia tutakapohitaji kuwakumbuka wale waliotuvuta nyuma wakati tunajiandaa kukimbia.

Mapunziko mema
 
Sitta ni nyota inayoendelea kung'aa ila mnajitahidi kwa nguvu zote Kuizima au kuifunika ..... Lakini kawaida panapo ukweli uongo hujitenga.......
Pia tukumbuke uongo hupaa ila ukweli hapanda ngazi... Hatua kwa hatua ... Vipingamizi vingi na miba ya kila aina mwisho wa siku ukifika juu haushuki ng'ooo ndo yanayomkuta sitta...

Mmekazana kupika fitna kuwa safari yake ya kisiasa imefika mwisho ila facts hamna!!!!!!!

No research... No right to speak....

No facts... No right to argue.......

Acheni fitna za kisiasa angalieni penye hali kwa maslahi y taifa.... Peace
 
Huyu mzee unaejaribu kumtetea hapa pamoja na kuongoza dharau na ubaguzi dhidi ya watanzania na kuligawa Taifa, kwenye nchi nyingine kama Israel angekuwa ameshapigwa risasi mpaka sasa kwa manufaa ya Taifa na watu wake-Hapa kwetu tu ndio bado tunamchekea kwa kuwa kila kitu tunasubiri hisani ya watawala
 
Tusubiri facts kutoka kwa wananchi.

Hata yeye anajua safari imekamilika, ni muda wa kubeba mizigo.
 
Ni mnafiki wa hatari huyu mzee, hata kuendesha bunge namna ile hakulenga kutetea maslahi ya watanzania bali alikuwa analipiza kisasa na kujijengea mazingira ya kuupata ukikwete mwakani. Hana lolote, halafu ni mbinafsi ndoo maana alijenga ofisi ya spika jimboni kwake Urambo. Yaani amekera sana, leo hii huyu Sita ni wa kuzuia watu kujadili mstakabali wa nchi yao? Hana hata aibu anamtuhumu Mengi of all the people. Si ni Sita huyu huyu alikubali mgogoro wa Mengi na Malima uibukie bungeni na kidogo avuruge kanuni za bunge leo hii anamuona Mengi ni tatizo? Huyu hata nikikutana nae ana kwa ana shikamoo yangu hapati.
 
Democratic Constitution Making

Njia zote halali mpaka sasa zimetumika lakini uelewi kwanini wengine wanakuwa wakorofi. Na awataki kuendelea kwa hatua kama zilivyopangwa na wanataka tuchukue hiyo rasimu ya wataalamu kama katiba yenyewe.

Kwanini rasimu lazima zijadiliwe na wataalamu na zibadilishwe inapobidi kukidhi uhalisia wa utekelezaji.

Unless labda njia hizo zilitumika na kukawa na national participation ina maana rasimu ni tathmini tu ya wananchi walioshiriki lakini hayo si matakwa ya wananchi sasa sijui kwanini watu wanapotosha ya kuwa watu millioni 46 wameamua hivyo tunapozungumzia muundo wa serikari na kama tutachukulia maoni ya muundo wa serikari na mawazo mengine yaliyotolewa kupitia rasimu ina maana hata tathmini inaonyesha asilimia kubwa yetu ya walioulizwa muundo wa serikari aukuwa tatizo.

Tatizo letu ni hili kweli rasimu ndio limetatua bila ya mjadala wa kitaifa? be it in the representative format. Tusipofanya hivyo tutakua tume address the following issues;

Ni hivi Mh jaji Joseph Sinde Warioba na tume wakae kimya rasimu wameshaikabidhi na waache mchakato uendelee alikadhalika UKAWA need to show maturity inorder to move forward agenda za watu binafsi hazina tija kwa mustakabali wa taifa wacha wananchi waamue mwishowe na hoja zipiganiwe bungeni democratically.


Acknowledgement: most of the arguments in this post were cited in the work of "Vivien Hart" (Democratic ConstitutionMaking)
 
It seems for you to show maturity is synonymous as to showing hypocrisy. To the contrary! A hypocrite fellow is as immature as an infant and UKAWA fellows are not like that!!
 
It seems for you to show maturity is synonymous as to showing hypocrisy. To the contrary! A hypocrite fellow is as immature as an infant and UKAWA fellows are not like that!!
Are you insinuating a constitution draft is beyond debates? if yes where does that legitimacy arise from democratically and what was the reason for the constitution assembly?.

Cambodia Democratic process

PUBLIC PARTICIPATION IN THE PROCESS

Pre- and Post-Constitution Public Education and Participation


Ndio sababu ya ulazima wa referendum kwanza na kutoa somo la uraia kuhusu muundo wa serikari hili wananchi wajue future inafananaje na waamue kwa uelewa in terms of their social contract hayo ya gharama za muungano yapo kwenye mistari ya chuki tu, cha muhimu wananchi waelewe fate ya serikari tatu na haki zao zinakuwaje kuwaje huko mbele jaji warioba awezi kuja kusema sababu za wananchi kuamua serikari tatu zaidi ya hadithi zakeza mahakama, devolution or kupigiana mizinga ya uraisi and other tosh can he seriously defend ya kuwa serikari tatu imetokana na wananchi kuelewa social contract zao maana hicho ndio cha muhimu kwa subjects si mizinga ya raisi.

Sasa wewe unatetea hoja ya UKAWA matakwa ya wananchi kwa line zipi za wananchi gharama za kuendesha serikari, mizinga ya raisi au mahakama za jaji warioba na hata hizo randama zinaelezea hoja za wananchi na wanavyoguswa mbona jaji Warioba aongelei argument hizo maana hiyo ndio perspective ya wananchi looked upon social contract and rights na si hadithi mahakama za mahakama or ritual za kufyatua mizinga.


DEMOCRATIC REPRESENTATION

Kwa sasa CCM inaingia bungeni katika mazingira ya pluralism ambapo wamejikuta na advantage iliyotokana na democratic elections kwenye bunge, na vyama vyote vinaingia kwa misingi hiyo hiyo through representative, sasa tatizo liko wapi wakati ndivyo mambo yanavyofanyika duniani.

Akili za kuambiwa changanya na zako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…